Mkuu wa mkoa wa Pwani, mhandisi
Evarist Ndikilo, wa pili kushoto akionyeshwa namna bidhaa mbalimbali
kama pilipili zinavyofungashwa katika kiwanda cha kusindika matunda cha
Elven Agri co. Ltd kilichopo Mapinga Bagamoyo. (picha na Mwamvua
Mwinyi)
Mkuu wa mkoa wa Pwani, mhandisi
Evarist Ndikilo, aliyeshika ndizi, akionyeshwa hatua za uzalishaji
katika usindikaji wa matunda kwenye kiwanda cha kusindika matunda cha
Elven Agri co. Ltd kilichopo Mapinga, Bagamoyo. (picha na Mwamvua
Mwinyi)
…………………………………………………………………………………..
Na Mwamvua Mwinyi, Bagamoyo
WAKULIMA wa matunda wametakiwa
kulima kwa kutumia mbegu bora na kilimo cha kisasa ili kupata soko
kwenye viwanda vinavyosindika zao hilo, ndani na nje ya nchi.
Aidha wananchi wameshauriwa
kulima kilimo kinachostahimili ukame ikiwemo
mahindi,mhogo,viazi vitamu
na mikunde ili kujihadhali na baa la njaa baadae
Hata hivyo wametakiwa kuhifadhi
chakula wakati wa mavuno utakapofika kwani kwa kufanya hivyo itawasaidia
kuwa na akiba ya kutosha.
Rai hiyo ilitolewa na mkuu wa
mkoa wa Pwani, mhandisi Evarist Ndikilo, alipotembelea kiwanda cha Elven
Agri company ltd kilichopo Mapinga na kiwanda cha Sayona
kinachomilikiwa na kampuni MAMA ya MMI steel,kilichopo kata ya Mboga
wilayani Bagamoyo.
Alieleza, wakulima wengi wanahitaji kulima kwa tija badala ya kupata hasara kwa kukosa masoko.
Mhandisi Ndikilo alisema, kwa
kutambua hilo, kuna kila sababu ya kubadilika kwa kuona umuhimu wa
kulima matunda yaliyo na rutuba, bora na yanayojiuza.
“Wataalamu wa kilimo, watendaji
wa halmashauri katika idara hii, mtoke maofisini muende kuwapa elimu
wakulima hawa ili waweze kujifunza kulima kwa kutumia mbegu za msimu
mfupi,kuweka pembejeo na kupalilia “
“Kwa kutoa elimu za mara kwa mara
kwa kufuata teknolojia za kisasa, lazima waende na wakati ili waweze
kunufaika kwa jasho lao “alisema mhandisi Ndikilo.
Mhandisi Ndikilo alielezea
kwamba, wakulima waondokane na Kilimo cha kizamani, badala yake walime
kilimo cha tija ili kujiinua kiuchumi na kimaendeleo.
Hata hivyo alisema, kiwanda cha Elven Agri .co. ltd,na Sayona kwa sasa vitakuwa ni mkombozi kwa wakulima hao wa matunda .
Mkuu huyo wa mkoa alifafanua,
kiwanda cha Elven kinahitaji tani nane na cha Sayona tani tisa kwa siku
hivyo vitakuwa msaada mkubwa kwa wakulima wa matunda kimkoa na Tanzania
kijumla.
Mkurugenzi mtendaji wa Elven Agri Company Ltd, Darpan Pindolia ,alisema kiwanda kwasasa kinazalisha kwa asilimia 20 pekee.
Mkurugenzi mtendaji wa Elven Agri Company Ltd, Darpan Pindolia ,alisema kiwanda kwasasa kinazalisha kwa asilimia 20 pekee.
Alibainisha, kiwanda
kinajishughulisha na kusindika matunda mbalimbali kama nanasi, ndizi,
maembe,pilipili na mapeasi ,kimejengwa kwa gharama za dollar mil.nne
sawa na sh.bil 10,kimeanza uzalishaji mwezi uliopita.
Nae afisa uhusiano wa kampuni za
MMI steel ikiwemo Sayona,Abubakar Mlawa ,alisema kiwanda cha Sayona
kimefikia asilimia 70 ya ujenzi na mwezi novemba mwaka huu kinatarajia
kuanza kazi.
Alieleza kiwanda hicho,kwasasa kimeajiri watu 100 wakiwemo mafundi ujenzi na kitakapoanza kazi kitaajiri watu 800.
Mlawa alisema,mahitaji makubwa ni
matunda hasa maembe,nyanya na matunda mengine hivyo wakulima wa matunda
wachangamkie fursa hiyo.
Kiwanda cha Sayona ni moja ya
uwekezaji mkubwa mkoani Pwani,na kinalenga kugharimu dollar mil.55 sawa
na sh.bil.120 katika ujenzi wake.
No comments:
Post a Comment