Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha
Gerson John Mdemu kuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali Ikulu jijini
Dar es Salaam.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimkabidhi
vitendea kazi Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali Gerson John Mdemu
mara baada ya kumuapisha Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza
Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali Gerson John Mdemu mara baada ya
kumuapisha Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa
katika picha ya pamoja na Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali Gerson John
Mdemu wa pili kutoka kushoto. Wengine katika picha ni Katibu Mkuu
Kiongozi Balozi Mhandisi John Kijazi, Mwanasheria Mkuu wa Serikali
George Masaju na Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) Biswalo Mganga mara baada
ya tukio la uapisho kukamilika.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
akisalimiana Kiongozi wa Chama cha Kikomunisti cha China Luo Zhijun
kutoka jimbo la Jiangsu nchini China.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza
na Kiongozi wa Chama cha Kikomunisti cha China Luo Zhijun kutoka
jimbo la Jiangsu nchini China, ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
akisalimiana na Balozi wa China hapa nchini lu youqing aliyeambatana na
Kiongozi huyo wa chama cha Kikomunisti cha China, Ikulu jijini Dar es
Salaam.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda Ikulu jijini
Dar es Salaam.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na
Kiongozi wa Chama cha Kikomunisti cha China Luo Zhijun kutoka jimbo
la Jiangsu nchini China mara baada ya kumaliza mazungumzo yao Ikulu
jijini Dar es Salaam.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa
katika picha ya pamoja na ujumbe wa kiongozi huyo wa chama cha
Kikomunisti cha China Luo Zhijun pamoja na Balozi wa China hapa nchini
lu youqing mara baada ya kumaliza Mazungumzo yao. Wengine katika picha
ni Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Mhandisi John Kijazi pamoja na Mkuu wa
mkoa wa dar es Salaam Paul Makonda. PICHA NA IKULU
Serikali imewataka wanamichezo kujiepusha na matumizi ya dawa za kuongeza nguvu mwilini au matumizi ya dawa
Na Anna Nkinda – Dodoma
Serikali imewataka wanamichezo
kujiepusha na matumizi ya dawa za kuongeza nguvu mwilini au matumizi ya
dawa zisiruhusiwa kwa wanamichezo kwa kufanya hivyo wanaweza kupata
madhara ya kiafya na kufungiwa kushiriki katika mashindano ya kitaifa
na kimataifa.
Mwito huo umetolewa leo na Naibu
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia Wambura
wakati akifunga mashindano ya michezo kwa wanafunzi wa vyuo vikuu
vilivyopo mkoani Dodoma yaliyofanyika katika uwanja wa Jamhuri uliopo
mkoani humo.
Mashindano hayo yaliyojumusha
wanafunzi kutoa vyuo vikuu vya Dodoma, Mipango, St. John na Chuo cha
Biashara (CBE) yaliandaliwa na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa Pensheni wa
PSPF .
Mhe. Wambura alisema kwa kipindi
cha mwaka 2015/16 wanamichezo 14 walichukuliwa vipimo vyao na kupelekwa
katika maabara za Kimataifa na wote kukutwa salama na hivyo kuwapongeza
wanamichezo hao ambao wameweza kujilinda kwa kutotumia dawa hizo.
Alisema, “Viongozi wote wa Vyama
vya Michezo, waalimu na madaktari wa wanamichezo tuungane kwa pamoja
kupiga vita matumizi ya dawa za kuongeza nguvu michezoni. Msisite
kuchukua hatua kali pale inapothibitika bila shaka yeyote kuwa
mwanamichezo ametumia dawa za kuongeza nguvu mwilini”.
Mhe. Naibu Waziri pia
aliwasisitiza wanafunzi wa vyuo vyote nchini kushiriki katika michezo na
kusoma kwa bidii ili waweze kujikwamua kiuchumi na kushiriki kikamilifu
katika ujenzi wa Taifa.
“Vijana wakitumia muda wao wa
ziada kushiriki katika Michezo watajiepusha na mazingira hatarishi
yatakayowapelekea kuwa wazurulaji, kupata maambukizi ya VVU, kutumia
dawa za kulevya na kushiriki katika vitendo vya uhalifu”, alisisitiza
Mhe. Wambura.
Aidha Mhe. Naibu Waziri huyo
aliwakumbusha Wajumbe wa Bodi ya Wadhamini wa PSPF waendelee kudhamini
michezo kama hiyo ili kuweza kuhamasisha vijana kushiriki katika michezo
kwani Michezo ni ajira, afya na inaimarisha umoja.
Dk. Shein azipamba timu za UMISSETA
Katibu
Mkuu Wizara ya Habari, Utalii, Utamaduni na Michezo Omar Hassan (King)
akizungumza na wanamichezo watakaoshiriki mashindao ya UMISETA wa Kanda
ya Unguja na Pemba katika Uwanja wa Amani kwa niaba ya Rais wa Zanzibar
wakati alipowakabidhi vifaa vya michezo timu zitakazoshiriki
mashindano hayo Mjini Mwanza kuanzia tarehe 13 mwezi huu.
Katibu
Mkuu Wizara ya Habari, Utalii, Utamaduni na Michezo Omar King kwa
niaba ya Rais wa Zanzibar akimkabidhi vifaa vya michezo Katibu Mkuu
Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Elimu Khadija Bakari Juma kwa ajili ya
wanafunzi watakaoshiriki mashindano ya UMISETA kuanzia tarehe 13 mwezi
huu Mkoani Mwanza. Picha na Makame Mshenga /Maelezo Zanzibar.
………………………………………………………………………………………
Na Kijakazi Abdalla-Maelezo
WANAMICHEZO wamekumbushwa kuzingatia nidhamu na uvumilivu wanapokuwa viwanjani.
Wito huo umetolewa na Rais wa
Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein,
katika hafla ya kukabidhi vifaa vya michezo kwa timu za skuli za
Zanzibar zitakazoshiriki mashindano ya UMISSETA inayotarajiwa kufanyika
jijini Mwanza baadae mwezi huu.
Akiwakilishwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo Omar Hassan ‘King’ katika uwanja wa Amaan leo, Dk. Shein amesema mambo hayo ndio msingi wa mafanikio kwa wanamichezo wakiwa kwenye mashindano au nje ya viwanja.
Akiwakilishwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo Omar Hassan ‘King’ katika uwanja wa Amaan leo, Dk. Shein amesema mambo hayo ndio msingi wa mafanikio kwa wanamichezo wakiwa kwenye mashindano au nje ya viwanja.
Aliwataka wanamichezo hao Mwanza,
kushirikiana na kuunganisha nguvu wakiwa jijini Mwanza ili waweze
kurudi na ushindi utakaoinua jina la Zanzibar katika medani ya michezo
nchini Tanzania.
Hata hivyo, Mhe. Rais hakuacha
kueleza jinsi anavyosikitishwa na kudorora kwa michezo humu visiwani,
ambako alisema kunasababishwa na utitiri wa timu nyingi.
“Jambo hili la kuwepo utitiri wa
timu ndilo linalodumaza michezo hapa Zanzibar na kuifanya baadhi yao
isipewe kipaumbele,” alisema.
Lakini amewasisitiza wanamichezo
hao kuelewa kwamba wana wajibu wa kushindana kadiri ya uwezo wao kwani
serikali inajitahidi kuwanjengea mazingira mazuri kwa kuwa inatarajia
kupata ushindi hasa katika michezo inayopendwa na mashabiki wengi
ikiwemo mpira wa miguu.
Mapema, Katibu Mkuu Wizara ya
Elimu na Mafunzo ya Amali Khadija Bakari Juma, akimkaribisha mgeni
rasmi katika hafla hiyo, alitoa shukurani zake kwa Rais wa Zanzibar
kutokana na msaada huo wa vifaa.
Alieleza matumaini yake kwamba
vifaa hivyo vitawapa hamasa zaidi washiriki wa mashindano hayo ili
wapate ushindi na kuweza kutembea kifua mbele.
Vifaa vilivyotolewa ni vya mpira
wa miguu, mpira wa wavu (volleyball) na mikono (handball), riadha
pamoja na mpira wa meza (table tennis).
Michuano ya UMISSETA inatarajiwa kuanza kutimua vumbi jijini Mwanza Juni 13 na kufikia tamati Juni 25, mwaka huu.
Katika mashindano hayo, Zanzibar itawakiliishwa na timu mbili ambazo ni kanda ya Unguja na ile ya Pemba.
MKUU WA MKOA MJINI MAGHARIBI AZINDUA MAONYESHO YA MRADI WA MJI MPYA WA ZANZIBAR UJULIKANAO KWA JINA LA NG’AMBO TUITAKAYO’
Katibu
Mtendaji Kamisheni ya Ardhi Zanzibar Ahmed Abdulrahman Rashid akitoa
maelezo juu ya Mpango Mkuu wa matumizi ya Ardhi wakati wa uzinduzi wa
Maonyesho ya Mradi wa Mji mpya wa Zanzibar uliofanyika Mnara wa
kumbukumbu ya Mapinduzi Kisonge Mjini Zanzibar.
Mwakilishi
wa Ubalozi wa Uholanzi Tanzania Eugen Gies akizungumza na wananchi
waliohudhuria uzinduzi wa maonyesho ya Mradi wa Ngambo tuitakayo katika
viwanja vya Mnara wa kumbukumbu ya Mapinduzi Mjini Zanzibar.
Mkuu
wa Mkoa Mjini Magharibi Ayoub Mohammed Mahmoud akitoa maelezo namna
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ilivyojiandaa katika kuwapatia
wananchi nyumba bora za kuishi wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Ngambo
Tuitakayo.
Watoto
wakiangalia na kufurahia mji mpya wa Zanzibar utakavyokuwa kupitia
Mradi wa Ngambo tuitakayo wakati wa uzinduzi wa maonyesho katika viwanja
vya Mnara wa kumbukumbu ya Mapinduzi. Picha na Makame Mshenga /Maelezo
Zanzibar.
RAIS DK SHEIN KATIKA MKUTANO WA VIONGOZI KASKAZINI A UNGUJA LEO
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti
wa CCM Zanzibar Dkt.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Viongozi
alipowasili katika viwanja vya Ukumbi wa Chuo cha Amali Mkokotoni leo
alipofika katika mkutano wa Mabalozi,Wenyeviti wa Matawi,Makatibu na
Maskani za CCM wa Wilaya ya Kaskazini “A” kwa ajili ya kuwashukuru na
kuwapongeza kwa ushindi uliopatikana katika Uchaguzi wa marudio
uliofanyika mwezi machi mwaka huu,[Picha na Ikulu.] 04/06/2016.
VISIMA VINGI DAR VIMECHIMBWA BILA KUFUATA UTARATIBU.
Na Fatma Salum- MAELEZO, Dodoma.
……………………………………
Serikali imesema kuwa visima
vingi Jijini Dar es Salaam vimechimbwa bila ya kufuata kanuni na
taratibu za uchimbaji hivyo maji yake si salama kwa matumizi ya
binadamu.
Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhe.
Mhandisi Gerson Lwenge aliyasema hayo wakati akiwasilisha hotuba ya
bajeti ya wizara yake Bungeni mjini Dodoma.
Mhe. Lwenge alibainisha kuwa
katika kudhibiti mlipuko wa ugonjwa wa Kipindupindu uliotokea mwezi
Agosti 2015 Jijini Dar es Salaam na kuenea nchini, Serikali ilifanya
uchunguzi wa sampuli za maji ya visima 108 vya jijini humo na matokeo
ya uchunguzi huo yalionesha kuwa visima 66 maji yake si salama.
“Wizara yangu kwa kushirikiana na
Wizara ya Afya na wadau wengine ilifanya ukaguzi na kupima uwepo wa
vimelea vya vijidudu vya ugonjwa huo katika visima vya maji
vinavyotumika jijini Dar es Salaam na sampuli za maji ya visima 108
zilichukuliwa, kati ya hivyo visima 20 vifupi na visima 46 virefu maji
yake yaligundulika kuwa si salama. Kwa ujumla visima vingi vilivyopo
kwenye maeneo ya watu vimechimbwa bila ya kufuata kanuni na taratibu.”
Alisema Mhe. Lwenge.
Aidha, Waziri Lwenge alisema kuwa
Serikali pia ilifanya ukaguzi wa ubora wa maji kwenye vyanzo vya maji
katika mikoa ya Mwanza, Arusha, Mara, Manyara, Kagera, Kigoma, Morogoro
na Dodoma ambapo vyanzo vya maji vipatavyo 600 vilikaguliwa na kubaini
kuwa maji yaliyo salama ni chini ya asilimia 40.
Mhe. Lwenge alieleza kuwa Serikali
kwa kushirikiana na Shirika la Afya Duniani (WHO) imekamilisha uandaaji
wa miongozo ya utekelezaji wa Mpango wa Usalama wa Maji (Water Safety
Plan) kwa Vyombo vya Watumiaji wa Maji na Mamlaka za Maji.
“Miongozo hiyo inakusudia
kuboresha huduma za upatikanaji wa maji safi na salama kwa Mamlaka za
Maji na Vyombo vya Watumiaji wa Maji Vijijini (COWSOs) kuanzia kwenye
chanzo cha maji hadi kwa mtumiaji.” Alifafanua Mhe. Lwenge.
Kutekelezwa kwa mpango huo
kutaboresha usimamizi wa usalama wa maji katika vyombo hivyo na
kuwaepusha wananchi kutumia maji yasiyo salama pamoja na kupunguza
upotevu wa maji katika mifumo ya kusambaza maji kote nchini.
SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI MKUU WA WILAYA AHIMIZA VYANZO VYA MAJI VILINDWE
![]() |
Mtendaji Mkuu wa Mamkala ya Mji Mdogo wa Ngaramtoni,Sophia Shoko akizungumza jambo katika maadhimisho hayo. |
![]() |
Diwani wa Kata ya Kiranyi ,halmashauri ya wilaya Arusha DC,John Seneu alikiwataka wananchi kutii sheria ili kulinda vyanzo vya maji. |
![]() |
Wanafunzi wa Shule ya Msingi ya Serikali ya mchepuo wa Kiingereza ya Arusha School wakiimba Shairi lao lenye kuhamasisha utunzaji wa mazingira na kupanda miti. |
![]() |
Baadhi ya viongozi kutoka halmashauri ya Arusha DC wakisikiliza kwa makini hotuba ya Mkuu wa wilaya. |
![]() |
Baadhi ya viongozi kutoka maeneo mbalimbali ya mkoa wa Arusha wadau wa taasisi binafsi na wananchi kwa pamoja wameshiriki kikamilifu Siku ya mazingira duniani. |
Kijana
wa Umoja wa Vijana wa CCM, Kibibi Duka akimvalisha skafu Msemaji wa
CCM, Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Christopher Ole Sendeka, alipowasili
Ofisi ya CCM y Wilaya ya Kilwa mkoani Lindi akiwa katika ziara ya
kukagua na kuimarisha uhai wa Chama wilayani humo leo.
Kijana
wa Umoja wa Vijana wa CCM, Ali Njonzi akitokwa na jasho jembemba wakati
wa Vijana wa umoja huo walipokuwa wakimpokea msemaji wa CCM,
Christopher Ole Sendeka katika Ofisi ya CCM wilaya ya Kilwa leo akiwa
katika ziara ya kukagua na kuimarisha uhai wa Chama
Msemaji
wa CCM, Cheristopher Ole Sendeka akimsalimia Katibu wa CCM Wilaya ya
Liwale Raphael Maumba, alipokuwa akisalimia viongozi mbalimbali wa CCM
mkoa wa Lindi, baada ya kuwasili ofisi ya CCM wilaya ya Kilwa leo akiwa
katika ziara ya kukagua na kuimarisha uhai wa Chama
Mwenyekiti
wa CCM mkoa wa Lindi Ali Mtopa akimuongoza Msemaji wa CCM, Christopher
Ole Sendeka kuingia Ofisi ya CCM wilaya ya Kilwa, alipowasili akiwa
katika ziara ya kukagua na kuimarisha uhai wa Chama leo
Msemaji
wa CCM Christopher Ole Sendeka akisaini kitabu cha wageni baada ya
kuwasili Ofisi ya CCM wilaya ya Kilwa, akiwa katika ziara ya kukagua na
kuimarsiha uhai wa Chama wilayani humo leo. Kushoto ni Mwenyekiti wa CCM
mkoa wa Lindi Ali Mtopa
Baadhi
ya wageni waliofuatana na semaji wa CCM, Christopher Ole Sendeka wakiwa
ukumbi wa Ofisi ya CCM, wakati Sendeka alipokuwa akizungumza na baadhi
ya viongozi wa CCM wilaya ya Kilwa mkoani Lindi leo.
Katibu
wa CCM mkoa wa Lindi Adelina Geffi akisoma taarifa ya Chama, Msemaji wa
CCM alipowasili Ofisi ya CCM wilaya ya Kilwa mkoani humo leo. Kushoto
ni Mwenyekiti wa CCM mkoa huo wa Lindi Ali Mtopa.
Msemaji
wa CCM Christopher Ole Sendeka akizungumza na viongozi wa CCM,
alipowasili katika Ofisi ya CCM wilaya ya Kilwa mkoani Lindi leo.
Kushoto ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Lindi Ali Mtopa.
Msemaji
wa CCM, Christopher Ole Sendeka akiselebuka na Vijana wa Umoja wa
Vijana wa CCM waliofika kumpokea katika Ofisi ya CCm wilaya ya Kilwa
mkoani Lindi leo kukagua na kuimarisha uhai wa Chama
Wazee
wa Kilwa mkoani Lindi wakimpokea kwa shamrashamra Msemaji wa CCM
Christopher Ole Sendeka, alipowasili katika ukumbi wa Hall Fair,
kuzungumza nao leo akiwa katika ziara ya kukagua na kuimarisha uhai wa
Chama wilayani Kilwa mkoani Lindi
Wazee
wa Kilwa mkoani Lindi wakimpokea kwa shamrashamra Msemaji wa CCM
Christopher Ole Sendeka, alipowasili katika ukumbi wa Hall Fair,
kuzungumza nao leo akiwa katika ziara ya kukagua na kuimarisha uhai wa
Chama wilayani Kilwa mkoani Lindi
Mwenyekiti
wa Wazee wa wilaya ya Kilwa mkoani Lindi, Mohammed Msinjepi
akimkaribisha Msemaji wa CCM, Christopher Ole Sendeka (katikati),
kuzungumza na wazee wa wilaya ya Kilwa, katika ukumbi wa Hall Fair leo.
Kushoto ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Lindi Ali Mtopa.
Hakim
Mstaafu Mzee Zuberi Liengama akisoma risala, kabla ya Msemaji wa CCM
Christopher Ole Sendeka kuzungumza na wazee wa wilaya ya Kilwa mkoani
Lindi leo
Hakim
Mstaafu Mzee Zuberi Liengama akimkabidhi risala baada ya kuisoma, kabla
ya Msemaji wa CCM Christopher Ole Sendeka kuzungumza na wazee wa wilaya
ya Kilwa mkoani Lindi leo
Mwenyekiti
wa CCM mkoa wa Lindi Ali Mtopa akimtambulisha kwa wazee wa wilaya ya
Kilwa, Msemaji wa CCM, Christopher Ole Sendeka, leo katika Ukumbi wa
Hall Fair
Msemaji
wa CCM, Cheristopher Ole Sendeka akizungumza na Wazee wa wilaya ya
Kilwa mkoani Lindi alipokuwatana nao katika ukumbi wa Hall Fair,
wilayani humo leo. PICHA ZOTE NA BASHIR NKOROMO
WAZIRI JANUARI MAKAMBA APANDA MITI UFUKWE WA BAHARI YA HINDI
Waziri
wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mh. January
Makamba akitia saini kitabu cha Wageni alipotembelea Kata ya Mbweni
iliyopo Manispaa ya Kinondoni kwa ajili ya shughuli za upandaji mikoko
katika eneo hilo.
Waziri
wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mh. January
Makamba akipanda mti aina ya mkoko katika fukwe za bahari ya hindi
katika eneo la Mbweni jijini Dar es Salaam. Upandaji huo wa mikoko ni
katika kuadhimisha wiki ya mazingira duniani, ambayo kilele chake ni
kesho
Waziri
wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mh. January
Makamba akishirikiana kupanda miti ya mikoko na wakazi wa kata ya
Mbweni jijini Dar es Salaam ikiwa ni kuelekea kilele cha siku ya
mazingira hapo tarehe 5 juni.
Waziri
wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mh. January
Makamba akifurahia jambo na Wanafunzi wa Shule ya Msingi Mbweni ambao
walijumuika pamoja naye kupanda mikoko katika fukwe za Mbweni jijini Dar
es salaam.
Waziri
wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mh. January
Makamba akiongea na Waandishi wa Habari (hawapo pichani) mara baada ya
kumaliza kupanda mikoko katika fukwe za bahari ya Hindi katika kata ya
Mbweni.
……………………………………………………………………………………………………………
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa
Rais Muungano na Mazingira Mh. January Makamba Ametoa wito kwa
Wananchi wa Kata ya Mbweni kutunza mazingira na kutoa kipaumbele kwa
mazingira. Aliyasema hayo wakati wa zoez la upandaji mikoko lilifanyika
katika fukwe za bahari ya Hindi zilizoko Mbweni.
Akiongoza Wananchi wa Kata hiyo
kupanda miche 5,000 ya mikoko , Waziri Mkamba alisititiza pia Wanafunzi
wa shule waliopo katika eneo hilo kupenda mazingira yao na kuyatunza ili
yawafae baadaye.
Wakisoma Risala yao , Wanawake wa
Mbweni walimuomba Waziri awasaidie kuwapatia vitendea kazi kwa ajili
ya kuhudumia mikoko pamoja na kumuomba awasaide kuwatatulia changamoto
wanazokutana nazo. Ikiwamo ya maafisa wa TRA kukata hovyo mikoko
wanapokua wanafanya doria katika fukwe zaMbweni.
Mwisho Waziri aliwahukuru
Wananchi wa Mbweni waliojitypkeza kujumuika naye katika zoezi hilo la
upandaji mikoko. Shuhuli za upandaji mikoko ni kuelekea maadhimisho ya
siku ya mazingira ambayo kilele chake ni tarehe 5 juni kila mwaka.
POLISI KUZIDI KUIMARISHA ULINZI KWA KUSHIRIKIANA NA VIONGOZI WA DINI, MADIWANI
Kamanda wa Polisi Mkoa wa
Arusha Naibu Kamishna (DCP) Charles Mkumbo akifungua kikao cha kujadili
amani katika mkoa wa Arusha ambacho kilifanyika katika bwalo la
Maofisa wa Polisi Arusha (Picha na Rashid Nchimbi wa Jeshi la Polisi
Arusha)
Meya wa halmashauri ya Jiji la Arusha Calist Lazaro akitoa mchango wake
wakati akichangia mada ya uimarishaji wa amani katika Mkoa wa Arusha
(Picha na Rashid Nchimbi wa Jeshi la Polisi Arusha)
Sheikh
wa wilaya ya Arusha Abraham Salum akisisitiza jambo wakati akitoa
mchango wake juu ya uimarishaji wa amani katika mkoa wa Arusha ( Picha
na Rashid Nchimbi wa Jeshi la Polisi Arusha
Padre Festus Mangwangi wa Parokia ya Mtakatifu Theresia akielezea
umuhimu wa amani ndani ya Jamii yetu wakati akichangia mada katika kikao
kilichofanyika jana ukumbi wa bwalo la Maofisa wa Polisi Arusha ( Picha
na Rashid Nchimbi wa Jeshi la Polisi Arusha)
Baadhi
ya viongozi wa dini, madiwani na askari Polisi waliohudhuria kikao cha
kujadili amani ya Mkoa wa Arusha kilichofanyika jana katika ukumbi wa
bwalo la Maofisa wa Polisi Arusha (Picha na Rashid Nchimbi wa Jeshi la
Polisi Arusha)
……………………………………………………………………………………………………………………………..
Na Rashid Nchimbi wa Jeshi la Polisi Arusha
Jeshi la Polisi Mkoani hapa
limefanya kikao ambacho kiliwashirikisha viongozi wa dini kutoka
madhehebu mbalimbali pamoja na Madiwani wa halmashauri ya jiji la Arusha
kwa nia ya kuimarisha amani na usalama.
Kikao hicho kilichofanyika jana
katika ukumbi wa Bwalo la Maofisa wa Polisi kiliwajumuisha watu zaidi
ya mia mbili; Maofisa wa Mkoa wa Jeshi hilo, viongozi wa dini wa
madhehebu yote, Madiwani, Wakaguzi wa Polisi wa Tarafa na Polisi wa
kata.
Akizungumza katika kikao hicho
Kamanda wa Polisi mkoani hapa Naibu Kamishna Charles Mkumbo ambaye
alikuwa mwenyeji wa kikao hicho alifungua kwa kusema kwamba Jeshi la
Polisi pekee haliwezi kukabiliana na uhalifu bali kwa kushirikiana na
viongozi wa dini na wa kisiasa wataweza kuushinda uhalifu.
Alisema makundi hayo ni wadau
wakubwa wa kuimarisha amani kutokana na ushawishi walionao kwa waumini
wao na wananchi wanawaongoza huku Jeshi hilo likiahidi kuwa bega kwa
bega hasa katika upokeaji wa taarifa za uhalifu na kuzifanyia kazi kwa
haraka.
Kamanda Mkumbo alisema kwamba
bila amani hakutakuwa na shughuli zozote za maendeleo ikiwemo uwezekaji
na hata waumini hawataweza kwenda Misikitini na Makanisani kutokana na
hofu ya kiusalama.
“Sote tunajukumu la kufichua
uhalifu na wahalifu kupitia taarifa za waumini wetu hasa kwa viongozi
wetu wa dini kuendelea kuhubiri na kutoa mawaidha katika Makanisa na
Misikiti huku Madiwani waendelee kufanya hivyo katika maeneo yao ya
kiutawala hasa wanapokutana na wananchi kwenye mikutano mbalimbali”.
Alisisitiza Kamanda Mkumbo.
Kwa upande wake Meya wa jiji la
Arusha Calist Lazaro alisema kwamba wananchi pamoja na viongozi wote
wasiwe na hofu kwa kuwa Jiji la Arusha linaongozwa na CHADEMA kwani wao
kama viongozi wa Siasa wanahitaji amani na wanalitambua jukumu hilo na
wataendelea kutoa ushirikiano na Jeshi la Polisi pamoja na vyombo vyote
vya usalama huku akiwataka baadhi ya askari wa Jeshi hilo kufuata haki
katika utendaji wa kazi zao.
Sheikh wa wilaya ya Arusha
Abraham Salum alisema kwamba kikao hicho kimekuja wakati muafaka kwani
mikoa ya Tanga na Mwanza kumejitokeza vitendo vya uvunjifu wa amani
matukio ambayo hapo awali hayakuwepo katika nchi yetu na kulishauri
jeshi hilo kuongeza weredi katika kupambana na uhalifu huku akiwataka
wananchi kutoa ushirikiano kwa Jeshi hilo.
Akichangia mjadala huo Padre
Festus Mangwangi wa Parokia ya Mtakatifu Theresia, alisema kwamba wao
kama viongozi wa dini wana dhamana kubwa ya kulisaidia Jeshi la Polisi
katika kuhubiri amani kupitia waumini wao. Alisema amani iliyopo
idumishwe kwani baadhi ya nchi zinavurugu na zinatamani amani iliyopo
hapa nchini.
Akihitimisha kikao hicho
kamanda Mkumbo aliwashukuru viongozi wote waliohudhuria kwa michango yao
yenye tija kwa mustakabali wa uimarishaji wa amani ndani ya mkoa wa
Arusha na kusema kwamba ana matumaini makubwa ya kupata ushirikiano toka
kwao naye kuahidi kutatua kero zilizowasilishwa na washiriki ambazo
zipo ndani ya uwezo wake.
NAIBU KATIBU MKUU WA WIZARA YA NISHATI NA MADINI DK. JULIANA PALLANGYO AFANYA ZIARA KATIKA KAMPUNI YA PUMA ENERGY
Naibu
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia Nishati,
Dk. Juliana Pallangyo (kushoto) akiwa ameambatana na Mkurugenzi Mkuu wa
Wakala wa Serikali wa Uagizaji wa Mafuta ya Pamoja (PBPA),Michael
Mjinja (kulia) mara alipowasili katika ofisi za Puma Energy jijini Dar
es Salaam kwa ajili ya kukagua shughuli zake.
Meneja
Afya, Usalama na Mazingira kutoka katika kampuni ya Puma Energy
Blasio Menchi (kulia) akielezea shughuli za kampuni hiyo mbele ya Naibu
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia Nishati,
Dk. Juliana Pallangyo pamoja na ujumbe wake.
Kutoka
kushoto Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini
anayeshughulikia Nishati Dk. Juliana Pallangyo, Kaimu Kamishna wa
Nishati na Maendeleo ya Petroli Nchini James Andelile, Mkurugenzi Mkuu
wa Wakala wa Serikali wa Uagizaji wa Mafuta ya Pamoja (PBPA),Michael
Mjinja,na Kaimu Kamishna wa Petroli ambaye pia ni Mjumbe wa Bodi ya
Wakurugenzi wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Nchini (TPDC) Mwanamani
Kidaya wakifuatilia kwa makini maelezo yaliyokuwa yanatolewa na Meneja
Afya, Usalama na Mazingira kutoka katika kampuni ya Puma Energy
Blasio Menchi (hayupo pichani) kwenye ofisi za Puma Energy jijini Dar es
Salaam.
Meneja
Uendeshaji kutoka Kampuni ya Puma Energy Lameck Hiliyai
(katikati) akielekeza jambo kwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati
na Madini anayeshughulikia Nishati Dk. Juliana Pallangyo (kushoto)
Kaimu Kamishna wa Nishati na Maendeleo ya Petroli Nchini James
Andelile (aliyekaa katikati) na Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Serikali
wa Uagizaji wa Mafuta ya Pamoja (PBPA),Michael Mjinja (kulia) katika
kikao hicho kwenye ofisi za Puma Energy jijini Dar es Salaam.
Naibu
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia Nishati
Dk. Juliana Pallangyo (kushoto) na Kaimu Kamishna wa Nishati na
Maendeleo ya Petroli Nchini James Andelile (kulia) wakibadilishana
mawazo katika kikao hicho.
Kaimu
Kamishna wa Nishati na Maendeleo ya Petroli Nchini James
Andelile,(kulia) akielezea jambo katika kikao hicho. Kushoto ni Naibu
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia Nishati Dk.
Juliana Pallangyo
Naibu
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia Nishati Dk.
Juliana Pallangyo akitoa maelekezo kwa kampuni ya Puma Energy katika
kikao hicho
No comments:
Post a Comment