Pages

Monday, July 11, 2022

MSAMAHA WA KODI YA ONGEZEKO LA THAMANI (VAT) CHACHU YA MAENDELEO YA UHIFADHI NA UTALII


Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti imeishauri serikali kuondoa kodi ya ongezeko la thamani (VAT) kwa miradi inayotekelezwa na taasisi za uhifadhi ili fedha hiyo iweze kutumika kufanya kazi kubwa zaidi ya kuimarisha uhifadhi na kukuza utalii.


Akizungumza katika majumuisho ya ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti Mwenyekiti wa Kamati Daniel Sillo (MB) alisema,

“Serikali iangalie uwezekano kwa siku zijazo kuondoa kodi ya ongezeko la thamani (VAT) ili kutopunguza fedha za utekelezaji. Tungepata msamaha wa kodi tungefanya kazi kubwa sana na kwa muda mfupi hivyo ni vizuri kuangalia hili kwa taasisi za uhifadhi.”



Wakitoa maoni katika majumuisho hayo baadhi ya wajumbe wa Kamati hiyo walipongeza kazi nzuri na kubwa iliyofanywa na TANAPA katika kusimamia miradi ya Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na Mapambano dhidi ya UVIKO -19.

“Tumeona jinsi ambavyo vitu vinafanyika katika ubora na tunaona nia njema ya kufikia malengo ya nchi. Katika taarifa ya matumizi na ulipaji wa fedha kwa wakandarasi unaona kazi kubwa sana iliyofanyika lakini malipo hajafanyika, hii inamaanisha kwamba TANAPA wameweza kutafuta wakandarasi wenye uwezo.” alisema Mhe. Issa Mtemvu.




No comments:

Post a Comment