KWA wasafiri wengi wanaotumia usafiriwa
barabara, hujipatia fursa ya kufanya manunuzi ya mahitaji yao ya
nyumbani, iwe mazao ya jamii ya mbogamboga, viazi, mahindi na hata
wanyama kama mbuzi na kuku, ama kwa hakika ni fursa nzuri wanayoipata
kununua mazao ambayo bado hayajachukua muda mrefu tangu kuvunwa tena kwa
bei nafuu sana. Miongoni mwa mazao yanayopatikana kwa wingi ni pamoja
na nyanya na vitunguu, lakini jambo la kusikitisha, pengine kutokana na
kutokuwepo kwa mipangom thabiti ya kuwainua wakulima hawa, mazao yao
huyauza kwa bei ya "kutupa"ni ndio maana wasafiri huchangamkia fursa
hiyo kununua bidhaa hizo kwa "fujo" tena wengine hunogew ahadi kuachwa
na vyombo vya usafiri kama ni abiria wa bus.
Mchuuzi wa mahindi akiwa katika harakati za kusaka wateja ambao ni abiria
Abiria akionyeshwa bidhaa na wachuuzi
Wanendesha magari wakiwa eneo la biashaya ya mazao ya matunda na mbogamboga barabara ya Msata Bagamoyo kwenye daraja la Ruvu
Mchuuzi wa kuku akiwa amebeba kuku zake tayari kwa kuuza tena bei poa ya shilingi kati ya elfu 10 na elfu 15
Akiwa na tabasamu, mchuuzi huyu wa nyanya, tayari ameliona gari linakaribia kuegesha ili kununua bidhaa zao
Wachuuzi wa mazao mbalimbali wakiwa wanawaonyesha abiria bidhaa zao
Mchuuzi wa nyanya akisubiri wateja
Huyu ni abiria akikimbilia basi baada ya
kuachwa, kutokana na "kunogewa" na manunuzi ya biadhaa zinazouzwa
kandokando ya barabara kuu ya Dar es Salaam, Dodoma eneo la katikati ya
Gairo na Dumila mkoani Morogoro
No comments:
Post a Comment