Pages

Wednesday, October 31, 2018

MIKAKATI YA KUTOKOMEZA MDUDU MBUNG’O DHIDI YA MIFUGO


 Mdudu mbung’o

Firmi Banzi Mtaalamu wa masuala ya Nyuklia.Mdudu mbung’o
Dkt. Imna malele-mtaalamu wa magonjwa ya mifugo akizungumza na wanahabari baada ya ufunguzi wa mafunzo
NA VERO IGNATUS-ARUSHA.
JUMLA ya nchi 10 duniani zimekutana jiji Arusha kwa lengo la kujifunza mbinu za kisasa na matumizi ya tecknolojia,katika kudhibiti magonjwa ya mifugo yanayo ambukizwa na mdudu mbung’o katika maeneo ya wafugaji na hifadhini.
Katika mazungumzo na wanahabari Mtaalam wa magonjwa ya mifugo Dkt Imna Malele amesema kuwa mdudu mbung’o amekuwa changamoto kubwa kwa wafugaji wengi na baadhi ya maeneo ya hifadhi hivyo ni wakati muafaka kutumia mbinu za kisasa katika kuangamiza mdudu huyo ambae amekuwa changamoto katika maeneo ya wafugaji na hifadhini.
Amesema kwa nchi ya Tanzania tatizo la kuwepo kwa magojwa yatokanayo na mdudu mbung’o bado ni kubwa,na limekuwa likipunguza nguvu kazi katika uzalishaji kupitia mazao yatokanayo na mifugo suala ambalo humnyima amani mfugaji endapo mifugo itaathirika na magojwa yatokanayo na mbung’o.
Mara baada ya kufungua mafunzo hayo maalum kwa niaba ya mkurugenzi mkuu wa tume ya nguvu za atomic nchini Prof Lazaro Busagala, Dkt. Firmi Banzi ambae pia ni mtaalamu wa masuala ya teknolojia na masuala ya nguvu za nyuklia  akatumia fursa hiyo kueleza matumizi ya teknolojia ya nyuklia nchini katika kupambana na mbung’o bila ya kuharibu mazingira ambapo amesema njia hiyo imekuwa na manufaa makubwa katika nchi mbalimbali duniani.
Nao baadhi ya washiriki akiwemo Deusdedit Malulu wakaeleza matarajio yao katika masuala ya utafiti dhidi ya kuangamiza mdudu aina ya mbung’o kwa mazingira salama ya utalii ambapo wamesema njia hiyo itasaidia kwa kiasi kikubwa katika jamii za wafugaji na maeneo ya hifadhini.
Mdudu mbung’o hueneza uonjwa wa malale ambao ni hatari kwa maisha ya binadamu ambapo pia njia ya matumizi ya nyuklia imetajwa kuwa ni miongoni mwa njia salama katika mapambano dhidi ya mbung’o ambapo njia hiyo imekuwa mkombozi zaidi katika visiwa vya zanzibar na maeneo mbalimbali nchini.

No comments:

Post a Comment