Pages

Tuesday, October 29, 2019

QNET INAHAMASISHA UTAFUTAJI WA MASOKO UNAOZINGATIA MAADILI KWA KUWAPA MAFUNZO WAWAKILISHI WAKE WA KUJITEGEMEA (IRs) KUPITIA QNETPRO



Meneja Mkuu wa QNET, kanda ya Kusini mwa Jangwa la Sahara ya Afrika, Bwana
Biram Fall.
***********************
QNET, Kampuni ya biashara ya mtandao inayoongoza duniani imesisitizia jitihada zake za
kuhakikisha kwamba wateja wake wote na wawakilishi wake wa kujitegemea (IRs) duniani kote hasa barani Afrika wanahudumiwa vizuri. QNET kupitia programu yake ya mafunzo ya mauzo ya mtandao ujulikanao kama QNETPRO inatoa mafunzo na kurudia kuwafundisha wawakilishi wake wa kujitegemea kwa lengo la kuwapatia weledi zaidi na kuwa na viwango bora vya maadili ya utendaji.
Kwa mujibu wa Meneja Mkuu wa QNET, kanda ya Kusini mwa Jangwa la Sahara ya Afrika, Bwana Biram Fall amesema. “QNET imejidhatiti katika kutengeneza wauzaji wa moja kwa moja wenye weledi zaidi katika sekta hii ya biashara ya mauzo ya moja kwa moja kwa njia ya mtandao. Tuna viwango vya juu vya utaalamu na kupitia QNETPRO, tunatoa elimu inayohitajika katika huduma kwa wateja, masoko na mauzo ya moja kwa moja kwa wawakilishi wetu wa kujitegemea. Tunatumia mbinu kama mafunzo ya ana kwa ana, semina zinazotolewa kwa njia ya mtandao, video, maonyesho na ushauri.”
QNETPRO inawezesha na kufundisha maadili ya msingi ya shauku, kujenga sifa au jina jema, maadili ya utendaji wa kibiashara, uwajibikaji, kufanya kazi kwa bidii, uaminifu, ukweli na kumiliki uwajibikaji.
Bwana Fall amesema. “Tunajitahidi katika kudumisha sifa njema ambazo zinastawi kwa uwajibikaji. Kujenga mauhisano ya kudumu na kuhamasisha kila mmoja afanye mambo sahihi na kudumu katika utamaduni wa uendeshaji wa biashara wenye uwajibikaji.”
Programu ya mafunzo na uthibitishaji ya QNETPRO ni jitihada za QNET za kukuza
ufahamu kwa kiwango cha juu na kuwakumbusha wawakilishi wote wa kujitegemea kuhusu umuhimu wa kujenga tabia ya kufanya biashara ya mauzo ya moja kwa moja kitaalamu wakati wote. Programu hii ina lengo la kufundisha kanuni zilizoko katika sera na taratibu za QNET kuwezesha uelewa bora na kutimiza vigezo.
Aliendelea bwana Fall. “QNET imeahidi kuipatia sekta ya mauzo ya moja kwa moja wawakilishi bora na wenye weledi zaidi katika kila kanda ambako inaendesha biashara zake. Sisi ni waanzilishi na sauti ya sekta ya mauzo ya moja kwa moja katika masoko mengi yanayochipukia na tunachukua jukumu hili kwa umakini mkubwa. Kusudio letu ni kuelimisha, kutaarifu na kufundisha wawakilishi wetu wa kujitegemea waweze kuwa na viwango vya juu katika kufanya biashara. Kama wajasiriamali wanaochipukia, sio tu kwamba wanajenga biashara inayowasaidia kuweza kuwa na uhuru wa kifedha, lakini
kikubwa ni kwamba wanaongoza wimbi kubwa la mabadiliko.”
Alihitimisha kuwa, “Katika QNET tunaamini katika utekelezaji wa yale yote
tunayoyasema. Tunataka uzingatiaji kamili wa kanuni za maadili za utendaji za QNET kama utimizaji wa vigezo vya sera na taratibu zetu. Wakati huu ambapo sekta ya mauzo ya moja kwa moja imekuwa ni kazi ya kitaaluma ya kukimbiliwa katika masoko mengi yanayoibukia, ni muhimu sana kwetu kuweka viwango vya juu. Tunachukulia ukiukaji wa sera na taratibu zetu kwa umakini mkubwa. Tunatekeleza majukumu yetu kwa vitendo kupitia katika mchakato wetu wa ukaguzi na upitiaji wa uadilifu wa mitandao yetu imara. Kwa miaka mingi QNET imesitisha vibali vya wawakilishi (IRs) wengi sana katika zaidi ya nchi 30 kwa kuthibitisha kuwa hawakutimiza vigezo, ukiukaji
wa sera, au utendaji usiozingatia maadili.”
Mwisho, kwa kupitia programu hii, QNET inaelimisha watu kwamba biashara hii ni ya muda mrefu. Ili waweze kujenga biashara ya kudumu na ambayo itawalipa kwa muda mrefu wanapaswa kufanya mambo yao kwa usahihi. Biashara hii haikukusudiwa kuwa ni kampeni ya muda mfupi, ni kuhusu kusisitizia ujumbe wa ustahimilivu kwa kila mmoja anayetaka kufanya biashara hii ya QNET.
QNET haitaki watu wafikirie kwamba biashara yake ni kama mpango wa kujipatia mafanikio haraka haraka au mfumo wa kujitajirisha haraka haraka. QNET inataka watu waone biashara hii kama fursa ya kweli ya kuwa mjasiriamali kwa kufuata utaratibu ule ule wa kufanya kazi kwa bidii na kujitolea na maadili ambayo yanatakiwa ili mtu aweze kujenga aina yeyote ile ya biashara ya kawaida.
Katika mwaka 2019 pekee, timu yetu ya wakufunzi wa QNETPRO wametoa mafunzo kwa zaidi ya IRs 35,000 katika vituo 35 duniani kote. Hii inajumuisha: Hong Kong, Singapore, Dubai, Uturuki, Sudan na Tanzania. Nchi nyingi katika ukanda wa Afrika magharibi (Ghana, Senegali, Ivory Coast, Mali, Burkina Faso, Togo, Cameroun, Guinea na Niger, Sierra Leone) pia wamepatiwa mafunzo ya QNETPRO.

No comments:

Post a Comment