NAIBU WAZIRI WA AFYA ZANZIBAR AWAANDALIA CHAKULA MADAKTARI KUTOKA HISPANIA
Profesa Jose Pinquet kulia
akitambulisha Timu ya Madaktari wanaotoa huduma za Matibabu ya Uti wa
Mgongo na Ubongo katika Hospitali ya Rufaa ya Mnazi mmoja kwa Naibu
Waziri wa Afya Zanzibar Mahmoud Thabit Kombo.
Baadhi ya Madaktari wanaotoa
huduma za Matibabu ya Uti wa Mgongo na Ubongo katika Hospitali ya Rufaa
ya Mnazi mmoja wakipata Cahakula cha Usiku kilichoandaliwa ni Naibu
Waziri wa Afya Zanzibar Mahmoud Thabit Kombo.
Profesa Jose Pinquet akizungumza
mara baada ya Chakula cha usiku kilichoandaliwa kwa ajili yao ambapo pia
alishukuru mashirikiano wanayopewa na Madaktari Wazawa katika hafla
iliyofanyika Hoteli ya Ocean View.
Naibu Waziri wa Afya Zanzibar
Mahmoud Thabit Kombo akizungumza na Madaktari wa kujitolea kutoka
Hispatinia mara baada ya Chakula cha usiku alichowaandalia kwa lengo la
kuwashukuru kutokana na mchango wao mkubwa wanaoutoa katika sekta ya
Afya Zanzibar, hafla hiyo ilifanyika Hoteli ya Ocean View.
Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar
WANAHABARI WASISITIZWA KUFUATA SHERIA ZA HABARI ZIZLIZOPO HUKU TAASISI ZAKIHABARI ZIKIFUATILIA KUPATIKANA SHERIA BORA
Mkuu wa Chuo cha Habari Zanzibar
Dkt. Aboubakar Rajab akitoa hutuba ya ufunguzi kwa niaba ya Katibu Mkuu
wa Wizara ya Habari Utamaduni Utalii na Michezo Zanzibar Ally Mwinyikai
katika Mkutano Mkuu wa Wadau wa Jumuiya ya Waandishi wa Habari Zanzibar
(ZPC) uliofanyika ukumbi wa Hoteli ya Zanzibar Ocean mjini Zanzibar
ambapo alisitiza wanahabari kuzingatia maadili ya kazi zao. Kulia ni
Katibu wa Tume ya Utangazaji Zanzibar Chande Omar na kushoto ni
Mwenyekiti wa ZPC Abdallah Mfaume.
Katibu wa Tume ya Utangazaji Zanzibar Chande akitoa Mada ya umuhimu wa kuzingatia Maadili kwa Wanahabari katika fani yao.
Makamu wa Rais wa Chama cha Siasa
ADA-TADEA akichangia katika Mkutano wa Wadau wa Mkutano wa Wadau wa ZPC
uliofanyika ukumbi wa Hoteli ya Zanzibar Ocean mjini Zanzibar.
Mkulima kutoka kikundi cha
Ushirika cha Bambi Mwaka Saburi akichangia katika Mkutano wa Wadau wa
ZPC uliofanyika ukumbi wa Hoteli ya Zanzibar Ocean mjini Zanzibar ambapo
alishauri Wanahabari kuandika zaidi habari za Vijijini bada ya mijini
pekee.
Katibu wa Jumuiya ya Waandishi wa
Habari Zanzibar (ZPC) Faki Mjaka akisoma maazimio ya Mkutano wa Wadau wa
ZPC uliofanyika ukumbi wa Hoteli ya Zanzibar Ocean mjini Zanzibar.
Baadhi ya Washiriki wa Mkutano wa
Wadau wa Zanzibar Press Club ZPC wakiwa katika Picha ya pamoja na Mgeni
rasmi wa Mkutano huo Dkt. Aboubakar Rajab wakatikati waliokaa huko
Hoteli ya Zanzibar Ocean mjini Zanzibar.
Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar
…………………………………………………………………………………………
Na Maelezo Zanzibar
Wanahabari wametakiwa kuendelea
kutii Sheria zilizopo zinazoongoza mwenendo wa utoaji wa habari nchini,
huku Taasisi za kihabari zikiendelea kufuatilia upatikanaji wa sheria
Bora za habari zinazoendana na wakati uliopo.
Hayo yameelezwa na Katibu wa Tume
ya Utangazaji Zanzibar Chande Omar alipokuwa akiwasilisha Mada katika
Mkutano Mkuu wa Wadau wa Jumuiya ya Waandishi wa Habari Zanzibar ZPC
uliofanyika ukumbi wa Hoteli ya Zanzibar Ocean mjini Zanzibar.
Amesema licha ya kuwepo kwa baadhi
ya Sheria za habari zilizopitwa na wakati, ni vyema Wanahabari
kuziheshimu na kuzitii huku juhudi mbalimbali zikifanywa na Wadau
kuondoa Sheria hizo.
Chande amefahamisha kuwa Taasisi
kama Vile Baraza la Habari Tanzania, Tume ya Utangazaji na Jumuiya ya
Waandishi wa Habari Zanzibar ZPC ni miongoni mwa Taasisi ambazo
zinafanya kazi za kuwepo kwa Sheria zinaendana na wakati kwa maslahi
mapana ya Taifa.
Aidha katika Mkutano huo
uliojumuisha Washiriki kutoka Taasisi mbalimbali za Serikali na Binafsi
maazimio mbalimbali yalipitishwa ikiwemo Wamiliki wa Vyombo vya Habari
na Waaandishi kwa ujumla kuzingatia Weledi katika utekelezaji wa
majukumu yao.
Azimio jingine ni kuhakikisha kuwa
Taasisi kama Vile Baraza la Habari Tanzania, Tume ya Utangazaji na
Jumuiya ya Waandishi wa Habari Zanzibar ZPC zinashiriki kikamilifu
katika kuhamasisha upatikanaji wa Maslahi bora kwa Wanahabari ili
kuwaepusha kupokea Zawadi kutoka Vyanzo vya habari ambazo hupelekea
kukiuka maadili yao.
Aidha wameazimia kujiepusha na Ushabiki wa Kisiasa ili kuepuka upendeleo wa habari wanazojitoa kwa jamii.
Mmoja wa Wachangiaji kutoka
Jumuiya ya Wakulima Mpwapwa amewaomba Waandishi wa habari kuandika pia
habari za watu wa shamba badala ya kuandika habari zinazohusu watu wa
mijini pekee.
Ametoa mfano kwamba katika
uchaguzi Mkuu uliopita habari zilizoandikwa zilihusu Watu wa Mijini
ambapo kwa upande wa Vijijini Waandishi walishindwa kuonekana kwenda
kuchukua habari.
Hata hivyo Washiriki wa Mkutano
huo pia Waliafiki wazo hilo na kuazimia kufanya kazi kizalendo na
kushirikisha makundi yote ya kijamii ikiwemo kuandika habari za Vijijini
ili kuibua Fursa na changamoto zinazowakabili.
Akitoa hutuba ya Ufunguzi Mkuu wa
Chuo cha Habari Zanzibar Dkt. Aboubakar Rajab kwa niaba ya Katibu Mkuu
wa Wizara ya Habari Utamaduni Utalii na Michezo Zanzibar Ally Mwinyikai
alisisitiza wanahabari kuzingatia maadili ya kazi zao ili waheshimike
katika jamii.
Amesema kukosekana kwa Maadili ya Habari hupelekea Migogoro mingi ikiwemo kuzalisha chuki na fitna miongoni mwa jamii husika.
Jumuiya ya Waandishi wa Habari
Zanzibar hufanya Mkutano Mkuu wa Wadau wake kila mwaka na kujadili mada
kulingana na wakati husika ambapo katika Mkutano huo Walijadili umuhimu
wa Waandishi kuzingatia Maadili katika kupatikana uchaguzi huru na
Wahaki.
PICHA ZA KUMBUKUMBU BAADA YA RAIS DKT JOHN POMBE JOSEPH MAGUFULI KUZINDUA BUNGE DODOMA
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana na wabunge muda
mfupi baada ya kuhutubia na kuzindua rasmi Bunge la 11 mjini Dodoma
Jumamosi Novemba 20, 2015
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana na Spika Mstaafu
Mhe Pius Msekwa huku Spika Mstaafu mwingine Mhe Anne Makinda akisubiri
zamu yake muda mfupi baada ya kuhutubia na kuzindua rasmi Bunge la 11
mjini Dodoma Jumamosi Novemba 20, 2015
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana na mmoja wa
wabunge muda mfupi baada ya kuhutubia na kuzindua rasmi Bunge la 11
mjini Dodoma Jumamosi Novemba 20, 201
Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akiwa
katika picha ya pamoja na Marais wastaafu Alhaj Ali Hassan Mwinyi, Dkt
Jakaya Mrisho Kikwete na Mhe. Benjamin William Mkapa muda mfupi baada
ya kuhutubia na kuzindua rasmi Bunge la 11 mjini Dodoma Jumamosi Novemba
20, 2015
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli katika picha ya pamoja na
viongozi wakuu na wabunge muda mfupi baada ya kuhutubia na kuzindua
rasmi Bunge la 11 mjini Dodoma Jumamosi Novemba 20, 2015
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akisikiliza kwa unyenyekevu
mawaidha toka kwa Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Alhaj Ali Hassan Mwinyi
muda mfupi baada ya kuhutubia na kuzindua rasmi Bunge la 11 mjini Dodoma
Jumamosi Novemba 20, 2015
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akiwa na Rais wa Zanzibar Dkt
Ali Mohamed Shein, Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Alhaj Ali Hassan
Mwinyi, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi na Spika
wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mhe Pandu Ameir Kificho muda mfupi
baada ya kuhutubia na kuzindua rasmi Bunge la 11 mjini Dodoma Jumamosi
Novemba 20, 2015
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli na Waziri Mkuu Mhe Majaliwa
Kassim Majaliwa wakijichanganya na wabunge kwenye mchapalo muda mfupi
baada ya kuhutubia na kuzindua rasmi Bunge la 11 mjini Dodoma Jumamosi
Novemba 20, 2015
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli na Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne
Dkt Jakaya Mrisho Kikwete na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo
Mhe Zitto Kabwe muda mfupi baada ya kuhutubia na kuzindua rasmi Bunge la
11 mjini Dodoma Jumamosi Novemba 20, 2015
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana na Mwenyekiti wa
CCM mkoa wa Mwanza Mhe Anthony Diallo muda mfupi baada ya kuhutubia na
kuzindua rasmi Bunge la 11 mjini Dodoma Jumamosi Novemba 20, 2015
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akiongea na wabunge na wageni
waalikwa kwenye mchapalo muda mfupi baada ya kuhutubia na kuzindua
rasmi Bunge la 11 mjini Dodoma Jumamosi Novemba 20, 2015. Ni hapo
alipoamuru kwamba zaidi ya shilingi milioni 200 zilizochangwa na
wafadhili kwa ajili ya mchapalo huo zitumike kwa kununulia vitanda vya
wagonja katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akimshukuru Spika Job Ndugai
wakati anaondoka baada ya kuhutubia na kuzindua rasmi Bunge la 11 mjini
Dodoma Jumamosi Novemba 20, 2015.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akimshukuru na kumkabidhi cheti
Mkurugenzi Mkuu wa PSPF Bw.Adam Mayingu kwa mchango wao kwenye
mchapalo muda mfupi baada ya kuhutubia na kuzindua rasmi Bunge la 11
mjini Dodoma Jumamosi Novemba 20, 2015.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akimshukuru na kumkabidhi cheti
mwakilishi wa Benki kwa mchango wao kwenye mchapalo muda mfupi baada
ya kuhutubia na kuzindua rasmi Bunge la 11 mjini Dodoma Jumamosi Novemba
20, 2015.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akipozi na badhi ya mabalozi
wa nchi za Kiafrika waliokaribishwa kwenye hafla ya kuhutubia na
kuzindua rasmi Bunge la 11 mjini Dodoma Jumamosi Novemba 20, 2015.
Picha na Muhidin Issa Michuzi wa Ikulu
MABONDIA TAMBA NA MWAKANSOPE KUPIGANA KESHO JUMAPILI MANZESE
| Mabondia Ibrahimu Tamba kushoto
akitunishiana misuli nas Baraka Mwakansope baada ya kupima uzito kwa
ajili ya mpambano wao wa ubingwa utakaofanyika manzese frends corner
siku ya jumapili .
picha na SUPER D BOXING NEWS …………………………………………………….. Na Mwandishi Wetu MABONDIA Ibrahimu Tamba wa Dar es salaam na Baraka Mwakansope wa Mbeya wamepima uzito kwa ajili ya mpambano wao wa ubingwa wa kg 72 utakaofanyika katika ukumbi wa frends corner manzese mpambano uho wa raundi kumi utanza saa kumi za jioni wakisindikizwa na mabondia mbalimbali ambapo bondia Pius Kazaula wa Morogoro atapambana na Chisora Mawe na Vicent Mbilinyi atapambana na Said Tompoo wa Bagamoyo na Julius Kisarawe atapambana na Ramadhani Kumbele mpambano wa ubingwa kg 51 na Mfaume Mfaume atamenyana na Mrisho Adam katika mpambano kg 63 raundi nne Mohamed Kashinde atakabiliana na Twawabu Issa na Iddi Kayumba atamenyana na Manny Issa
Katika mpambano huo siku hiyo kutakuwa na uzwaji wa DVD za
mafunzo ya mchezo wa ngumi kali pamoja na kutambua sheria zake zikiwa
na mabondia wakali kama vile
Floyd Mayweathar,Manny Paquaio, Saul ‘canelo’ alverez ,Mike Tyson,Mohamed Ali,Ferex Trinidad,Miguel Cotto na wengine wengipia kuta kuwa na vifaa vya mchezo vitakaokuwa vikitolewa na Kocha Rajabu Mhamila ‘Super D’ kwa mabondia watakaofanya vizuri siku hiyo na vingine kuuzwa kwa pesa taslimu na kocha huyo kwa ajili ya kuamasisha |
Dk.Ali Mohamed Shein ATEMBELEA MIRADI YA MAENDELEO MJINI UNGUJA
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Zanzibar Dk.Ali
Mohamed Shein akipata maelezo kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi wa mamlaka ya
Mji Mkongwe wa Zanzibar Nd,Mussa Awesu Bakari wakati alipokuwa
akiangalia ramani ya Mradi wa ujenzi wa Ukuta wa Forodhani Mjini Unguja
leo akiwa katika ziara maalum ya kutembelea maendeleo ya Miradi mbali
mbali Mjini,
[Picha na Ikulu.]
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein akimuuliza suala Kaimu
Mkurugenzi wa mamlaka ya Mji Mkongwe wa Zanzibar Nd,Mussa Awesu Bakari
wakati alipokuwa akiangalia Mradi wa ujenzi wa Ukuta wa Forodhani
Mjini Unguja leo akiwa katika ziara maalum ya kutembelea maendeleo ya
Miradi mbali mbali Mjini,
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Zanzibar Dk.Ali
Mohamed Shein (kulia) akipata maelezo ya ramani ya ujenzi wa Mtaro wa
maji ya Mvua katika viwanja wa mnazi mmoja kutoka kwa Mhandisi wa
Manispaa ya Zanzibar Mzee Khamis Juma wakati alipotembelea mradi huo wa
ujenzi unaojengwa na kampuni ya CRJ kutokaChina,
WAZIRI MKUU MAJALIWA KWENYE HAFLA FUPI YA KUZINDUA BUNGE
Waziri Mkuu, Majaliwa Kassim
Majaliwa akizungumza na Mke wa Rais Mstaafu wa Awamu ya Nnne , Mama
Salma Kikwete katika hafla fupi iliyoyofanyika kwenye viwanja vya Bunge
mjiniDodoma baada ya Rais John Magufuli kuzindua Bunge Novemba 2015.
Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Dkt.
Jakaya Mrisho Kikwete na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa Kassim
wakizungumza na baadhi ya wabunge na waalikwa waliohudhuria hafla fupi
iliyofanyika kwenye viwanja vya bunge mjini Dodoma baada ya Rais John
Magufuli kuzindua Bunge Novemba 20, 2015.
Waziri Mkuu, Majaliwa Kassim
Majaliwa akisalimiana na mbunge wa Mufindi, Cosato Chumi katika hafla
fupi ya kuzindua bunge iliyofanyika kwenye viwanja vya Bunge Mjini
Dodoma Novemba 20, 2015. Katkati ni Mbunge wa ROrya Lameck Airo.
Waziri Mkuu, Majaliwa Kassim
Majaliwa akizungumza na Spika wa Bunge Job Ndugai (kushoto) , Mkewe
Mary (wapili kushoto) na Katibu wa Bunge Dkt. Thomas Kashilila
(wapili kulia) katika hafla ya kuzindua Bunge iliyofanyika kwenye
viwanja vya Bunge mjini Dodoma Novemba 20, 2015.
(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
HAFLA BAADA YA RAIS KULIHUTUBIA BUNGE MJINI DODOMA JANA
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania,Mhe. Samia Suluhu Hassan, akizungumza jambo na
Sophia Simba kwenye Viwanja vya Bunge mjini Dodoma, wakati wa hafla fupi
ya Coktail (Mchapalo) iliyofayika baada ya Rais Magufuli kulihutubia
Bunge jana jioni Nov 20, 2015.
Waziri Mkuu wa awamu ya Tano, Mhe.
Majaliwa Kassim Majaliwa, akizungumza jambo na Rais staafu wa awamu ya
sita wa Zanzibar, Aman Abeid Karume, wakati wa hafla fupi ya Coktail
(Mchapalo) iliyofayika baada ya Rais Magufuli kulihutubia Bunge jana
jioni Nov 20, 2015 kwenye Viwanja vya Bunge mjini Dodoma.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, akisalimiana na baadhi ya
Viongozi wakati wa hafla fupi ya Coktail (Mchapalo) iliyofayika baada ya
Rais Magufuli kulihutubia Bunge jana jioni Nov 20, 2015 kwenye Viwanja
vya Bunge mjini Dodoma.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, akizungumza jambo na Waziri
Mkuu mstaafu, Joseph Warioba wakati wa hafla fupi ya Coktail (Mchapalo)
iliyofayika baada ya Rais Magufuli kulihutubia Bunge jana jioni Nov 20,
2015 kwenye Viwanja vya Bunge mjini Dodoma.
Rais Magufuli (katikati)
akizungumza jambo na Rais wa Zanzibar, Mohamed Ali Shein (kushoto) na
Rais Mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi, wakati wa hafla fupi
ya Coktail (Mchapalo) iliyofayika baada ya Rais Magufuli kulihutubia
Bunge jana jioni Nov 20, 2015 kwenye Viwanja vya Bunge mjini Dodoma.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, akizungumza jambo na Mbunge
wa Shinyanga mjini, Stephen Masele, wakati wa hafla fupi ya Coktail
(Mchapalo) iliyofayika baada ya Rais Magufuli kulihutubia Bunge jana
jioni Nov 20, 2015 kwenye Viwanja vya Bunge mjini Dodoma.
Makamu wa Rais Mstaafu wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza jambo
na baadhi ya viongozi wakati wa hafla fupi ya Coktail (Mchapalo)
iliyofayika baada ya Rais Magufuli kulihutubia Bunge jana jioni Nov 20,
2015 kwenye Viwanja vya Bunge mjini Dodoma.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, akizungumza jambo na mmoja
kati ya wageni waalikwa wa Kimataifa, wakati wa hafla fupi ya Coktail
(Mchapalo) iliyofayika baada ya Rais Magufuli kulihutubia Bunge jana
jioni Nov 20, 2015 kwenye Viwanja vya Bunge mjini Dodoma.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, akizungumza jambo na Vijana
wa UVCCM, wakati wa hafla fupi ya Coktail (Mchapalo) iliyofayika baada
ya Rais Magufuli kulihutubia Bunge jana jioni Nov 20, 2015 kwenye
Viwanja vya Bunge mjini Dodoma.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, akizungumza jambo na Mkuu wa
Mkoa wa Dodoma, Chiku Gallawa, Spika wa Bunge, Job Ndugai na Katibu
wake, baada ya hafla fupi ya Coktail (Mchapalo) iliyofayika baada ya
Rais Magufuli kulihutubia Bunge jana jioni Nov 20, 2015 kwenye Viwanja
vya Bunge mjini Dodoma.
Picha na OMR
No comments:
Post a Comment