Mswada wa sheria mtandao nchini
Thailand uliwekwa mezani kujadiliwa takriban wiki kadhaa zilizo pita.
Muswada huo ambao ulikua ukingoja kupitishwa kua sheria umepelekea
kelele nyingi Nchini humo ambapo wananchi wake walitaka ufanyiwe
marekebisho kabla ya kua sheria huku wengine wakiukataa kabisa.
Wana usalama mtandao nchini humo
walijaribu kutoa ufafanuzi ambao haukuzaa matunda na hatimae kutaka
msaada kutoka kwa wanausalama mtandao wa maeneo mengine.
Wiki mbili zilizo pita wahalifu
mtandao Nchini humo walitangaza kushambulia tovuti za serikali ili
kushinikiza mamlaka kufanyia kazi marekebisho ya sheria hizo za mtandao
ambazo walidai hawakukubaliana nazo – Baadae walianza kushambulia tovuti
mbali mbali na kusababisha mtafaruku mkubwa.
Tovuti ya polisi ya nchini humo
(Royal Thai Police Office) ni miongoni mwa tovuti zilizo shambuliwa
kimtandao ambapo ilidukuliwa na baadae kuangushwa kabisa. Kitu ambacho
kilipelekea hasira kwa vyombo vya ulinzi na usalama vya nchi hiyo.
Naibu waziri mkuu na waziri wa
ulinzi Mh. Prawit Wongsuwon, alitangaza kukamata washukiwa tisa (9) wa
uhalifu huo mtandao pamoja na vifaa vyao huku akiongeza ya kua serikali
ya nchi hiyo haita linyamazia tukio hilo na kusema watachukua hatua
stahiki kwa kila atakae thibitika na uhalifu huo.
No comments:
Post a Comment