Pages

Friday, December 30, 2016

Apple kuanza utengenezaji wa simu mpya India


apple
Baada ya muda mrefu wa vuta nivute na Serikali, kampuni ya simu ya kimarekani Apple wako tayari kuanza utengenezaji wa simu mpya za mkononi nchini India kuanzia mwezi April 2017.
Apple imeungana na kampuni nyingine Taiwan ya utengenzaji wa simu, Wistron kuweka mazingira mazuri ya kibiashara kuanza utengenezaji wa simu mpya katika mji wa Bangalore, Wistron wameweka mazingira katika mji wa Peenya, katika mji wa viwanda karibu Bangalore.
Kampuni hiyo kubwa ya utengenezaji ipo imezamiria kutengeneza simu katika masoko ya India na Bangalore, kampuni hiyo ya Apple inataka mradi huo mkubwa uanze mara moja.
Pamoja na mambo mengine kampuni hiyo ya Apple bidhaa zake nyingi zinatengenezwa China na kampuni ya Foxcom, ambao tayari wana kiwanda India.
Kuweka kiwanda cha kutengeneza simu za Apple katika soko la India ni mkakati mzuri na kabambe wa kibiashara ambapo itafanya bidhaa zao kuwa zenye ubora na gharama nafuu kwa watumiaji wa bidhaa zao bara la Asia.
apple-iphone-7-17
Shar

No comments:

Post a Comment