NA JACQUILINE MRISHO - MAELEZO
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imevuka lengo la ukusanyaji wa
kodi wa jumla ya kiasi cha shilingi trilioni 1 sawa na asilimia 95.6
tofauti na lengo lililokuwa limekusudiwa la kukusanya trilioni 1.1 kwa mwezi
Julai 2016.
Kiasi hicho ni sawa na ongezeko la asilimia 15.43 ukilinganisha
na makusanyo ya awali ya mwaka 2015 ambapo mamlaka hiyo ilikusanya jumla ya
kiasi cha shilingi Bilioni 914.
Takwimu hizo zimetolewa na Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa
Mlipa Kodi wa TRA, Richard Kayombo, (pichani), wakati wa mkutano na waandishi wa habari leo
jjijini Dar es Salaam.
“Kwa mwezi Julai mwaka huu makusanyo yameongezeka kwa asilimia
15.43 ukilinganisha na kipindi cha mwezi Julai 2015 ambapo tulikusanya shilingi
Bilioni 914” alisema Kayombo.
Aidha aliongeza kuwa mamlaka imeweka mikakati thabiti ya
kuhakikisha kuwa inafikia au inavuka lengo la Serikali la kukusanya shilingi
trilioni 15.1 kwa mwaka wa fedha 2016/2017 huku mkakati mmoja wapo ukiwa ni
kuhakikisha kuwa walipa kodi wapya wanasajiliwa zaidi.
Bw. Kayombo aliongeza kuwa mkakati mwingine ni kuhuisha taarifa
za walipa kodi kwa kuhakikisha kwamba namba za utambulisho wa mlipa kodi (TIN)
zisizotumika zinafutwa katika mfumo wa TRA.
Pia amefafanua kuwa maandalizi ya kuhuisha taarifa za walipa
kodi yapo katika hatua za mwisho ikiwemo upigaji picha,uchukuaji wa alama za
vidole pamoja na vielelezo muhimu.
TRA inawakumbusha wananchi kuhakikisha wanakagua tiketi/
risiti zao za manunuzi na kuangalia usahihi wa pesa walizolipa na uhalali wa
risiti yenyewe.
CHAMA CHA WAFANYAKAZI COTWU (T) KANDA YA DAR ES SALAAM CHAFANYA MKUTANO WAKE MKUU HOTELI YA VILA JIJINI DAR ES SALAAM LEO
Kaimu Mkurugenzi, Tume ya Usuluhishi na
Uamuzi (CMA), Shanes Nungu (katikati), akihutubia wakati akifungua
mkutano mkuu wa Chama cha Wafanyakazi wa Sekta ya Mawasiliano na
Uchukuzi Tanzania COTWU (T), Kanda ya Dar es Salaam leo asubuhi. Kushoto
ni Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Mussa Mwakalinga na Mwenyekiti wa
chama hicho Kanda ya Dar es Salaam, George Faustine.
Wanawake waliochaguliwa kushika nafasi mbalimbali katika chama hicho wakiwa katika picha ya pamoja.
Wanawake wajumbe wa chama hicho Kanda ya Dar es Salaam wakiwa katika picha ya pamoja kwenye mkutano huo.
Vigogo wa chama hicho wakiteta jambo kabla ya kuanza kwa mkutano huo. Kutoka kulia ni Mwenyekiti
wa chama hicho Kanda ya Dar es Salaam, George Faustine, Katibu wa chama
hicho Kanda ya Dar es Salaam, Elisa Luvigo na Naibu Katibu Mkuu wa
chama hicho Kanda ya Dar es Salaam, Mussa Mwakalinga.
Wajumbe wakiwa kwenye mkutano huo.
Baadhi ya wajumbe wa Chama cha
Wafanyakazi wa Sekta ya Mawasiliano na Uchukuzi Tanzania COTWU (T),
Kanda ya Dar es Salaam wakiimba wimbo wa mshikamano katika mkutano mkuu
wa chama hicho uliofanyika Dar es Salaam leo asubuhi.
Wajumbe wakionesha mshikamano wao wakati wakiimba wimbo maalumu wa mshikamano.
Katibu wa chama hicho Kanda ya Dar es Salaam, Elisa Luvigo akizungumza katika mkutano huo.
Makatibu wa matawi wa chama hicho wakiwa
katika picha ya pamoja na mgeni rasmi, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume
ya Usuluhishi na Uamuzi Tanzania (CMA), Shanes Nungu (wa tatu kushoto).
Mwenyekiti wa chama hicho Kanda ya Dar es Salaam, George Faustine (kulia), akizungumza wakati akimkaribisha mgeni rasmi.(Imeandaliwa na mtandao wa www. habari za jamii.com-simu namba 0712-727062)
Mkuu wa mkoa wa Mwanza, John Mongela (wa
pili kulia, akikagua banda la Benki Kuu, kwenye Maonesho ya Nanenane
yanayofanyika kwenye uwanja wa Nyamuhongolo Jijini Mwanza, kwa mikoa ya
Kanda ya Ziwa.
Na BMG
Mkuu wa mkoa wa
Mwanza, John
Mongela, ameiagiza Mamlaka ya Usimamizi wa Biashara Tan-trade
kukamilisha ramani ya viwanja vya Nyamuhongolo vinavyotumika kwa
maonesho ya Wakulima na Wafugaji Nanenane ili kuanza ujenzi wa majengo
ya kudumu kwenye viwanja hivyo.
Akifungua rasmi
jana maonesho ya Nanenane yanayohusisha mikoa ya Kanda
ya ziwa, Mongela, alisema kukamilika kwa ramani hiyo kutaharakisha
kuanza kwa ujenzi wa mabanda ya kudumu kwenye viwanja hivyo ili
kuwezesha kuendelea kwa shughuli mbalimbali hata maonesho
yatakapomalizika.
Alisema mkoa wa
Mwanza kwa kushirikiana na mikoa mingine ya kanda ya ziwa, umejipanga
kuandaa maonesho ya Nanenane kitaifa ndani ya miaka miwili ijayo, hivyo
ujenzi wa mabanda hayo utachangia kuongeza hamasha ya mikoa hiyo kuwa
mwenyeji.
Aidha mkuu huyo wa
mkoa wa Mwanza ameungana na mwenzake wa mkoa wa Shinyanga, Zainab
Telack, kuwahamasisha wakulima wa mikoa hiyo kufufua kilimo
cha pamba ambacho amesema kitachangia kufufua viwanda mbalimbali na
kuongeza fursa za ajira hasa kwa vijana na hivyo kukuza pato
la familia na taifa kwa ujumla.
Kwa upande wao
baadhi ya washiriki wa maonesho hayo zikiwemo taasisi za serikali na
wajasirimali, wamesema kumekuwa na mwamko mkubwa wa wananchi kutembelea
maonyesho hayo tofauti na maonesho ya miaka iliyopita.
Kwa upande wake
mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya maonesho hayo, Damian Chang’a,
amesema maonesho ya mwaka huu yanashirikisha jumla ya Halmashauri 18
kutoka mikoa ya Mwanza, Geita, Shinyangana na Mara huku mikoa ya Simiyu
na Kagera ikishindwa kushiriki.
Itakumbukwa
kwamba, alieyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhandisi Evarist Ndikilo,
ambaye sasa ni Mkuu wa Mkoa wa Pwani, nae aliwahi kutoa ahadi kama
aliyoitoa Mongela, katika Maonesho ya Nanenane miaka iliyopita.
Mkuu wa mkoa wa Mwanza, John Mongela,
akisaini kitabu cha wageni kwenye banda la Benki kuu, kwenye maoneshp ya
Nanenane Jijini Mwanza.
Mkuu wa mkoa wa Mwanza, John Mongela (kushoto), akifuatilia jambo kwenye maonesho ya Nanenane Jijini Mwanza.
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack (kushoto) akiteta jambo na Mkuu wa mkoa wa Mwanza, John Mongella (kulia).
Viongozi mbalimbali wakiwa kwenye Maonesho ya Nanenane Kanda ya Ziwa.
Burudani ya asili kutoka kikundi cha ngoma za asili Bujora
Mchezo wa nyoka kutoka Bujora
Wapiga picha wakifuatilia wacheza ngoma kutoka Bujora
Taasisi ya Kuzuia na Kutokomeza Ukatili
wa Watoto Majumbani, Foundation Karibu Tanzania pia inatoa elimu kwenye
Maonesho ya Nanenane Jijini Mwanza.
Mgeni
Rasmi katika mahafali ya Shule ya awali ya Brookhouse International
Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Mh. Mhandisi Stella
Manyanya akitoa Hotuba kwa wanafunzi pamoja na wageni waalikwa
Mwalimu wa Taaluma wa Brookhouse International School Omega Kessy akitoa neno la utangulizi wakati wa mahafali hayo.
Mwalimu
Mkuu wa Sunrise Nursery and Primary School Bw. Onesphor Vitalis akitoa
utambulisho kwa wageni waalikwa waliofika katika Mahafali hayo ya shule
ya awali.
Mkurugenzi
Mkuu wa Sunrise Nursery and Primary School Bi. Marry Shirima akitoa
maelezo ya kina juu ya shule hiyo, kumshukuru mgeni rasmi kufika katika
mahafali hayo ya watoto wa shule ya awali pamoja kuwapongeza kwa
kuhitimu
Mgeni Rasmi katika mahafali ya Shule ya awali ya Brookhouse
International School Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na
Ufundi Mh. Mhandisi Stella Manyanya akimpa mmoja wa watoto cheti cha kuhitimu Elimu ya awali
Mh. Mbunge wa Jimbo la Kawe Halima Mdee akiwa katika mahafali hayo
Mgeni
Rasmi katika mahafali ya Shule ya awali ya Brookhouse
International School Naibu Waziri wa Elimu Mh. Mhandisi Stella Manyanya
akiadhimisha siku yake ya Kuzaliwa hapa akimlisha keki Mkurugenzi mkuu
wa Shule hiyo Mary Shirima
Wahitimu wa Shule ya awali wakionesha uwezo wao wa kusoma kwa makini
Wahitimu wa Shule ya awali wakionesha uwezo wao wakitoa Burudani kwa kucheza moja ya ngoma za asili za hapa Tanzania
Watoto wa Shule ya awali ya Brookhouse
International School ambao wanandoto ya kuja kuwa Marubani wakiwa wanaelezea juu ya ndoto zao
Walimu nao hawakuwa nyuma waliendelea na Burudani
Baadhi ya wahitimu wa shule ya awali wakiwa katika sherehe yao
Baadhi ya wanafunzi wanaobaki wakiwa katika mahafali hayo
Wazazi wa watoto wanaosoma shule hiyo pamoja na wageni waalikwa wakiwa katika mahafali ya shule ya awali ya Brookhouse.
Picha na Fredy Njeje wa Blogs za Mikoa
Mkuu
wa wilaya ya Ilala Mh. Sophia Mjema akizungumza kwa unyenyekevu mbele
ya Wazee wa CCM wilaya ya Ilala wakati alipokutana nao ili
kujitambulisha na kufahamiana nao baada ya kuanza kazi kama mkuu wa
wilaya hiyo, Aliwaomba wazee hao kushirikiana naye bega kwa bega na
kumpa ushauri wa kila mara ili aweze kutekeleza majukumbu yake ya
kuwaletea maendeleo wananchi wa wilaya hiyo na kufanikisha mipango ya
Rais Mh. Dk John Pombe Magufuli ili kutekeleza kwa ufanisi ilani ya
uchaguzi ya CCM, Katika picha kushoto ni Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya
Ilala Ndugu Asaa Simba , Mkutano huo ulifanyika kwenye ofisi za CCM
wilaya ya Ilala.
Mwenyekiti
wa CCM Wilaya ya Ilala Ndugu Asaa Simba akimkaribisha mkuu wa wilaya ya
Temeke Mh. Sophia Mjema ili kuongea na wazee wa CCM wilaya ya Ilala.
Mkuu
wa wilaya ya Ilala Mh. Sophia Mjema akimsikiliza Katibu wa CCwilaya ya
Ilala Bw. Kafuge Joel alipokuwa akizungumza mambo kadhaa kabla ya
umkaribisha mwenyekiti wake ili kumkaribisha mkuu wa wilaya.
Baadhi ya wazee wa CCM wilaya ya Ilala wakiwa katika mkutano huo uliowakutanisha na Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mh. Sophia Mjema.
Baadhi ya wazee wa CCM wilaya ya Ilala wakiwa katika mkutano huo uliowakutanisha na Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mh. Sophia Mjema.
NA
KHALFAN SAID NA MWASHIRIKAYA HABARI
BILIONEA
Donald Trump, ambaye anataka kuwa Rais wa Marekani, ameendelea “kupigwa madongo”
kutoka kila kona, kufuatia kauli zake za “kukurupuka” ambazo ni tata na kali.
Akizungumza
kwenye mkutano wa pamoja na Waziri Mkuu wa Singapore Lee Hsien Loong na
waandishi wa habari Ikulu ya White Hosue siku mbili zilizopita, Obama amemualezea
Donald Trump kuwa ana uelewa mdogo kwenye masuala ya msingi ya Ulaya, Mashariki
ya Kati na Asia, na kwamba anasikitika kuwa Tajiri huyo hakujiandaa kuwa Rais.
“Maoni
haya siyo yangu pekee bali pia ni maoni ya Viongozi wengine mashuhuri kama Spika
wa Baraza la Wawakilishi anayetoka chama chake cha Republicans, Paul Ryan na Kiongozi
wa walio wengi wa Baraza la Senet, Mitch McConnell”, Obama alishangazwa na
viongozi hao waandamizi wa Republicans, na kusema, “Swali nafikiri ni wao
kujiuliza, kama kama wamekwishatoa maonyo mara kadhaa tena kwa hisia kali
kwamba semayo Trump si sahihi, sasas ni vipi tena bado mnamkumbatia, hii ina
maana gani kwenye chamachenu kuwa huyu ndiye mpeperusha bendera wenu kwenye
uchaguzi wa Rais wa Marekani.” Alishangazwa Obama.
“Madongo” hayo hayakuishia hapo, Mjumbe wa Baraza la
Congress anayetokachama cha Republicans, Adam Kinzinger, amesema, haoni maana yoyote ya
kumuunga mkono mgombea wa chama chake Donald Trump, ilhali mgombea huyo
anaonyesha tabia za kushangaza ukitazama mlolongo wa matukio wiki hii. “Mimi ni
Mmarekani kabla ya kuwa mwana Republica.” Alisema Kinzinger katika kipindi cha CNN cha Situation Room kinachoendeshwa
na mangazaji wa televisheni hiyo Wolf
Blitzer
Naye Rais wa Ufaransa Fracoise Holande amesema kauli za Trump zinatia kichefuchefu, na kuonya madhara makubwa yataikumba Dunia kama Tajiri huyo atachaguliwa kuwa Rais wa Marekani.
Naye
Mwakilishi wa Baraza la Congres kutoka New York ambaye ni mwanachama wa
Republican,Richard Hanna, yeye amebainisha wazi kuwa kutokana na mlolongo wa
matamshi na visa visivyoeleweka vya mgombea wao Dolald Trump, yeye atampigia
kura mgombea wa chamacha Democrat, Bibi. Hillary Clinton, ameandikakwenye barua
yake iliyokwenda sambamba na mahojiano na mtandao wa Syracuse.com “Chama change
cha Republican kinazidi kupoteza mwelekeo wa uwezo wake wa kuteua wagombea
Urais wanaoweza kuletea chama ushindi, na Trump hafai kukiongoza chama wa Urais
wa Marekani.” Alibainisha Hanna.
Hasira za
Wamarekani, kuhusu Donald Trump, zimeongezeka kufuatia kauli zake kuhusu Rais
wa Russia, Vladimir Putin, na wazazi wa Mwanajeshi Musilamu wa Marekani
aliyeuawa akiwa vitani Kapteni Humayun Khan.
Wakati
hayoyakiendelea mgombea wa Urais wa nchi hiyo kutoka chama cha
Democrat, Bibi Hillary Clinton, yeye amechagua kukaa kimya bila hata
kutia neno kwani upepo sasa unavuma upande wake
Adam Kinzinger
Richard Hanna
Bibi. Hillary Clinton
Fracoise Holande
Seneta, Mitch McConnell
Paul Ryan






























No comments:
Post a Comment