Pages

Friday, February 5, 2016

Serikali imeombwa kuzifadhili Asasi za kiraia zinazotoa Elimu ya Mpiga kura

DSC00131
Na Waandishi wa NEC, Mbeya
Serikali imeombwa kuzifadhili Asasi za kiraia zinazotoa Elimu ya Mpiga kura ili ziweze kuwaelimisha wananchi kwa wakati umuhimu wa kupiga kura katika uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani.
Katika Uchaguzi Mkuu uliopita Tume ya Taifa ya Uchaguzi ilitoa vibali vya kutoa Elimu ya Mpiga kura kwa Asasi za kiraia 447 kutoka maeneo mbalimbali nchini lakini ni asasi chache zilizofanikiwa kupata fedha kutoka kwa wafadhili kwa ajili ya kutoa elimu hiyo.
Wakizungumza kwenye Mkutano wa tathmini ya Elimu ya Mpiga Kura kati ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi na Asasi za Kiraia uliofanyika leo jijini Mbeya, wawakilishi wa Asasi hizo walisema Elimu ya Mpiga Kura inapaswa kutolewa mapema kwani katika Uchaguzi Mkuu uliopita asasi zilipata fedha kipindi kifupi kabla ya kufanyika Uchaguzi Mkuu.
Walisema kutokana na Asasi nyingi kutokupata fedha kutoka kwa wafadhili, Elimu ya Mpiga Kura haikuweza kuwafikia wananchi wengi zaidi na hivyo kusababisha baadhi ya wananchi wengi kutojitokeza kupiga kura na kura nyingi kuharibika.
Aidha, wajumbe hao pia wameitaka Tume ya Taifa ya Uchaguzi kusimamia na kuratibu Elimu ya Mpiga Kura ili iwe endelevu badala ya kusubiri kutoa Elimu hiyo katika kipindi cha Uchaguzi Mkuu pekee.
Naye Msimamizi wa Uchaguzi wa jiji la Mbeya Dkt. Samwel Lazaro amezitaka Asasi za kiraia kuhakikisha zinatoa elimu hiyo mpaka kwenye maeneo ya vijijini ambapo wananchi hawapati taarifa za kutosha ukilinganisha na maeneo ya mijini.
Alisema Elimu hiyo ikitolewa kwa ufasaha itasaidia kupunguza idadi ya kura zinazoharibika na kuongeza idadi ya wananchi wanaojitokeza kupiga kura wakati wa uchaguzi Mkuu.
Katika uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015, jumla ya wananchi milioni  22,658,247 waliandikishwa kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura ambapo kati ya hao, 15,596,110 sawa na asilimia 67 waliojiandikisha walijitokeza kupiga kura. Kura zilizoharibika au kukataliwa zilikuwa ni 402,248 sawa na asilimia 2.5.
Mkutano wa Tathmini ya Elimu ya Mpiga Kura kati ya Tume na Asasi za Kiraia ulizishirikisha Asasi za kiraia zaidi ya 15 kutoka mikoa mitatu ya Mbeya, Rukwa na Katavi zilizopewa kibali na Tume ili kutoa elimu ya mpiga kura katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.

KATIBU MKUU WA CCM NDUGU ABDULRAHMAN KINANA AWATEMBELEA WAHADZABE NA KUSHIRIKI SHUGHULI ZA MAENDELEO KWA JAMII HIYO

1
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipozi kwa picha na Mwenyekiti wa Jamii ya Wahadzabe Chifu Edward Mashimba kushoto na Mama Sara Philipo mwenye nyumba hiyo wakati alipozungumza na chifu huyo leo, Katika ziara hiyo Kinana katika kijiji cha Kibampa na  kukagua miradi mbalimbali ya jamii hiyo ya Kihadzabe ikiwemo maji, mabweni ya watoto wa jamii hiyo pamoja na zahanati iliyopo katika kijiji cha Munguli kata ya Mwangeza wilaya ya Mkalama mkoani Singida.
 Mkuu wa Mkoa wa Singida Ndugu Parseko Kone amewajengea mabweni na kuwawekea mradi wa maji, Umeme na kuwafundisha kilimo cha mihogo na mazao mengine ili kuweza kujikimu kwa chakula kwani jamii ya kabila hilo inakula nyama, mizizi ya miti na asali.
Lakini pia vijana hamsini wa Kabila hilo wamejiunga na jeshi la wananchi kwa mpango mkuu wa mkoa wa Singida Ndugu Parseko Kone na  serikali kwa kuwaendeleza kielimu na kimaendeleo, kuna vijana wengine sitini wataingizwa jeshini ikiwa ni mkakati wa kuielimisha jamii hiyo ili kubadili maisha bila kuharibu mila yao.(PICHA NA JOHN BUKUKU-FULLSHANGWE-MKALAMA -SINGIDA)
2
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akijadiliana jambo Mwenyekiti wa Jamii ya Wahadzabe Chifu Edward Mashimba wakati alipotembelea na kujadiliana naye mawili matatu.
3
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana na Mama Sara Philipo mwenye nyumba hiyo wakitoka nje mara baada ya Kinana kuzungumza na Chifu Edward Mashimba.
4
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akijadiliana jambo Mwenyekiti wa Jamii ya Wahadzabe Chifu Edward Mashimba
5
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia wananchi hao wa jamii ya Wahadzabe huku  Mwenyekiti wa Jamii ya Wahadzabe Chifu Edward Mashimba akitafsiri  katika kijiji cha Kibampa kata ya Mwangeza. 
6
Baadhi ya wananchi wakiwa katika mkutano huo wakimsikiliza Ndugu Abdulrahman Kinana hayupo pichani wakati alipokuwa akiwahutubia.
7
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki katika kazi ya kupanda mbegu ya muhogo na vijana wa Kihadzabe katika shamba darasa ililopo kijiji cha Kibampa kata ya Mwangezi ikiwa ni mafunzo ya kilimo kwa jamii hiyo.
9 10
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiangalia ngoma ya jamii hiyo wakati alipokuwa akiwasili kijiji cha Kibampa.
11
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kucheza ngoma ya asili ya jamii ya Kihadzabe.
13
Msafara wa  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana ukikatisha misitu na mabonde wakati ukielekea kata ya Mwangeza kijiji cha Kibampa ambako jamii hiyo inaishi.
15
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisaklimiana na vijana wa kisukuma aliowakuta wakipalilia shamba, vijana hao walimweleza Kinana kuwa wanahitaji serikali iwatengenezee barabara yao jambo ambalo litarahisha hata uuzaji wa mazao yao.
16
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikagua mradi wa maji katika kijiji cha Munguli ambao umejengwa maalum kwa ajili ya jamii hiyo anayetoa maelekezo ni Mkuu wa wilaya ya Mkalama Ndugu Christopher Ngubiagai.
17
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikagua mabweni ya watoto wa jamii ya Kihadzabe yaliyojengwa na Mkuu wa Mkoa wa Singida Dk. Parseko Kone  katika kijiji cha Munguli  mabweni hayo yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 60 wa kiume 30 na wakiume 30 yamejengwa maalum kwa ajili ya jamii kulia  ni Mkuu wa wilaya ya Mkalama Ndugu Christopher Ngubiagai.
18
Baadhi ya wananfunzi wa shule hiyo
19
Mwalimu Mkuu wa shule hiyo ya Munguli Athman Kinyere akisoma taarifa ya shule hiyo  kwa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana
20
Hii ni moja ya nyumba zinazotumiwa na jamii hiyo ya Kihadzabe.
21
Baadhi ya wananchi wa jamii hiyo wakiwa katika mkutano 
23
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikagua mtambo wa Sola unaoendesha maji katika  mradi wa maji wa kijiji cha Munguli ambao umejengwa maalum kwa ajili ya jamii hiyo anayetoa 

TFF YAONYA UPANGAJI WA MATOKEO

gs 
Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) limewaonya viongozi wa vilabu, wachezaji, waamuzi na wasimamizi wa mchezo kutojihusisha na upangaji wa matokeo (Match fixing) katika michezo inayoendelea sasa katika ligi za ngazi mbalimbali za nchini.
TFF imejipanga na inasimamia vizuri michezo ya Ligi Kuu (VPL), Daraja la Kwanza (FDL), Daraja la Pili (SDL) na Azam Sports Federation Cup (ASFC) inayoendelea na yoyote atakayebainika kujihusisha na mchezo huo wa upangaji matokeo, hatua kali za kinidhamu zitachukuliwa.
Katika michezo yote inayoendelea TFF ina maofisa wake wanaofuatilia kwa ukaribu michezo hiyo, hivyo endapo kiongozi, mchezaji, msimamizi au mwamuzi atabainika kujihusisha na upangaji wa matokeo hatua kali zitachukuliwa .
TFF inawaomba viongozi, wachezaji, wasimamizi wa michezo na waamuzi kutojihusisha na mchezo huo wa upangaji wa matokeo kwani kufanya hivyo ni kukiuka katiba, sheria na kanuni zinaongoza mpira wa miguu nchini.

MAGALA 275 KUJENGWA KUDHIBITI UKOSEFU WA CHAKULA NCHINI

images(
Na Raymond Mushumbusi-Dodoma)
……………………………………..
Serikali katika kuongeza na kuimarisha uhakika na usalama wa chakula hapa nchini, Serikali imepanga kujenga maghala 275 kwa awamu katika sehemu zenye uzalishaji mkubwa wa zao la mahindi ambapo hadi sasa jumla ya maghala 125 yanaendelea kujengwa na kukarabatiwa katika maeneo hayo.
Akifafanua hilo wakati akiharisha shughuli za Mkutano wa Pili wa Bunge la 11 lilikuwa na vikao 9 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa,Majaliwa amesema Serikali imejipanga katika kuondoa tatizo la upungufu wa chakula nchini kwa kujenga magala mengi zaidi ya kuhifadhi chakula katika maeneo mbalimbali yenye changamoto za upungufu wa chakula.
Mhe. Kassim Majaliwa,Majaliwa amesema hali ya chakula kwa mwaka 2015/2016 katika maeneo mengi ya nchi imeendelea kuwa ya kuridhisha kufuatia mavuno mazuri yaliyopatikana msimu wa kilimo wa 2014/2015 na takwimu za Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi zinaonesha kuwa albaki kutoka msimu uliopita nchi ilikuwa na ziada ya chakula licha ya kuwepo kwa maeneo machache ambayo hayakuwa na chakula.
“Kutokana na uzalishaji wa mazao ya chakula kwa msimu wa 2014/2015 kuwa Tani milioni 15.5 na mahitaji ya chakula kwa mwaka 2015/2016 kuwa Tani milioni 12.9 hivyo nchi imejitosheleza kwa chakula kwa ziada ya Tani milioni 2.5 sawa na asilimia 120 na napenda kuwahakikishia Watanzania kuwa Serikali itaendelea kuhudumia maeneo yote yenye uhaba wa chakula”
“Ili kukabiliana na hali ya uhaba wa chakula katika maeneo hayo, Serikali inaendelea kutoa chakula katika maeneo hayo ambapo jumla ya Tani 23,871.6 za chakula zilitengwa kwa ajili hiyo na hadi kufikia tarehe 17 Januari, 2016, jumla ya Tani 11,860.8 zilikuwa zimechukuliwa toka Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) kwenda kwenye Halmashauri za Wilaya zenye upungufu wa chakula kwa ajili ya usambazaji pia natoa wito kwa Halmashauri ambazo hazijachukua mgao wao kufanya hivyo mara moja ili Wananchi katika maeneo hayo wasizidi kuathirika” Alisema Mhe. Majaliwa.
Aidha, Mhe Kassim Majaliwa,Majaliwa amesema Serikali kwa kupitia Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) inaendelea kujenga maghala ya kimkakati kwa ajili ya kuhifadhi akiba ya Taifa na Kwa sasa ghala moja lenye uwezo wa kuhifadhi Tani 5,000 limeshajengwa Wilayani Mbozi Mkoani Mbeya na Serikali imepata mkopo wenye masharti nafuu kutoka Serikali ya Poland ambao utawezesha kujenga vihenge vya kisasa (silos) vyenye uwezo wa kuhifadhi Tani 160,000 na maghala yenye uwezo wa kuhifadhi Tani 90.
Ameongeza kuwa Pamoja na hatua zinazochukuliwa na Serikali, amewataka viongozi wa Mikoa, Wilaya na watendaji katika Halmashauri zote Nchini kuwahamasisha Wananchi kutumia vizuri mvua zinazonyesha nchini kote kwa kulima kwa bidii ili kuweza kuvuna na kujiwekea akiba ya chakula cha kutosha kwa ajili ya kaya zao wakati wote wa mwaka na wawahamasishe wafanyabiashara na wadau wengine kusaidia Serikali kuchukua chakula kutoka maeneo yenye ziada na kupeleka katika maeneo yenye upungufu na kwa kuzingatia maelekezo haya pamoja na juhudi za Serikali zilizooneshwa, tatizo la uhaba wa chakula nchini litapungua, kama siyo kumalizika kabisa.
Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa,Majaliwa amehairisha Mkutano wa Pili Bunge amehairisha shughuli za Bunge mpaka tarehe 19 mwezi April 2016 saa 3 Asubuhi likaporejea katika Mkutano wa kujadili Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2016/2017.

UJUMBE KUTOKA CHUO CHA ULINZI WA TAIFA WATEMBELEA MAKAO MAKUU YA JESHI LA MAGEREZA

1
Kamishna wa Fedha na Utawala wa Jeshi la Magereza, Gaston Sanga akisalimiana na Kaimu Mkuu wa Chuo cha Ulinzi wa Taifa, Bregedia Jenerali, Jairos Mwaseba alipotembelea Makao Makuu ya Jeshi la Magereza, Jijini Dar es Salaam akiwa pamoja na Washiriki wa Mafunzo katika chuo hicho cha Ulinzi wa Taifa(hawapo pichani) leo Februari 5, 2016(kushoto) ni Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza, Dkt. Juma Malewa.
2
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja akisalimiana na Mkufunzi wa Chuo cha Ulinzi wa Taifa ambaye ni raia kutoka China(katikati) ni Kaimu Mkuu wa Chuo cha Ulinzi wa Taifa, Bregedia Jenerali, Jairos Mwaseba alipotembelea Makao Makuu ya Jeshi la Magereza, Jijini Dar es Salaam akiwa pamoja na Washiriki wa Mafunzo katika chuo hicho cha Ulinzi wa Taifa(hawapo pichani) leo Februari 5, 2016.
3
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja akiongea na Ujumbe kutoka Chuo cha Ulinzi wa Taifa(hawapo pichani). Ujumbe huo wa Washiriki wa Mafunzo wametembelea Ofisi za Makao Makuu ya Jeshi la Magereza katika ziara yao ya Mafunzo kuhusu Uendeshaji wa shughuli za Magereza hapa nchini.
4
Wakufunzi wa Chuo cha Ulinzi wa Taifa wakifuatilia kwa makini mazungumzo kati yao na Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja(hayupo pichani). Kushoto ni Kaimu Mkuu wa Chuo cha Ulinzi wa Taifa, Bregedia Jenerali, Jairos Mwaseba.
5
Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza, Dkt. Juma Malewa akitoa maelezo mafupi kwa Washiriki wa Mafunzo kutoka Chuo cha Ulinzi wa Taifa walipotembelea Kiwanda cha Gereza Kuu Ukonga kwa ziara yao ya Mafunzo(kushoto) ni Mkuu wa Magereza Mkoa wa Dar es Salaam, Kamishna Mwandamizi wa Magereza, Augustine Mboje.
6
Baadhi ya Washiriki wa Mafunzo kutoka chuo cha Ulinzi wa Taifa wakimwangalia mmoja wa wafungwa ambaye amepatiwa ujuzi gerezani wa kukata vitambaa vya nguo tayari kwa kushona nguo za wafungwa wliopo magerezani kama anavyoonekana katika picha katika Kiwanda cha Gereza Kuu Ukonga, Jijini Dar es Salaam.
(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).

RAIS MHE. DKT. MAGUFULI AWASALIMIA WAKAZI WA MOROGORO PAMOJA NA KUKAGUA BARABARA YA MOROGORO-DODOMA ENEO LA KIBAIGWA.

1
Msafara wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli ukipita katika eneo la Msamvu mjini Morogoro kuelekea Dodoma.
2
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwasalimia wakazi wa Msamvu mjini Morogoro wakati akiwa njiani kuelekea Dodoma.
3 4
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwasalimia wakazi wa Wami dakawa mkoani Morogoro wakati akiwa njiani kuelekea Dodoma.
7
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwasalimia wakazi wa eneo la Magole mkoani Morogoro.
5 6
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia ukarabati unaondelea katika barabara kuu ya Morogoro-Dodoma eneo la Kibaigwa . sehemu ya barabara hiyo inakarabatiwa chini ya usimamizi wa Wakala wa Barabara nchini TANROADS.
PICHA NA IKULU

DINAH SAMANYI: MIAKA 39 YA CCM, MAKADA WATULIE NDANI YA CHAMA ILI WASIJUTE BAADAE.

New PictureDinah Somba Samanyi ambae ni Katibu wazWazazi (CCM) Mkoani Mwanza.
…………………………………………………………………………………….
Na:George Binagi-GB Pazzo @BMG
Ikiwa hii leo ni Maadhimisho ya Miaka 39 tangu kuzaliwa kwa Chama cha Mapinduzi CCM, Wanachama wake wametakiwa kutulia ndani ya Chama hicho badala ya kujitoa katika chama jambo ambalo huwafanya baadae kujutia.
Kauli hiyo imetolewa Mkoani Mwanza na Katibu wa Wazazi wa Chama hicho Ndg.Dinah Somba Samanyi, wakati akizungumza na BMG, kuhusiana na maadhimisho ya miaka 39 ya CCM mwaka huu 2016.
Samanyi ametanabaisha kwamba, mwaka huu ikiwa ni miaka 39 tangu CCM kuasisiwa February 05,1977 ikiwa ni baada ya Muungano wa wa vyama viwili vya ASP kutoka Zanzibar na TANU kutoka Tanganyika, ni vyema wanachama wake wakawa waadilifu na kuepukana na tabia zisizo za kimaadili ambazo ni pamoja na kujitoa ndani ya chama hicho kama ambavyo baadhi yao wameshuhudiwa wakifanya jambo ambalo hata hivyo huwafanya baadae kulijutia.
Kuhusu maadhimisho amesema “Chama kimejipanga vizuri katika kuadhimisha Siku hii na tangu kuzinduliwa Kitaifa kwa sherehe za maadhimisho haya kule Zanzibar, kumekuwa na shughuli mbalimbali zinazolenga kuimarisha uhai wa chama pamoja na kushiriki shughuli tofauti tofauti za kijamii”.
Samanyi amebainisha “Katika Mkoani Mwanza kila Wilaya imepewa fursa ya kuandaa shughuli mbalimbali kwa ajili ya maadhimisho haya. Jumuiya mbalimbali ikiwemo Jumuiya ya Wazazi zimeshiriki shughuli tofauti tofauti kama vile kutembelea mashuleni, kufanya usafi wa mazingira pamoja na kutembelea wagonjwa Mahospitalini”.
Nao baadhi ya makada wa vyama vya siasa Mkoani Mwanza wametoa maoni yao kuhusiana na miaka 39 ya CCM kikiwa ni chama kinachoongoza Serikali, ambapo Kada wa CCM Sarah Ramadhan anasema anasema kuwa miaka 39 ya chama hicho, taifa limepiga hatua kubwa kimaendeleo ikilinganishwa na miaka iliyopita huku Amos Joseph ambae ni Kada ya Chadema akisema kuwa miaka 39 ya uongozi wa CCM taifa limeshindwa kutatua changamoto za kimaendeleo ikizingatiwa kwamba maendeleo yaliyopatikana hayaendani na raslimali za asili zilizopo nchini.
Pengine Maoni ya Makada hao ni fursa nyingine ya kuiwezesha CCM kuzidi kuwatumikia vyema Watanzania ili miaka 40 ijayo mwakani kusiwepo na utofauti wa kimtizamo pindi makada wa vyama vya siasa watakapokuwa wakitoa tena maoni yao.
Kitaifa Sherehe za Miaka 39 ya Kuasisiwa Chama cha Mapinduzi CCM kwa mwaka huu, zilizinduliwa Visiwani Zanzibar na Dkt.Ali Mohamed Shein ambae ni Makamu Mwenyekiti wa CCM Taifa na kilele chake kinahitimishwa Mjini Singida katika Uwanja wa Namfua ambapo zitahitimishwa na Mwenyekiti wa Chama hicho Taifa Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete.

STATEMENT BY UNFPA EXECUTIVE DIRECTOR, DR. BABATUNDE OSOTIMEHIN, ON THE ZIKA VIRUS

Press Conference by Dr. Babatunde Osotomehin, Executive Director, United Nations Population Fund (UNFPA), to brief on the General Assembly High-level event on the Demographic Dividend and Youth Employment.UNFPA, the United Nations Population Fund, is closely monitoring the outbreak of the Zika virus and warning about its potentially adverse effects on the health of women and babies, particularly in Latin America. We are also closely monitoring its possible spread to other regions.
UNFPA will continue to lead efforts to promote widespread information about the virus and about voluntary family planning. Given reported cases of Zika virus transmission through sexual contact, the role of UNFPA as the world’s leading agency on reproductive and maternal health, and the biggest public sector supplier of family planning commodities, including condoms, is ever more pertinent.
Women and girls should be able to make informed decisions about their reproductive health and family planning methods, and to protect themselves and their babies if they decide to be pregnant. UNFPA will continue to work with countries around the world to scale up access to information and to a wide range of voluntary family planning commodities so that women can make informed decisions and protect themselves.

Kambi ya Upinzani yatangaza Mawaziri wake

index 
(Na Raymomd Mushumbusi-Dodoma)
…………………………………………..
Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni Mhe Freeman Mbowe Mbunge wa Hai (CHADEMA) ametangaza rasmi Baraza la Mawaziri vivuli litakalosaidiana na Serikali katika kuendesha shughuli za kimaendeleo.
Akitangaza Mawaziri hao vivuli kiongozi huyo wa Kambi Rasmi ya Upinzani amesema anawaomba Mawaziri wa Wizara husika kuwapa ushirikiano wale wote walioteuliwa kuwa Mawaziri vivuli katika Kambi ya Upinzani ili kupeleka mbele gurudumu la maendeleo nchini.
Waliotangazwa Katika Orodha hiyo ni Pamoja na Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi, Utumishi na Utawala Bora Jaffar Michael, Manaibu wake ni Joseph Nkundi na Ruth Mollel, Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira Ali Saleh Abdalla na Naibu wake ni Pauline Gekul, Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu: Sera, Bunge, Kazi Vijana, Ajira na Walemavu Esther Bulaya na Manaibu ni Yusuph Makame na Maftah Abdalla, Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi ina mawaziri wawili ambao ni Magdalena Sakaaya na Emmaculate Swari Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Inj. James Mbatia na Naibu Waziri Willy Kombucha.
Aidha ameendelea kuwataja Mawaziri wengine kuwa ni Waziri wa Fedha na Mipango Halima Mdee na Naibu Waziri ni David Silinde, Waziri wa Nishati na Madini
John Mnyika na Naibu Waziri ni John Heche, Waziri wa Katiba na Sheria Tundu Lissu na Naibu Waziri Abdalla Mtolela, Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afika Mashariki, Kikanda na Kimataifa Peter Msigwa na Naibu Waziri Riziki Shaghal, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Juma Omari na Naibu Waziri Mwita Waitara, Waziri ya Mambo ya Ndani Godbless Lema na Naibu Waziri Masoud Abdalla, Waziri ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Wilfred Lwakatare na
Naibu Waziri Salum Mgoso.
Wengine walioteuliwa katika Baraza kivuli ni Waziri wa Maliasili na Utalii Esther Matiko na Naibu Waziri Cecilia Pareso, Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Anthony Komu na Naibu Waziri Cecil Mwambe, Waziri wa Elimu, Sayansi Teknolojia na Ufundi Suzan Lyimo Naibu Waziri Dkt. Ali Suleiman Yusuph, Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Godwin Mollel na Naibu Waziri Zubeda Sakul, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Joseph Mbilinyi na Naibu Waziri Devotha Minja na Waziri wa Maji na Umwagiliaji Hamidu Hassan na Naibu Waziri Peter Lijualikali.

LIGI KUU YA VODACOM RAUNDI YA 18 WIKIENDI HII

vpl18Ligi Kuu ya Vodacoma Tanzania bara raundi ya 18 inatarajiwa kuendelea wikiendi hii kwa michezo nane kuchezwa katika viwanja mbalimbali nchini, Jumamosi ukichezwa mchezo mmoja na Jumapili kuchezwa kwa michezo saba.
Jumamosi ligi ya kuu ya Vodacom itaendelea kwa mchezo mmoja tu, ambapo katika uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga, African Sports watawakaribisha Stand United kutoka mkoani Shinyanga.
Michezo saba itachezwa siku ya Jumapili ambapo maafande wa JKT Ruvu watakuwa wenyeji wa Young Africans katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam, Mbeya City dhidi ya Tanzania Prisons uwanja wa Sokoine jijini Mbeya, na Ndanda FC watawakaribisha Mtibwa Sugar katika uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini Mtwara.
Kagera Sugar watacheza dhidi ya Simba SC katika uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga, Azam FC watawakaribisha Mwadui FC uwanja wa Chamazi, Majimaji dhidi ya Mgambo uwanja wa Majimaji mjini Songea na Toto Africans watawakaribisha Coastal Union uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.

MATUKIO KUTOKA BUNGENI MJINI DODOMA

5
Waziri mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Mbunge wa Ilemela na Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angelina Mabula kwenye  jengo la Utalwala la Bunge mjini Dodoma Februari 5, 2016.
6
Waziri Mkuu, Kassim Majliwa akisalimiana na Mbunge wa Longido, Onesmo Ole- Nangole kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma Februari 5, 2016.
7
Waziri Mkuu, Kassim Majliwa akisalimiana na Mbunge wa Simanjiro , James Ole Millya (kulia)kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma Februari 5, 2016. Katikati ni Mbunge wa longido, Onesmo Ole Nangole.
8
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari (katikati) na Mwenyekiti wa Baraza la Vijana la CHADEMA (BAVICHA), Patrobas katambi (kulia) kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma Februari 5, 2016.
9
Waziri Mkuu, Kassim Majliwa akizungumza na Mbunge wa Arumeru Mashariki Joshua Nassari  kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma Februari 5, 2016.
(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

JAJI MKUU WA ZANZIBAR ATANGAZA MAADHIMISHO YA WIKI YA SHERIA ZANZIBAR

1
Jaji Mkuu wa Zanzibar Omar Othman Makungu akizungumza na waandishi wa habari Ofisini kwake Vuga, Mjini Zanzibar, kuhusiana  na maadhimisho ya  wiki ya Sheria Zanzibar iliyoanza tarehe 5 mwezi huu.
3Rais wa Wanasheria Zanzibar Omar Saidi akitoa ufafanuzi kuhusu jumuiya hiyo inavyotoa huduma za kisheria kwa wananchi kwenye mkutano ulioitishwa na Jaji Mkuu wa Zanzibar uliozungumzia wiki ya sheria Zanzibar.
2 Baadhi ya Waandishi wa Habari walioshiriki mazungumzo ya Jaji Mkuu wa Zanzibar kuhusu wiki ya Sheria Zanzibar  inayoanza tarehe 5 mwezi huu wakisikiliza kwa makini mazungumzo hayo.
4Hakimu anaeshughulikia kesi za watoto katika Mahakama ya Vuga Mjini Zanzibar Sabra Ali Mohd akielezea changamoto zinazoikabili kesi za watoto kwenye mkutano huo.
PICHA NA ABDALLA OMAR-HABARI MAELEZO ZANZIBAR

MATUKIO KATIKA KIKAO CHA BUNGE MJINI DODOMA

1
Waziri wa fedha na Mipango Mhe. Dkt Philip Mpango (Kulia) pamoja na Waziri wa Elimu,Ufundi,Sayansi na Teknolojia Mhe. Prof Joyce Ndalichako wakiwasili katika ukumbi wa Bunge kushiriki kikao cha 9 cha Bunge la 11 linaloendelea Mjini Dodoma.
2
Askari wa Bunge akiweka Siwa katika ukumbi wa Bunge kuashiria kuanza kwa kikao cha 9 cha Bunge la 11 linaloendelea Mjini Dodoma.
3
Naibu Spika wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt Tulia Ackson akiongoza kikao cha 9 cha Bunge la 11 linaloendelea Mjini Dodoma.
4
Naibu wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt Ashatu Kijaji wakatiakitoa Taarifa ya Utendaji wa  Soko la Bima Nchini kwa kipindi cha Mwaka unaoishia tarehe 31 Desemba,2014 wakati wa  kikao cha 9 cha Bunge la 11 linaloendelea Mjini Dodoma.
5
Waziri wa Elimu,Ufundi,Sayansi na Teknolojia Mhe. Prof Joyce Ndalichako akiwasilisha Taarifa ya mwaka ya chuo Kikuu Cha Dodoma kwa mwaka wa Fedha 2013/2014 katika kikao cha 9 cha Bunge la 11 linaloendelea Mjini Dodoma.
6
Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi akiteta jambo na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa Mhe.Dkt Hussein Ali Mwinyi wakati wa katika kikao cha 9 cha Bunge la 11 linaloendelea Mjini Dodoma.
Picha na Raymond Mushumbusi MAELEZO

JESHI LA POLISI LIMEJIPANGA KUIMARISHA ULINZI WAKATI WA UPIGAJI KURA KWENYE UCHAGUZI WA MARUDIO ZANZIMBAR.

index2 
Na Maanja Mabula  –Pemba
…………………………………………………
Kamishna wa Jeshi la  Polisi Zanzibar Hamdan Omar Makame amesema kwamba Jeshi hilo limejipanga kuimarisha ulinzi katika maeneo yote ya Unguja na Pemba wakati wa upigaji kura kwenye uchaguzi wa marudio .
 Akizungumza na gazeti hili Kisiwani Pemba Kamishna Hamdan amewatoa hofu  wananchi kuwa hakuna  mwananchi  mwenye sifa ya kupiga kura ambaye hataweza kwenda kupiga kura tarehe 20 machi mwaka huu wakati wa uchaguzi wa marudio  kutokana na sababu za vitisho .
Amesema kwamba tayari Jeshi la Polisi limeanza kutengeneza mazingira ambayo yatawaweza wananchi kila mmoja kuwa huru na kuhakikisha kuwa usalama wa nchi utaendelea kudumishwa .
Katika mazungumzo na gazaeti hili katika Makao Makuu wa Jeshi hilo Mkoa wa Kaskazini Pemba , Kamishna Hamdan amefahamisha hakuna mwananchi ambaye hatapiga kura kutokana na vitisho , labda aache kwa sababu zake mwenyewe .
“Hakuna mwananchi ambaye atapata fursa ya kupiga kura kwa sababu za vitisho , labda yeye asiende kwa sababu anazozijua yeye , lakini sio suala la vitisho ulinzi utaimarishwa maeneo yote ya Unguja na Pemba ”alisisitiza Hamdan .
Aidha Kamishna Hamdan amesema pamoja na kazi ya ulinzi wa wananchi na mali zao  kuwa ni Polisi , lakini iko haja kwa wananchi nao kuwapa ushirikiano askari pindi wanapobaini kuwa viasharia vya vitisho au uvunjifu wa amani .
Ameeleza kwamba ni kazi ya Jeshi la Polisi kuona  wanannchi wanaishi kwa amani katika nchi yao na wanafanya mambo kwa mujibu wa sheria , na kuongeza tayari changamoto zinazojitokeza ikiwemo vitisho wanazifahamu na wanazifanyia kazi ili zisilete athari wakati wa zoezi la uchaguzi .
“Niwahakikishie wananchi kwamba changamoto  zinazojitokeza ikiwemo vitisho tunazifahamu  , na tunashukuru wanazisema wazi wazi , labda niwahakikishie wananchi tumejipanga kuzikabili ili zisileta madhara  kabla na baada ya uchaguzi huo ”alifahamisha .
Kamishna Hamdan  pia ameeleza  kwamba Jeshi limejipanga pia kubadilisha mfumo wa kusimamia ili changamoto zilizojitokeza katika uchaguzi uliofanyika 25, oktoba mwaka jana wazigeuze kuwa fursa .
Akizungumza ulinzi katika maeneo ya Visiwa Vidogo vidogo , amesema kwamba watawatumia askari shehia kutoa taarifa ili waweze kuyafikia maeneo yote huku akisisitiza kwamba namba za simu za makanda wa Polisi Mikoa yote ziko wazi na zinafahamika na wananchi waliowengi .
“Sisi tupo wengi na maeneo yote tunayafahamu , kwa hili tutawatumia zaidi askari wetu wa shehia na kikubwa zaidi ni kwamba makamanda wote wa mikoa Zanzibar namba zao za simu ziko wazi muda wote wananchi wanatakiwa kuwapigia na kuwaeleza changamoto zinazowakabili ”alieleza.
Hata hivyo alisema kwamba Jeshi la Polisi litafanya kazi kwa karibu na Serikali za  Shehia kwa kuwatumia masheha na kamati zao kuhakikisha taarifa zote za uvunjifu wa amani zinaripotia na zinachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria .

Geita nayo yachomoza Tamasha la Pasaka

index 
Na Mwandishi Wetu
…………………………………….
KAMATI ya Maandalizi ya Tamasha la Pasaka imeiteua Wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga kuwa eneo mojawapo litakalofikiwa na tamasha hilo linalotarajia kufanyika Machi 28 Wilayani humo.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi ya Tamasha la Pasaka 2016, Alex Msama Kahama ni eneo la tatu litakalofikiwa na Tamasha la Pasaka mwaka huu.
Msama alisema wamepokea idadi kubwa ya maombi kutoka kwa wakazi wa Wilaya hiyo kama ilivyokuwa mikoa ya Geita na Mwanza.
Msama alisema Tamasha hilo kwenye mikoa ya Geita litafanyika Machi 26 huku Mwanza litafanyika Machi 27 na kumalizia Kahama.
“Kamati yangu imepokea idadi kubwa ya maombi kutoka mikoa hiyo mitatu, hivyo hapana budi kuikubalia kwa sababu tunafanya kazi ya Mungu kupitia muziki wa Injili hasa waimbaji mahiri wa muziki huo,” alisema Msama.
Msama alitumia fursa hiyo kwa wakazi wa mikoa ambayo imefanikiwa kupata baraka ya kufikiwa na tamasha hilo na maeneo ya karibu kujitokeza kwa wingi kwa sababu ya umuhimu wa tamasha hilo kwa jamii hasa katika maeneo ya wenye uhitaji maalum kama yatima, walemavu na wajane.
“Hili Tamasha lina umuhimu wake hasa kuzungumza na Mungu sambamba na kufikisha matakwa ya jamii yenye uhitaji maalum ambao hawana pa kukimbilia,” alisema Msama.

Serikali yatoa tamko kuhusu udhalilishaji wa mwanafunzi wa kitanzania India

images(Na Raymond Mushumbusi-MAELEZO)
…………………………………..
Serikali imetoa tamko la kulaani kitendo kilichotokea nchini India kwa mwanafunzi wa kike wa kitanzania kuvuliwa nguo na kutembezwa barabarani ambapo Serikali kupitia Wizara ya Mambo ya Nje,Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na kimataifa imetoa tamko la kulaani suala hilo kwa kuitaka Serikali ya india kuchukua hatua.
Akitoa tamko hilo Bungeni Mjini Dodoma Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa Balozi Dkt Augustine Mahiga amesema ni kweli kwamba kuna mwanafunzi wa kike wa kitanzania alifanyiwa kitendo cha udhalilishaji nchini India kwa kuvuliwa nguo na kutembezwa barabarani suala ambalo lilizua mijadala mikubwa nchini kuhusu udhalilishaji huo.
“Wizara yetu imezungumza na Balozi wa India nchini na kumweleza ni kwa jinsi gani watanzania wamefadhaika na kusononeshwa na kitendo alichofanyiwa mtanzania mwenzao huko India na Balozi alituhakikishia kwamba amewasiliana na Waziri wa Mambo ya Nje wa nchi yake na kusema Serikali ya India kwa kushirikiana na Jeshi la polisi nchini humo wamefanikisha kuwakamata wote waliohusika na kitendo hicho na kuwafikisha mahakamani kujibu mashataka hayo”
“ Pia Serikali ya India imeahidi kutoa ulinzi kwa wanafunzi wa kitanzania na wenye asilia ya Afrika wanaosoma huko ili kuwalinda na kuwaepusha na vitendo hivyo vinavyofanya na raia ambao hawana nia njema kwa mahusiano mazuri ya kimataifa yaliyopo kati ya India na Tanzania”Alisema Mhe. Mahiga.
Serikali ya Tanzania imekuwa na mahusiano mazuri na Serikali ya India kwa miaka mingi sasa na kutokana na kitendo hiki kilichotokea nchini India,Waziri wa Mambo ya Nje ya India amefatana na Balozi wa Tanzania nchini humo kwenda Mji wa Bangalo ili kuongea na wanafunzi wakitanzania na wale wenye asili ya Afrika wanaosoma huko ili kujenga mahusiano mazuri na wazawa ikiwa ni jitihada za kupunguza vitendo hivyo kutokea mara kwa mara.

Waganga wanaochochea mauaji ya walemavu wa ngozi kushughulikiwa

index1Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe.Hamad Yussuf Massauni akijibu hoja mbalimbali kuoka kwa Wabunge mbalimbali katika kikao cha 9 cha Bunge la 11 linaloendelea Mjini Dodoma.
………………………………………………………………………………
Na Raymond Mushumbusi MAELEZO
Serikali kupitia Jeshi la Polisi imekua ikifanya operesheni maalum za mara kwa mara za kukamata waganga wa jadi wanaopiga ramli chonganishi ambazo ni kichocheo kikubwa cha ukatili dhidi ya walemavu wa ngozi nchini.
Akijibu swali la Mhe.Mgeni Jadi Kadika Mbunge wa Viti Maaalum(CUF) lililouliza Serikali ina mpango gani wa kuwalinda na kuhakikisha usalama wa maisha ya watu wenye ulemavu wa ngozi,Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe.Hamad Yussuf Massauni amesema Serikali imeanzisha vituo vya kuwahudumia watu wenye ulemavu wa ngozi ambavyo vimesaidia kuimarisha ulinzi ikiwa ni pamoja na Polisi kuwatumia Polisi Jamii kutoa elimu kwa umma juu ya madhara ya vitendo vya kikatili vya mauaji na kujeruhi vinavyofanywa na baadhi ya watu kwa msukumo wa imani potofu za ushirikina.
“Kwa takwimu halisi tulizonazo tangu mwaka 2006 mpaka 2015 jumla ya mauaji ya walemavu wa ngozi 43 yametokea na jumla ya watuhumiwa 133 walikamatwa kuhusika na vitendo hivyo na watuhumiwa 19 walihukumiwa adhabu ya kifo”
“ Katika kupambana na vitendo hivi Jeshi la Polisi linakumbwa na changamoto mbalimbali zikiwemo uhaba wa askari katika kuhudumia wananchi ambapo kwa Tanzania askari mmoja anahudumia wananchi 1000 mpka 1500 ikiwa ni nje ya matakwa ya kimataifa ya askari mmoja kuhudumia wananchi 400 mpka 450 na uhaba wa magari kwa ajili ya doria mbalimbali ambapo takribani magari 387 yamegawanywa katika maeneo mbalimbali nchini ili bado tunaendelea kupambana na kutatua changamoto hizi kadri ya bajeti iyakavyoruhusu” Alisema Mhe.Massauni.
Wizara kupitia Jeshi la Polisi ikishirikiana na Kamati za Ulinzi na Usalama za Vijiji,Kata,Wilaya, na Mikoa imeanzisha vikosikazi(TASK FORCES) hususani kwenye Mikoa na Wilaya zilizokithiri matukio ya ukatili dhidi ya walemavu wa ngozi ambapo Vikosikazi hivyo hukusanya taarifa za kiintelejensia na kuzifanyia kazi.

Billioni 60 kufufua General Tyres Arusha

index
Waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji Mhe. Charles John Mwijage akijibu hija mbalimbali toka kwa wabunge katika kikao cha 9 cha Bunge la 11 linaloendelea Mjini Dodoma.
Picha na Raymond Mushumbuai MAELEZO.
………………………………………………………………….
Shillingi Billioni 60 zinategemea kutumika kufufua kiwanda ya matairi cha General Tyres kilichopo Jijini Arusha ambacho kimesharudi mikononi mwa Serikali, na fedha hizo zitatumila kurekebisha mitambo ya umeme ya kiwanda hicho na kupata mitambo mipya itakayoendana na teknolojia ya utengenezaji wa matairi duniani.
Akijibu swali la Mhe. Joshua Nassari Mbunge wa Arumeru Mashariki (CHADEMA) lililouliza ni lini serikali itafufua kiwanda cha matairi cha General Tyres kilichopo Jijini Arusha kwani ni tegemeo kwa ajira kwa wananchi wa Jijini la Arusha,Waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji Mhe.Charles John Mwijage amesema kiwanda hicho kimesharudi mikononi mwa Serikali na wako mbioni kukifufua ili kianze kufanya kazi ya kuzalisha matairi nchini.
“ Tumeanzisha viwanda nchi ili kuzalisha bidhaa na kutoa ajira kwa watanzania na sio kuwatesa wananchi kwa kukosa ajira au kuagiza bidhaa ambazo tunaweza kuzalisha hapa hapa nchini, hivyo basi Serikali kupitia Wizara yangu tutatenga fedha kwa ajili ya kufufua kiwanda hiki ili kianze kufanya kazi mara moja”
“ Sio tu tutafufua kiwanda cha General Tyres pekee bali tunafatilia viwanda vyote ambavyo vimekiuka sheria na kanuni kwa kutoviendeleza viwanda hivyo ili kuvirudisha mikononi mwa Serikali au kuwatafuta wawekezaji wengine watakaoweza kuviendesha viwanda hivyo” Alisema Mhe. Mwijage.
Aidha Mhe. Charles John Mwijage amesema ni kweli makampuni mengi yaliyobinafsishwa hayakufanya vizuri katika uendeshaji wake ukiacha mifano ya makampuni machache yanayofanya vizuri yakiwemo Tanzania Breweries Limited (TBL),Morogoro Polyester 21st Century na Tanzania Cigarette Company Limited (TCC), hivyo Wizara yangu ikishirikiana na Msajili wa Hazina juu ya Viwanda ilifanya tathmini iliyoonesha kuwa mashirika mengi yaliyobinafsishwa hawakutekeleza mikataba ya mauziano kikamilifu.
Ameongeza kuwa lengo ni kuhakikisha makampuni yote haya yanazalisha kwa tija ili tupate bidhaa,kodi ya Serikali na ajira kwa wananchi wa Tanzania ili kutimiza adhma ya Mhe.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.John Pombe Joseph Magufuli ya kuwa na Tanzania yenye viwanda kwa maendeleo ya taifa.
Serikali kupitia Wizara yetu inaboresha mazingira ya uwekezaji hali itakayowajengea imani kwa wawekezaji na kupelekea kupanua zaidi shughuli zao za kibiashara na pia kuendeleza mpango wa Viwanda vidogo na vya kati unaoshirikisha SIDO na Halmashauri za Wilaya na Mikoa ili kuanzisha Viwanda vya Mkoa vya kuongeza thamani ya bidhaa za Kilimo,Uvuvi na ufugaji kupitia njia hii ajira nyingi zitaongezeka na kupunguza tatizo la ajira nchini.

MWAKALEBELA AKANUSHA TUHUMA DHIDI YAKE

 KUKANUSHA UPOTOSHAJI DHIDI YANGU
Na Ripota wa Sufianimafoto, Dar
Kumekuwa na upotoshwaji wa taarifa zinazosambaa juu ya aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa miguu nchini TFF, na Mkuuwa Wilaya ya Wanging’ombe, Fredrick Wilfred Mwakalebela, ambapo baadhi ya vyombo vya habari kama Magazeti na mitandao ya kijamii vimekuwa viripoti tofauti.
Akizungumza na mtandao huu, wa Sufianimafoto.com kwa njia ya simu, Mwakalebela alisema kuwa zimekuwepo taarifa za upotoshwaji dhidi yake baada ya kuibuka kesi ya mtuhumiwa aliyepandishwa Kizimbani mwenye jina linalofanana na lake mwenye jina la David John Mwakalebela (56).
Aidha Mwakalebela alisema kuwa Mtuhumiwa huyo, aliyewahi kuichezea timu ya Yanga ya jijini Dar es Salaam, na timu ya Taifa, wakati yeye akiwa ni Katibu Mkuu wa TFF, alipandishwa kizimbani yeye na aliyewahi kuwa Mr. Tanzania 2015, Muhammad Khalil (32) wakikabiliwa na mashitaka saba likiwemo la kuishi nchini bila kibali na kumsaidia Mshitakiwa kutoa taarifa za uongo.
Kutokana na kufanana kwa majina hayo,kumekuwepo na sintofahamu na usumbufu mkubwa kwa Mhe. Mkuu wa Wilaya huyo ya Wanging’ombe huku ndugu, jamaa na marafiki wakihaha huku na huko na wengine wakimpigia simu kwa mshituko, jambo ambalo si la kweli.
”Zimeene taarifa potofu juu yangu zikielekeza tuhuma hizo dhidi yangu kwa makusudi au kwa kutofahamu jambo ambalo ni Hatari kwa Mimi binafsi, familia na marafiki kwa ujumla, nawaomba wahusika wawe wakifuatilia undani wa stori yenyewe ili kupata uhakika kabla ya kuanza kueneza uzushi na kuzua taflani,
Aidha napenda kuwapa pole wanafamilia yangu, ndugu, jamaa na marafiki kwa usumbufu wote uliojitokeza kwao kutokana na sintofahamu hii na kusababisha kadhia dhidi yako”. alisema Mwakalebela
Mtuhumiwa David Mwakalebela, akiwasili Mahakamani,ambaye amefananishwa na Fredrick Mwakalebela.

Ziara ya Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano katika Kituo mahiri cha Taifa cha Kutunzia kumbukumbu

1
Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Faustin Kamuzora(wa pili kushoto) akisikiliza maelekezo kutoka kwa Meneja Mradi bw. Xiong Hazbin (Kushoto) na kulia ni Mkurugenzi wa TEHAMA Eng. Peter Philip katika ziara ya kutembelea kituo mahiri cha taifa cha kutunzia kumbukumbu kilichopo kijitonyama jijini Dar es Salaam.
3
Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Faustin Kamuzora(kushoto) akimsikiliza maelekezo kutoka kwa Mkurugenzi wa TEHAMA wa Wizara hiyo Eng. Peter Philip kuhusu mitambo ya kupozea umeme iliyoko katika kituo mahiri cha taifa cha kutunzia kumbukumbu kilichopo kijitonyama jijini Dar es Salaam.
4
Mitambo ya kupozea umeme iliyopo katika kituo mahiri cha taifa cha kutunzia kumbukumbu kijitonyama jijini Dar es Salaam.
5
Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Faustin Kamuzora(kulia) akiongozana na Mkurugenzi wa TEHAMA wa Wizara hiyo Eng. Peter Philip na baadhi ya maaafisa wa Wizara wakati wa ziara ya kukagua kituo mahiri cha taifa cha kutunzia kumbukumbu kilichopo kijitonyama jijini Dar es Salaam.
6
Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Faustin Kamuzora(kushoto) akipewa maelezo ya namna hali ya usalama inavyozibitiwa katika kituo mahiri cha taifa cha kutunzia kumbukumbu kilichopo kijitonyama jijini Dar es Salaam kutoka kwa Mkurugenzi wa TEHAMA Eng. Peter Philip .
7
Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Faustin Kamuzora(kushoto) akionyeshwa mitungi ya kuzimia moto Salaam kutoka kwa Mkurugenzi wa TEHAMA Eng. Peter Philip alipofanya ziara yake ya kutembelea kituo mahiri cha taifa cha kutunzia kumbukumbu kilichopo kijitonyama jijini Dar es .
8
Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Faustin Kamuzora(kushoto) akionyeshwa sehemu ya chumba cha kuhifadhia Jenereta kilichopo katika kituo mahiri cha taifa cha kutunzia kumbukumbu kijitonyama jijini Dar es Salaam ,kutoka kwa Mkurugenzi wa TEHAMA Eng. Peter Philip .
(Picha na Lorietha Laurence-Maelezo)

JUMUIYA YA MARADHI YA SARATANI ZANZIBAR YAAADHIMISHA SIKU YA SARATANI DUNIANI KWA MKUTANO WA WAANDISHI WA HABARI

1
Mwenyekiti wa Jumuiya ya maradhi ya saratani Zanzibar Dkt. Msafiri Marijani akizungumza na waandishi wa habari katika Ofisi ya Jumuiya hiyo Mpendae ikiwa ni maadhimisho ya siku ya saratani duniani, kushotoni kwake ni Mkurugenzi wa Utumishi na uendeshaji Wizaraya ya Afya,
2Baadhi ya waandishi wa habari wakimsikiliza Mwenyekiti wa Jumuiya ya maradhi ya saratani Zanzibar kwenye maadhimisho ya siku ya saratani Zanzibar.
3Mkurugenzi wa Utumishi na uendeshaji Wizaraya ya Afya Zanzibar ndugu Omar Mwinyi Kondo akizungumza na waandishi katika maadhimisho ya siku ya saratani duniani yaliyofanyika Ofisi ya Jumuiya Mpendae, (kulia)
4Picha ya pamoja ya mgeni rasmi katika maadhimisho ya siku ya saratani duniani ndugu Omar Mwinyi Kondo (kati) mwenye suti na baadhi ya viongozi na waandishi wa habari waliohudhuria.
PICHA NA MAKAME MSHENGA/MAELEZO ZANZIBAR
……………………………………………………………………………
RAMADHANI ALI/MAELEZO ZANZIBAR
Mwenyekiti wa Jumuiya ya maradhi ya Saratani Zanzibar Dkt. Msafiri Marijani ameitanabahisha jamii kwamba maradhi ya saratani yamekuwa janga linalosumbua dunia nzima kwa sasa na kila mmoja anawajibu wa kusaidia katika kukabiliana na maradhi hayo sugu.
Akizungumza na waandishi wa habari katika Ofisi ya Jumuiya hiyo Mpendae nje kidogo ya Mjini Zanzibar, ikiwa ni maadhimisho ya siku ya saratani duniani, Dkt. Marijani amesema mtu anaweza kujikinga na maradhi hayo iwapo hatua za mapema zitachukuliwa.
Amezitaja hatua zinazopaswa kuchukuliwa na wananchi katika kukabiliana na saratani kuwa ni kujenga mwamko wa kuchunguza afya mara kwa mara ili kugundua mapema iwapo mtu anazo dalili za maradhi hayo.
Amesema hatua nyengine ni kuacha kutumia bidhaa zinazotokana na tumbaku, ulevi wa kupindukia, kupunguza matumizi ya mafuta kwenye chakula, kutumia zaidi vyakula vya matunda na mbogamboga na kujenga tabia ya kufanya mazoezi kila siku.
Dkt. marijani amewakumbusha wananchi kuwa saratani ni uvimbe mpya kwenye mwili na baada ya muda mfupi huzalisha chembechembe zinazosababisha athari kubwa na kama haikuwahiwa mapema inasababisha donda kubwa na kuwa halitibiki tena.
“Saratani inaweza kuzuilika iwapo itawahiwa mapema, tuongezeni nguvu kukabiliana nayo vyenginevyo inaweza kuathiri wananchi wengi kwani gharama ya matibabu yake ni kubwa na wagonjwa wengi hushindwa na kupoteza maisha,” alisisitiza Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo.
Amesema saratani ya matiti na shingo ya kizazi ndizo zinaongoza kwa wanawake Zanzibar na saratani ya tenzi dume inaongoza kwa upande wa wanaume.
Mwenyekiti huyo wa Jumuiya ya maradhi ya Saratani Zanzibar, ambae ni Daktari bingwa wa uchunguzi wa saratani, amewaeleza waandishi wa habari kwamba mpaka hivi sasa hakuna takwimu rasmi za wagonjwa wa maradhi hayo Zanzibar lakini Hospitali ya Ocean Road ya Dar es salaam imekuwa ikipokea wagonjwa 1,000 kila mwaka kutoka Zanzibar mbali na wagonwa wengine wanaopelekwa nje ya nchi na wanaobakia majumbani kupatiwa dawa mbadala.
Amesema kutokana na kadhia hiyo mwaka 2013 ilianzishwa Jumuiya ya kupambana na saratani Zanzibar ikiwa na lengo la kutoa elimu kwa jamii juu ya njia za kujikinga na kuishauri serikali njia zinazofaa kupunguza ongezeko la maradhi hayo.
Ameitaka Serikali kuongeza wataalamu na dawa za kupunguza maumivu katika hospitali kuu ya Mnazimmoja na hospitali nyengine za Zanzibar kwani zimekuwa hazitoshi.
Akizungumza katika maadhimisho hayo, Mkurugenzi wa Utumishi na Uendeshaji Wizara ya Afya Ndugu Omar Mwinyi Kondo amewapongeza wanachama wa Jumuiya hiyo kwa juhudi kubwa wanayochukua kuelimisha jamii kujikinga na saratani.
Amewahakikishia viongozi wa Jumuiya hiyo kwamba Serikali itaanzisha utaratibu rasmi wa kuwasajili wagonjwa wa saratani na kuongeza huduma za matibabu Hospitali kuu ya Mnazimmoja hasa dawa za kupunguza maumivu na wataalamu.
ujumbe wa mwaka huu katika siku ya saratani duniani ni mimi na wewe tunaweza kujikinga na saratani.
IMETOLEWA NA HABARI MAELEZO ZANZIBAR

MWENYEKITI WA CCM DK. JAKAYA KIKWETE AWASILI MKOANI SINGIDA TAYARI KWA MAADHIMISHO YA MIAKA 39 YA CCM.

1
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM na Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. Jakaya Kikwete akisalimiana na Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Ndugu Abdulrahman Kinana wakati alipowasili mkoani Singida tayari kwa maadhimisho ya Miaka 39 ya kuzaliwa kwa CCM yanayotarajiwa kufanyika Februari 6 mwaka huu  siku ya Jumamosi kwenye uwanja wa Namfua mkoani humo, Kauli Mbiu ya maadhimisho ya mwaka huu ni “Kufanya Kazi”(PICHA NA JOHN BUKUKU-FULLSHANGWE-SINGIDA)
2
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM na Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. Jakaya Kikwete akisalimiana na viongozi mbalimbali wa chama cha Mapinduzi mkoani Singida wakati alipowasili mjini Singida.
3
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM na Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. Jakaya Kikwete akizungumza na Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Ndugu Abdulrahman Kinana  wa pili  kutoka kulia  baada ya kuwasili mjini Singida , Kutoka kushoto ni Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Mkuu wa mkoa wa Singida Mh. Parseko Kone.
4
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM na Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. Jakaya Kikwete akifurahia jambo na Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Ndugu Abdulrahman Kinana wakati walipokuwa na mazungumzao katikati ni Mkuu wa wilaya ya Singida Said Amanzi.
5 6
Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo akifurahia jambo na Kamanda wa polisi mkoa wa Singida ACP. Thobias Sedoyeka.
7
Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Ndugu Abdulrahman Kinana.
9

MUDHIHIRI M. MUDHIHIRI AZINDUA KITABU MWELE BIN TAABAN

8
 Kutoka kulia ni Msanii Mrisho Mpoto, Abdallah Mkumbila (Muhogo Mchungu), Mudhihir Mudhihir, Majid Mswahili Majidi na Masoud Kipanya wakizindua kitabu cha Mwele bin Taabani.
10
 Mudhihir Mudhihir ambaye ndio mtunzi wa kitabu hicho akielezea maudhui ya kitabu kwa ufasaha.
11
 Majid Mswahili, mchambuzi wa maswala ya kiuchumi,siasa na jamii kutoka katika Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam akisisitiza jambo wakati wa uzinduzi huo.
12
Abdallah Mkumbila (Muhogo Mchungu) akielezea baadhi ya vipengele vya kitabu huku akiwasihi watanzania kukisoma kitabu hicho kwani kina mafunzo kwa wanajamii.
…………………………………………………………………….
Na Mwandishi Wetu
Mudhihiri Mohamed Mudhihiri ambaye ni mwanasiasa mkongwe na mtunzi mahiri wa vitabu leo hii jijini Dar Es Salaam amezindua kitabu chake cha Riwaya ya Mwele Bin Taaban.
Kitabu cha Mwele bin Taabani, tayari ameshakiingiza sokoni, kimebeba uhalisia wa maisha ya Mtanzania wa hali ya chini ambaye anakumbana na madhila, ambayo msingi wake ni utawala na watawala wanaojali zaidi masilahi yao, kuliko ya wapiga kura wao.
‘Mwele bin Taabani’ ni riwaya inayoyaakisi magumu ya Watanzania wengi hasa wa vijijini ambao wanalima sana, lakini wanavuna kidogo huku wakikosa watu wa kuwasemea na kusikiliza matatizo yao pamoja na kuwapo kwa Serikali ambayo imekuwa ikikusanya kodi kila uchwao kwenye mazao yanayozalishwa na mafukara hao.
Ukifanikiwa kukisoma kitabu hicho na kukielewa, hakika utakubaliana na mtunzi wake kuwa amedhamiria kufikisha sononeko la wananchi masikini kwa viongozi Serikalini.
Kwa kulifahamu hilo, Mudhihiri kwa kauli yake amesema kitabu hicho kinafaa sana ndani ya Serikali ya awamu ya Tano inayoongozwa na Rais John Magufuli kwani ndiyo mkongojo mujarabu kwa masaibu ya Wanakazamoyo (Wananchi).
Mbali na kitabu cha Mwele bin Taabani, vingine vipo kwenye ngazi ya muswaada ambavyo ni Msaliti, Nyungu ya Mawe, Nasaha za Mswahili na Viungo vya Ushairi.
Kwa mujibu wa Mudhihiri, tafsiri ya Mwele ni mgonjwa. Mwele bin Taabani kwa muktadha wa riwaya hii si mwanadamu bali ni kadhia ya ustawi duni wa jamii ya Wanakazamoyo.
Pia kitabu hiki kinafaa mashuleni na vyuoni. EMAC wametaka kitumike kidato cha tano na sita na vyuoni pia na hivi sasa Wahadhiri nchini wameonesha dhamira ya kukitumia kitabu hiki katika fasihi kwa ngazi ya uzamili.
Mikakati inaendelea ili kukifikisha kwenye maeneo mbalimbali ya nchi kwa bei nafuu isiyozidi shilingi 6,500.

MADIWANI WA CHADEMA WALALAMIKA KUBURUZWA NA MSTAHILI MEYA WA JIJI LA MWANZA

John Pambalu ambae ni diwani wa Kata ya Butimba (Chadema) akiwasilisha mchango wake katika kikao cha baraza la madiwani Jijini Mwanza.
Na:George Binagi-GB Pazzo
Madiwani wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo
Chadema Jijini Mwanza, wamemlalamikia Mstahiki Meya wa Jiji hilo kwa madai ya kuliongoza kibabe baraza la Madiwani.
Wakizungumza baada ya kikao cha baraza la Madiwani kilichoketi hii leo, Madiwani hao wamelalamikia kitendo cha kuzuiliwa kujadili taarifa ya Kamati ya fedha iliyowasilisha katika kikao hicho
kwa madai kwamba jukumu la baraza hilo ni kupitisha taarifa hiyo na si
kuijadili.
Samwel Range ambae ni diwani wa Kata
ya Pamba pamoja na John Pambalu ambae ni diwani wa Kata ya Butimba (Wote
Chadema), wamesema wamesikitishwa kuona kanuni za vikao zikivunjwa huku
madiwani wakinyimwa fursa ya kujadili taarifa ya kamati ya fedha
iliyowasilishwa.
“Tumeshuhudia utawala wa kibabe
ukianza katika halmashauri yetu huku mhe.Mwenyekiti wa kikao (Meya) pamoja na
Mkurugenzi wake wakiamua kutofuata kanuni na kuamua kufuata matakwa yao
binafsi. Tumeletewa taarifa ya kamati ya fedha, wakati wa kujadili tunaambiwa hakuna
sababu ya kuijadili isipokuwa kuipitia na kuiidhinisha taarifa hiyo, kitu
ambacho madiwani wa Chadema na Upinzani tunakilalamikia”. Alisema Pambalu.
Nae Samwel Range amesema “Kamati ya
fedha haina mamlaka ya kuidhinisha chochote ndani ya halmashauri ya Jiji la
Mwanza. Inapaswa ilete taarifa yake na kuileta katika baraza la Madiwani ambapo
sisi tunauwepo wa kuikubali au kuikataa”.
Hata hivyo malalamiko hayo yamepingwa
na James Bwire ambae ndie Mstahiki Meya wa Jiji la Mwanza na diwani wa Kata ya
Mahina (CCM), ambapo amefafanua kwamba malalamiko ya madiwani wa Chadema hayana
msingi wowote ikizingatiwa kwamba taarifa iliyowasilishwa na kamati ya fedha
iliishajadiliwa ndani ya kamati hivyo hakukuwa na umuhimu wa kuijadili tena
ndani ya baraza la madiwani bali kuipokea na kuipitisha.
Baraza la Madiwani Jijini Mwanza linaundwa
na Madiwani 24 na linaongozwa na Chama cha Mapinduzi CCM kwa upande wa Mstahiki
Meya pamoja na Naibu Meya ambapo kuna Madiwani 19 kutoka CCM huku Chama cha
Demokrasia na Maendeleo Chadema kikiwa na Madiwani Watano.
Kutokana na Uwiano huyo, Madiwani wa Chadema
wanalalamika kuburuzwa katika baraza hilo kutokana na uchache wao, madai ambayo
hata hivyo yanapingwa na Madiwani kutoka CCM ambao wanasema suala lolote lenye
maslahi kwa umma linapewa nafasi sawa ndani ya baraza hilo bila kujadi itikadi
za vyama vya siasa. 
Kushoto ni Naibu Meya Jiji la Mwanza, Katikati ni Mstahiki Meya na Kulia ni Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza
Waheshimiwa Madiwani Jijini Mwanza
Waheshimiwa Madiwani Jijini Mwanza
Watendaji wa Idara mbalimbali Jijini Mwanza.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli Mgeni Rasmi Siku ya Sheria nchini, Asisitiza Ufanisi wa Mahakama na utoaji wa Haki kwa Wakati

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akipokewa na Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Mohamed Chande Othman leo jijini Dar es salaam wakati wa maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini. Rais, Dkt. John Magufuli alikua mgeni rasmi. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli (katikati) akisalimiana na Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson wakati wa maadhimisho ya Siku ya Sheria leo jijini Dar es salaam.
 Wimbo wa Taifa ukipigwa wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Sheria. Kulia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli (Kulia) akiwa na Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Mohamed Chande Othman 
Baadhi ya Viongozi waliohudhuria Maadhimisho ya Siku ya Sheria wakiwa wamesimama wakati wimbo wa Taifa ukipigwa. Kutoka kulia ni Jaji Mkuu wa Kenya Dkt. Willy Mutunga, Jaji Kiongozi wa Tanzania Mhe. Shaaban Lila (katikati) na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Said Mecki Sadiki.
Baadhi ya Viongozi wa vyombo vya ulinzi na usalama  nchini na wadau muhimu wa Mahakama waliohudhuria Maadhimisho ya Siku ya Sheria wakitoa heshima zao wakati wimbo wa Taifa ukipigwa.
Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Charles Rwechungura akitoa salam na ujumbe wa Chama hicho wakati wa maadhimisho ya Siku ya Sheria leo jijini Dar es salaam.
Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue (kulia) akifuatilia hotuba zilizokuwa zikitolewa na viongozi mbalimbali wakati wa maadhimisho ya Siku ya Sheria. Kulia kwake ni Mtendaji Mkuu wa Mahakama Bw. Hussein Katanga.
 Jaji Mkuu wa  Mkuu wa Tanzania Mhe. Mohamed Chande Othman akiwahutubia viongozi, mabalozi na wageni mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi waliohudhuria maadhimisho ya Siku ya Sheria.
Continue reading →

RAIS MAGUFULI AZINDUA MWAKA MPYA WA KIMAHAKAMA (SIKU YA SHERIA) JIJINI DAR ES SALAAM

5
Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Mohamed Chande Othman akisoma hotuba yake kabla ya kumkaribisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli  wakati wa uzinduzi wa Mwaka Mpya wa Mahakama katika Siku ya Sheria Duniani katika uwanja wa Mahakama mtaa wa Chimala eneo la Ocean Road jijini Dar es salaam leo Jumatano February 4, 2016.
7
6
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akihutubia wakati wa uzinduzi wa Mwaka Mpya wa Mahakama katika Siku ya Sheria Duniani katika uwanja wa Mahakama mtaa wa Chimala eneo la Ocean Road jijini Dar es salaam leo Jumatano February 4, 2016
PICHA NA IKULU

Bodi ya Filamu yafanya kikao cha mapitio ya Filamu ya “DADA”

3
Mkurugenzi Msaidizi wa Maendeleo ya Jamii kutoka Wizara ya Afya na Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bibi.Costancia Gabusa (katikati) akichangia mada wakati wa kikao cha kupitia Filamu ya “DADA” kilichofanyika katika ofisi za Bodi ya Filamu Tanzania leo jijini Dar es Salaam. Kikao hicho kimejumuhisha wajumbe kutoka Ofisi ya Uhamiaji Makao Makuu, Jeshi la Polisi, Wizara ya Afya na Maendeleo ya jinsia, wazee na watoto na TCRA.Kulia ni Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania Bibi. Joyce Fissoo na kushoto ni Afisa Utamaduni kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bw. Fredrick Mgaza.
2
Katibu Mtendaji waBodi ya Filamu Bibi. Joyce Fissoo akielezea jambo wakatika wa kikao kazi kwa ajili ya mapitio ya Filamu ya “DADA” iliyowasilishwa ofisini kwake kwa ajili ya ukaguzi leo jijini Dar es Salam.Kushoto ni Mtengenezaji na Mmiliki wa Filamu hiyo Bi. Christina Mroni.
  4
Wajumbe wa kikao cha mapitio ya Filamu ya “DADA” wakifuatilia Filamu hiyo leo jijini Dar es Salaam.
1
Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania Bibi. Joyce Fissoo (mwenye gauni la kitenge) akiwa na baadhi ya Wajumbe wa kikao cha mapitio ya Filamu ya “DADA” wakifuatilia Filamu hiyo leo jijini Dar es Salaam.Kushoto ni Muongozaji wa na Mmiliki wa Filamu hiyo Bi. Christina Mroni.
Picha na Frank Shija,WHUSM

No comments:

Post a Comment