Baadhi ya Majengo mapya ya Kituo cha Afya Mnazi Mmoja
Waziri Jafo akiwa na baadhi ya viongozi na wananchi katika kituo cha Afya Mnazi mmoja
………………………..
Wananchi wa eneo la Mnazi Mmoja
Katika Wilaya ya Lindi wameishukuru Sana Serikali ya awamu ya tano kwa
kuwajengea kituo cha afya cha Kisasa Sana katika eneo lao. Shukran hizo
zilitolewa leo April 2 wakati wa Ziara ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais
TAMISEMI wilayani humo alipokuwa akifanya ukaguzi wa miradi ya maendeleo
inayo simamiwa na TAMISEMI.
ujenzi wa Kituo cha Afya Mnazi
mmoja kimeleta ukombozi kwa wananchi wa eneo hilo kwani
kwa muda mrefu
wamekuwa wakitaabika sana kufuata huduma bora za afya katika hospitali
ya Mkoa Lindi ambayo ipo mbali kutokea eneo hilo.
Katika ziara hiyo waziri Jafo
amewapongeza viongozi na wananchi wa wilaya ya Lindi kwa usimamizi mzuri
wa mradi huo. Hata hivyo Jafo amewasisitiza wananchi kutunza
miundombinu iliyojengwa.
No comments:
Post a Comment