Wafanya kazi nchini wametakiwa kuhamasishana na kujiunga katika
mfuko wa hifadhi ya jamii ZSSF ili waweze kujisaidia na kujikwamua na
hali ngumu ya kimaisha pindipo wanapofikia umri wa kustaafu
Wito huo umetolewa na waziri wa katiba na sheria Mhe.Khamis Juma
Mwalimu katika hafla ya ufunguzi wa mkutano wa tano wa wadau wa ZSSF
uliofanyika huko kwenye ukumbi wa Uhuru kariako Mjiniz Zanzibar
Amesema kuwa “wafanyakazi wengi hawana muamko wa kujiunga
katika mfuko jambo ambalo linawafanya kukosa mafao yatakayo wasaidia
wakati wa kustaafu” hivyo kuwashauri wafanya kazi wa ZSSF kutoa elimu kwa wananchi ili waweze kujiunga na mfuko huo wafaidike
Aidha Mh.Khamis amekadhi zawadi zawadi kwa wachangiaji bora wa mfuko mkuu na wa ZVSSS na kwa wafanyakazi bora wa tasisi hio
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa ZSSF Bi Sabra Issa Machano
amewataka wafanya biashara kujiunga na mfuko wa hiyari ambao una mafao
ya muda mfupi na muda mrefu
Kauli mbiu ya mkutano huo wa tano wa washirika wa zssf kwa mwaka huu ni “mikataba ya kazi ni nguzo ya wanachama wa ZSSF”
No comments:
Post a Comment