Meneja wa Usimamizi wa Maduka ya
kubadilishia Fedha za Kigeni Benki Kuu ya Tanzania BoT Bw. Lameck Kakulu
akiwasilisha mada ya mwitikio wa wawekezaji kuwekeza kwenye dhamana za
Serikali katika semina ya waandishi wa habari inayoendelea kwenye tawi
la BoT jijini Arusha.
Bw. Victor Tarimu akiwasilisha mada katika semina hiyo inayoendelea kwenye tawi la BoT jijini Arusha.
Mwanasheria wa Benki Kuu ya Tanzania Amedeus Shayo akiwasilisha mada kuhusu sheria ya Huduma ndogo za fedha katika semina hiyo.
Msemaji wa Wizara ya Fedha Bw. Benny Mwaipaja akichangia mada katika semina hiyo.
Baadhi ya maofisa wa Benki Kuu ya Tanzania wakifuatilia mada zilizokuwa zikiwasilishwa na watoa mada.
Dk. Deogratias Assey Meneja
Udhibiti wa Ustahimilivu wa Sekta ya Fedha na Usimamizi wa Majanga
akiwasilisha mada kuhusu udhibiti na ustahimilivu wa fedha.
Bw Richard Malisa Kaimu
Mkurugenzi wa Bodi ya Bima ya Amana Benki Kuu ya Tanzania BoT
akiwasilisha mada kuhusu kazi za bodi hiyo.
Vick Msima
Meneja Msaidizi Idara ya Uhusiano wa Umma na Itifaki akimkaribisha
Meneja wa Usimamizi wa Usimamizi wa Maduka ya kubadilishia Fedha za
Kigeni Benki Kuu ya Tanzania BoT Bw. Lameck Kakulu ili kutoa mada katika
semina hiyo.
Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Tafiti za Uchumi BoT, Dkt. Suleiman Misango wa pili kutoka kulia na Vick Msima
Meneja Msaidizi Idara ya Uhusiano wa Umma na Itifaki wa kwanza kulia
pamoja na maofisa wa BoT tawi la Arusha wakifuatilia majadiliano katika
semina hiyo.
……………………………………………………
Meneja wa Usimamizi wa Usimamizi
wa Maduka ya kubadilishia Fedha za Kigeni Benki Kuu
ya Tanzania BoT Bw.
Lameck Kakulu amesema kwa kipindi cha mwaka kuanzia juni mpaka Desemba
2019 Benki Kuu imeshuhudia kuongezeka kwa uwekezaji kwenye minada ya
dhamana za serikali.
Amesema kumekuwa na ongezeko la
asilimia 103 ukilinganisha na kiwango ambacho serikali ilipanga kukikopa
katika kipindi hiki cha nusu ya mwaka.
Bw. Lameck Kakulu ameongeza kuwa
hii imeeenda sambamba na kupungua kwa riba hasa za dhamana za serikali
ambapo zimepungua kutoka asilimia 8.5 mpaka 5 kwa kipindi kama hicho
mwaka 2018/19.
Bw. Lameck Nakulu amesema hayo
wakati akizungumza na waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali mara
baada ya kuwasilisha mada ya mwitikio wa wawekezaji kuwekeza kwenye
dhamana za Serikali katika semina ya waandishi wa habari inayoendelea
kwenye tawi la BoT jijini Arusha.
Ameongeza kuwa kwa upande wa
washiriki mabenki yameendelea kuongezeka kwenye kushiriki kutoka
asilimia 67 huku mifuko ya Pensheni ushiriki wao katika minada ukipanda
kutoka asilimia 8 mpaka asiimia 20 na kwa upande wa wekezaji binafsi
mwitikio umepanda kutoka asilimia 2 mpaka 6 hata ambapo hivyo uko chini
BoT ingependa uongezeke zaidi.
“Ongezeko hili linatokana na
jitihada za Benki Kuu na Wizara ya fedha kufanya uhamasishaji na na
kuwapa uelewa wadau wa shughuli za kiuchumi kwamba ukiwekeza kwenye
dhamana za serikali huwezi kupoteza fedha zako ulizowekeza”.
Kipato ni kikubwa kwa sababu
riba zinazotolewa kwenye hizi dhamana za seikali ni kubwa na unao uwezo
wa kuziuza kwenye soko la upili na pia unaweza kuzitumia kama dhamana
katika taasisi zingine za fedha ili kukopa”. Amesema Bw. Lameck Nakulu.
Ameongeza kuwa ili kuongeza
ushiriki wa wawekezaji wadogo BoT imeendelea na jitihada kwa
kushirikiana na CMSA na Wizara ya Fedha kuhakikisha kwamba inaendeleza
Platfom ambayo itasaidia wawekezaji wadogo kushiriki kikamilifu katika
minada ya dhamana za serikali ambayo inaweza kukamilika kukamilika
mwakani.
Wawekezaji wadogo wataweza
kushiriki kwenye minada kwa kutumia simu na kwa kiwango kidogo cha
fedha, kwa sababu kiwango cha sasa cha shilingi 500 bado kinonekana ni
kikubwa na tunadhani hilo litaongeza kwa kiasi kikubwa wawekezaji wadogo
kushiriki katika shughuli za uchumi wa nchi na kuongeza pato la
serikali.
No comments:
Post a Comment