Waziri
Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa (mwenye tai ya mistari), akiangalia "ramani"
ya jinsi gesi asilia inavyovunwa, kuchakatwa, kutunzwa na kusafirishwa
kwa watumiaji, wakati alipotembela banda la Shirika la Manedeleo ya
Petroli nchini (TPDC), kwenye maonesho ya biashara na uwekezaji katika
viwanja vya chou cha ualimu Mtwara Novemba 1, 2019. Kushoto kwa Waziri
Mkuu ni Mkurugenzi Mkuu wa TPDC, Dkt. James Matarajio, wakwanza kulia ni
Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Innocent Bashungwa na wakwanza
kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Gelasius Byakanwa
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Uwekezaji, Angela Kairuki (kushoto) wakipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), James Mataragio (wa tatu kushoto) kuhusu mtandao visama vya gesi vya Songosongo na Mtwara pamoja na mtandao wa usambazaji na matumizi wa gesi hiyo. Alikuwa akikagua Maonesho ya Biashara Mtwara kabla ya kufungua Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa huo, Novemba 1, 2019. Wa nne kushoto ni Waziri wa Biashara na Viwanda, Innocent Bashungwa
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Uwekezaji, Angela Kairuki (kushoto) wakipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), James Mataragio (wa tatu kushoto) kuhusu mtandao visama vya gesi vya Songosongo na Mtwara pamoja na mtandao wa usambazaji na matumizi wa gesi hiyo. Alikuwa akikagua Maonesho ya Biashara Mtwara kabla ya kufungua Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa huo, Novemba 1, 2019. Wa nne kushoto ni Waziri wa Biashara na Viwanda, Innocent Bashungwa
Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akihutubia kongamano la biashara na uwekezaji mkoani Mtwara
Mkurugenzi Mkuu wa TPDC, Dkt. James Matarajio akihutubia kongamano la biashara na uwekezaji mkoani Mtwara
Mkurugenzi Mkuu wa TPDC, Dkt. James Matarajio akihutubia kongamano la biashara na uwekezaji mkoani Mtwara
Mtaalamu
wa Miamba, wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Nchini (TPDC), Lucas
Luhaga (kushoto), akiwapatia maelezo Mkurugenzi wa Taasisi ya Tafiti za
Kiuchumi na Kijamii Nchini (ESRF), Dkt. Tausi Kida (katikati) na
Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP),
Bi.Christine Musisi kuhusu namna gesi asilia inavyozalishwa, kuchakatwa
na kusafirishwa kutoka kwenye chanzo hadi kwa watumiaji wakati wa
maonesho ya Biashara na Uwekezaji kwenye viwanja vya Chuo cha Ualimu .
Mkurugenzi
Mkuu wa TPDC Dkt. James Matarajio (wapili kulia), akizungumza jambo na Kaimu
Mkurugenzi wa Kampuni tanzu ya TPDC ya GASCO Mhandisi Baltazar Mrosso (wapili
kulia), Afisa Mkuu wa Fedha kiwanda cha saruji Dangote Bw.Host Mapondera na
Meneja Mawasiliano na Mahusiano wa TPDC, Bi. Marie Mselemu kwenye banda la TPDC
wakati maonesho ya biashara na uwekezaji kwenye viwanja vya Chuo cha Ualimu
Mtwara
Mkurugenzi
Mkuu wa TPDC Dkt. James Matarajio (kulia), akiteta jambo na Afisa Mkuu wa Fedha
kiwanda cha saruji Dangote kilichoko Mkoani Mtwara Bw.Host Mapondera wakati
afisa huyo alipotembelea banda la TPDC kwenye maonesho ya biashara na uwekezaji
kwenye viwanja vya Chuo cha Ualimu Mtwara
WAZIRI
Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa ametembelea
banda
la Shirika la Maendeleo ya Petroli Nchini (TPDC) kwenye maonesho ya
biashara na uwekezaji mkoani Mtwara yaliyokwenda sambamba na kongamano
lililowaleta pamoja wawekezaji na
uzinduzi wa muongozo wa uwekezaji mkoani humo kwenye viwanja vya chuo
cha
Ualimu Mtwara.
Waziri
Mkuu alipokelewa na Mkurugenzi Mkuu wa TPDC Dkt. James Matarajio ambaye
alimpa maelezo ya shughuli mbalimbali zinazotekelezawa na Shirika hilo ikiwa ni pamoja
na shughuli za maendeleo ya utafiti na utafiti wa mafuta na gesi na uzalishaji,
biashara ya mafuta na gesi na mipango na uwekezaji.
TPDC
inashiriki maonesho hayo ambayo ni sehemu ya kongamano la uwekezaji
mkoani
Mtwara lililokwenda sambamba na uzinduzi wa muongozo wa uwekezaji mkoani
Mtwara
(MIG) ambapo wawekezaji wa ndani na nje walihudhuria na kupata nafasi ya
kusikiliza fursa mbalimbali za uwekezaji zinazopatikana mkoani humo
ambapo TPDC ilitumia fursa hiyo kuwahakikishia wawekezaji kuwa gesi ya
kutosha inapatikana.
Akizungumza
kwenye kongamano hilo, Waziri Mkuu aliwahimiza wawekezaji wa ndani na nje ya
nchi kufika mkoani Mtwara ili kuwekeza katika maeneo mbalimbali kama vile
kilimo, uvuvi, ufugaji, ujenzi wa miundombinu na kubwa zaidi viwanda kwani kuna
gesi ya kutosha inayopatikana mkoani humo.
Miongoni
mwa wateja wakubwa wa TPDC wanaonunua gesi ni pamoja na Shirika la Umeme
Tanzania TANESCO na kiwanda cha sarufi cha Dangote kilichoko Mkoani Mtwara
No comments:
Post a Comment