Mkuu wa mkoa wa Pwani, mhandisi
Evarist Ndikilo, wa katikati akizungumza jambo na uongozi wa chama cha
umwagiliaji Ruvu (CHAURU), na viongozi wa wilaya, wakati alipotembelea
chama hicho. (picha na Mwamvua Mwinyi)
Mkuu wa mkoa wa Pwani, mhandisi
Evarist Ndikilo, wa kwanza kulia akitoa maelekezo kwa mwenyekiti wa
chama cha umwagiliaji Ruvu (CHAURU) sadala Chacha mwenye kofia. (picha
na Mwamvua Mwinyi)
…………………………………………………………………………
Na Mwamvua Mwinyi,Chalinze
SERIKALI mkoani Pwani ,imetoa
siku saba kwa uongozi uliopita wa Chama Cha Umwagiliaji Ruvu
(CHAURU)kukamatwa na polisi pamoja na mwekezaji wa
kichina ,kampuni ya
M/S Guoming Tang walieingia nae mkataba feki uliogharimu dollar 35,000.
Aidha uongozi huo umetakiwa kufanya makabidhiano na uongozi mpya uliochaguliwa ndani ya wiki moja .
Mkuu wa mkoa wa Pwani mhandisi
,Evarist Ndikilo,alitoa agizo hilo,baada ya kutembelea chama hicho cha
umwagiliaji ,kujionea namna wanavyoendeleza kilimo,wanavyojiendesha na
changamoto zao.
Alieleza ,uongozi mpya unashindwa
kutekeleza majukumu yake kwasasa kutokana na uongozi uliopita kugomea
kufanya makabidhiano ya baadhi ya mali hali inayowapa wakati mgumu
uongozi mpya kutekeleza majukumu yake.
Mhandisi Ndikilo,alimuagiza
kamanda wa polisi mkoani humo,kamishna msaidizi mwandamizi Onesmo
Lyanga,kushughulikia agizo hilo ili hatua za kisheria na uchunguzi
uchukue nafasi yake.
“Ni lazima mkataba huo upitiwe
upya,na mhakikishe wote wanatiwa nguvuni na mchina wao ,ili kueleza
kwanini wanang’ang’ania mali za chama na kuingia mkataba batiri kinyume
na taratibu”alisisitiza.
Mhandisi Ndikilo ,alieleza kuna
kitu kipo nyuma ya pazia ,ambacho kina manufaa ya matumbo ya uongozi huo
kwakuwa haiwezekani washindwe kufanya makabidhiano hadi leo .
Katika hatua nyingine aliuagiza
uongozi mpya kufanya tathmini ya vifaa vinavyotakiwa kwenye kinu cha
mashine ya kukobolea mpunga ,ambayo haifanyikazi .
Aliwataka pia kukifanyia usafi na
kuweka mazingira yake kwenye hali ya usafi tofauti na alivyokuta baada
ya kutembelea kwani siyo mazingira mazuri na hayaridhishi.
Nae mwenyekiti wa ushirika huo, Sadala Chacha,alipokea maagizo waliyopewa kutoka kwa mkuu wa mkoa huyo na kusema watayasimamia .
Awali alieleza uongozi uliopita
umeshindwa kuwapa ushirikiano na kufanya makabidhiano hadi sasa suala
ambalo linawapa wakati mgumu.
Akizungumzia suala la mwekezaji
wa kichina ,Sadala alisema hawamtambui mwekezaji huyo na hawajui mkataba
wake,na wala hawajakabidhiwa mkataba huo .
Sadala alisema ,mbali ya
mwekezaji huyo kuingia mkataba usiojulikana kwa wanachama pia amezuia
maji yasiingie kwenye mashamba ya wanachama zaidi ya 800 hali
inayokwamisha juhudi za uendelezaji kilimo.
Kutokana na mwekezaji kufunga maji,amewanyima huduma wanaolima shamba namba 9, 10, 12, 13 na kuendelea wasipate huduma.
No comments:
Post a Comment