Mkurugenzi wa utawala na
rasilimali watu wizara ya ujenzi Ziana Mlawa (Katikati)akiwataka
wanawake kuchangamukia fursa za ujenzi wa matengenezo ya barabara wakati
wa kufungua mafunzo ya siku 12 yaliyofanyika mkoani Morogoro ambayo ni
mafunzo ya hatua za awali za ukandarasi kwa kutumia teknolojia stahiki
na nguvu kazi .
Washiriki hao wa mafunzo ya
wanawake katika kutekeleza ukandarasi kwa kutumia teknolojia na nguvu
kazi yaliyofanyika chuo cha ujenzi mkoani Morogoro wakitazama na
kufatilia kwa makini ushauri wa Mkurugenzi wa utawala na rasilimali watu
wizara ya ujenzi Ziana Mlawa.
Mratibu wa kitengo cha
ushirikishwaji wa wanawake katika kazi za barabara mhandisi Gradness
Kitaly akitoa taarifa ya mafuzo kwa mgeni rasmi Ziana Mlawa na
changamoto zinazowakabili wanawake katika kujisajiri ili kutekeleza
shughuli za ujenzi na matengenezo ya barabara .
Wanawake kutoka mikoa nane hapa
nchini waliohudhuria mafunzo ya ukandarasi kwa kutumia teknolojia
stahiki na nguvu kazi mkoani Morogoro wakiwa katika picha ya pamoja na
mgeni rasmi Ziana Mlawa (watatu kutoka kulia ) akifatiwa na mkuu wa chuo
cha ujenzi Mkoani Morogoro Mlyapali.
Wanawake waliohudhuria mafunzo ya
ya awali ya ukandarasi kwa kutumia teknolojia stahiki na nguvu kazi
yaliyofanyika mkoani Morogoro wakifatilia kwa makini maelekezo ya mgeni
rasmi ambaye pia ni Mkurugenzi wa utawala na rasilimali watu wizara ya
ujenzi Ziana Mlawa (hayupo kweye picha).
No comments:
Post a Comment