Naibu
Katibu Mkuu OR-TAMISEMI, Dkt.Dorothy Gwajima, akitoa maelekezo kwa
Halmashuri zingine nchini kwenda kujifunza na kuiga mfano wa Halmashauri
ya Wilaya ya Rorya ilivyofanya vizuri kwenye fedha Bil.1.5 za Ujenzi wa
Hospitali ya Wilaya
Mkurugenzi
wa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya, Charles Chacha, akimuelezea Naibu
Katibu Mkuu jinsi walivyofanikisha ujenzi huo, pembeni yake ni mmoja ya
Wastaafu ambaye wanamtumia kama afisa ugavi kwenye Halmashauri hiyo
akisaidiana na maafisa Ugavi wa Halmashauri kutokana na umahiri wake
katika kazi hiyo.
Moja ya Jengo la Hospitali hiyo kama linavyo onekana ni jengo la Utawala.
Naibu Katibu Mkuu akiwasalimia Wagonjwa katika kituo cha Afya Otegi ambacho nacho alikitembelea.
Mtaalam
Mhandisi aliyeambatana na Msafara wa Naibu Katibu Mkuu, akitoa
maelekezo kwa Wataalam Wahandisi wa Halmashauri wakati wa Ziara hiyo
Mkuu
wa Wilaya ya Rorya Simon Chacha, akimuelezea Naibu Katibu Mkuu juu ya
namna wananvyofanya ujenzi huo wa Hospitali ya Wilaya.
……………………….
Na. Atley Kuni- OR-TAMISEMI, Mara
Halmashauri ya Wilaya ya Rorya imefanya vizuri katika mradi wa ujenzi wa Hospitali ya
Wilaya unaondelea kujengwa hivi sasa, hali hiyo
imepelekea Naibu Katibu Mkuu anayeshughulika afya Dkt. Dorothy Gwajima,
OR-TAMISEMI kutoa pongezi huku akiziagiza Halmashauri zingine kote
nchini kuiga mfano wa Halmashauri hiyo. Siri ya mafanikio ya ujenzi huo
uliofikia zaidi ya asilimia 80 umetokana na umoja, mshikamano na
maelewano baina ya viongozi wa Halmashauri na Wilaya.Na. Atley Kuni- OR-TAMISEMI, Mara
Halmashauri ya Wilaya ya Rorya imefanya vizuri katika mradi wa ujenzi wa Hospitali ya
Akizungumza katika ziara hiyo
Naibu Katibu Mkuu, alisema hatua kubwa iliyofikiwa haina budi kupongezwa
na kila mpenda maendeleo wa nchini, kwani yapo maeneo mengi ya nchi
ambayo yalipata fedha za awamu ya kwanza shilingi bilioni 1.5 kama
ilivyo Halmashauri ya Rorya, lakini mpaka hivi sasa wanabishana wapi
Hospitali ijengwe huku wananchi wakiendelea kukosa huduma.
“Nikiri waziwazi kwakweli nyie
mmekuwa wa mfano sana na hali hii ndio kurejesha fadhili kwa Rais wetu
kipenzi cha watanzania Dkt. John Pombe Magufuli”, alisema Gwajima na
kuongeza “ninatamani wengine wakaijua siri hii ya mafanikio, kwakuwa
kuna Halmashauri huko sehemu zingine tulizopita ni vituko vitupu, pesa
wamepelekewa toka Januari lakini hadi leo wanashindana wapi ijengwe
Hospitali,” alishangazwa Dkt. Gwajima.
Kwa upande wao viongozi na
Wataalam wa Halmashauri hiyo, walisema siri kubwa ni mshikamano na
maelewano baina yao wenyewe lakini pia mawazo kutoka kwa wataalam.
Mkuu wa Wilaya ya Rorya Simoni Chacha, alisema, kikubwa walichokifanya mara baada yakupokea fedha walikaa kwa pamoja na kuweka mikakati ya namna ya ujenzi utakavyo endeshwa na kwakiasi kikubwa waliwashirikisha baadhi ya wataalam wastaafu.
“Sisi Mhe. Naibu Katibu Mkuu, hatukutaka kujifungia ndani wenyewe tuliwahusisha wataalam wastaafu, lakini sisi Kamati ya Ulinzi na Usalama katika maeneo yote tulikubaliana lazima tuwasikilize wataalam kwa ushauri wao na sisi kama wasimamizi hatukupuuza ushauri wao” alisema Chacha.
Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya hiyo Charles Chacha, alisema mara kadhaa Mhandisi na Mganga Mkuu wa Wilaya na wataalam wenzao walipokutana na jambo likawatatiza, basi waliwaomba ushauri na walijadili kwa pamoja namna yakutatua tatizo.
“Mhe. Naibu Katibu Mkuu, kwakuwa hapakuwepo na muongozo wakuteua kamati baada ya mvutano niliamua kufanya maamuzi magumu ikiwapo hili lakuwashirikisha wataalam wastaafu akiwapo Afisa Ugavi wetu ambaye kila siku jukumu alilonalo ni jinsi gani anapokea vifaa na kuvitoa kwenye vitabu vyetu kwa utaratibu na kwakweli amekuwa msaada sana,” alisema Mkurugenzi.
Nao wataalama Wahandisi wanao simamia shughuli za ujenzi walisema, kufikia asilimia zaidi ya 85 ya ujenzi haikuwa kazi ndogo kwani kila mara wamekuwa wakifanya vikao eneo la kazi na kupitia kila kinachofanyika na wakifika mahali wakashindwa kuelewana wanakwenda kwa Mkurugenzi wa Halmashauri na kwa aajili yakupata ushauri alisema Mhandisi wa Halmashauri hiyo.
Mkuu wa Wilaya ya Rorya Simoni Chacha, alisema, kikubwa walichokifanya mara baada yakupokea fedha walikaa kwa pamoja na kuweka mikakati ya namna ya ujenzi utakavyo endeshwa na kwakiasi kikubwa waliwashirikisha baadhi ya wataalam wastaafu.
“Sisi Mhe. Naibu Katibu Mkuu, hatukutaka kujifungia ndani wenyewe tuliwahusisha wataalam wastaafu, lakini sisi Kamati ya Ulinzi na Usalama katika maeneo yote tulikubaliana lazima tuwasikilize wataalam kwa ushauri wao na sisi kama wasimamizi hatukupuuza ushauri wao” alisema Chacha.
Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya hiyo Charles Chacha, alisema mara kadhaa Mhandisi na Mganga Mkuu wa Wilaya na wataalam wenzao walipokutana na jambo likawatatiza, basi waliwaomba ushauri na walijadili kwa pamoja namna yakutatua tatizo.
“Mhe. Naibu Katibu Mkuu, kwakuwa hapakuwepo na muongozo wakuteua kamati baada ya mvutano niliamua kufanya maamuzi magumu ikiwapo hili lakuwashirikisha wataalam wastaafu akiwapo Afisa Ugavi wetu ambaye kila siku jukumu alilonalo ni jinsi gani anapokea vifaa na kuvitoa kwenye vitabu vyetu kwa utaratibu na kwakweli amekuwa msaada sana,” alisema Mkurugenzi.
Nao wataalama Wahandisi wanao simamia shughuli za ujenzi walisema, kufikia asilimia zaidi ya 85 ya ujenzi haikuwa kazi ndogo kwani kila mara wamekuwa wakifanya vikao eneo la kazi na kupitia kila kinachofanyika na wakifika mahali wakashindwa kuelewana wanakwenda kwa Mkurugenzi wa Halmashauri na kwa aajili yakupata ushauri alisema Mhandisi wa Halmashauri hiyo.
Ujenzi wa Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Rorya, umefikia
asilimia zaidi ya 80 kwa majengo yote yaliyo elekezwa na serikali
kujengwa, Majengo hayo ni pamoja na jengo la wagonjwa wa nje asilimia
88, jengo la Maabara asilimia 87, jengo la Mionzi asilimia 87, na jengo
la uzazi asilimia 86. Majengo mengine ni jengo la ufuaji 87 pamoja na
jengo la Utawala asilimia 84, huku wakitazamia kukamilisha asilimia
zilizobakia ndani ya miezi miwili ijayo ili huduma kwa wananchi zianze
kutolewa.
Naibu Katibu Mkuu, yupo kwenye ziara yakukagua shughuli za
Miradi ya Maendeleo hususan sekta ya afya, ambapo katika siku ya kwanza
ametembelea Mradi wa Hospitali ya Wilaya ya Rorya, Kituo cha Afya Otegi,
Hospitali ya Mji wa Tarime , kituo cha Afya Magoma na Kituo cha Afya
Nyamwaga ambacho kilisajiliwa kama zahanati lakini kwa sasa kutokana
uhitaji na ukarabati mkubwa unaoendelea, Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo
ameomba kipewe hadhi ya Hospitali ya Wilaya
No comments:
Post a Comment