Pages

Friday, May 1, 2015

UCHAGUZI CCM 2015: Mwigulu Lameck Nchemba Mbunge wa Jimbo la Iramba Magharibi

Mbunge wa Jimbo la Iramba Magharibi, Mwigulu Lameck Nchemba  

 

Historia yake
Mwigulu Lameck Nchemba alizaliwa Januari 7, 1975 mkoani Singida, hivyo alifikisha miaka 40 Januari 7, mwaka huu. Kwa sasa yeye ni Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) upande wa Tanzania Bara na ni Naibu Waziri wa Fedha.
Mwigulu alianza masomo yake katika Shule ya Msingi Makunda wilayani Iramba, Singida mwaka 1987 na kuhitimu mwaka 1993. Alijiunga na Shule ya Sekondari Ilboru kwa masomo ya kidato cha I – IV mwaka 1987 – 1993 kisha akafaulu na kuanza kidato cha V na VI Mazengo Sekondari, Dodoma.
Baada ya kukamilisha masomo yake ya kidato cha sita, Mwigulu alichaguliwa kujiunga Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) akisomea masuala ya Uchumi. Alihitimu Shahada ya Kwanza ya Uchumi mwaka 2004 na kupata daraja la kwanza, akaunganisha kusomea Shahada ya Uzamili ya Uchumi ambayo aliikamilisha mwaka 2006.
Baada ya kukamilisha masomo yake, Mwigulu alijiunga na utumishi wa umma katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT), kitengo cha sera za uchumi, akiwa mchumi daraja la I na wakati huohuo akiendelea na harakati za siasa ndani ya CCM.
Nyota yake kisiasa ilianza kung’ara mwaka 2001 alipochaguliwa kuwa mjumbe wa vijana wa Wilaya ya Iramba, mwaka 2008 akawa mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (Nec) na mwaka huohuo, akachaguliwa kuwa Mjumbe wa Mkutano Mkuu kupitia Umoja wa Vijana (UVCCM). Mwigulu ameoa na ana watoto.
Mbio za ubunge
Mwigulu anatoka katika familia ya kawaida ya wazazi wasio na uwezo sana. Yeye mwenyewe anasema kama isingelikuwa “sera ya kutoa mikopo kwa wanafunzi,” basi asingelisoma. Pamoja na umasikini wa familia yake, yeye alikuwa na ndoto kubwa, alihitaji kuwa mwakilishi wa wananchi wa jimbo alilozaliwa ili atumie elimu na uzoefu wake kuwasaidia wananchi.
Mwaka 2010, Mwigulu aliacha kazi nzuri pale BoT akajitosa kwenye kinyang’anyiro cha kuusaka ubunge wa Jimbo la Iramba Magharibi. Alitumia vizuri udhaifu wa Mbunge wa Iramba Magharibi wakati huo, Juma Hassan Kilimba, akaomba ridhaa kwa chama chake na kufikia hatua ya kura za maoni ambako alimshinda Kilimba kwa kura chache na kufanikiwa kuteuliwa na CCM kuwania nafasi hiyo.
Katika uchaguzi wa jumla, nguvu ya Mwigulu iliamsha uimara wa CCM akapata asilimia 87.6 dhidi ya asilimia 9.4 za vyama vyote vya upinzani, akawa Mbunge wa Jimbo la Iramba.
Mwigulu aliendelea na safari yake ya utumishi kwa wana Iramba Magharibi na ilipofika Aprili 2011, Katibu Mkuu wa CCM wa wakati huo, Yussuf Makamba na sekretarieti nzima walipojiuzulu ili kutekeleza ile dhana ya “kujivua gamba,” chama hicho kilimteua Mwigulu kushikilia wadhifa wa Katibu wa Uchumi na Fedha chini ya Katibu Mkuu mpya, Wilson Mkama.
Katika uchaguzi mkuu wa viongozi wa CCM Novemba 2012, Mkama alipumzishwa katika majukumu yake na CCM ilijiunda upya, sekretarieti ikiwekwa chini ya Katibu Mkuu, Abdulrahman Kinana. Mwigulu alipanda kisiasa na kuwa Naibu Katibu Mkuu Bara.
1 | 2 | 3 | 4 | 5 | 6 | 7 Next Page»

No comments:

Post a Comment