JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO
Wizara ya Afya, Maendeleo ya
Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imepata kibali cha mpango wa Ajira ya
dharura kwa wataalamu wa “fani za Tabibu na Wauguzi. Mpango huu
utaendeshwa chini ya mradi, kwa ufadhili wa fedha za Mfuko wa CDC, Award
No. 5U2GGH001062-03 kwa muda wa miaka miwili.
Mradi utaajiri watumishi 192 ambao
watapangiwa kufanyakazi kwenye halmashauri za wilaya 40 zenye uhaba
mkubwa wa watumishi wa kutoa huduma za afya hasa kwa waathirika wenye
virusi vya UKIMWI. Watumishi hawa watalipwa mishahara na stahiki
nyingine kwa kufuata taratibu na kanuni za serikali. Watumishi
wanaotakiwa ni Tabibu Wasaidizi (Clinical Assistant) 95 wenye ngazi ya
Astashahada (Certificate in Clinical Medicine) na Wauguzi (Enrolled
Nurses) 97 wenye ngazi ya Astashahada (Certificate in Nursing and
midwifery).
Wizara inakaribisha maombi ya kazi
kutoka kwa watanzania wenye sifa zilizotajwa hapo juu, wawe na cheti
cha kumaliza kidato cha nne pamoja na cheti cha taaluma aliyosomea
kutoka kwenye chuo kinachotambuliwa na serikali. Barua ya maombi ioneshe
wilaya ambayo mtumishi atapenda apangiwe kufanyakazi kati ya wilaya
zilizopendekezwa hapo chini. Mwisho wa kupokea maombi ni tarehe
14/12/2016.
Maombi yote yatumwe kwa:-
Katibu Mkuu
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,
6 Samoral Machel Avenue,
S.L.P 9083,
11478, Dar es Salaam.
Tanzania
05/12/2016
Orodha ya Halmashauri za Wilaya na idadi Watumishi waliopendekezwa.
Na. | Mkoa | Halmashauri (Wilaya) | Tabibu Wasaidizi | Wauguzi Wasaidizi | Jumla |
1 | Arusha | 1. Arusha CC | 3 | 3 | 6 |
2 | Dar es Salaam | 2. Ilala MC | 3 | 3 | 6 |
3. Kinondoni MC | 3 | 3 | 6 | ||
4. Temeke MC | 3 | 3 | 6 | ||
3 | Dodoma | 5. Dodoma MC | 2 | 3 | 5 |
4 | Geita | 6. Geita DC | 2 | 2 | 4 |
5 | Iringa | 7. Mufindi DC | 3 | 3 | 6 |
8. Iringa MC | 2 | 2 | 4 | ||
6 | Kagera | 9. Bukoba DC | 3 | 3 | 6 |
10. Muleba DC | 2 | 2 | 4 | ||
7 | Kigoma | 11. Kigoma Ujiji MC | 2 | 3 | 5 |
8 | Kilimanjaro | 12. Moshi DC | 3 | 3 | 6 |
9 | Lindi | 13. Lindi MC | 2 | 2 | 4 |
10 | Mara | 14. Musoma MC | 2 | 2 | 4 |
15. Rorya DC | 2 | 2 | 4 | ||
11 | Mbeya | 16. Chunya DC | 2 | 2 | 4 |
17. Kyela DC | 3 | 3 | 6 | ||
18. Mbarali DC | 2 | 2 | 4 | ||
19. Mbeya CC | 3 | 3 | 6 | ||
20. Mbeya DC | 3 | 3 | 6 | ||
21. Mbozi DC | 2 | 2 | 4 | ||
22. Rungwe DC | 2 | 2 | 4 | ||
12 | Morogoro | 23. Morogoro MC | 3 | 3 | 6 |
13 | Mwanza | 24. Nyamagana MC | 3 | 3 | 6 |
25. Sengerema DC | 2 | 2 | 4 | ||
14 | Njombe | 26. Njombe TC | 2 | 2 | 4 |
27. Wanging’ombe DC | 2 | 2 | 4 | ||
15 | Rukwa | 28. Sumbawanga DC | 2 | 2 | 4 |
29. Sumbawanga MC | 2 | 2 | 4 | ||
16 | Ruvuma | 30. Mbinga DC | 2 | 2 | 4 |
31. Songea MC | 2 | 2 | 4 | ||
17 | Shinyanga | 32. Kahama DC | 2 | 2 | 4 |
33. Kahama TC | 3 | 3 | 6 | ||
34. Shinyanga MC | 2 | 2 | 4 | ||
18 | Tabora | 35. Igunga DC | 2 | 2 | 4 |
36. Nzega DC | 2 | 2 | 4 | ||
37. Tabora MC | 3 | 3 | 6 | ||
19 | Tanga | 38. Korogwe TC | 2 | 2 | 4 |
39. Muheza DC | 2 | 2 | 4 | ||
40. Tanga CC | 3 | 3 | 6 | ||
Jumla | 95 | 97 | 192 |
No comments:
Post a Comment