Pages

Saturday, December 31, 2016

Taasisi ya wanaharakati ya Bibi. Siti bint Saad yakutana na wanahabari


duu
Na Khadija Khamis –Maelezo  Zanzibar .
Mwenyekiti wa Taasisi ya Mwanaharakati  Bibi Siti bint Saad, Bi Nasra Moh’d Hilali amewataka wanawake kushikamana kwa pamoja kupinga udhalilishaji wa kijinsia kwa wanawake na watoto .
Kauli hiyo ameitoa alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari Ofisi kwake ndani ya Wizara ya Habari  Utalii Utamaduni na Michezo  Kikwajuni Mjini Zanzibar.

Alisema udhalilishaji wa kijinsia umekithiri katika maeneo  mbali mbali ya Zanzibar jambo ambalo linapelekea kudhoofisha maendeleo nchini hivyo amewashauri akinamama kupiga vita vitendo hivyo .
Katika kupambana na  vitendo hivyo Bi Nasra ameitaka jamii kujenga mashirikiano ya pamoja katika mfumo mzima wa  malezi ya watoto na kuona watoto  ni wa jamii  na sio ya wazazi wawili pekee.
“Tujiunge  kwa pamoja tuseme hatutaki udhalilishaji na  tusiiachie Serikali pekee kwani suala hilo ni kubwa na linaathiri watu wengi kisaikolojia,”alisema Bi. Nasra
Alieleza tukio la hivi karibuni la  mwanamke kuchomwa moto na mpenzi wake  katika kijiji cha Paje linaonyesha udhalilishaji uliokithiri  katika jamii   na kuchangia kupoteza nguvu kazi ya taifa.
Alifafanua kuwa kauli mbaya  wanazotoa wanaume kwa wake zao zinachangia udhalilishaji uliowazi na amewataka akinababa kuwa na kauli nzuri kwa familia  zao.
 Aidha aliwataka akinamama  kuwa tayari  kutoa taarifa wanapobaini  dalili za mtoto wa jirani  anataka kudhalilishwa  ili hatua za kuzuia vitendo hivyo ziweze kuchukuliwa kwa haraka.

No comments:

Post a Comment