Pages

Tuesday, December 6, 2016

TANGAZO LA KAZI MRADI WA AJlRA YA DHARURA KATlKA SEKTA YA AFYA


uhuruggggggggggggggggg
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imepata kibali cha mpango wa Ajira ya dharura kwa wataalamu wa “fani za Tabibu na Wauguzi. Mpango huu utaendeshwa chini ya mradi, kwa ufadhili wa fedha za Mfuko wa CDC, Award No. 5U2GGH001062-03 kwa muda wa miaka miwili.

Mradi utaajiri watumishi 192 ambao watapangiwa kufanyakazi kwenye halmashauri za wilaya 40 zenye uhaba mkubwa wa watumishi wa kutoa huduma za afya hasa kwa waathirika wenye virusi vya UKIMWI. Watumishi hawa watalipwa mishahara na stahiki nyingine kwa kufuata taratibu na kanuni za serikali. Watumishi wanaotakiwa ni Tabibu Wasaidizi (Clinical Assistant) 95 wenye ngazi ya Astashahada (Certificate in Clinical Medicine) na Wauguzi (Enrolled Nurses) 97 wenye ngazi ya Astashahada (Certificate in Nursing and midwifery).
Wizara inakaribisha maombi ya kazi kutoka kwa watanzania wenye sifa zilizotajwa hapo juu, wawe na cheti cha kumaliza kidato cha nne pamoja na cheti cha taaluma aliyosomea kutoka kwenye chuo kinachotambuliwa na serikali. Barua ya maombi ioneshe wilaya ambayo mtumishi atapenda apangiwe kufanyakazi kati ya wilaya zilizopendekezwa hapo chini. Mwisho wa kupokea maombi ni tarehe 14/12/2016.
Maombi yote yatumwe kwa:-

Katibu Mkuu
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,
6 Samoral Machel Avenue,
S.L.P 9083,
11478, Dar es Salaam.
Tanzania
05/12/2016

Orodha ya Halmashauri za Wilaya na idadi Watumishi waliopendekezwa.
Na. Mkoa Halmashauri  (Wilaya) Tabibu Wasaidizi Wauguzi Wasaidizi Jumla
1 Arusha 1. Arusha CC 3 3 6
2 Dar es Salaam 2. Ilala MC 3 3 6
3. Kinondoni MC 3 3 6
4. Temeke MC 3 3 6
3 Dodoma 5. Dodoma MC 2 3 5
4 Geita 6. Geita DC 2 2 4
5 Iringa 7. Mufindi DC 3 3 6
8. Iringa MC 2 2 4
6 Kagera 9. Bukoba DC 3 3 6
10. Muleba DC 2 2 4
7 Kigoma 11. Kigoma Ujiji MC 2 3 5
8 Kilimanjaro 12. Moshi DC 3 3 6
9 Lindi 13. Lindi MC 2 2 4
10 Mara 14. Musoma MC 2 2 4
15. Rorya DC 2 2 4
11 Mbeya 16. Chunya DC 2 2 4
17. Kyela DC 3 3 6
18. Mbarali DC 2 2 4
19. Mbeya CC 3 3 6
20. Mbeya DC 3 3 6
21. Mbozi DC 2 2 4
22. Rungwe DC 2 2 4
12 Morogoro 23. Morogoro MC 3 3 6
13 Mwanza 24. Nyamagana MC 3 3 6
25. Sengerema DC 2 2 4
14 Njombe 26. Njombe TC 2 2 4
27. Wanging’ombe DC 2 2 4
15 Rukwa 28. Sumbawanga DC 2 2 4
29. Sumbawanga MC 2 2 4
16 Ruvuma 30. Mbinga DC 2 2 4
31. Songea MC 2 2 4
17 Shinyanga 32. Kahama DC 2 2 4
33. Kahama TC 3 3 6
34. Shinyanga MC 2 2 4
18 Tabora 35. Igunga DC 2 2 4
36. Nzega DC 2 2 4
37. Tabora MC 3 3 6
19 Tanga 38. Korogwe TC 2 2 4
39. Muheza DC 2 2 4
40. Tanga CC 3 3 6
Jumla 95 97 192

No comments:

Post a Comment