Pages

Friday, May 1, 2015

UCHAGUZI CCM 2015: Dk Hussein Mwinyi, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

 
Na Julius Mtatiro
Kwa ufupi
Dk Mwinyi alianza safari yake ya elimu ya Msingi jijini Dar es Salaam kati ya mwaka 1972 – 1976, Shule ya Msingi Oysterbay. Kati ya mwaka 1984–1985 wazazi wake walimhamishia Misri na akasoma katika Shule ya Msingi “Manor House Junior” ambako alihitimu elimu ya msingi. Shule hii ilikuwa na hadhi ya “Middle School za Tanzania” kwa wakati huo. Mwinyi alipelekwa Misri kwa sababu baba yake, Ali Hassan Mwinyi, alikuwa balozi wa Tanzania nchini Misri wakati huo.


Historia yake
Dk Hussein Mwinyi alizaliwa Desemba 23, 1966 huko Unguja, Zanzibar (Desemba mwaka huu atatimiza miaka 49). Dk Mwinyi ni mtoto wa Mzee Ali Hassan Mwinyi (Rais wa Awamu ya Pili wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania) na mama Sitti Mwinyi. Kwa sasa Dk Mwinyi ni Mbunge wa Kwahani Zanzibar na ni Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa katika Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Dk Mwinyi alianza safari yake ya elimu ya Msingi jijini Dar es Salaam kati ya mwaka 1972 – 1976, Shule ya Msingi Oysterbay. Kati ya mwaka 1984–1985 wazazi wake walimhamishia Misri na akasoma katika Shule ya Msingi “Manor House Junior” ambako alihitimu elimu ya msingi. Shule hii ilikuwa na hadhi ya “Middle School za Tanzania” kwa wakati huo. Mwinyi alipelekwa Misri kwa sababu baba yake, Ali Hassan Mwinyi, alikuwa balozi wa Tanzania nchini Misri wakati huo.
Aliporejea Tanzania, alipelekwa Shule ya Sekondari Azania na kuendelea na masomo ya kidato cha I – IV mwaka 1982 – 1984. Alipohitimu kidato cha nne alipelekwa Shule ya Sekondari Tambaza kusoma kidato cha tano peke yake mwaka 1984 -1985.
Dk Mwinyi tangu zamani ni mtu wa kupenda kusaidia watu, aliomba na kuchaguliwa kusomea utabibu wa binadamu. Alianza masomo ya udaktari nchini Uturuki mwaka 1985 kwenye Shule ya Utabibu ya Chuo Kikuu cha Marmara na kuhitimu Shahada ya Utabibu wa Binadamu mwaka 1992.
Kwa sababu hakumaliza kidato cha VI, alipokuwa huko ughaibuni alipitia masomo ya mwaka mmoja ya kujiandaa na udahili wa Chuo Kikuu “Pre University Studies”. Chuo cha Marmara kinapokea hata wanafunzi wa kidato cha nne kuanza kusomea shahada ya utabibu lakini lazima wapitie mwaka mmoja wa maandalizi kama alivyofanya Mwinyi.
Alipohitimu shahada ya kwanza alirejea Tanzania na kufanya kazi kwa mwaka mmoja katika Hospitali ya Taifa Muhimbili. Mwaka 1993, Mwinyi aliendelea na masomo ya juu ya utabibu kwa kuunganisha, safari hii akipelekwa Uingereza katika Hospitali ya Hammersmith ambako alihitimu shahada ya uzamili ya utabibu mwaka 1994 na kuunganisha shahada ya uzamivu ya udaktari hapohapo Hammersmith na kuhitimu mwaka 1997.
Alirejea nchini kwa mara nyingine na kufanya kazi katika hospitali ya Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Herbert Kairuki (HKMU) kwa miaka miwili hadi mwaka 1999.
Mwaka 2000, Dk Mwinyi alizidisha nguvu yake ndani ya CCM kwa kugombea ujumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC), akashinda na mwaka 2007 aligombea tena NEC na kushinda na tangu wakati uo aliteuliwa kuingia kwenye Kamati Kuu ya CCM hadi leo hii.
Dk Mwinyi amemuoa Mariam Herman na wana watoto wanne; Ibrahim, Jamila, Tariq na Sitti.
Mbio za ubunge
Dk Mwinyi alijitosa kwenye siasa mwaka 1999 akiliwania Jimbo la Mkuranga mkoani Pwani (Bara) na kushinda. Alipokuwa mbunge, Rais Benjamin Mkapa alimteua kuwa Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, alikaa katika wadhifa huo hadi mwaka 2005.
1 | 2 | 3 | 4 Next Page»

No comments:

Post a Comment