Pages

Saturday, December 3, 2016

MWANAFUNZI WA KIDATO CHA TATU ANUSURIKA KUFA MARA BAADA YA KUBAKWA NA KUTELEKEZWA KORONGONI


Image result for KAMANDA WA POLISI
ARUSHA MKUMBO
Kamanda wa Polisi Mkoani Arusha Charles Mkumbo
Na Woinde Shizza,Meru

MWANAFUNZI wa kidato cha tatu katika shule ya sekondari Kitefu iliyopo
Meru  mkoani Arusha amenusurika kufa mara baada ya kubakwa na kuteketezwa
kwenye  korongo la mchanga na kusababishiwa  maumivu makali
yaliyomsababishia kushindwa kuendelea na masomo yake kwa muda.

Akielezea tukio hilo  mwanafunzi huyo ambae amehifadhiwa jina kwa sababu za
kimaadili alisema kuwa tukio hilo lilitokea novembar 13 majira ya saa 12.30
alipotoka kwa kinyozi.

Alisema kuwa ghafla akiwa anarudi nyumbani alikutana na mtu huyo
aliyemfanyia kitendo hicho na kuanza kumkaba shingoni na kumziba mkono ili
asitoe sauti na ndipo alipomfanyia kitendo hicho cha ukatili ambacho
kimemfanyia ashindwe kuendelea na masomo yake vizuri.

"Nilijitahidi sana kupiga kelele ila kutokana na alivyokuwa amenikaba
shingoni alinifanyia kitendo hiki kikatili ambacho kimejipelekea nishindwe
kuendelea na masomo yangu kwani baada ya vipimo nimeonekana aliniumiza
sehemu nyingi ikiwemo hata kifua changu"alisema mwanafunzi huyo.

Kwa upande wake mama mzazi wa mwanafunzi huyo aliyejitambulisha Rambikiaeli
Akyoo  alisema kuwa kutokana na vitendo vya ukatili kukithiri kwa mabinti
zao ni vema serikali ikawa inawachukulia hatua mapema wanaohusika kwani
tangu akamatwe mtuhumiw huyo na kupellekwa kituoni bado hajasomewa shtaka
linalomkabili hivyo kufanya wanaohusika na vitendo hivyo kuona wako sawa
kwa vile hakuna hatua kali inayochukuliwa mapema dhidi ya matukio hayo

Nae mkuu wa shule hiyo Nkoe Nicolaus  alisema kuwa tukio hilo limemfanya
mwanafunzi huyo aathirike kisaikolojia kwani tangu afanyiwe ukatili huo
ameshindwa kiendelea na masomo yake vizuri hivyo anawashauri wazazi wa
binti huyo kumuhamisha shule hiyo na kumuhamishia nyingine ili kimbadilisha
mawazo ya kifkra.

Kwa upande wake mwenyekiti wa kitongoji cha kitefu tanesco Samweli Matayo
alikiri kutokea kwa tukio hilo katika kitongoji chake na kusema kuwa mara
baada ya taarifa walifanikiwa kumtia hatiani mtuhumiwa aliyetambulika kwa
jina la Wilson  Elias ambae ndie  aliyehusika na ukatili huo  na kumfikisha
katika kituo kidogo cha polisi usa river ili kukabiliana na shutuma hizo.

Kamanda wa  polisi  Charles Mkumbo amethibitisha kukamatwa kwa
mtuhumiwa huyo ambapo limesema
kuwa mtuhumiwa alikamatwa kwa rb namba RB/R/4250/2016  na atafikishwa
mahamani upelelezi ukikamilika.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akisalimiana na Balozi wa Cuba nchini Mhe. Jorge Luis Lopez Tormo alipowasili nyumbani kwa Balozi huyo mapema leo kusaini kitabu cha maombolezo kufuatia kifo cha Rais Msataafu wa Cuba Fidel Castrol, Jijini Dar es Salaam 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akimfariji Balozi wa Cuba nchini Mhe. Jorge Luis Lopez nyumbani kwake Jijini Dar es Salaam kabla ya kusaini kitabu cha maombolezo
Mhe. Waziri Balozi Dkt. Augustine Mahiga akitoa heshima mbele ya picha ya  Rais wa zamani wa Cuba hayati Fidel Castro alipoenda kusaini kitabu cha maombolezo
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akisaini kitabu cha maombolezo 


At the refugee camps pregnant and nursing women as well as children under the age of five receive supplementary nutritious foods which can help in the fight against undernutrition.
Refugees in Tanzania receive a food basket from WFP including maize meal, pulses, salt, vegetable oil and fortified porridge mix.
A father and his children enjoy lunch cooked with food from WFP’s food basket at Nyarugusu Refugee Camp.(PHOTO:
COURTESY OF WFP)


 
Tanzania security officer, (R), screens the arrival refugees from Burundi, at Kigoma port early 2015.(PHOTO; LIBRARY)

Ireland helps maintain critical support to refugees in Tanzania


Mshauri Mwelekezi wa Masuala ya Jinsia kutoka “Women Fund” Profesa Ruth Meena akitoa mada.

 Mshauri Mwelekezi wa Masuala ya Jinsia kutoka “Women Fund” Profesa Ruth Meena (kulia), akiwasilisha mada juu ya jinsi ya kuingiza masuala ya jinsia katika mpango kazi wa taasisi wakati wa kikao kazi cha watumishi kutoka Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa kilicho fanyika leo katika Ukumbi wa ofisi za Bunge jijini Dar es Salaam.
 Mafunzo yakitolewa.
Picha ya pamoja na mkufunzi.

(

No comments:

Post a Comment