Pages

Friday, November 3, 2017

NAIBU WAZIRI DK.NDUNGULILE AZINDUA CHETI CHA MFUMO WA UHAKIKI UBORA WA HUDUMA KATIKA KIWANGO CHA KIMATAIFA TFDA

1
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akiwa katika picha ya pamoja na watendaji wa TFDA  wakati akizindua CHETI CHA MFUMO WA UHAKIKI UBORA WA HUDUMA KATIKA KIWANGO CHA KIMATAIFA CHA ISO 9001-2015 tukio lililofanyika katika viunga vya Mamlaka hiyo jijini Dar es Salaam.
2
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akitoa maelekezo mbele ya Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula, Dawa na Vipodozi (TFDA)  Hiiti Sillo wakatikati na Mwenyekiti wa Bodi ya TFDA Dkt Ben Moses.
3
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile  na watendaji wa TFDA wakiwa wameshishika cheti cha mfumo wa Uhakiki Bora katika Kiwango cha Kimataifa Cha Iso 9001-2015.
4
Meneja Uchunguzi wa Dawa na Vipodozi Dkt. Yonah Hebron akitoa maelekezo mbele ya Naibu Waziri Dkt. Faustine Ndugulile wakati akitembelea maabara katika viunga vya Mamlaka hiyo jijini Dar es Salaam, kulia kwa Naibu Waziri ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula, Dawa na Vipodozi (TFDA)  Hiiti Sillo.
5
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile wakwanza kushoto akisindikizwa na Mkurugenzi Mkuu TFDA wapili,  Mwenyekiti wa Bodi ya TFDA Dkt. Ben Moses wa tatu, na wa mwisho ni Meneja uchunguzi wa chakula  Dkt. Mziray
DSC_0485
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akiangalia baadhi ya bidhaa zinazopelekwa TFDA kwa ajili ya Uchunguzi
…………………………………………………………………………………….
NA WAMJW-DAR ES SALAAM
Mamlaka ya Chakula , Dawa na Vipodozi TFDA imetakiwa kuboresha udhibiti wa uingizaji wa  Dawa, Vipodozi na Chakula nchini  kiholela ili kulinda afya ya Watanzania .
Hayo yamesemwa  na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile wakati wa kuzindua CHETI CHA MFUMO WA UHAKIKI UBORA WA HUDUMA KATIKA KIWANGO CHA KIMATAIFA CHA ISO 9001-2015 leo jijini Dar es Salaam.
“Dawa ni kitu nyeti sana, hatuwezi kuruhusu dawa feki kuingia nchini, mnafanya kazi nzuri sana katika nyanja hii  na muendelee na mpango huu ili kudhibiti uingizaji wa vyakula visivyokidhi viwango na...
mahitaji ya watanzania, ” alisema Dkt.  Ndugulile.
Aidha Dkt. Ndugulile amesema kuwa TFDA wanatakiwa kuzingatia muongozo wa kupitisha vyakula na vipodozi kwenye mipaka ya nchi kwa kuzingatia ubora na viwango vilivyoweka katika kudhibiti uingizaji mbovu wa vyakula.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa TFDA Bw. Hiiti Silo amesema kuwa ili kuendelea kukidhi matakwa ya wateja na mahitaji yao wameamua kuendana na kiwango cha kimataifa na kuwaita ISO kuja kuhakiki ambapo wamefanikiwa kukidhi na kupata cheti.
“Shirika la Viwango la Kimataifa ISO limehakiki ubora wa huduma zetu katika kukidhi mahitaji na matakwa ya watumiaji wa huduma zetu na kutupatia cheti kinachoturuhusu kutoa huduma nchini” alisema Bw. Silo.
Aidha Bw. Silo amesema kuwa wapo bega kwa bega na Serikali ya awamu ya tano ianyoongozwa na Rais Dkt. John pombe Magufuli katika kusogeza mbele gurudumu la afya hapa nchini kupitia taasisi  ya TFDA.

No comments:

Post a Comment