Pages

Friday, July 26, 2019

RAIS DKT. MAGUFULI AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA MRADI WA KUFUA UMEME WA MAJI KATIKA MTO RUFIJI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mkewe Mama Janeth Magufuli, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Waziri wa Nishati wa Misri Dkt. Mohamed Shaker, Waziri wa Nishati Medard Kalemani pamoja na viongozi wengine akisikiliza namna mradi wa Kuzalisha umeme Megawati 2115 katika eneo la mto Rufiji utakavyokuwa ukifanya kazi mara baada ya kukamilika.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Waziri wa Nishati wa Misri Dkt. Mohamed Shaker wakivuta utepe kuashiria uwekaji wa Jiwe la Msingi mradi wa Ujenzi wa Kuzalisha umeme Megawati 2115 katika eneo la mto Rufiji katikati ya Morogoro na Pwani.


 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza Waziri wa Nishati wa Misri Dkt. Mohamed Shaker mara baada ya kuweka Jiwe la Msingi mradi wa Ujenzi wa Kuzalisha umeme Megawati 2115 katika eneo la mto Rufiji katikati ya Morogoro na Pwani.


 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia pamoja na viongozi wengine mara baada ya tukio hilo la uwekaji wa Jiwe la Msingi.




 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mkewe Mama Janeth Magufuli, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Waziri wa Nishati wa Misri Dkt. Mohamed Shaker, Waziri wa Nishati Medard Kalemani pamoja na viongozi wengine akisikiliza namna mradi wa Kuzalisha umeme Megawati 2115 katika eneo la mto Rufiji utakavyokuwa ukifanya kazi mara baada ya kukamilika.


 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia michoro ya ujenzi huo mkubwa wa kufua umeme.


 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi kabla ya kuweka jiwe la msingi mradi wa Kuzalisha umeme Megawati 2115 katika eneo la mto Rufiji.


 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Waziri wa Nishati wa Misri Dkt. Mohamed Shaker wakati wakielekea kwenda kuweka jiwe hilo la msingi.


  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akikata utepe kuashiria uzinduzi wa mitambo itakayotumika katika mradi huo mkubwa wa kufua umeme.




 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia eneo la bonde katika mto Rufiji mara baada ya kuweka jiwe la msingi la mradi huo wa umeme.


 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwasalimia wananchi mara baada ya kuwasili katika eneo la Mradi.


Eneo la mto Rufiji ambalo litatumika katika ujenzi huo wa kufua umeme kama linavyoonekana. PICHA NA IKULURAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, Julai 26, 2019 ameweka jiwe la msingi la ujenzi wa mradi wa ...kuzalisha umeme wa Megawati 2115 katika mto rufiji mkoani Pwani ambao utakamilika Juni 2022.
Sherehe za uwekaji jiwe hilo la msingi zimefanyika kandokando ya eneo ambalo bwawa litajengwa na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa, Naibu Spika wa Bunge, Mhe. Dkt. Tulia Ackson, Waziri wa Nishati wa Misri Mhe.Dkt. Mohammed Shaker,  Waziri wa Nishati Dkt. Medard Kalemani, Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Dkt. Hamisi Kigwangallah, Manaibu Waziri, viongozi wa vyombo vya ulinzi na usalama na viongoze wengine wa ngazi mbalimbali.

Ujenzi wa bwawa hilo utagharimu kiasi cha Shilingi za Kitanzania Trilioni 6.5 na litakuwa bwawa kubwa kabisa katika ukanda wa Afrika Mashariki na la nne kwa ukubwa barani Afrika.

Katika hotuba yake, Mhe. Rais alisema kwa kutambua mapenzi na maono ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, amependekeza bwawa hilo lipewe jina la Bwawa la Nyerere.

Rais Magufuli ameipongeza Wizara ya Nishati kwa utekelezaji wa mradi huo na ameeleza kwamba Serikali imechukua hatua ya ujenzi wa bwawa hilo ili kuongeza uzalishaji wa nishati ya umeme kutoka Megawati 1,601 zinazozalishwa hivi sasa hadi kufikia Megawati 10,000 ifikapo mwaka 2025.

Aidha Mhe. Rais amewataka wakandarasi (Arab Contractors na Elsewedy) kutoka nchini Misri kabla ya Juni 2022 hasa ikizingatiwa hakuna tatizo la fedha ili Watanzania waanze kunufaika mapema.

No comments:

Post a Comment