Pages

Monday, March 26, 2018

WANANCHI BUKOBA WADAI VITAMBULISHO VYA TAIFA VITAWASAIDIA KUONDOKANA KERO ZA MIPAKANI


IMG_8491
Wakazi wa kata ya Nshambia wakiwa katika foleni ya kusubiri kupigwa picha wakati wa zoezi la Usajili Vitambulisho vya Taifa; pamoja na mvua kubwa zilizokuwa zikiendelea kunyesha.
IMG_8492
Pichani ni Afisa uhamiaji Bw. Issa Juma akifanya mahojiano na Bi. Kemilembe Ishengoma wakati wa zoezi la uandikishaji Vitambulishi vya Taifa kwa wakazi wa Manispaa ya Bukoba Mjini.
IMG_8515
Pichani ni Bi. Hadija Abeid, Afisa Usajili Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa akitoa maelekezo kwa wananchi wa kata ya Nshambya waliojitokeza kusajiliwa wakati wa zoezi la uandikishaji Vitambulisho vya Taifa.
IMG_8523
Pichani ni Bw. Daniel Michael  Afisa Usajil akimsaidia Bi. Monica Kagasheki kukamilisha zoezi la uchukuaji alama za vidole wakati wa Usajili wa Vitambulisho vya Taifa.
IMG_8534
Baadhi ya wakazi wa kata ya Nshambya wakisubiri kukamilisha usajili wa Vitambulisho vya Taifa wakati zoezi hilo likifanyika katika kituo cha Chuo kikuu Huria kata ya Nshambya Manispaa ya Bukoba.
…………………
Wananchi mkoani Kagera wameeleza kero kubwa wanayoipata, ukiwemo usumbufu mkubwa wanapokuwa kwenye shughuli zao nje ya mkoa hasa maeneo ya mpakani kwa kukosa Vitambulisho vya Uraia.
Hayo wameeleza wakiwa kwenye vituo vya Usajili unaoendelea mkoani humo;  ukihusisha
Wilaya zote za Mkoa Kagera.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti wananchi hao wamedai kuwa lengo la kujitokeza kwa wingi ni kutokana na umuhimu wa Vitambulisho hivi; kwani wengi wao hupata shida pindi wanapotoka nje ya mkoa wao ikizingatiwa kuwa mkoa huo upo pembezoni kabisa mwa nchi ya Tanzania.
Wakazi wa kata ya Nshambya Wilaya ya Bukoba ni miongoni mwa wananchi waliojitokeza licha ya changamoto ya mvua kubwa zinazoendelea kunyesha.
Akizungumzia zoezi hilo; Kaimu mtendaji kata ya Nshambya Bi Fatma Christian Majengo, amesema wananchi waliojitokeza ni wengi na kuwataka wananchi wa eneo hilo kutokubali kuuziwa fomu za Vitambulisho vya Taifa, kwani fomu hizo zinatolewa.
Kwasasa zoezi hilo limekuwa linaendeshwa kwa Kata ili kutoa fursa kwa kila mwananchi kupata fursa ya kusajiliwa; hivyo wananchi wametakiwa kuwa makini kufuatilia ratiba ya lini zoezi litafika kwenye Kata zao.

No comments:

Post a Comment