Makamu wa Rais wa Shirikisho la Wenye Viwanda Tanzania( CTI) Bw. Shabir Zavery
akizungumza na waandishi wa habari katika semina iliyowashirikisha
wanachama wa Shirikisho la wenye Viwanda Tanzania (CTI) na Wakala wa
Usalama na afya mahala pa kazi (OSHA) iliyofanyika kwenye hoteli ya New
Afrika jijini Dar es salaam.
Makamu wa Rais wa Shirikisho la Wenye Viwanda Tanzania( CTI) Bw. Shabir Zavery kulia pamoja na washiriki wengine wa semina hiyo wakifuatilia mada za semina hiyo.
Meneja wa Wakala wa Afya na
Usalama mahali pa kazi ‘OSHA’ kanda ya Mashariki Jerome Materu akitoa
mada usalama na afya wakati wa semina hiyo iliyofanyika kwenye hoteli ya
New Africa jijini Dar es salaam.
Joyce Mwambungu Mwanasheria Mkuu
wa Wakala wa Afya na Usalama mahali pa kazi ‘OSHA’ akifafanua masuala
mbalimbali ya kisheria wakati alipotoa mada katika semina hiyo.
Bw. Frank Dafa Mtaalam wa Sera za Biashara (CTI) akichangia hoja katika semina hiyo.
Picha mbalimbali zikionesha baadhi ya washiriki wa semina hiyo wakichangia hoja katika semina hiyo.
Makamu
wa Rais wa Shirikisho la Wenye Viwanda Tanzania( CTI) Bw. Shabir
Zavery ameishukuru Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) kwa
kutoa elimu kwa
wanachama wake kuhusu masuala mbalimbali ya usalama na
afya mahali pa kazi.
Bw.
Zavery ameyasema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari katika
semina iliyowakutanisha wanachama wa Shirikisho na Wakala wa Usalama na
Afya Mahali pa Kazi (OSHA) ilyofanyika kwenye hoteli ya New Africa
jijini Dar es Salaam.
Bw. Shabbir Zavery amesema OSHA
inafanya kazi kubwa kuhakikisha wafanyakazi wanapotekeleza majukumu yao
kazini suala la usalama na afya zao linazingatiwa na kutiliwa mkazo ili
kuwe na tija ya kazi viwandani.
Ameongeza kwamba Maofisa wa OSHA
wamekuwa wakifanya kazi nzuri kwa kutoa maelekezo na mafunzo badala ya
kukomoa hii inatufanya wamiliki wa viwanda kufuata na kuzingatia
maelekezo na taratibu zinazotolewa na maofisa kutoka Wakala wa Usalama
na Afya Mahali pa Kazi (OSHA).
Ameongeza kwamba semina hiyo inayotolewa kwa wanachama wa Shirikisho
la Wenye Viwanda Tanzania (CTI) na Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa
kazi OSHA ina lengo la kuwapa uelewa wa kutosha wanachama kuhusu
Taratibu,Kanuni na Sheria za usalama na afya zinazomlinda mfanyakazi ili
kutekeleza majukumu yake kwa tija awapo kazini.
Ameongeza kuwa OSHA imefanya
mageuzi makubwa kwa kuondoa baadhi ya tozo zilizokuwa zikikwamisha
utekelezaji wa baadhi ya majukumu yetu hivyo kusababisha usumbufu kwa
wamiliki wa viwanda tunawashukuru sana Wakala wa Usalama na Afya Mahali
pa kazi (OSHA)kwa hatua hiyo.
Bw. Shabir ameipongeza serikali
ya awamu ya tano chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Yanzania Dkt.
John Pombe Magufuli kwa juhudi zake inazozifanya kuhakikisha Tanzania
inafikia uchumi wa kati wa viwanda ifikapo mwaka 2025.
No comments:
Post a Comment