Mjumbe
wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Mwenyekiti
wa CCM Taifa na Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kwenye Ofisi
ndogo ya CCM Lumumba jijini Dar es salaam leo Februari 02, 2016 wakati
Makamu wa Rais alipotembelea katika Ofisi hiyo (Picha na OMR)
Mtambuzi
wa miradi kutoka Wakala wa Nishati Vijini, Mhandisi Elneema Mkumbo
akitoa maelezo juu ya utekelezaji wa miradi ya REA, kwa Mkuu wa Shirika
la Kimataifa la Maendeleo la Sweden( SIDA) Maria Van Berlokom (
aliyeweka mikono kifuania) ambao ni miongoni mwa wafadhili wa miradi
hiyo akiwa na ujumbe wake pamoja na wadau wengine wa maendeleo ikiwemo
Shirika la Maendeleo la Ujerumani( GIZ) wakati wakikagua utekelezaji wa
miradi ya REA katika mikoa ya kanda ya kaskazini.
Muonekano
wa nyumba zilizounganishwa na huduma ya umeme unaotekelezwa na Wakala
wa Nishati vijijini REA katika kijiji cha Kwedizinga mkoani Tanga.
……………………………………………………………………………………
Na Mwandishi Wetu
Shirika
la Kimataifa la maendeleo la Sweden( SIDA), limeridhishwa na
utekelezaji wa miradi ya Umeme inayofahiliwa na Shirika hilo hususan
usambazaji wa umeme vijijini unaotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini
REA kwa kushirikiana na Shirika la Umeme nchini( Tanesco), katika
maeneo mbalimbali nchini.
Mkuu wa Shirika la Kimataifa la maendeleo la Sweden( SIDA) Maria Van Berlekom amesema hayo mara baada ya kuona maendeleo ya wananchi wa vijijini wakati wa ziara yake ya kutembelea utekelezaji wa miradi hiyo katika mikoa ya kanda ya kaskazini .
Mkuu wa Shirika la Kimataifa la maendeleo la Sweden( SIDA) Maria Van Berlekom amesema hayo mara baada ya kuona maendeleo ya wananchi wa vijijini wakati wa ziara yake ya kutembelea utekelezaji wa miradi hiyo katika mikoa ya kanda ya kaskazini .
VIONGOZI WA NGAZI YA VIJIJI WATAKIWA KUSHIRIKI KATIKA KUTOKOMEZA UGONJWA WA KIPINDUPINDU HADI KUFIKIA MACHI 30 MWAKA HUU
………………………………………………………………………
Na.Catherine Sungura_Dodoma
Viongozi
wote kuanzia ngazi ya vijiji wametakiwa kushiriki kikamilifu katika
kutokomeza ugonjwa wa kipindupindu hadi kufikia tarehe 30 machi mwaka
huu
Wito
huo umetolewa leo na waziri wa afya,maendeleo ya jamii,jinsia,wazee na
watoto,Ummy Mwalimu wakati alipokutana na kikosi kazi cha cha udhibiti
wa kipindupindu Mkoa wa Dodoma
“Kipindupindu
siyo suala ya afya peke yake,bali ni suala mtambuka hivyo sekta zote
zinapaswa kujumuika katika kupambana na kutokomezwa ugonjwa Huu
Ummy
alisema kipindupindu bado ni changamoto na nina janga hivyo kila mikoa
inatakiwa kuliwekea kipaumbele kwakuwa ugonjwa huo unaua kwa haraka
hivyo viongozi wote washiriki kikamilifu na si kuwaachia waganga.wakuu
wa mikoa au wilaya
Aidha
alisema licha ya kuwa na sheria ndogo Za kila halmashauri za kusimamia
usafi na mazingira lakini katika kudhibiti kuenea kwa kipindupindu
lazima liatakuja suala la kufungia biashara hususan za
mbogamboga,matunda pamoja na chakula”suala la kukusanya mapato lipo na
litaendelea kuwepo lakini suala la kipindupindu linapoteza maisha,maisha
hayatafutwi lakini pesa zinatafutwa lakini ukikosea utapoteza maisha ya
watu wengi”
Ummy
alisema tangu kipindupindu kiingie nchini agosti mwaka jana,halmashauri
zimetumia pesa nyingi katika kutokomeza ugonjwa huo,lakini wangeweza
kuzuia mapema,pesa hizo.zingeenda kutatua tatizo la madawati katika
shule za msingi nchini
“Mnapoona
hamjaridhika na uendeshaji wa migahawa,msisite kuzifungia mara
moja,mapato mtakusanya haraka kwa kuwa na nguvu za pamoja baada ya
kutokomeza ugonjwa na kuweza kuingiza mapato mengi na kwa haraka tofauti
na kuwa na hilo tatizo
Hatahivyo alizitaka vikosi vyote vya mikoa nchi,kuwashirikisha wadau wote wakiwemo viongozi wa dini zote kuweza kuelimisha kuweza kutoa elimu ya jinsi gani ya kujikinga na ugonjwa wa kipindupindu kwa waumini wao
Hatahivyo alizitaka vikosi vyote vya mikoa nchi,kuwashirikisha wadau wote wakiwemo viongozi wa dini zote kuweza kuelimisha kuweza kutoa elimu ya jinsi gani ya kujikinga na ugonjwa wa kipindupindu kwa waumini wao
Mkoa
wa dodoma umetumia takribani shilingi milioni 124 za kitanzania toka
kipindupindu,hadi leo kuna wagonjwa wanne katika kambi ya kipindupindu
wilaya ya bahi,jumla ya wagonjwa 450 waliugua na vifo12,wilaya
zilizoathirika ni bahi,dodoma mjini na chamwino
Unilever yaendelea kuwazawadia wanafunzi shule mbambali
Mwanafunzi
wa darasa la tano wa shule ya msingi Maarifa, Gongo la Mboto, jijini
Dar es Salaam Ester Lawrence akipokea fulana kutoka kwa Balozi wa Blue
Band Neema Upendo shuleni hapo jana akiwa ni mmoja wa washindi wa
shindano la Blue Band ‘Kula Tano’ linalowamasisha wanafunzi kutambua
umuhimu wa kula vyakula vyenye virutubisho. Kushoto ni mwalimu wa
michezo Edith Katundu.
Mkutano wa kuhifadhi urithi wa utamaduni na ubunifu viwanda katika sekta ya utamaduni wafungwa jijini Dar es Salaam
Kaimu Mkurugenzi Idara ya Sanaa
kutoka Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Bi.Leah
Kihimbi(aliyesimama) akifunga mkutano wa urithi wa utamaduni na ubunifu
viwanda katika sekta ya utamaduni uliokuwa na dhumuni la kuwajengea
uwezo wasanii wa sanaa mbalimbali ili waweze kuhamasisha jamii katika
kuwaletea maendeleo chanya.
Washiriki wa mkutano wa urithi wa
Utamaduni na ubunifu Viwanda katika sekta ya utamaduni wakimskiliza kwa
makini Kaimu Mkurugenzi Idara ya Sanaa kutoka Wizara ya
Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Bi.Leah Kihimbi(hayupo Pichani) wakati
alipokuwa akifunga mkutano huo leo jijini Dar es Salaam.
Kaimu Mkurugenzi Idara ya Sanaa
kutoka Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Bi.Leah Kihimbi
akipokea moja ya zawadi ya mfuko kutoka umoja wa nchi za ulaya (EU)
kutoka kwa Afisa Miradi sehemu ya Uchumi na utawala kutoka umoja huo Bi
Alexa DU PLESSIS wakati wa mkutano wa urithi wa utamaduni na ubunifu
viwanda katika sekta ya utamaduni leo jijini Dar es Salaam.
Kaimu Mkurugenzi Idara ya Sanaa
kutoka Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Bi.Leah kihimbi
akiongea jambo na mkuu wa Idara ya uchumi na utawala kutoka umoja wa
nchi za ulaya(EU).Bw.Olivier Coupleux wakati wa mkutano wa urithi wa
utamaduni na ubunifu viwanda katika sekta ya utamaduni uliokuwa na
dhumuni la kuwajengea uwezo wasanii wa sanaa mbalimbali ili waweze
kuhamasisha jamii katika kuwaletea maendeleo chanya.
MANISPAA YA ILEMELA YAWEKA MSIMAMO WAKE DHIDI YA WAFANYABIASHARA WA HOTEL NA NYUMBA ZA KULALA WAGENI.
Mkurugenzi
wa Manispaa hiyo John Wanga akitoa ufafanuzi kwa Wanahabari juu ya tozo
ya Kodi ya Malazi kwa wafanyabiashara wa hotel na nyumba za kulala
wageni.
Wafanyabiashara wa Hotel na
Nyumba za Kulala Wageni katika Manispaa ya Ilemela Mkoani Mwanza, Wametakiwa kufanya
biashara zao kwa mjibu wa kanuni na sheria za biashara zao ikiwemo kulipa
ushuru na kodi mbalimbali kama ilivyoidhinishwa na Serikali.
Nyumba za Kulala Wageni katika Manispaa ya Ilemela Mkoani Mwanza, Wametakiwa kufanya
biashara zao kwa mjibu wa kanuni na sheria za biashara zao ikiwemo kulipa
ushuru na kodi mbalimbali kama ilivyoidhinishwa na Serikali.
Kauli
hiyo imetolewa hii leo na Mkurugenzi wa Manispaa hiyo John Wanga, katika Kikao
cha Viongozi wa Manispaa ya Ilemela na Wafanyabiashara hao, juu ya Ufafanuzi wa
Sheria ya Kodi ya Malazi, ambayo imeanza kukusanywa kwenye Hotel pamoja na
nyumba zote za kulala wageni.
hiyo imetolewa hii leo na Mkurugenzi wa Manispaa hiyo John Wanga, katika Kikao
cha Viongozi wa Manispaa ya Ilemela na Wafanyabiashara hao, juu ya Ufafanuzi wa
Sheria ya Kodi ya Malazi, ambayo imeanza kukusanywa kwenye Hotel pamoja na
nyumba zote za kulala wageni.
“Kama
una wajibu wa kulipa kodi Majengo, leseni ya biashara, mabango, ushuru wa
malazi, ushuru wa huduma na kodi nyingine zote zilizo kisheria, ni vyema
ukalipa bila kushurutishwa. Kutokufanya hivyo utatufanya twende kwenye ule
mkono mwingine ambao tusingependa sana kuutumia ambao ni kushurutishana”.
Amesema Wanga.
una wajibu wa kulipa kodi Majengo, leseni ya biashara, mabango, ushuru wa
malazi, ushuru wa huduma na kodi nyingine zote zilizo kisheria, ni vyema
ukalipa bila kushurutishwa. Kutokufanya hivyo utatufanya twende kwenye ule
mkono mwingine ambao tusingependa sana kuutumia ambao ni kushurutishana”.
Amesema Wanga.
Hata
hivyo licha ya agizo hilo, Wafanyabiashara katika Manispaa hiyo wameiomba
Serikali kuwapunguzia mzigo wa Kodi walionao kwa kuwa hivi sasa wanakabiriwa na
mzigo mkubwa wa kodi pamoja na Ushuru jambo ambalo wamesema ni tofauti na ahadi
ya kuondoa kero ya kodi mbalimbali aliyoitoa Mhe.Rais John Pombe Magufuli wakati
wa Kampeni zake.
hivyo licha ya agizo hilo, Wafanyabiashara katika Manispaa hiyo wameiomba
Serikali kuwapunguzia mzigo wa Kodi walionao kwa kuwa hivi sasa wanakabiriwa na
mzigo mkubwa wa kodi pamoja na Ushuru jambo ambalo wamesema ni tofauti na ahadi
ya kuondoa kero ya kodi mbalimbali aliyoitoa Mhe.Rais John Pombe Magufuli wakati
wa Kampeni zake.
“Kodi
zimekuwa nyingi sana kwa sisi wafanyabiashara wa Hotel na Guest Houses (nyumba
za kulala wageni), kwa mfano kodi ya majengo, leseni ya biashara, ardhi,
mabango na nyinginezo. Yaani nyumba moja inakuwa na kodi zaidi ya 11 sasa
itafika sehemu tutashindwa kufanya biashara. Sisi tuko tayari kulipa kodi ya majengo,
ardhi na leseni hivyo serikali iangalie namna ya kutusaidia”. Alisema Nuru
Ramadhan ambae ni mmoja wa wamiliki wa nyumba ya kulala wageni katika Manispaa
ya Ilemela na kuungwa mkono na wenzake.
zimekuwa nyingi sana kwa sisi wafanyabiashara wa Hotel na Guest Houses (nyumba
za kulala wageni), kwa mfano kodi ya majengo, leseni ya biashara, ardhi,
mabango na nyinginezo. Yaani nyumba moja inakuwa na kodi zaidi ya 11 sasa
itafika sehemu tutashindwa kufanya biashara. Sisi tuko tayari kulipa kodi ya majengo,
ardhi na leseni hivyo serikali iangalie namna ya kutusaidia”. Alisema Nuru
Ramadhan ambae ni mmoja wa wamiliki wa nyumba ya kulala wageni katika Manispaa
ya Ilemela na kuungwa mkono na wenzake.
Hawa
Waziri ambae ni Mwanasheria wa Manispaa ya Ilemela, amewasihi Wafanyabiashara
hao kuwa tayari kulipa kodi zilizopo kisheria, ikiwemo Kodi ya Malazi huku
wakiendelea kujenga hoja Serikalini ili Sheria hizo zifanyiwe marekebisho
bungeni na hatimae kupunguzwa.
Waziri ambae ni Mwanasheria wa Manispaa ya Ilemela, amewasihi Wafanyabiashara
hao kuwa tayari kulipa kodi zilizopo kisheria, ikiwemo Kodi ya Malazi huku
wakiendelea kujenga hoja Serikalini ili Sheria hizo zifanyiwe marekebisho
bungeni na hatimae kupunguzwa.
Awali
Wafanyabiashara wa Hotel na Nyumba za Kulala Wageni, walikuwa wakilipa Kodi ya
Malazi ambayo ni asilimia 20 ya mapato yanayotokana na malipo ya kila mteja,
kabla ya kodi hiyo kusitishwa na Serikali ambapo hata hivyo imerejeshwa tena na
Wafanyabiashara hao wanatakiwa kulipa kodi ya asilimia 10 ya mapato
yanayotokana na mteja badala ya 20 kama ilivyokuwa awali.
Wafanyabiashara wa Hotel na Nyumba za Kulala Wageni, walikuwa wakilipa Kodi ya
Malazi ambayo ni asilimia 20 ya mapato yanayotokana na malipo ya kila mteja,
kabla ya kodi hiyo kusitishwa na Serikali ambapo hata hivyo imerejeshwa tena na
Wafanyabiashara hao wanatakiwa kulipa kodi ya asilimia 10 ya mapato
yanayotokana na mteja badala ya 20 kama ilivyokuwa awali.
Kikao juu ya tozo ya Kodi ya Malazi kwa wafanyabiashara wa hotel na nyumba za kulala wageni kikielendelea
Afisa
biashara Manispaa ya Ilemela Mkoani Mwanza akitoa ufafanuzi juu ya tozo
ya Kodi ya Malazi kwa wafanyabiashara wa hotel na nyumba za kulala
wageni
Hawa
Waziri ambae ni Mwanasheria wa Manispaa ya Ilemela Mkoani Mwanza akitoa
ufafanuzi kwa wanahabari juu ya tozo ya Kodi ya Malazi kwa
wafanyabiashara wa hotel na nyumba za kulala wageni
Cyprian
Oyier ambae ni mmoja wa wafanyabiashara wa hotel Manispaa ya Ilemela
akiwasilisha hoja zake katika kikao juu ya tozo ya Kodi ya Malazi kwa
wafanyabiashara wa hotel na nyumba za kulala wageni
Lemmy
Muganyizi Mboyelwa ambae ni mmoja wa wamiliki wa nyumba ya kulala
wageni katika Manispaa ya Ilemela akiwasilisha hoja zake katika kikao
juu ya tozo ya Kodi ya Malazi kwa wafanyabiashara wa hotel na nyumba za kulala wageni
Nuru
Ramadhani ambae ni mmoja wa wamiliki wa nyumba ya kulala wageni katika
Manispaa ya Ilemela akiwasilisha hoja zake katika kikao juu ya tozo ya Kodi ya Malazi kwa wafanyabiashara wa hotel na nyumba za kulala wageni
Melikior
Fundi Minsa ambae ni mmoja wa wamiliki wa nyumba ya kulala wageni
katika Manispaa ya Ilemela akiwasilisha hoja zake katika kikao juu ya tozo ya Kodi ya Malazi kwa wafanyabiashara wa hotel na nyumba za kulala wageni
Wafanyabiashara
wa hotel na nyumba za kulala wageni katika Manispaa ya Ilemela wakiwa
katika kikao cha ufafanuzi juu ya kuanza kutumika kwa kodi ya Malazi
Wafanyabiashara
wa hotel na nyumba za kulala wageni katika Manispaa ya Ilemela wakiwa
katika kikao cha ufafanuzi juu ya kuanza kutumika kwa kodi ya Malazi
Kushoto
ni Stella Lwakatare ambae ni Afisa Biashara Mkuu katika Manispaa ya
Ilemela Mkoani Mwanza akifafanua jambo kwenye kikao cha Wafanyabiashara wa hotel na nyumba za kulala wageni katika Manispaa ya Ilemela juu ya kuanza kutumika kwa kodi ya Malazi.
Katikani ni Mkurugenzi wa Manispaa hiyo John Paul Wanga na Kulia ni Peter Revelian ambae ni Mwekahazina wa Manispaa ya Ilemela.
Watumishi wa idara mbalimbali katika Manispaa ya Ilemela Mkoani Mwanza.
WAZIRI WA MAMBO YA NJE AUGUSTINE MAHIGA ALA KIAPO CHA UBUNGE LEO
Naibu Spika wa Bunge, Dkt Tulia
Ackson akimwapisha Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika ya
Mashariki na Kikanda, Augustono Mahiga , Bungeni mjini Dodoma Februari
2, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
UTEUZI – TRL
Waziri wa Ujenzi,
Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa amemteua Bwana Masanja
Kungu Kadogosa kuwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania
(TRL), ambako anakwenda kuchukua nafasi ya Mhandisi Elias Mshana ambaye
anastaafu hivi karibuni.
Kabla ya Uteuzi huo Bwana Masanja
Kadogosa alikuwa Mkurugenzi Idara ya Mikopo Benki ya Rasilimali
Tanzania (TIB). Uteuzi huo unaanza mara moja.
Imetolewa na;
Kitengo cha Mawasiliano Serikalini.
02 Februari, 2016
MALINZI AMPONGEZA KIKWETE
“Familia
ya mpira wa miguu inajua umuhimu wa chanjo na hasa katika maendeleo ya
vipaji na wanamichezo kwa ujumla na jinisi chanjo inavyoweza kuwapa
watoto siyo tu fursa ya maendeleo bali pia haki ya kuishi” ilisema
sehemu ya barua hiyo iliyosainiwa na Rais wa TFF, Jamal Malinzi.
Katika
barua hiyo, Malinzi ameelezea furaha ya TFF kuona kiongozi wa Tanzania
akiongoza mapambano ya kuokoa afya na uhai wa kizazi cha sasa na kijacho
katika Afrika na dunia kwa ujumla.
“TFF
itaunga mkono juhudi zako ili kufanikisha malengo yaliyowekwa na
ushirika wa chanjo” ilimalizia barua hiyo ambayo nakala yake imetumwa
kwa Rais wa Caf, Issa Hayatou.
WANANCHI WA JIMBO LA BUMBULI WAMPONGEZA WAZIRI MAKAMBA
NA RAISA SAIDI, BUMBULI.
SERIKALI ya Tanzania imevunja rasmi mkataba na mwekezaji
wakiwanda cha kuzalisha Chai cha Mponde kilichopo wilayani Bumbuli
Mkoani Tanga na kuamuru kitwaliwe na kianze kazi mara moja.
SERIKALI ya Tanzania imevunja rasmi mkataba na mwekezaji
wakiwanda cha kuzalisha Chai cha Mponde kilichopo wilayani Bumbuli
Mkoani Tanga na kuamuru kitwaliwe na kianze kazi mara moja.
Akizungumza katika mkutano uliowajumuisha wadau wazao la
chai,Msajili wa Hazina Laurence Mafuru amesema kuwa kwa mamlaka
aliyopewa amevunja rasmi mkataba huo kwasababu Mwekezaji
aliyekuwepo kashindwa kutekeleza makubaliano yaliyoweka .
chai,Msajili wa Hazina Laurence Mafuru amesema kuwa kwa mamlaka
aliyopewa amevunja rasmi mkataba huo kwasababu Mwekezaji
aliyekuwepo kashindwa kutekeleza makubaliano yaliyoweka .
Mafuru alisema kuwa wamefikia uwamuzi huo kutokana na
kujiridhisha pamoja na kupitia mikataba walioingia na mwekezaji
huyo ndipo serikali imeamua ikirudishe kiwanda hicho mikononi
mwa Wizara ya Viwanda na Biashara ili utaratibu mpya wa
uendeshwaji wa kiwanda uanze huku Bodi ya Chai Tanzania
ukiendelea kukisimamia mpaka hapo serikali itakapotafuta mwekezaji
mwingine.
kujiridhisha pamoja na kupitia mikataba walioingia na mwekezaji
huyo ndipo serikali imeamua ikirudishe kiwanda hicho mikononi
mwa Wizara ya Viwanda na Biashara ili utaratibu mpya wa
uendeshwaji wa kiwanda uanze huku Bodi ya Chai Tanzania
ukiendelea kukisimamia mpaka hapo serikali itakapotafuta mwekezaji
mwingine.
Mei mwaka 2013, wakulima wa chai waliitisha mkutano na kumwalika
Mbunge wa Jimbo la Bumbuli Januari Makamba na kueleza kutokuwa na
imani na mwekezaji na Chama cha Wakulima wa Chai cha Usambara (UTEGA)
na kuamua kukifunga kiwanda licha ya Mbunge kuwasihi wasichukue uamuzi
huo wa hasira.
Mbunge wa Jimbo la Bumbuli Januari Makamba na kueleza kutokuwa na
imani na mwekezaji na Chama cha Wakulima wa Chai cha Usambara (UTEGA)
na kuamua kukifunga kiwanda licha ya Mbunge kuwasihi wasichukue uamuzi
huo wa hasira.
Tangu wakati huo jitihada nyingi zimefanyika zikiongozwa na Mheshimiwa
Makamba kuhakikisha kwamba kiwanda kinafunguliwa na wakulima wanauza
chai yao.
Makamba kuhakikisha kwamba kiwanda kinafunguliwa na wakulima wanauza
chai yao.
‘’ Tuliteseka kwa muda mrefu na leo Serikali imefanya uamuzi
wa kukirudisha kiwanda mikononi mwetu, Tunaishukuru Serikali kwa
kutusaidia sisi wananchi tulioteseka kwa muda mrefu ,” Alisema
Challes Ngovi ambaye ni mkulima wa chai Mponde.
wa kukirudisha kiwanda mikononi mwetu, Tunaishukuru Serikali kwa
kutusaidia sisi wananchi tulioteseka kwa muda mrefu ,” Alisema
Challes Ngovi ambaye ni mkulima wa chai Mponde.
Hata hivyo Mafuru alibainisha kuwa ucheleweshaji wa kukifungua
kiwanda hicho ulitokana na utaratibu uliokuwa ukifanywa na Serikali
na baada ya kujiridhisha ndipo ikaamua kumuandikia rasmi
barua Mwenyekiti wa Utega inayoonyesha kuvunjwa kwa mkataba huo
na kuamuru kiwanda kirudi Serikalini.
kiwanda hicho ulitokana na utaratibu uliokuwa ukifanywa na Serikali
na baada ya kujiridhisha ndipo ikaamua kumuandikia rasmi
barua Mwenyekiti wa Utega inayoonyesha kuvunjwa kwa mkataba huo
na kuamuru kiwanda kirudi Serikalini.
Kwa upande wake, Mbunge wa Bumbuli January Makamba alisema kwamba
kazi waliyomtuma wananchi ya kukirudisha kiwanda mikononi mwao
imekamilika ingawa imechukua muda mrefu.
kazi waliyomtuma wananchi ya kukirudisha kiwanda mikononi mwao
imekamilika ingawa imechukua muda mrefu.
Makamba ambaye pia ni Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais
anayeshughuliokia Mazingira na Muungano alitumia nafasi hiyo
kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Magufuli kwa
kuingilia kati mgogoro huo ambao umedumu kwa zaidi miaka mitatu
na hatimae kuumaliza.
anayeshughuliokia Mazingira na Muungano alitumia nafasi hiyo
kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Magufuli kwa
kuingilia kati mgogoro huo ambao umedumu kwa zaidi miaka mitatu
na hatimae kuumaliza.
Hata hivyo Mwenyekiti wa Umoja wa Wakulima wa Chai Usambara UTEGA
William Shelukindo aliilaumu serikali kutoka na uamuzi wake wa
kukitaifisha kiwanda hicho bila ya kutoa nafasi kwa mwekezaji kuweza
kujitetea kwani ni ameshindwa kuzalisha.
William Shelukindo aliilaumu serikali kutoka na uamuzi wake wa
kukitaifisha kiwanda hicho bila ya kutoa nafasi kwa mwekezaji kuweza
kujitetea kwani ni ameshindwa kuzalisha.
“Serikali katika hili imeshindwa kutupa nafasi ya kujitetea ili kuweza
kujua sababu za kushindwa kuzalisha ,lakini kwa sasa hatuna cha
kufanya zaidi ya kutekeleza matakwa yao”alisema Shelukindo.
kujua sababu za kushindwa kuzalisha ,lakini kwa sasa hatuna cha
kufanya zaidi ya kutekeleza matakwa yao”alisema Shelukindo.
Ambapo Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mwantumu Mahiza alisema kuwa siku 90 za
kupeleka malalamiko na utetezi kwa seriklai zilishatangazwaa na
kumalizika kilichobaki ni utekelezaji wa kanuni na taratibu za
serikali kukichukuwa kiwanda na kuanza uzalishaji .
kupeleka malalamiko na utetezi kwa seriklai zilishatangazwaa na
kumalizika kilichobaki ni utekelezaji wa kanuni na taratibu za
serikali kukichukuwa kiwanda na kuanza uzalishaji .
“Niwaombe wananchi hakikisheni mnazalisha zao hilo kwa wingi ili
kiwanda kiweze kufanyakazi na kuboresha uchumi wa kila mmoja
wenu,wilaya,mkoa na taifa kwa ujumla kwani Bumbuli mnategemea zao la
chai kwa kiasi kikubwa.
kiwanda kiweze kufanyakazi na kuboresha uchumi wa kila mmoja
wenu,wilaya,mkoa na taifa kwa ujumla kwani Bumbuli mnategemea zao la
chai kwa kiasi kikubwa.
Wakati huo huo,Wananchi waishio maeneo mbalimbali katika Jimbo la
Bumbuli wilayani Lushoto mkoani Tanga wamempongeza Waziri wa Nchi
Ofisi ya Makamu wa Rais anayeshughulikia Muungano na Mazingira kwa
hatua ya kuwasaidia kuishawishi serikali kukipatia ufumbuzi mgogoro wa
kiwanda cha chai cha Mponde.
Bumbuli wilayani Lushoto mkoani Tanga wamempongeza Waziri wa Nchi
Ofisi ya Makamu wa Rais anayeshughulikia Muungano na Mazingira kwa
hatua ya kuwasaidia kuishawishi serikali kukipatia ufumbuzi mgogoro wa
kiwanda cha chai cha Mponde.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti na mwandishi wa habari hizi, mmoja ya
wakulima hao,Swahiba Mbili alisema kuwa kufunguliwa utawasaidia
wananchi ambao walikuwa na changamoto ya mazao yao kuharibika shambani
kupata soko la uhakika ambalo linaweza kuwainua kimaisha.
wakulima hao,Swahiba Mbili alisema kuwa kufunguliwa utawasaidia
wananchi ambao walikuwa na changamoto ya mazao yao kuharibika shambani
kupata soko la uhakika ambalo linaweza kuwainua kimaisha.
Swahiba alisema kuwa wao kama wakulima pamoja na kuishukuru serikali
kutwaa kiwanda lakini wanamshukuru Januari Makamba kwa sababu hakuweza
kuwa mbali nao kwenye kipindi chote wakati kiwanda hicho kimefungwa na
kuaidi kumpa ushirikiano katika kipindi cha kuwatumikia wananchi hao.
kutwaa kiwanda lakini wanamshukuru Januari Makamba kwa sababu hakuweza
kuwa mbali nao kwenye kipindi chote wakati kiwanda hicho kimefungwa na
kuaidi kumpa ushirikiano katika kipindi cha kuwatumikia wananchi hao.
fastjet yaongeza ndege ya tano
Dar es Salaam, Januari
28, 2016-Fastjet
Tanzania imeongeza ndege nyingine aina ya Airbus A319 kwenye idadi ya ndege zake nne na hivyo kuliweka shirika hilo la ndege la
gharama nafuu kuendelea na mipango yake ya kupanuka.
28, 2016-Fastjet
Tanzania imeongeza ndege nyingine aina ya Airbus A319 kwenye idadi ya ndege zake nne na hivyo kuliweka shirika hilo la ndege la
gharama nafuu kuendelea na mipango yake ya kupanuka.
“Ndege
za fastjet kwa hivi sasa ni nne na zote zinatumika na ongezeko la ndege ya tano ni jibu kwenye mikakati yetu ya kupanuka pamoja na hitaji la kuongeza uwezo
wa kubeba kwenye safari zetu za ndani na za kimataifa”, alisema Meneja Mkuu wa fastjet Tanzania, John Corse.
za fastjet kwa hivi sasa ni nne na zote zinatumika na ongezeko la ndege ya tano ni jibu kwenye mikakati yetu ya kupanuka pamoja na hitaji la kuongeza uwezo
wa kubeba kwenye safari zetu za ndani na za kimataifa”, alisema Meneja Mkuu wa fastjet Tanzania, John Corse.
Ndege hiyo ya nyongeza inafanya jumla ya
nafasi inayokuwepo kwa siku kwenye safari kwa ajili ya wateja kufikia 1,000.
nafasi inayokuwepo kwa siku kwenye safari kwa ajili ya wateja kufikia 1,000.
Fastjet ilianza safari zake nchini mwaka 2012na hivi sasa inajiendesha kwa kutumia
ndege tano aina ya A319 kwenye mtandao
wake wa safari ambao unahusisha Dar es Salaam, Mbeya, Mwanza, Kilimanjaro na
Zanzibar na kuifanya ijikite kuufanya usafiri wa anga ndani ya Tanzania watu
wote waumudu.
ndege tano aina ya A319 kwenye mtandao
wake wa safari ambao unahusisha Dar es Salaam, Mbeya, Mwanza, Kilimanjaro na
Zanzibar na kuifanya ijikite kuufanya usafiri wa anga ndani ya Tanzania watu
wote waumudu.
Hali kadhalika ilianzisha safari za kimataifa
kwenda Entebbe nchini Uganda, Nairobi Kenya, Harare Zimbabwe, Johannesburg Afrika Kusini
na Lusaka nchini Zambia katika kipindi cha miaka mitatu ya kuendesha shughuli
zake.
kwenda Entebbe nchini Uganda, Nairobi Kenya, Harare Zimbabwe, Johannesburg Afrika Kusini
na Lusaka nchini Zambia katika kipindi cha miaka mitatu ya kuendesha shughuli
zake.
“Tangu tuanze safari zetu tumeshabeba abiria
zaidi ya 1,800,000 ambapo utafiti wetu unaonesha kuwa zaidi ya theluthi moja ya abiria wetu walikuwa ndio mara yao ya kwanza
kumudu kusafiri kwa ndege”, anasema
Corse.
zaidi ya 1,800,000 ambapo utafiti wetu unaonesha kuwa zaidi ya theluthi moja ya abiria wetu walikuwa ndio mara yao ya kwanza
kumudu kusafiri kwa ndege”, anasema
Corse.
Aliendelea kusema,
“kuongeza ndege nyingine kwenye safari zetu kunatupa fursa muhimu ya
kuongeza masafa kwa njia zetu zilizopo ili kukidhi
mahitaji ya wateja, na na inasaidia kwenye lengo letu la kuongeza njia
moja ya kimataifa kwenye mtandao wetu kwa mwaka huu 2016”.
mahitaji ya wateja, na na inasaidia kwenye lengo letu la kuongeza njia
moja ya kimataifa kwenye mtandao wetu kwa mwaka huu 2016”.
Hali kadhalika, Corse anabainisha kuwa ndege
hiyo mpya inamanisha kuwa fastjet ni sawia
na ni kubwa katika kutosheleza kupanuka kwa shughuli za fastjet.
hiyo mpya inamanisha kuwa fastjet ni sawia
na ni kubwa katika kutosheleza kupanuka kwa shughuli za fastjet.
Ndege hiyo A319 ambayo ni Airbus ni ya injini mbili ambazo zinatoa kiwango cha juu cha ufanisi
pamoja na kiwango cha chini kabisa cha madhara kwenye mazingira, ikiwa ni
nyongeza kwenye viwango vya juu vya hali
ya kuliwaza ndani ya ndege hiyo ya kisiasa.
pamoja na kiwango cha chini kabisa cha madhara kwenye mazingira, ikiwa ni
nyongeza kwenye viwango vya juu vya hali
ya kuliwaza ndani ya ndege hiyo ya kisiasa.
Ndege hiyo ina uwezo wa kubeba abiria 156 ambaop wanamudu viwango vya chini vya
kuendesha mtindo wa maisha wa gharama nafuu ambao unaendeshwa na Fastjet
Tanzania.
kuendesha mtindo wa maisha wa gharama nafuu ambao unaendeshwa na Fastjet
Tanzania.
Baadhi ya njia muhimu ambazo ndege hiyo mpya
itakuwa inahudumia ni njia mpya iliyoanzisjhwa hivi karibuni kati ya Dar es Salaam na Nairobi, Kilimanjaro na Nairobi na Dar es Salaam kwenda Zanzibar ambazo zote zilianza kwa mara ya kwanza Januari 11, 2016. njia hizi mpya zote ni kielelezo muhimu muda mrefu kwenye
upanuzi wa njia za fastjet kitaifa na
kimataifa.
itakuwa inahudumia ni njia mpya iliyoanzisjhwa hivi karibuni kati ya Dar es Salaam na Nairobi, Kilimanjaro na Nairobi na Dar es Salaam kwenda Zanzibar ambazo zote zilianza kwa mara ya kwanza Januari 11, 2016. njia hizi mpya zote ni kielelezo muhimu muda mrefu kwenye
upanuzi wa njia za fastjet kitaifa na
kimataifa.
Fastjet inatarajia
kuongeza ndege zaidi kwenye njia yake ya Kenya kutokana na mahitaji ya
wateja kuongezeka kunakosababisha na kumudu, usalama, kasi na huduma
kwa wakati, na hali
kadhalika imeshajionesha kuwa kuna matarajio ya kuzindua
safari kati ya Zanzibar na Nairobi
na hali kadhalika kati ya Dar es Salaam na Mombasa baadaye mwaka 2016.
kadhalika imeshajionesha kuwa kuna matarajio ya kuzindua
safari kati ya Zanzibar na Nairobi
na hali kadhalika kati ya Dar es Salaam na Mombasa baadaye mwaka 2016.
“Usafiri wa
anga unaoumudu ni muhimu kwenye kukuza uchumi wa Tanzanoa, hususani
kwenye kukuza sekta za biashara na utalii”, alisema
Corse.
Corse.
Hali kadhalika Corse alibainisha kuwa ndege hiyo mpya inamaanisha kwamba ndege za
Fastjet zitatosheleza kiasi cha kutosha kusaidia kwenye changamoto za usimamizi na uendeshaji iwapo
ndege moja miongoni mwake itakuwa haifanyi kazi au kama ipo kwenye matengenezo au ukarabati wa lazima.
Fastjet zitatosheleza kiasi cha kutosha kusaidia kwenye changamoto za usimamizi na uendeshaji iwapo
ndege moja miongoni mwake itakuwa haifanyi kazi au kama ipo kwenye matengenezo au ukarabati wa lazima.
MATUKIO YA PICHA KATIKA KIKAO CHA BUNGE MJINI DODOMA
Naibu Spika Mhe.Dkt Tulia Ackson
akiingia Bungeni tayari kuongoza Kikao cha 6 cha Mkutano wa pili wa
Bunge la 11 linaloendelea Mjini Dodoma.
Mhe. Balozi Dkt Augustine Maiga akuungia Bungeni tayari kwa kuapishwa.
Naibu Spika Mhe.Dkt Tulia Ackson akimwapisha Mhe. Balozi Dkt Augustine Maiga.
Naibu Spika Mhe.Dkt Tulia Ackson akiongoza Kikao cha 6 cha Mkutano wa pili wa Bunge la 11 linaloendelea Mjini Dodoma.
Waziri Mkuu Mhe.Kassim
Majaliwa,majaliwa akiteta jambo na Mwanasheria Mkuu wa Serikali
Mhe.George Masaju wakati kuongoza Kikao cha 6 cha Mkutano wa pili wa
Bunge la 11 linaloendelea Mjini Dodoma.
Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa
na Michezo Mhe.Nape Moses Nnauye akifatilia Kikao cha 6 cha Mkutano wa
pili wa Bunge la 11 linaloendelea Mjini Dodoma.
Waziri wa Maliasili na Utalii
Mhe.Prof Jumanne Maghembe akijibu hoja toka kwa Wabunge mbalimbali
katika Kikao cha 6 cha Mkutano wa pili wa Bunge la 11 linaloendelea
Mjini Dodoma.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa
Rais Muungano na Mazingira Mhe.January Makamba akijibu hoja toka kwa
Wabunge mbalimbali katika Kikao cha 6 cha Mkutano wa pili wa Bunge la
11 linaloendelea Mjini Dodoma.
Baadhi ya wageni wakifatilia Kikao cha 6 cha Mkutano wa pili wa Bunge la 11 linaloendelea Mjini Dodoma.
Picha na Raymond Mushumbusi MAELEZO
TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA KWA VYOMBO VYA HABARI
WAZEE WAWILI WAMEUAWA KIKATILI WILAYANI KYELA MKOANI MBEYA KUTOKANA NA IMANI ZA KISHIRIKINA.
MWANAFUNZI WA SHULE YA MSINGI MAPAMBANO JIJINI MBEYA AFARIKI DUNIA PAPO HAPO BAADA YA KUGONGWA NA GARI.
MWANAFUNZI WA SHULE YA MSINGI MAPAMBANO JIJINI MBEYA AFARIKI DUNIA PAPO HAPO BAADA YA KUGONGWA NA GARI.
MWENDESHA PIKIPIKI AFARIKI DUNIA KATIKA AJALI ILIYOHUSISHA GARI KUGONGANA NA PIKIPIKI.
KATIKA TUKIO LA KWANZA:
WAZEE WAWILI WAKAZI WA KITONGOJI CHA BULINDA WILAYA YA KYELA MKOANI MBEYA WALIOFAHAMIKA KWA MAJINA YA 1. GENELI KAPWELA [65] NA 2. RAHABU BUNGULU [70] WALIUAWA KWA KUKATWA NA VITU VYENYE NCHA KALI SEHEMU MBALIMBALI ZA MIILI YAO NA KISHA KUCHOMWA MOTO NA WANANCHI WALIOAMUA KUJICHUKULIA SHERIA MKONONI.
MIILI YA MAREHEMU ILIKUTWA KATIKA NYUMBA WALIMOKUWA WAKIISHI MNAMO TAREHE 01.01.2016 MAJIRA YA SAA 08:00 ASUBUHI HUKO KITONGOJI CHA BULINDA, KIJIJI/KATA YA MATEMA, TARAFA YA NTEMBELA WILAYA YA KYELA MKOA WA MBEYA.
KATIKA TUKIO HILO, GENELI KAPWELA ALIUAWA KWA KUTENGANISHWA KICHWA NA KIWILIWILI NA KUKATWA MKONO WA KUSHOTO NA VIUNGO HIVYO HADI SASA HAVIJULIKANI VILIPO NA RAHABU BUNGULU ALIUAWA KWA KUCHOMA NA KITU CHENYE NCHA KALI NA WANANCHI WALIOAMUA KUJICHUKULIA SHERIA MKONONI.
INADAIWA KUWA, WANANCHI HAO WALIVAMIA NYUMBA WALIYOKUWA WAKIISHI MAREHEMU KISHA KUWAKATA NA VITU VYENYE NCHA KALI NA BAADA YA KUTEKELEZA MAUAJI HAYO, WATU HAO WALIANGUSHA NYUMBA WALIYOKUWA WAKIISHA AMBAYO ILIKUWA IMEJENGWA KWA MIANZI NA KISHA KUICHOMA MOTO.
CHANZO CHA TUKIO HILO NI IMANI ZA KISHIRIKINA KWANI MAREHEMU WALIKUWA WANATUHUMIWA KULETA UGONJWA WA KIPINDUPINDU KIJIJI HAPO KWA NJIA ZA KISHIRIKINA. WATU WAWILI WAMEKAMATWA KWA MAHOJIANO KUHUSIANA NA TUKIO HILO AMBAO NI 1. ALIKO MWAMTOBE [47] MKAZI WA MATEMA NA 2. ALISOLOMON MWAMTOBE [49] MKAZI WA KITONGOJI CHA BULINDA.
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI MWANDAMIZI WA POLISI AHMED Z. MSANGI ANATOA WITO KWA JAMII KUACHA IMANI POTOFU ZA KISHIRIKINA KWANI ZINA MADHARA MAKUBWA KATIKA JAMII.
WAZEE WAWILI WAKAZI WA KITONGOJI CHA BULINDA WILAYA YA KYELA MKOANI MBEYA WALIOFAHAMIKA KWA MAJINA YA 1. GENELI KAPWELA [65] NA 2. RAHABU BUNGULU [70] WALIUAWA KWA KUKATWA NA VITU VYENYE NCHA KALI SEHEMU MBALIMBALI ZA MIILI YAO NA KISHA KUCHOMWA MOTO NA WANANCHI WALIOAMUA KUJICHUKULIA SHERIA MKONONI.
MIILI YA MAREHEMU ILIKUTWA KATIKA NYUMBA WALIMOKUWA WAKIISHI MNAMO TAREHE 01.01.2016 MAJIRA YA SAA 08:00 ASUBUHI HUKO KITONGOJI CHA BULINDA, KIJIJI/KATA YA MATEMA, TARAFA YA NTEMBELA WILAYA YA KYELA MKOA WA MBEYA.
KATIKA TUKIO HILO, GENELI KAPWELA ALIUAWA KWA KUTENGANISHWA KICHWA NA KIWILIWILI NA KUKATWA MKONO WA KUSHOTO NA VIUNGO HIVYO HADI SASA HAVIJULIKANI VILIPO NA RAHABU BUNGULU ALIUAWA KWA KUCHOMA NA KITU CHENYE NCHA KALI NA WANANCHI WALIOAMUA KUJICHUKULIA SHERIA MKONONI.
INADAIWA KUWA, WANANCHI HAO WALIVAMIA NYUMBA WALIYOKUWA WAKIISHI MAREHEMU KISHA KUWAKATA NA VITU VYENYE NCHA KALI NA BAADA YA KUTEKELEZA MAUAJI HAYO, WATU HAO WALIANGUSHA NYUMBA WALIYOKUWA WAKIISHA AMBAYO ILIKUWA IMEJENGWA KWA MIANZI NA KISHA KUICHOMA MOTO.
CHANZO CHA TUKIO HILO NI IMANI ZA KISHIRIKINA KWANI MAREHEMU WALIKUWA WANATUHUMIWA KULETA UGONJWA WA KIPINDUPINDU KIJIJI HAPO KWA NJIA ZA KISHIRIKINA. WATU WAWILI WAMEKAMATWA KWA MAHOJIANO KUHUSIANA NA TUKIO HILO AMBAO NI 1. ALIKO MWAMTOBE [47] MKAZI WA MATEMA NA 2. ALISOLOMON MWAMTOBE [49] MKAZI WA KITONGOJI CHA BULINDA.
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI MWANDAMIZI WA POLISI AHMED Z. MSANGI ANATOA WITO KWA JAMII KUACHA IMANI POTOFU ZA KISHIRIKINA KWANI ZINA MADHARA MAKUBWA KATIKA JAMII.
KATIKA TUKIO LA PILI:
MWANAFUNZI WA SHULE YA MSINGI MAPAMBANO ILIYOPO JIJINI MBEYA ALIYEFAHAMIKA KWA JINA LA FELISTA MWANSASU [12] AMEFARIKI DUNIA PAPO HAPO BAADA YA KUGONGWA NA GARI LENYE NAMBA ZA USAJILI T.949 CVS AINA YA MITSUBISHI FUSO LILILOKUWA LIKIENDESHWA NA NSAJIGWA ALISALA [39] MKAZI WA MBEYA.
TUKIO HILO LIMETOKEA MNAMO TAREHE 01.01.2016 MAJIRA YA SAA 07:50 ASUBUHI HUKO MAENEO YA MAFIATI, KATA YA MUUNGNANO, TARAFA YA IYUNGA, JIJI NA MKOA WA MBEYA KATIKA BARABARA YA MBEYA/TUNDUMA.
CHANZO CHA AJALI KINACHUNGUZWA. MWILI WA MAREHEMU UMEHIFADHIWA HOSPITALI YA RUFAA MBEYA. DEREVA AMEKAMATWA, UPELELEZI UNAENDELEA.
MWANAFUNZI WA SHULE YA MSINGI MAPAMBANO ILIYOPO JIJINI MBEYA ALIYEFAHAMIKA KWA JINA LA FELISTA MWANSASU [12] AMEFARIKI DUNIA PAPO HAPO BAADA YA KUGONGWA NA GARI LENYE NAMBA ZA USAJILI T.949 CVS AINA YA MITSUBISHI FUSO LILILOKUWA LIKIENDESHWA NA NSAJIGWA ALISALA [39] MKAZI WA MBEYA.
TUKIO HILO LIMETOKEA MNAMO TAREHE 01.01.2016 MAJIRA YA SAA 07:50 ASUBUHI HUKO MAENEO YA MAFIATI, KATA YA MUUNGNANO, TARAFA YA IYUNGA, JIJI NA MKOA WA MBEYA KATIKA BARABARA YA MBEYA/TUNDUMA.
CHANZO CHA AJALI KINACHUNGUZWA. MWILI WA MAREHEMU UMEHIFADHIWA HOSPITALI YA RUFAA MBEYA. DEREVA AMEKAMATWA, UPELELEZI UNAENDELEA.
KATIKA TUKIO LA TATU:
MWENDESHA PIKIPIKI ALIYEFAHAMIKA KWA JINA LA ASIFIWE MWANTOBE [25] MKAZI WA TUNDUMA MKOANI MBEYA AMEFARIKI DUNIA BAADA YA PIKIPIKI ALIYOKUWA AKIENDESHA KUGONGANA NA GARI LENYE NAMBA ZA USAJILI T. 975 CPS AINA YA TATA BUS LILILOKUWA LIKIENDESHWA NA EMANNUEL ADAM [36] MKAZI WA MBEYA.
TUKIO HILO LIMETOKEA MNAMO TAREHE 01.01.2016 MAJIRA YA SAA 18:00 JIONI HUKO MAPOROMOKO KATIKA BARABARA YA TUNDUMA/MBEYA, WILAYA MOMBA, MKOA WA MBEYA.
INADAIWA KUWA, MARA BAADA YA AJALI HIYO PIKIPIKI ALIYOKUWA AKIENDESHA MAREHEMU ILITOROSHWA NA WATU WASIOJULIKANA. MWILI WA MAREHEMU UMEHIFADHIWA KITUO CHA AFYA TUNDUMA. CHANZO CHA AJALI KINACHUNGUZWA. DEREVA WA BASI AMEKAMATWA NA UPELELEZI UNAENDELEA.
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI MWANDAMIZI WA POLISI AHMED Z. MSANGI ANATOA WITO KWA MADEREVA KUWA MAKINI WANAPOTUMIA VYOMBO VYA MOTO IKIWA NI PAMOJA NA KUFUATA NA KUHESHIMU SHERIA NA ALAMA ZA USALAMA BARABARANI ILI KUEPUKA AJALI ZINAZOEPUKIKA. AIDHA ANATOA WITO KWA WATUMIAJI WENGINE WA BARABARA KUWA MAKINI KATIKA MATUMIZI YA BARABARA HASA KWA KUFUATA SHERIA ZA BARABARANI.
MWENDESHA PIKIPIKI ALIYEFAHAMIKA KWA JINA LA ASIFIWE MWANTOBE [25] MKAZI WA TUNDUMA MKOANI MBEYA AMEFARIKI DUNIA BAADA YA PIKIPIKI ALIYOKUWA AKIENDESHA KUGONGANA NA GARI LENYE NAMBA ZA USAJILI T. 975 CPS AINA YA TATA BUS LILILOKUWA LIKIENDESHWA NA EMANNUEL ADAM [36] MKAZI WA MBEYA.
TUKIO HILO LIMETOKEA MNAMO TAREHE 01.01.2016 MAJIRA YA SAA 18:00 JIONI HUKO MAPOROMOKO KATIKA BARABARA YA TUNDUMA/MBEYA, WILAYA MOMBA, MKOA WA MBEYA.
INADAIWA KUWA, MARA BAADA YA AJALI HIYO PIKIPIKI ALIYOKUWA AKIENDESHA MAREHEMU ILITOROSHWA NA WATU WASIOJULIKANA. MWILI WA MAREHEMU UMEHIFADHIWA KITUO CHA AFYA TUNDUMA. CHANZO CHA AJALI KINACHUNGUZWA. DEREVA WA BASI AMEKAMATWA NA UPELELEZI UNAENDELEA.
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI MWANDAMIZI WA POLISI AHMED Z. MSANGI ANATOA WITO KWA MADEREVA KUWA MAKINI WANAPOTUMIA VYOMBO VYA MOTO IKIWA NI PAMOJA NA KUFUATA NA KUHESHIMU SHERIA NA ALAMA ZA USALAMA BARABARANI ILI KUEPUKA AJALI ZINAZOEPUKIKA. AIDHA ANATOA WITO KWA WATUMIAJI WENGINE WA BARABARA KUWA MAKINI KATIKA MATUMIZI YA BARABARA HASA KWA KUFUATA SHERIA ZA BARABARANI.
Imesainiwa na:
[AHMED Z. MSANGI – SACP]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.
[AHMED Z. MSANGI – SACP]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.
DC KINONDONI, PAUL MAKONDA APOKEA SARUJI MIFUKO 1640 KUTOKA KWA WADAU WA MAENDELEO KWA AJILI YA UJENZI WA SHULE ZA SEKONDARY
Mkurugenzi
Mtendaji wa Kampuni ya Duma, Areeq Amran Mohamed (kulia), akimkabidhi
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda mfuko mmoja wa saruji kati ya
640 aliyoitoa kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa Shule za Sekondari za
wilaya hiyo Dar es Salaam leo asubuhi. Katika makabidhiano hayo Makonda
alipokea mifuko 500 ya saruji kutoka kwa Mwenyekiti wa Jumuia ya Wazazi
Taifa ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Abdallah Bulembo na Askofu mstaafu
wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dk.Alex Malasusa
aliyetoa mifuko 500.
Mwenyekiti wa Jumuia ya Wazazi Taifa ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Abdallah Bulembo (kulia), akimkabidhi saruji hiyo DC Makonda.
Lori lilibeba saruji hiyo likiwa eneo la tukio.
DC Makonda na wageni wake wakiwa eneo la tukio kabla ya makabidhiano ya saruji hiyo.
Mhe. Bulembo akihojiwa na waandishi wa habari baada ya kukabidhi msaada huo.
Wanahabari wakizungumza na watoa msaada huo.
Serikali kuimarisha miundombinu kuboresha Utalii nchini.
Picha na raymond Mushumbusi MAELEZO
………………………………………………….
Raymond Mushumbusi MAELEZO
Serikali
imejipanga kuimarisha miundombinu inayoelekea kwenye mbuga za wanyama
na vituo vingine vya utalii nchini ili kuboresha utalii wa ndani na wa
nje ya nchi kwa kujenga barabara ili kuwezesha watalii kufika kwa
urahisi katika sehemu za vivutio vya kiutalii.
Akijibu swali la Mhe.Risala Said Kabongo Mbunge wa Viti Maalum (CHADEMA) lililoulizwa serikali ina mikakati gani kuboresha miundombinu ya barabara, malazi na viwanja vya ndege katika hifadhi, Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Ramo Makani amesema jitihada zimefanya na zinaendelea kufanywa ili kuboresha na kuimarisha barabara mbalimbali zinazoelekea katika hifadhi mbalimbali nchini kwa kiwango cha lami ili kuongeza wigo wa watalii kutembelea maeneo hayo kwa urahisi.
Amezitaja barabara ambazo zilizoko kwenye mpango wa kuziboreshwa ili kurahisisha watalii kuyafikia maeneo hayo kuwa ni barabara ya Sumbawanga-kasanga, barabara ya Kigoma kuelekea kusini hadi Kalya na Mwese.
“Sio tutaboresha barabara tu ila tunaviangalia pia viwanja vya ndege vinavyotumika kwa kuviimarisha na kuviboresha viwanja vya ndege vya Songwe,Kigoma na Mpanda ambavyo vitasaidia kufikika kwa urahisi maeneo ya vivutiio”
“ Tunaendelea kuvutia wawekezaji binafsi kutoa huduma mbalimbali za watalii kama malazi na mpka sasa tumetoa vibali 11 kwa wawekezaji kuwekeza katika malazi yaani Hoteli za kitalii katika Hifadhi za Ruaha,Mikumi,katavi na Mahale na uwekezaji huo uko katika hatua za utekelezaji” Alisema Mhe. Ramo Makani.
Wizara kwa kushirikiana an Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) na Shirika la USAID inaandaa mikakati ya kuendeleza na kuutangaza utalii kwenye maeneo mbalimbali na kuboresha miundombimu ili kuwezesha watalii kufikia vivutio kiurahisi.
Akijibu swali la Mhe.Risala Said Kabongo Mbunge wa Viti Maalum (CHADEMA) lililoulizwa serikali ina mikakati gani kuboresha miundombinu ya barabara, malazi na viwanja vya ndege katika hifadhi, Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Ramo Makani amesema jitihada zimefanya na zinaendelea kufanywa ili kuboresha na kuimarisha barabara mbalimbali zinazoelekea katika hifadhi mbalimbali nchini kwa kiwango cha lami ili kuongeza wigo wa watalii kutembelea maeneo hayo kwa urahisi.
Amezitaja barabara ambazo zilizoko kwenye mpango wa kuziboreshwa ili kurahisisha watalii kuyafikia maeneo hayo kuwa ni barabara ya Sumbawanga-kasanga, barabara ya Kigoma kuelekea kusini hadi Kalya na Mwese.
“Sio tutaboresha barabara tu ila tunaviangalia pia viwanja vya ndege vinavyotumika kwa kuviimarisha na kuviboresha viwanja vya ndege vya Songwe,Kigoma na Mpanda ambavyo vitasaidia kufikika kwa urahisi maeneo ya vivutiio”
“ Tunaendelea kuvutia wawekezaji binafsi kutoa huduma mbalimbali za watalii kama malazi na mpka sasa tumetoa vibali 11 kwa wawekezaji kuwekeza katika malazi yaani Hoteli za kitalii katika Hifadhi za Ruaha,Mikumi,katavi na Mahale na uwekezaji huo uko katika hatua za utekelezaji” Alisema Mhe. Ramo Makani.
Wizara kwa kushirikiana an Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) na Shirika la USAID inaandaa mikakati ya kuendeleza na kuutangaza utalii kwenye maeneo mbalimbali na kuboresha miundombimu ili kuwezesha watalii kufikia vivutio kiurahisi.
MSANII WA FILAMU ROSE NDAUKA NA MENEJA WAKE WAZINDUA JARIDA LITAKALOKUWA LIKITOKA KWA WIKI MARA MOJA
Msanii
wa Filamu nchini, Rose Ndauka (kushoto) na Meneja wake Ramaehan Mwanana
wakionesha Jarida jipya litakalojulikana kama Rozzie Magazine wakati
wa uzinduzi uliofanyika jijini Dar es Salaam juzi.
Meneja wa Ndauka Ramaehan Mwanana (kulia), akizungumza katika uzinduzi huo.
Rose Ndauka, akizungumza katika uzinduzi huo.
…………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………
Na Dotto Mwaibale
MSANII wa filamu Tanzania, Rose Ndauka amezindua jarida jipya liitwayo Rozzie litakalotoka mara moja kwa kila mwezi.
Akizungumza
jijini Dar es Salaam juzi, wakati wa uzinduzi huo, Rose alisema dhumuni
kubwa la jarida hilo ni kuelimisha, kuiburudisha, kuikosoa na
kuichochea jamii katika kufikia malengo yao ya kimaisha kwa ujumla na
kujenga taifa bora lenye maendeleo.
“Pia
katika kurasa za ndani za jarida hilo zipo kurasa zilizobeba mambo ya
fasheni, maisha pamoja na mambo mbalimbali yanayoikosoa jamii pale
inapokosea,” alisema.
Alisema
kuwa lengo la kutoa jarida hilo ni kuwafikia watanzania wote na nakala
yake itapatikana kwenye mtandao ya kijamii mara moja kwa kila wiki.
Alisema
magazine hiyo anaitoa bure kiwa watanzania wote na litakuwa likitoa
taarifa taarifa mbalimbali kwenye mitandao yote ya kijamii ambayo ni
Facebook, Instagram, Twitter na You Tube.
Meneja
wa jarida la Rozzie, Ramadhani Mwanana, alisema wameanza kwa
kuchapisha kopi 5,000 na jinsi wanavyoendelea waziongeza nyingi zaidi.
Alisema
jarida hilo ltasambazwa katika mikoa yote hapa nchini kwa kutumia
magari makubwa ya mikoani, maduka mbalimbali pamoja na nyingine
zitakazowezesha watanzania kupata magazine hiyo.
Mpango wa TASAF Awamu ya Tatu kuboreshwa
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe Angella Kairuk
akijibu maswali toka kwa wabunge katika kikao cha 6 cha Bunge la 11
linaloendelea Mjini Dodoma. Picha na raymond Mushumbusi MAELEZO
…………………………………………………………………………………
(Na Raymond Mushumbusi-MAELEZO)
Serikali imejipanga kuborsha
zaidi mpango wa kunusuru Kaya masikini nchi ujulikanao kama TASAF kwa
awamu ya tatu kwa kutengeneza miundombinu mizuri ya kutambua Kaya
zinazolengwa na kuondoa malalamiko ya wananchi kuwa mpango huu umekuwa
ni wa Kaya chache na fedha hizo utolewa kwa upendeleo.
Akijibu swali la Mhe.Magdalena
Hamisi Sakaya Mbunge wa Kaliua (CUF) lililouliza ni vigezo gani
vinatumika kuondoa Kaya zilizopendekezwa kwenye mradi na kubakiza Kaya
chache, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na
Utawala Bora Mhe. Angella Kairuki amesema mpango wa kunusuru Kaya
maskini hutambulishwa kijijini na wataalam kutoka Halmashauri husika kwa
kusimamiwa na uongozi wa kijiji kisha kuweka vigezo vya Kaya maskini.
“ Wakusanya taarifa huchaguliwa
kutoka miongoni mwa vijana wanaoishi kijijini hapo na kupitia nyumba kwa
nyumba kuorodhesha Kaya ambazo zinakidhi vigezo vilivyoanishwa na
mkutano wa Kijiji ila bado kuna malalamiko yanayotolewa kuwa Kaya
maskini zinaachwa na kupewa Kaya nyingine ambazo sio maskini kwa
kuliona tatizo hilo suala hili tunalifanyia uchunguzi na tunaomba watu
watoe taarifa ikiwa wataona ukiukwaji wa uorodheshaji wa Kaya
zitakazohusika na mpango huu ili hatua ziweze kuchukuliwa dhidi ya
yoyote atakaye bainika kufanya hivyo”
“ Mpaka sasa kutokana malalamiko
yaliyojitokeza katika kuorodhesha Kaya maskini zinazotakiwa kuwezeshwa
na mpango huu tumewaajibisha watendaji toka Wilaya za Karagwe, Kagera na
Kibondo, Kigoma na tuomba kupewa taarifa kwa sehemu yoyote ambapo
kutatokea tatizo kama hili na tutachukua hatua mara moja kuokoa fedha
zilizotakiwa kwenda kusaidia watu husika” Alisema Mhe Angella Kairuki.
Aidha Mhe. Angella Kairuki
ameongeza kuwa kuna taarifa zinazoenezwa kuwa fedha za mpango wa TASAF
Awamu ya Tatu ni fedha za freemasons, taarifa hizo sio za kweli kwani
fedha hizi zizantolewa na Serikali ili kusaidia Kaya maskini ili ziweze
kujikwamua kiuchumi kwa kuweza kupata Elimu Malazi na chakula bora.
TASAF ni mpango wa kunusuru Kaya
maskini na imekuwa katika awamu tatu mpaka hadi sasa kwa ajili ya
kuwezesha Kaya maskini kujikwamua kiuchumi.
Serikali itaendelea kuwafungia mageti watumishi
Na.Catherine Sungura-Nzega
Serikali haitokuwa tayari kuwaona
watumishi wa umma wachache wakinufaika na kufaidi pesa za walipa kodi
hususan wa kipatao cha chini na wale maskinini
Hayo yamesema wilayani hapa na
Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto,
Dkt.Hamisi Kigwangwalla alipokuwa akiwahutubia wananchi wa wilaya hiyo
Dkt.Kigwangwalla alisema serikali
ya awamu ya tano inawataka watumishi wote nchini kufanya kazi za
kuwahudumia wananchi na kuacha uzembe kwani awamu hii haiwezi
kuwavumilia watumishi wa namna hiyo.
“Serikali haitowav umilia
watumishi wazembe,hivyo tutaendelea kuwafungia mageti na kuwashughulikia
wale wazembe,tunataka watumishi wa umma wafanye kazi ya kuwahudumia
wananchi kwa ufanisi,mtumishi akizembea tutamtumbua majipu,akichelewa
tunamfungia geti na akiiba tunafilisi pamoja na kumpeleka jela,hii ndiyo
serikali ya hapa kazi tu”
Aidha alisema serikali ya awamu
ya tano inataka kero za wananchi zifanyiwe kazi na kutekeleza ahadi zote
za ilani ya uchaguzi ya ccm zinatimizwa.
“hatutomuonea mtu,lakini
tutafanyia kazi pale penye matatizo,tunataka Tanzania mpya ya mwaka 2015
inakua,hatutaki hadithi wala ahadi”
Hatahivyo aliwataka wazazi wote
wenye watoto wenye umri wa kwenda shule kuwapeleka watoto wao kuanza
masomo kwani elimu kwa sasa ni bure na hakuna michango yoyote.
“natoa wito kwa walimu wote
wasitoze michango yeyote wala ushuru kwa wazazi wanaowapeleka
kuwaandikisha watoto shule kwani shule zimepatiwa pesa za kuendeshea
shule hizo.
Dkt. Kigwangwalla aliwakumbusha
watumishi wa umma kujipanga na kama watagundulika ni majipu bali
hawatosita kuwatumbua hadi kina kitoke,usaha na damu kutoka bila huruma
Waziri Suleiman Jafo:Serikali kuongeza ajira
Naibu waziri Ofisi ya Rais Tawala
za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe Suleiman Jafo akijibu maswali toka
kwa wabunge katika kikao cha 6 cha Bunge la 11 linaloendelea Mjini
Dodoma. Picha na Raymond Mushumbusi MAELEZO
………………………………………………………………………………………………….
(Na Raymond Mushumbusi-MAELEZO)
Serikali katika mwaka wa fedha
2016/2017 imepanga kuongeza ajira kwa vijana ili kukabiliana na
changamoto ya ukosefu wa ajira kwa vijana wengi wa kitanzania kwa
kuongeza ajira na kuwezesha wengine kujiajiri kupitia mifuko ya
uwezeshaji toka Halmashauri za Wilaya nchini.
Akijibu swali la Mhe.Mgumba
Tebweta Omary Mbunge wa Morogoro Kusini (CCM) lenye sehemu a na b
lililouliza Serikali itaanza lini kuwawezesha vijana wa Jimbo la
Morogoro Kusini Mashariki kifedha ili waweze kujiajiri na kuondokana na
tatizo la ajira na umaskini ,Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa
na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe Suleiman Jafo amesema vijana
katika Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro Kusini Mashariki wamekuwa
wakiwezeshwa kiuchumi kupitia fedha za Mfuko wa Maendeleo ya Vijana
ambapo kila Halmashauri hupaswa kutenga asilimia 5 ya mapato yake ya
ndani kila mwaka kwa ajili ya vijana.
Mhe Suleiman Jafo ameongeza kuwa
katika Bajeti ya mwaka 2014/2015,Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro
ilifanikiwa kutoa Shillingi Millioni 10.3 kwa vikundi vya vijana 19 kwa
ajili ya kutekeleza shughuli mbalimbali za kiuchumi na katika Bajeti ya
mwaka wa fedha 2015/2016 vikundi vya vijana vilitengewa Shilllingi
Millioni 87.5 ili kuviwezesha kiuchumi kwa kujiajiri.
“ Katika kutatua changamoto
zilizopo kwa vijana tunawawezesha kifedha ili kujiajiri ili kumekuwa na
tatizo la fedha kuchelewa kufika kwa walengwa ila Serikali kupitia
Wizara yangu tunalifanyia kazi ili fedha zifike kwa wakati na tumetenga
Shillingi Millioni 50 kwa kila kijijikwa ajili ya kuwezesha vijana
walioko katika vikundi mbalimbali mfano SACCOS ili waweze kujiajiri na
kujikwamua kiuchumi kwa kujiondoa katika hali ya umaskini”
“ Napenda kuwaomba wabunge
tusaidiane sababu wao wanahusika katika kamati za fedha za Halmashauri
za Wilaya, waende wakasimamie hizo fedha kwa ajili ya kuwezesha vijana
zitoke na ziwasaidie walengwa” Alisema Mhe Jafo.
Aidha Mhe Suleiman Jafo amesema
kuwa Serikali imetenga Shillingi Billioni 233 kwa ajiri ya kuajiri
vijana wapya takribani 71,408 kati ya hao watumishi wapya wa Afya
wanatarajiwa kuwa takribani 10,871 na Waalimu 40,000 kwa nchi nzima ili
kupunguza tatizo la ajira kwa vijana wanaomaliza vyuo mbalimbali nchini.
Serikali kupitia Halmashauri za
Wilaya imejipanga katika kuwawezesha vijana katika maeneo yao kujikwamua
kiuchumi kwa kujiajiri na kwa mwaka wa fedha 2016/2017 Serikali
itaboresha zaidi mifuko ya kuwezesha vijana katika Halmashauri za Wilaya
kwa kununua vifaa zaidi vya kujifunza stadi mbalimbali za kazi
zitakazowezesha vijana wengi zaidi kuwa na ujuzi utakaowasaidia
kujipatia kipato na kujikwamua kiuchumi.
MTUMISHI WA WIZARA YA HABARI AFARIKI KWA AJALI YA GARI.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo Profesa Elisante Ole Gabriel ameitumia
salamu za Rambirambi familia ya Mzee Dellan Tarmo kufuatia kifo cha
kijana wao mpendwa Jovitha Dellan kilichotokea kwa ajali ya gari mkoani
Arusha juzi tarehe 31.1.2016.
“Pokea rambirambi zangu za dhati, sote kwa pamoja tumepoteza kijana mchapakazi, hodari na aliyepen
da kushirikiana na wenzake katika kazi zake, hakika tutamkumbuka siku zote” Katibu Mkuu amesema.
da kushirikiana na wenzake katika kazi zake, hakika tutamkumbuka siku zote” Katibu Mkuu amesema.
Katibu Mkuu, Pia amemtumia salamu
za pole kwa Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu(KBF) na Wafanyakazi wote
wa Bodi ya Filamu Tanzania.
“Nimepokea taarifa za kifo
cha Jovitha Dellan kwa huzuni kubwa, najua machungu na maumivu mliyonayo
kwa kuondokewa na kiungo muhimu katika utendaji wenu, poleni sana,
niko nanyi katika msiba huu mzito kwenu”, amesema Katibu Mkuu huyo.
Katibu Mkuu amesema pamoja na
kwamba kifo hakiepukiki, bado ni kitu ambacho kinashtua, kuhuzunisha na
kuleta unyonge mkubwa kwa wafiwa katika jamii.
“Naungana nanyi katika
kipindi hiki kigumu kumuombea kijana wetu Jovitha Dellan ili mwenyezi
Mungu ampe mapumziko mema ya Milele” Mwenyezi Mungu awatie nguvu, awape uvumilivu na subira katika kipindi hiki”.
“Niko nanyi katika kipindi hiki kigumu kwa hali na mali, nawaomba msijisikie wapweke” Katibu Mkuu amesema na kuwatakia utulivu na amani katika kipindi hiki cha msiba mkubwa kwa familia.
Marehemu Jovitha Dellan
amefariki juzi tarehe 31 Januari, 2016 mkoani Arusha ambapo alikuwa
njiani kurejea kazini jijini Dar es salaam.
Marehemu Jovitha Dellan anatarajiwa kuzikwa wiki hii mkoani Manyara .
Jovitha Dellan alikuwa ni Afisa Utamaduni aliyekuwa akifanya kazi
katika Bodi ya Filamu Tanzania iliyopo chini ya Wizara ya Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo.
Mungu ailaze Roho ya Marehemu Jovitha Dellan mahali Pema Peponi, Amina.
WASANII WATAKIWA KUEPUKA RUSHWA KWENYE KAZI ZA SANAA
…………………………………………………………………………………………………….
Na Mwandishi Wetu
Wasanii nchini wametakiwa
kujituma na kutengeneza kazi za Sanaa zenye ubora na kuachana na dhana
ya kutegemea rushwa na hongo katika kuyafikia mafanikio yao kisanaa.
Wito huo umetolewa mapema wiki
hii na wadau wa Sanaa kwenye programu ya Jukwaa la Sanaa ambayo
huandaliwa na Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) na kufanyika kwa mwezi
mara mbili siku ya Jumatatu kwenye ukumbi wa Baraza hilo.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti
wadau hao walisema kwamba kumekuwa na wimbi la wasanii na mameneja wa
wasanii kutegemea rushwa za fedha na wengine kufikia hatua kutoa rushwa
za ngono ili kufanikiwa kisanaa hasa katika kuvishawishi vituo vya radio
na televisheni kucheza nyimbo zao.
“Ukweli ni kuwa rushwa na hongo
zinaendekezwa na wasanii walioshindwa. Msanii anayejitambua hawezi kutoa
rushwa ili wimbo wake uchezwe. Lazima wasanii waachane na dhana hii
potofu, waelewe kwamba kazi ya Sanaa iliyo bora itapendwa tu na
kukubalika na jamii” alisema Nkwama Bhallanga ambaye ni Msanii wa Sanaa
za Maonesho.
Kwa upande wake Katibu wa chama
cha wachezesha disko (TDMA) Asanterrabi Mtaki alisema kuwa dhana kwamba
wasanii lazima wahonge watangazaji au ma DJs ili nyimbo zao zichezwe ni
potofu na ni chanzo cha kutangaza muziki au kazi za Sanaa zisizo bora na
kuziacha zile zenye ubora.
“Kama wimbo wako ni mzuri kwa
nini uhonge au utoe rushwa ili uchezwe? Hapa ndipo tatizo la kuendekeza
kazi mbovu za Sanaa linapoanzia. Muziki wa wenye fedha na wanaohonga
ndiyo unasikika, ule mzuri unaondaliwa na wasanii wasiyo na uwezo
haupati nafasi” alisema Mtaki.
Alitoa wito kwa wasanii kufikiria
njia mbadala za kutangaza nyimbo zao hasa kumbi za disko badala ya
kutegemea vituo vya radio pekee.
Awali akizungumza kwenye Jukwaa
la Sanaa, Msanii na mshindi wa shindano la Airtel Trace Music Star
Mayunga Malini alisema kuwa wasanii hawana budi kujituma, kutafuta fursa
na kuzitumia ipasavyo hasa kwa kutumia muda mwingi kubuni kazi zenye
ubora.
Aliongeza kuwa, wasanii hawana
budi kuachana na dhana ya utegemezi na kutegemea fedha na hongo katika
kupata mafanikio kwani kazi za Sanaa zikitengenezwa kwa ubora na kwa
kuzingatia vigezo vyote zitapendwa na kutuzwa tu.
Mwamuzi wa kwanza mtanzania wa mchezo wa Baseball.
Kijana Innocent Kennedy ni
mtanzania mwenye umri wa miaka 19 tu na kwasasa amekuwa ni gumzo kwa
vyama vya kulipwa vya mchezo huu wa baseball barani Asia hususani nchini
Japan.
Innocent ameonyesha umahiri mkubwa wa kuamua na kwa mara ya kwanza alishiriki katika kuamua mashindano ya Africa ya kutafuta uwakilishi wa kombe la Dunia la mchezo huu, mashindano yaliyofanyika nchini Kenya katika jiji la Meru hapo Disemba, 2014.
Kwasasa kijana Innocent anaendelea na masomo yake ya ICT jijini Dar es Salaam na ametenga muda wake wa kila siku ya Jumamosi kuanzia saa 13 :30 hadi saa 18:30 jioni kufika viwanjani Azania Sekondari kushiriki mazoezi ya timu ya Taifa ya baseball.
Katibu mkuu wa mchezo wa Baseball bwana Alpherio Nchimbi alipoulizwa juu ya ndoto ya kumuendeleza kijana huyo, bwana Nchimbi alisema kwa kifupi kuwa lengo kuu ni kuzalisha akina Innocent wengi lakini kwa Innocent anafanyiwa mipango mahususi ya kumpeleka nchini Japan kwa mafunzo zaidi.
Innocent ameonyesha umahiri mkubwa wa kuamua na kwa mara ya kwanza alishiriki katika kuamua mashindano ya Africa ya kutafuta uwakilishi wa kombe la Dunia la mchezo huu, mashindano yaliyofanyika nchini Kenya katika jiji la Meru hapo Disemba, 2014.
Kwasasa kijana Innocent anaendelea na masomo yake ya ICT jijini Dar es Salaam na ametenga muda wake wa kila siku ya Jumamosi kuanzia saa 13 :30 hadi saa 18:30 jioni kufika viwanjani Azania Sekondari kushiriki mazoezi ya timu ya Taifa ya baseball.
Katibu mkuu wa mchezo wa Baseball bwana Alpherio Nchimbi alipoulizwa juu ya ndoto ya kumuendeleza kijana huyo, bwana Nchimbi alisema kwa kifupi kuwa lengo kuu ni kuzalisha akina Innocent wengi lakini kwa Innocent anafanyiwa mipango mahususi ya kumpeleka nchini Japan kwa mafunzo zaidi.
WITO UMETOLEWA KWA WAMILIKI WA SILAHA KUHAKIKI SILAHA ZAO KWA WAKATI
Kamanda Liberatus Sabas, alipokuwa akifunga Kampeni za ABIRIA PAZA SAUTI, Jijini Arusha,
………………………………………………………………………….
Na Vero Ignatus wa Wazalendo 25 Blog, Arusha.
Jeshi la
polisi mkoa wa Arusha limewataka watu wote wanaomiliki silaha kwa njia
halali wafike kwenye kituo cha polisi kuhakiki silaha zao na kuzilipia
kama inavyostahili na kwa kufuata utaratibu kama sheria inavyoagiza.
Hayo ya mesemwa Kamanda wa polisi mkoa wa Arusha Liberatus Sabas, kwamba kila mwaka huwa kila mwenye silaha anafika polisi na silaha yake na vitabu vyake kwaajili ya kuihahiki na kuilipia kama inavyostahili ,na kama zipo tuhuma zozote kutokana na matumizi ya silaha, itasimamishwa kwaajili ya taratibu zingine na kunyang’anywa hadi hapo jeshi litakapojiridhisha kuwa silaha hiyo matumizi yake ni sahihi ama siyo sahihi
Hayo ya mesemwa Kamanda wa polisi mkoa wa Arusha Liberatus Sabas, kwamba kila mwaka huwa kila mwenye silaha anafika polisi na silaha yake na vitabu vyake kwaajili ya kuihahiki na kuilipia kama inavyostahili ,na kama zipo tuhuma zozote kutokana na matumizi ya silaha, itasimamishwa kwaajili ya taratibu zingine na kunyang’anywa hadi hapo jeshi litakapojiridhisha kuwa silaha hiyo matumizi yake ni sahihi ama siyo sahihi
Kamanda amesema utaratibu huu
huwa unaratibiwa na makao makuu ya jeshi la polisi kwaajili ya kuhakiki
silaha ,ikiwa ni pamoja na kulipia mapato ya serikali ,amewataka watu
wanaomiliki silaha wafuate masharti yake kama inavyotakiwa, nawakumbuke
sheria inambana kila mtu mara anapotenda kosa ,na kama mtu akiitumia
ndivyosivyo atanyang’anywa silaha kwa kutumia sheria iliyowekwa.
Ameongeza
kuwa wapo watu ambao wamewatishia silaha wenzao,na wengine kesi zao zipo
tayari na zingine zimefutiwa umiliki kwa mujibu wa sheria, amesema
kimsingi kabla mtu hajakabidhiwa silaha ili amiliki, yapo masharti
yakufuata na yapo kwenye kitabu kile cha leseni anachopewa wakati wa
umiliki, amesema kuwa ukitoka nje ya hayo masharti huna sifa ya kumiliki
silaha.
Kamanda Sabas ametoa anagalizo kwa wamiliki wa silaha na kusema kuwu silaha ya moto siyo kama panga,silaha hiyo ukiifanyia kosa mara moja yaweza kuua mtu au watu hivyo amewataka kuwa makini sana katika ufuatiliaji wa umiliki, pamoja na namna zinavyotunzwa,amesema jeshi la polisi lipo makini kufuatilia kwa ukaribu wakithibitisha silaha haitunzwi kama inavyostahili utanyang’anywa.aidha amesema kwa wazee amabao umri wao umeenda nab ado wanamiliki silaha huwa wanaichukua na kuihifadhi .
Kamanda Sabas ametoa anagalizo kwa wamiliki wa silaha na kusema kuwu silaha ya moto siyo kama panga,silaha hiyo ukiifanyia kosa mara moja yaweza kuua mtu au watu hivyo amewataka kuwa makini sana katika ufuatiliaji wa umiliki, pamoja na namna zinavyotunzwa,amesema jeshi la polisi lipo makini kufuatilia kwa ukaribu wakithibitisha silaha haitunzwi kama inavyostahili utanyang’anywa.aidha amesema kwa wazee amabao umri wao umeenda nab ado wanamiliki silaha huwa wanaichukua na kuihifadhi .
Amehitimisha
kwa kusema kuwa kila , mtu amnayetaka kumiliki silaha, kamati za ulinzi
na usalama kuanzia kwenye kata ,Wilaya, Mkoa wakamuidhinisha kuwa na
silaha afuate masharti na kuitunza silaha isije ikaangukia kwenye mikono
ya wahalifu wakaitumia isivyo halali sheria itafuata mkondo wake,
Silaha huwa zinatakiwa kulipiwa kila mwaka kuanzia mwezi julai hadi
septemba ukichelewa kulipia unapigwa penati kwa mujibu wa sheria.
MADEREVA DALADALA JIJINI MWANZA WATISHIA KUGOMA IKIWA MAJIPU YA TAX BUBU HAYATATUMBULIWA.
Ridhione
Senga (wa pili kushoto) ambae ni Mwenyekiti wa Madereva wa Daladala
wanaofanya shughuli zao katika barabara ya Bugarika-Mzunguko Jijini
Mwanza, jana akilalamikia suala la uwepo wa tax bubu linalowasumbua
katika shughuli zao.
Alisema
licha ya madereva wa tax bubu wanaobeba abiria kama daladala katika
eneo wanalofanyia kazi hususani kubeba abiria wanaoenda na kutoka katika
hospitali ya Rufaa ya Bugando kuzuiliwa, bado madereva hao wa tax bubu
wameendelea na biashara hiyo kama kawaida.
Senga
alibainisha kwamba hatua hiyo inawaweka katika wakati mgumu katika
kutimiza majukumu yao kutokana na kupata hasara kila kukicha ambapo
amesema ikiwa itaendelea wataitisha mgomo ili kushinikiza kilio chao
kufanyiwa kazi.
“Sisi
tunalipa mapato, lakini jambo la ajabu hawa madereva wa tax bubu ambao
hawana leseni ya kubeba abiria wamekuwa ndio wanafanya kazi ya daladala
licha ya kupigwa marufuku katika kikao tulichokaa ijumaa iliyopita baina
ya Sumatra, halmashauri ya Jiji, Polisi, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa
Mwanza pamoja na wawakilishi wengine bila kuwasahau viongozi wa daladala
na tax. Kama hali hii itaendelea tutafanya mgomo hapa na hakuna huduma
yoyote ya kubeba abiria itakayotolewa”.Alisema Senga.
Ramadhan
Idd ambae ni Kaimu Mwenyekiti wa Madereva wa daladala za
Bugarika-Muzunguko Jijini Mwanza aliunga mkono hoja ya mwenyekiti huyo
na kusema kuwa ikiwa mamlaka husika zitashindwa kutatua suala la tax
bubu katika eneo hilo, wao watachukua hatua ya kusitisha huduma ya
usafirishaji katika barabara hiyo ya Bugarika-Buzuruga.
“Hizi
tax bubu tunasikia ni za wakubwa na ndiyo maana hawa madereva
wanaoziendesha wana jeuri mno. Sisi tunasema haya ni majipu na
tunawaomba viongozi wengine wakubwa akiwemo Mhe.Magufuli, waangalie huku
Jijini Mwanza maana kuna majipu makubwa ya kutumbua”.Alisema Athuman
Bin Malick ambae ni mmoja wa madereva wa daladala za Bugarika-Mzunguko
Jijini Mwanza.
Kaptaini
Michael Rogers ambae ni Afisa Mfawidhi wa Sumatra Mkoani Mwanza,
ameshauri suala hilo kutatuliwa na jeshi la polisi kitengo cha usalama
barabarani kwa kuwa ndilo lenye jukumu la kukamata vyombo vya usafiri
vinavyofanya kazi kwa kukiuka sheria na taratibu zilizoweka na mamlaka
husika ikiwemo halmashauri ya Jiji Mwanza ambayo ndiyo inasimamia
taratibu la utendaji kazi wa tax.
Juhudi
za kuwatafuta madereva wa tax hizo zinazodaiwa kufanya kazi kinyume cha
sheria (tax bubu) bado zinaendelea ili kujua kuzungumzia malalamiko
yanayowakabiri.
Ramadhan Idd ambae ni Kaimu Mwenyekiti wa Madereva wa daladala za Bugarika-Muzunguko akitoa malalamiko yake.
Athuman Bin Malick ambae ni mmoja wa madereva wa daladala za Bugarika-Mzunguko Jijini Mwanza.
Kulia ni Kaptaini Michael Rogers ambae ni Afisa Mfawidhi wa Sumatra Mkoani Mwanza akitoa ufafanuzi wake.
MPANGO WA KUSAIDIA KAYA MASIKINI WANUFAISHA KAYA MILIONI 1.1 NCHINI
Mpango
wa Kijamii wa Uzalishaji Salama ili kusaidia kaya masikini kupambana na
umasikini (PSSN) umefanikiwa kuwa na matokeo mazuri kwa kusaidia kaya
Milioni 1.1 nchini na kusaidia juhudi za serikali kupambana na
umasikini.
Hayo
yamefahamika wakati washirika wa maendeleo ambao ni Umoja wa Mataifa,
Benki Kuu ya Dunia, Serikali ya Uingereza kupitia kitengo cha Maendeleo
ya Kimataifa, Irish Aid, USAID, Shirika la Ushirikiano wa Kimataifa la
Sweden (SIDA) walipotembelea miradi ya maendeleo katika wilaya za
Unguja, Chamwino, Babati, Sumbawanga (Manispaa na Wilaya), Singida na Hanang kwa kipindi cha siku tatu kuanzia Januari, 19 hadi 22.
Bi.
Kazijya Kila ambaye ni mmoja wa wanufaikaji wa fedha akitoa ushuhuda
kuhusu mradi wake wa chakula ulivyowezeshwa na TASAF ambapo hadi hivi
sasa anatengeneza faida ya Shilingi 7000 kwa siku na kabla ya kuwezeshwa
alikuwa akikaa nyumbani na mama yake bila kuingiza kipato chochote.
Katika
Mpango huo ambao utekelezwaji wake unasimamiwa na Mfuko wa Maendeleo ya
Jamii (TASAF) unafanyika Tanzania Bara na Tanzania visiwani ukiwa na
lengo la kuzisaidia kaya masikini pesa za matumizi ili kukidhi mahitaji
ya kupata chakula pamoja na kuwawezesha kusaidia watoto wao kupata elimu
jambo ambalo linaonekana kuzaa matunda kwa maeneo mengi ikiwepo
Tanzania visiwani.
Serikali
ya Tanzania imekuwa ikisaidia na washirika wa maendeleo ili kupunguza
umaskini uliokithiri kwa wananchi wake na mwaka 2013 iliweka mpango wa
kusaidia kaya masikini 275,000 kwa kipindi cha miaka mitano na tangu
ianzishe mpango huo ilifanikiwa kusaidia kaya 275,000 kwa mwaka 2013
pekee katika wilaya nane nchini.
Mtaalamu
Mwandamizi wa Masuala ya Jamii kutoka Benki ya Dunia, Bw. Muderis
Abdulahi Mohamed (kushoto) na Msimamizi wa mpango wa PSSN, Bw. Ramadhani
Madari wakifuatilia kipindi cha maswali na majibu kwa wanufaikaji wa
fedha hizo.
Na
mpaka kufikia sasa mpango huo umeshatoa malipo mara 12 na jumla ya kaya
masikini milioni 1.1 zimeshafaidika na mpango huo ikiwa ni kwa wilaya
161 na vijiji 9789 nchini.
Malengo
ya serikali ya Tanzania na mashirika ya kimataifa ni kuhakikisha
kufikia mwaka 2030 kunakuwa hakuna masikini hivyo ni wajibu wa kila nchi
kuhakikisha inawasaidia wananchi wake ili wajijengee uwezo wa
kujitegemea na kuondoka katika janga la umasikini.
Asilimia kubwa ya wanufaikaji wa mpango huo ni wanawake, kama wanavyoonekana pichani.
Mkurugenzi
wa Huduma za jamii kutoka Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF), Amadeus
Kamagenge akizungumza na wanufaikaji wa mpango wa TASAF (hawapo
pichani).
Mkurugenzi
wa Huduma za jamii kutoka Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF), Amadeus
Kamagenge (kushoto) akifurahi jambo na Mtaalamu Mwandamizi wa Masuala ya
Jamii kutoka Benki ya Dunia, Bw. Muderis Abdulahi Mohamed.
Timu ya TASAF na wadau wa maendeleo wakifuatilia kwa umakini yaliyokuwa yakijiri katika mkutano huo.
Mtaalamu Mwandamizi wa Masuala ya Jamii kutoka Benki ya Dunia, Bw. Muderis Abdulahi Mohamed na Aine Mushi wa UN/NRA.
Bi Jabo Omari Othman akiwa kwenye shamba lake alilonunua kutokana na fedha za TASAF visiwani Unguja.


No comments:
Post a Comment