Pages

Thursday, December 29, 2016

KATIBU MKUU OFISI YA MAKAMU WA RAIS AKAGUA UJENZI WA MIFUMO YA MAJI TAKA


kt
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Prof. Faustin Kamuzora (kulia) akimsikiliza Diwani wa Kata ya Buguruni Mhe. Adam Fugame (Kushoto)  wakati wa ziara ya kikazi ya kukagua ujenzi wa mfereji wa maji taka katika eneo la Ilala Bungoni, Jijini Dar es Salaam.
kt-1Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala Bw. Palela Msongela (kushoto) akiongea na Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Prof. Faustin Kamuzora mara baada ya kukagua ujenzi unaoendelea katika mfereji wa kupitisha maji taka eneo la Ilala Bungoni
kt-2
Gervas wa Kampuni ya Dezo Civil Contractors Co. Ltd akifanunua jambo kwa Prof Kamuzora, Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, katika eneo la Temeke ambapo Kampuni hiyo imepewa kazi ya kusafisha na kujenga mfumo wa maji taka. Katikati ni Bw. Motongori Chacha, Afisa Mazingira Manispaa ya Temeke.
kt-3
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Prof. Faustin Kamuzora (kushoto) akimsikiliza Bi. Ukende Mkumbo kutoka Taasisi ya Mwalimu Nyerere Kigamboni akifafanua hatua za ujenzi wa ukuta katika eneo lao. Katikati ni mwakilishi kutoka Kampuni ya Dezo Civil Contractors Co. Lt
kt-4
Sehemu ya Ukuta wa Obama/Ocean Road ukarabati ukiendelea
…………
Na Lulu Mussa
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Prof. Faustin Kamuzora ameuagiza ungozi wa Dezo  Civil Constractors Co. Ltd kuhakikisha ujenzi wa Miundombinu ya maji taka katika Manispaa za Ilala na Temeke unakamilika kwa muda uliopangwa na kwa ubora wa hali ya juu kwa kuzingatia makubaliano yaliyopo katika mkataba.

Akikagua ujenzi unaoendelea wa miundombinu hiyo, katika Wilaya ya Ilala eneo la Bungoni, Prof. Kamuzora amemtaka Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala Bw. Palela Msongera kuhakikisha changamoto zinazojitokeza katika ujenzi huo zinatatuliwa mara moja ikiwa ni pamoja na utupaji wa taka maji na taka ngumu katika mfereji huo unaojengwa.
Awali Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala Bw. Palela Msongela alimueleza Katibu Mkuu kuhusu changamoto zinazohusu mazingira hususan uhaba wa miundombinu ya mifumo ya maji taka na ujenzi wa makazi holela unaosababisha udhibiti hafifu wa taka.
Aidha, Prof. Kamuzora amewataka watendaji wa Manispaa ya Ilala kuwaelimisha wananchi juu ya athari zinazoweza kujitokeza kwa kutiririsha maji machafu kuwa ni pamoja na milipuko ya magonjwa hususan kipindupindu na kuhatarisha afya za wakazi hao.
Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Buguruni Bw. Adam Fugame amemhakikishia Prof Kamuzora kuwa ataongea na wananchi katika Kata yake na kusisitiza matumizi sahihi ya sheria ndogondogo za mitaa walizojiwekea ikiwa ni pamoja na kuwatoza faini wananchi wanaokiuka taratibu hizo.
“Nikuhakikishie, kwa kupitia mikutano na vikao na wananchi katika Kata yangu, tutazidi kusisitiza juu ya jambo hili na kuweka sheria kali zaidi kwa watakao kaidi”. Alisisitiza Mhe. Diwani Fugame
Ujenzi huo wa  Ukuta wa (Obama/Ocean Road na Kigamboni) na Miundombinu ya maji taka katika Manispaa za Ilala na Temeke unatekelezwa chini ya Ofisi ya Makamu wa Rais chini ya Mradi wa Kuhimili Mabadiliko ya Tabianchi. Mradi huu unafadhiliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa kuhusu Mazingira (UNEP). Kampuni ya Dezo Civil Contractors ndio inafanya ujenzi huu na unatarajiwa kuzinduliwa hivi karibuni na kazi zinatarajiwa kukamilika mwezi Julai 2017.
(Picha na Habari na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini – Ofisi ya Makamu wa Rais.)

No comments:

Post a Comment