Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya PanAfrican Energy David K. Roberts
(kulia) akimuelezea jambo Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini
Prof. Justin Ntalikwa wakati wa ziara yake huko Songosongo katika visima
vya gesi asilia.
Ni katika ziara ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Prof. Justin Ntalikwa katika visiwa vya Songosongo.
PanAfrican
Energy Operational SH Engineer, Onestus Mujemula akielezea jambo kwa
wana habari katika ziara ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini
huko Songosongo kwenye visima vya gesi, kutoka kushoto ni PanAfrican
Energy Country Chairman Patrick Rutabanzibwa, Katibu Mkuu wa Wizara ya
Nishati na Madini Prof. Justin Ntalikwa na CSR Manager Andrew Kashangaki
(wakwanza kulia)
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Prof. Justin Ntalikwa
akipata maelezo ya mradi kutoka PanAfrican Energy Operational SH
Engineer Onestus Mujemula kuhusu mradi wa uchimbaji gesi asilia katika
visima vinne uliomalizika kwa kutumia mtambo wa kisasa wa “RIG”
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Prof. Justin Ntalikwa
akiongea na wana habari wakati wa ziara yake ya kikazi katika visiwa vya
Songosongo.
MO DEWJI BLOG YAWANASA LIVE WAFANYAKAZI WA TAMBAZA WAKIOMBA RUSHWA (PICHA&SAUTI)
Agizo la serikali kuzuia usafiri wa
bodaboda mjini umegeuka kuwa kitega uchumi kwa baadhi ya vijana
walioajiriwa kuhakikisha agizo inatekelezwa.
Hii imethibitika baada ya mwandishi
wa Mo Dewji Blog kufumania tukio la vijana wa jiji wakidai rushwa wazi
wazi bila woga kwa mwendesha pikipiki wa magurudumu watatu maarufu kama
bajaji.
Kachero wetu (jina limehifadhiwa) alifanikiwa kupata picha za wala rushwa pamoja na kunasa sauti za tukio lote.
Baadhi ya wafanyakazi wa Tambaza wakiwa pembezoni ya barabara katika daraja la Salenda.
Mmoja wa mfanyakazi wa Tambaza akisimamisha bajaji.
Wafanyakazi wa Tambaza wakizungumza na dereva wa bajaji na kumuomba rushwa ya shilingi 10,000
Katibu wa Jumuiya na Taasisi ya Kiislam
Tanzania, Sheikh Ponda Issa Ponda (kushoto), akizungumza na waandishi wa
habari Dar es Salaam leo, Februari 3,2016. wakati akitoa taarifa ya
kupinga kurudiwa kwa uchaguzi mkuu wa Zanzibar.Sheikh hiyo machachari
"amemzodoa" sheikh wa mkoa wa Dar es salaam, Alhad Musa Salim, ambaye
alinukuliwa akisema, kiongozi wa Uamsho ambaye yuko korokoroni
akikabiliwa na mashtaka ya kusababisha hofu Kyle Zanzibar, Sheikh Farid,
kuwa ameridhia uchaguzi wa Zanzibar kurudiwa. "Mimi nimemtembelea Leo,
(Jana Feb 2, 2016), sheikh Farid na baada ya kumuuliza KUHUSU taarifa ya
sheikh Alhadi, alipinga vikali nakukanusha maneno hayo." Sheikh Ponds
aliwaambia waandishi wa habari.
Msemaji wa Jumuiya na Taasisi ya Kiislam Tanzania, Sheikh Rajab Katimba akitoa ufafanuzi zaidi kuhusu kurudiwa kwa uchaguzi huo Zanzibar.
Sheikh Ponda akisalimiana na mwanahabari Said Powa wa gazeti la Tanzania Daima baada ya kumaliza kuzungumza na wanahabari.
Sheikh Ponda akiondoka baada ya kuzungumza na wanahabari.
Mbunge wa Mtera, Livingstone Lusinde akizungumza Bungeni Mjini Dodoma Februari 3, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mbunge wa Manyovu, Albert Obama Ntabaliba kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma Februari3, 2016. (Picha na ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majliwa akizungumza na Mbunge wa Kibaha Vijijini, Hamoud Abuu Jumaa (katikati) na Mbunge wa Bukoba Vijijini Jasson Rweikiza kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma Februari 3, 2016. (picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akiteta na Mbunge wa Gairo, Ahmed Shabiby kwenye
viwanja vya Bunge mjini Dodoma Februari 3, 2016. (Picha na Ofisi ya
Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mbunge wa Manyovu, Albert Obama Ntabaliba kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma Februari3, 2016. (Picha na ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majliwa akizungumza na Mbunge wa Kibaha Vijijini, Hamoud Abuu Jumaa (katikati) na Mbunge wa Bukoba Vijijini Jasson Rweikiza kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma Februari 3, 2016. (picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
:Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akisalimiana kwa furaha na wakaazi wa Kituo cha Makazi ya Wazee na Watu Walemavu cha Nunge,
Kigambo ni,
jijini Dar es salaam alikotembelea na kusikiliza mahitaji yao pamoja na
kutoa msaada wa mchele kilo 3000, Unga kilo 3000 na Maharage Kilo 1200
ikiwa msaada wake kwa wazee na walemavu hao, Leo February 3, 2016.
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akiweka saini katika kitabu cha wageni
mara baada ya kuwasili katika Kituo cha Makazi ya Wazee na Watu Walemavu
cha Nunge,
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akitembelea chumba cha kujifungulia cha
zahanati ya Kituo cha Makazi ya Wazee na Watu Walemavu cha Nunge,
Kigamboni,
jijini Dar es salaam alikotembelea na kusikiliza mahitaji yao pamoja na
kutoa msaada wa mchele kilo 3000, Unga kilo 3000 na Maharage Kilo 1200
ikiwa msaada wake kwa wazee na walemavu hao.
Mkuu wa wilaya ya Temeke Mhe Sophia Mjema akimkaribisha Mke wa Rais Mama
Janeth Magufuli kuhutubia wakaazi wa Kituo cha Makazi ya Wazee na Watu
Walemavu cha Nunge,
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akihutubia wakaazi wa Kituo cha Makazi ya Wazee na Watu Walemavu cha Nunge,
Kigambo ni,
jijini Dar es salaam alikotembelea na kusikiliza mahitaji yao pamoja na
kutoa msaada wa mchele kilo 3000, Unga kilo 3000 na Maharage Kilo 1200
ikiwa msaada wake kwa wazee na walemavu hao.
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akimkabidhi mchele, unga na maharage
Mzee Anthony Kingongoti Mwenyekiti wa wakaazi wa Kituo cha Makazi ya
Wazee na Watu Walemavu cha Nunge,
Kigambo ni,
jijini Dar es salaam alikotembelea na kusikiliza mahitaji yao pamoja na
kutoa msaada wa mchele kilo 3000, Unga kilo 3000 na Maharage Kilo 1200
ikiwa msaada wake kwa wazee na walemavu hao.
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akimkabidhi mchele, unga na maharage
Mzee Anthony Kingongoti Mwenyekiti wa wakaazi wa Kituo cha Makazi ya
Wazee na Watu Walemavu cha Nunge,
Kigambo ni,
jijini Dar es salaam alikotembelea na kusikiliza mahitaji yao pamoja na
kutoa msaada wa mchele kilo 3000, Unga kilo 3000 na Maharage Kilo 1200
ikiwa msaada wake kwa wazee na walemavu
Mzee Anthony
Kingongoti Mwenyekiti wa wakaazi wa Kituo cha Makazi ya Wazee na Watu
Walemavu cha Nunge, akitoa shukrani kwa niaba ya wenzake
Meneja Mawasiliano wa Mamlaka ya
Mawasiliano Tanzania TCRA Innocent Mungy, akizungumza na waandishi wa
habari Zanzibar kuhusiana na kutambua Simu Feki na kudhibiti uingiaji wa
Simu hizo Tanzania na kueleza mwisho wa matumizi wa simu hizo Nchini
Tanzania ni Juni 2016. Mkutano huo umefanyika katika ukumbi wa hoteli ya
Zanzibar Ocean View Kilima Zanzibar na kuwashirikisha waandishi wa
Vyombo mbali mbali vilioko Zanzibar.
Naibu Mkurugenzi Masuala ya Watumiaji wa
Huduma za Mawasiliano TCRA Thadayo Ringo, akizungumza na waandishi wa
habari jinsi ya kutambua Simu feki wakati wa mkutano huo na waandishi wa
habari Zanzibar uliofanyika katika ukumbi wa hoteli ya Zanzibar Ocean
View Kilimani Zanzibar, Amesema utambuzi wa kujua simu yako kama ni
orijinali unaweza kupiga namba kuaza na Nyota Reli 06 Reli . *# 06# na
utapata ujumbe wa Simu yako kwa Mfano zitakuja tarakimu 15 mfano
IMEI 12456789067654 Na Kupiga 15090 Ujumbe wa kukuelewesha kama ni simu
yako orijino. kwa mfano kama huu Sony Mobile Communications AB -SONY
C5555 - Xperia. huu ni mfano wa kujua simu orijino.
Naibu Mkurugenzi Masuala ya Watumiaji wa
Huduma za Mawasiliano Thadayo Ringo akionesha mfano wa simu orijino kwa
waandishi wa habari wakati wa mkutano huo uliofanyika katika ukumbi wa
hoteli ya Zanzibar Ocean View Kilimani Zanzibar.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya simu za mikononi Tigo,
Diego Gutierrez,
akizungumzia uzinduzi huo uliofanyika kwenye Hoteli ya Hyatt Regency,
jijini Dar es Salaam usiku wa Februari 2, 2016. (Picha na K-VIS MEDIA/Khalfan Said)
NA K-VIS MEDIA/Khalfan Said
KAMPUNI ya simu za mikononi Tigo, imezindua huduma ya bure ya
WhatsApp kwa wateja wake kuanzia Usiku wa Februari 2, 2016, wateja watakuwa
wanachat bure. Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo, Diego Gutierrez amewaambia wageni waalikwa kwenye uzinduzi
huo uliofanyika kwenye hoteli ya Hyatt Regency The Kilimanjaro Hotel jijini Dar
es Salaam
“Ushirikiano huu ni wakwanza
nawaina yake katika sekta ya mawasiliano hapanchini.” Aliandika Diego kwenye
WhatsApp yale iliyorushwa moja kwa moja kupitia screen kubwa iliyokuwa
ukumbini.
“Ushirikiano huu wa
kihistoria una maa kuwa, wateja wa Tigo sasa ni sehemu ya familia kubwa ya
kimataifa ya watumiaji Milioni 900 na huduma ya WhatsApp Duniani.” Alisema
Mkurugenzi huyo Mtendaji wa Tigo.
“Na hii ni namna yetu ya
kutoa shukrani za dhati kwa wateja wetu kwa kuwapa huduma bora na za viwango
vya juu zaidi kwa lengo la kuwafurahisha wateja wetu wa tigo.” Alimaliza ujumbe
wake Mkurugenzi huyo wa tigo.
Tigo ambayo kwa sasa ina
jumla ya wateja Milioni 10 waliosajiliwa na kutoa ajira 300,000 kote nchini
ilianzishwa mnamo mwaka 1994.
Ujumbe wa Mkurugenzi Mtendajiwa Tigo
Ilikuwa ni furaha na usiku wa mask
wakichukua Selfie tayari kWhatsaap jamaa na marafiki bureeee
Wageni waalikwa wakifuatilia
Diego Gutierrez, akiandika ujumbe wa uzinduzi wa Whatsaap ya bure
Diego Gutierrez, akizungumza jambo na msanii maarufu wa vichekesho hapa nchini, JOTI, (katikati) na meneja wake Betty Nelson
Diego akiwashukuru washereheshaji
JI MKUU WA KENYA AFURAHIA UTENDAJI WA MAHAKAMA YA TANZANIA.
Jaji
Mkuu wa Kenya Mhe. Dkt. Willy Mutunga (katikati) akizungumza na
waandishi wa habari kuipongeza Mahakama ya Tanzania kwa utendaji wake wa
kusikiliza na kuamua mashauri mengi yanayopelekwa mahakamani. Kushoto
ni Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Mohamed Chande Othman na Kulia ni Jaji
Kiongozi Mhe. Shaan Lila.
Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Mohamed Chande Othman akizungumzia ujio wa Jaji Mkuu wa Kenya.
…………………………………………………………………………………………………………
Na. Aron Msigwa –MAELEZO.
Jaji Mkuu wa Kenya Mhe. Dkt. Willy
Mutunga ameipongeza Mahakama ya Tanzania kwa utendaji wake wa
kusikiliza na kuamua mashauri mengi yaliyopelekwa mahakamani kwa mwaka
wa sheria uliopita wa 2015 na kutoa wito kwa watendaji wa Mahakama ya
Tanzania kuendelea kufanya vizuri licha ya changamoto mbalimbali
wanazokabiliana nazo.
Jaji Mkuu wa Kenya ametoa pongezi
hizo mbele ya waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam mara baada ya
kukutana na kuongea na Majaji wa Mahakama Kuu na Mahakama ya Rufani
Tanzania kufuatia mwaliko alioupata wa kuhudhuria maadhimisho ya Siku ya
Sheria nchini yatakayofanyika Februari 4 mwaka huu.
Mhe. Dkt. Mutunga amesema kuwa
nchi ya Kenya mpaka sasa ina mashauri yapatayo 300,000 ambayo bado
hayajaamuliwa na kuongeza kuwa asilimia 5 ya wananchi wa Kenya ndio
hupeleka mashauri yao Mahakamani huku asilimia 95 iliyobaki wakitafuta
ufumbuzi wa kesi zao nje ya Mahakama.
“Ni kweli Tanzania mnafanya vizuri
katika katika kusikiliza mashauri kwa haraka, asilimia 95 ya Wakenya
hutafuta ufumbuzi wa kesi zao kwa viongozi wa kidini na Kimila kutokana
na baadhi yao kukosa fedha za kutosha za kufuatilia na kugharamia kesi
zao” Amesema.
Ameongeza kuwa Mahakama ya Kenya
kwa mwaka huu 2016 imejipangia malengo ya kuhakikisha kuwa inasuluhisha
mashauri yote ndani ya mwaka mmoja ili kuongeza ufanisi na imani kwa
wananchi.
Ameeleza kuwa Tanzania ina jambo
la kujifunza kutoka Kenya kufuatia mageuzi ya Katiba iliyoyafanya mwaka
2010 hususan kwenye baadhi ya maeneo ikiwemo na nafasi ya Mahakama
kwenye Katiba Mpya ambayo Tanzania inaendelea na mchakato wake.
Akizungumzia mageuzi hayo ambayo
tayari Kenya imeyafanya kufuatia kuwepo kwa Katiba mpya Mhe. Mutunga
amesema kuwa ni pamoja kupungua kwa madaraka ya Rais katika kuteua
Majaji, na nafasi za Majaji kutangazwa na watu kupeleka maombi na sifa
zao kujadiliwa ambapo wananchi huruhusiwa kutoa maoni kwa Tume ya
Mahakama ya Kenya kuhusu majaji hao kabla ya kuapishwa.
Aidha, ameeleza kuwa Watanzania
wana kila sababu ya kujivunia umoja na mshikamano uliopo ambao
umesababishwa na waasisi wa taifa hilo huku akibainisha kuwa majadiliano
na upatikanaji wa Katiba Mpya utafanywa na Watanzania wenyewe kwa kuwa
Watanzania ni walimu na mfano wa kuigwa katika Jumuiya ya Afrika
Mashariki.
Kwa upande wake Jaji Mkuu wa
Tanzania Mhe. Mohamed Chande Othman akizungumzia ujio wa Jaji Mkuu wa
Kenya amesema kuwa Mahakama ya Tanzania imenufaika na ujio wake kwa kuwa
iko kwenye maadhimisho ya Wiki ya Sheria ambayo huwakutanisha wadau
mbalimbali wa sharia kujadili changamoto na mafanikio ya Sekta ya Sheria
nchini.
Amesema kuwa kufuatia ziara ya
Jaji Mkuu wa Kenya Mahakama ya Tanzania imejifunza masuala mbalimbali
ambayo ni muhimu katika ufanisi wa shughuli zake ikiwemo Maslahi ya
Watumishi wa Mahakama, Jukumu la Mahakama kutafsiri Katiba kwa kuangalia
historian a uchumi pia kuazima baadhi ya hukumu zilizotolewa nchini
Kenya kama ushauri.
Aidha, amebainisha kuwa Mahakama
ya Tanzania inao wajibu wa kuendelea kuongeza uwazi katika upatikanaji
wa watendaji wake wenye nia ya kuwatumikia wananchi na kuboresha njia za
kuwapata majaji.
SHEIKH ISSA PONDA APINGA MARUDIO YA UCHAGUZI MKUU ZANZIBAR
Katibu
wa Jumuiya na Taasisi ya Kiislam Tanzania, Sheikh Issa Ponda (kushoto),
akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam leo, wakati akitoa
taarifa ya kupinga kurudiwa kwa uchaguzi mkuu wa Zanzibar.
Msemaji wa Jumuiya na Taasisi ya Kiislam Tanzania, Sheikh Rajab Katimba akitoa ufafanuzi zaidi kuhusu kurudiwa kwa uchaguzi huo Zanzibar.
Sheikh Ponda akisalimiana na mwanahabari Said Powa wa gazeti la Tanzania Daima baada ya kumaliza kuzungumza na wanahabari.
Sheikh Ponda akiondoka baada ya kuzungumza na wanahabari.
MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA AKUTANA NA UONGOZI WA BENKI YA CRDB NA BENKI YA POSTA TANZANIA
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan,
akizungumza na Uongozi wa Benki ya CRDB ulioongozwa na Mkurugenzi
Mtendaji wa Benki hiyo Dkt. Charles Kimei wakati Uongozi huo
ulipomtembelea Makamu wa Rais Ofisini kwake Ikulu Dar es salaam leo
Februari 03,2016 kwa lengo la kumuelezea kuhusu Banki hiyo itakavyoweza
kusaidia wajasiriamali wadogo wadogo.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan
katikati akiwa katika picha ya pamoja na Uongozi wa Benki ya CRDB
ulioongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo Dkt. Charles Kimei
wakati Uongozi huo ulipomtembelea Makamu wa Rais Ofisini kwake Ikulu Dar
es salaam leo Februari 03,2016 kwa lengo la kumuelezea kuhusu Banki
hiyo itakavyoweza kusaidia wajasiriamali wadogo wadogo.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan,
akizungumza na Uongozi wa Benki ya Posta Tanzania wakati Uongozi huo
ulipomtembelea Makamu wa Rais Ofisini kwake Ikulu Dar es salaam leo
Februari 03,2016 kwa lengo la kumuelezea kuhusu Banki hiyo itakavyoweza
kusaidia wajasiriamali wadogo wadogo.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan
katikati akiwa katika picha ya pamoja na Uongozi wa Benki ya Posta
Tanzania wakati Uongozi huo ulipomtembelea Makamu wa Rais Ofisini kwake
Ikulu Dar es salaam leo Februari 03,2016 kwa lengo la kumuelezea kuhusu
Banki hiyo itakavyoweza kusaidia wajasiriamali wadogo wadogo.
(Picha na OMR)
HAKUNA MGOMO WA MADAKTARI MASWA-DED
Na Benedict John-MAELEZO-Dar es salaam.
………………………………………………..
Mkurugenzi
Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Simiyu Trasias Kagenzi amekanusha
madai yaliyoandikwa na baadhi ya vyombo vya Habari kuhusiana na taarifa
za kufanyika kwa mgomo unaotarajiwa kufanywa na baadhi ya Madaktari na
Wauguzi katika Hospitali mkoani Simiyu na kusema habari hizo sio za
kweli.
Kauli
hiyo ameitoa leo katika mahoajiano na Mwandishi wa Habari hii juu ya
kuwepo kwa mgomo huo ambapo alifafanua kuwa, taarifa hiyo haina ukweli
wowote kwani siku ya tarehe 02 Februari mwaka huu, alikuwa na kikao na
watumishi wote wa Hospitali hiyo ambapo kati ya mambo walioyajadili ni
stahili na hali ya kazi hospitalini hapo.
”Hapa
wilayani kwetu kuna baadhi ya waandishi ambao hawazingatii maadili ya
kazi zao hasa kwa kuandika habari zisizo na ukweli, nimeshangaa kusikia
taarifa hii kwasababu ukweli ni kwamba mimi nilikaa na watumishi wote
jana wakiwemo madaktari, wauguzi na madereva na moja ya mambo
tuliyojadili ni pamoja na mishahara yao na posho zao, na tulimaliza
kikao chetu kwa amani kabisa, sasa waandishi kama hawa tunawaita
makanjanja maana haina ukweli wowote”, alisema Kagenzi.
Aliongeza
kuwa, kitendo walichokifanya baadhi ya waandishi hao kuandika habari
hiyo sio jambo la busara kwani linaleta mkanganyiko na chuki baina ya
watumishi na viongozi wao na hata kwa serikali yao na amelaani jinsi
waandishi hao wanavyotumia kalamu zao vibaya kwa kupotosha umma wa
watanzania
”Inasikitisha
kwa kweli mtu anakurupuka bila kuwasiliana na Utendaji Mkuu wa
Hospitali na kuanza kuanza kukutana na madaktari anaowajua na kuanza
kuandika taarifa kama hizi na kuzirusha katika vyombo vya habari”,
alisisitiza Kagenzi.
Mkurugenzi
huyo amewataka waandishi wa habari kuzingatia maadili ya kazi zao ili
waweze kuandika habari ambazo zinatoa picha halisi badala ya
kuwaogopesha wananchi na hivyo kushindwa kwenda kupata huduma.
Kwa
upande wake Afisa Habari wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Bi. Stella Kalinga
alieleza kuwa baada ya kufuatailia taarifa aligundua kuwa siyo za kweli
kwani hakuna dalili yoyote ya mgomo kwa watumishi hao wa afya na wako
kazini wakiendelea na majukumu yao kama kawaida.
MATUKIO KATIKA KIKAO CHA BUNGE MJINI DODOMA
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiteta na Mbunge wa Gairo, Ahmed Shabiby kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma Februari 3, 2016.
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mbunge wa Manyovu, Albert Obama
Ntabaliba kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma Februari3, 2016.
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Mbunge wa Kibaha Vijijini Hamoud
Abuu Jumaa kwenye viwanja vya Bunge mJini Dodoma, Februari 3, 2016
Waziri Mkuu, Kassim Majliwa
akizungumza na Mbunge wa Kibaha Vijijini, Hamoud Abuu Jumaa (katikati)
na Mbunge wa Bukoba Vijijini Jasson Rweikiza kwenye viwanja vya Bunge
mjini Dodoma Februari 3, 2016.
Mbunge wa Mtera, Livingstone Lusinde akizungumza Bungeni Mjini Dodoma Februari 3, 2016.
(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
CFAO MOTORS YAFANYA ONYESHO LA BIASHARA YA MAGARI AINA YA SUZUKI KATIKA JENGO LA PSPF GOLDEN JUBILEE TOWERS
Gari hilo la Suzuki Vitara linavyoonekana kwa nyuma.
Gari hilo aina ya Suzuki Grand Vitara linavyoonekana ubavuni.
Moja
ya Suzuki magari ya CFAO yaliyopo kwenye maonyesho ya bidhaa mpya
walizonazo katika jengo la PSPF Golden Jubilee Tower lililopo Posta
jijini Dar es Salaam.
Suzuki hiyo inavyookena upande wa nyuma.
Gari ndogo Suzuki OMNI inavyookena kwa mbele.
upande
wa ndani unaogawa gari hilo la Suzuki ambao unaonesha upande wa dereva
na upande ambao mtu anaweza kutumia kwa kuweka mizigo na mambo mengine.
upande wa nyuma wa ndaniu wa gari hilo aina Suzuki OMNI.
…………………………………………………………………………
Kampuni ya uuzaji magari ya CFAO
imefanya onyesho la kuonyesha bidhaa mpya walizonazo katika jengo la
PSPF Golden Jubilee Tower lililopo Posta jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na Modewji Blog,
Meneja Masoko wa CFAO Motors, Sheikha Said amesema sababu ya kampuni
hiyo kufanya onyesho katika jengo hilo ni kuwaonyesha wateja wa kampuni
hiyo bidhaa mpya walizonazo katika sehemu zao wanazouzia magari
(showroom).
Amebainisha kuwa, mbali na
kuwaonyesha wateja lakini pia kuwaonyesha wafanyakazi na wananchi
mbalimbali ambao walikuwa hawajui bidhaa zinazopatikana CFAO Motors au
kwa wengine kuwa na shughuli nyingi hivyo kushindwa kufika katika
‘showroom’ zao na kupitia onyesho hilo wataweza kupata magari katika
maeneo yao ya kazi.
“Tupo hapa kwa hili kuwasogezea
huduma watu wa aina mbalimbali na wafanyakazi wa taasisi mbalimbali
waone bidhaa tulizonazo,” alisema Bi. Said.
Nae Afisa Mauzo wa Suzuki, David
Kritsos alisema kupitia onyesho hilo wananchi na wafanyakazi wa ofisi
mbalimbali wanaweza kununua magari wanayopendelea na wanaweza kusaidiwa
na CFAO Motors kupata mkopo benki ili waweze kupata fedha za kununua
magari hayo na kulipa mkopo taratibu.
Alisema CFAO ndiyo kampuni pekee
nchini yenye nafasi ya kusambaza bidhaa za Suzuki na magari yote
wanayoyauza bado ni mapya yakiwa bado hayajatumika kabisa.
Showroom hiyo itaendelea hadi hapo 4 Februari.
DK. SALIM KUZINDUA KITUO CHA UTAFITI NA MAFUNZO YA UYOGA CHA CHUO KIKUU CHA KAIRUKI
Makamu
Mkuu wa Chuo cha Kumbukumbu ya Kairuki, Prof. Keto Mshigeni akizungumza
na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kuhusu maadhimisho ya 17 ya kumbukumbu ya Prof. Hubert Kairuki yatakayofanyika kuanzia Februari 4. Kushoto ni Ofisa Habari wa chuo hicho, Abraham Mwalugeni.
Makamu
Mwenyekiti wa Shirika la Afya na Elimu la Kairuki (KHEN), Dk. Muganyizi
Kairuki, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo,
kuhusu maadhimisho ya 17 ya kumbukumbu ya Prof. Hubert
Kairuki yatakayofanyika Februari 4. Katikati ni Makamu Mkuu wa Chuo cha Kumbukumbu
ya Kairuki, Prof. Keto Mshigeni na Ofisa Habari wa chuo hicho, Abraham Mwalugeni.
Kairuki yatakayofanyika Februari 4. Katikati ni Makamu Mkuu wa Chuo cha Kumbukumbu
ya Kairuki, Prof. Keto Mshigeni na Ofisa Habari wa chuo hicho, Abraham Mwalugeni.
…………………………………………………………………………………..
Katika kuadhimisha miaka 17 ya
kumbukuzi ya mwaasisi wa chuo kikuu cha kumbukumbu ya Hubert kairuki
kuanzia tarehe 4 hadi 6 Feb ambayo itakuwa ni siku ya kilele.Mh Dr
Salmin
Ahmed Salim ambaye pia ndio mkuu wa chuo hicho atazindua jengo la
utafiti na mafunzo ya Uyoga lililopo huko Boko katika eneo la chuo hicho.
Sambamba na uzinduzi huo pia shughuli nyingine katika kumbukizo hizo itakuwa ni pamoja na muhadhara kuhusu Uyoga utakaotolewa na
Profesa Keto Mshigeni ambaye ndiye makamu mkuu wa chuo hicho na mwanasayansi aliyebobea katika tafiti za uyoga.
Pia hospital ya Kairuki it ataendesha zoezi maalum la upimaji na matibabu ya
macho bila ya malipo kwa siku mbili mfululizo.
Pia patakuwepo matembezi ya hiara kwa ajili ya kusaidia wanawake wenye matatizo ya
saratani ya kizazi.
Aidha wanafunzi wa zamani wa chuo hicho waliopo Mwanza na mikoa ya kanda ya ziwa wataadhimisha
kumbukizo hizo kwa kufanya zoezi la kupima afya
bure kwa wakazi wa huko.
Ahmed Salim ambaye pia ndio mkuu wa chuo hicho atazindua jengo la
utafiti na mafunzo ya Uyoga lililopo huko Boko katika eneo la chuo hicho.
Sambamba na uzinduzi huo pia shughuli nyingine katika kumbukizo hizo itakuwa ni pamoja na muhadhara kuhusu Uyoga utakaotolewa na
Profesa Keto Mshigeni ambaye ndiye makamu mkuu wa chuo hicho na mwanasayansi aliyebobea katika tafiti za uyoga.
Pia hospital ya Kairuki it ataendesha zoezi maalum la upimaji na matibabu ya
macho bila ya malipo kwa siku mbili mfululizo.
Pia patakuwepo matembezi ya hiara kwa ajili ya kusaidia wanawake wenye matatizo ya
saratani ya kizazi.
Aidha wanafunzi wa zamani wa chuo hicho waliopo Mwanza na mikoa ya kanda ya ziwa wataadhimisha
kumbukizo hizo kwa kufanya zoezi la kupima afya
bure kwa wakazi wa huko.
Wananchi wahimizwa kujitokeza kupima Saratani.
MAMA JANETH MAGUFULI ATEMBELEA KAMBI YA WAZEE WASIOJIWEZA NA WALEMAVU YA NUNGE, KIGAMBONI, DAR ES SALAAM LEO
Mke
wa Rais Mama Janeth Magufuli akiweka saini katika kitabu cha wageni mara
baada ya kuwasili katika Kituo cha Makazi ya Wazee na Watu Walemavu cha
Nunge, Kigamboni, jijini Dar es salaam alikotembelea na kusikiliza
mahitaji yao pamoja na kutoa msaada wa mchele kilo 3000, Unga kilo 3000
na Maharage Kilo 1200 ikiwa msaada wake kwa wazee na walemavu hao.
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli
akisikiliza taarifa kutoka kwa Bw. Ojuku Mgedzi, Mkuu wa Kituo cha
Makazi ya Wazee na Watu Walemavu cha Nunge, Kigamboni,
jijini Dar es salaam alikotembelea na kusikiliza mahitaji yao pamoja na
kutoa msaada wa mchele kilo 3000, Unga kilo 3000 na Maharage Kilo 1200
ikiwa msaada wake kwa wazee na walemavu hao.
Mke
wa Rais Mama Janeth Magufuli akipokea taarifa kutoka kwa Bw. Ojuku
Mgedzi, Mkuu wa Kituo cha Makazi ya Wazee na Watu Walemavu cha Nunge, Kigamboni,
jijini Dar es salaam alikotembelea na kusikiliza mahitaji yao pamoja na
kutoa msaada wa mchele kilo 3000, Unga kilo 3000 na Maharage Kilo 1200
ikiwa msaada wake kwa wazee na walemavu hao.
Mke
wa Rais Mama Janeth Magufuli akioneshwa maeneo mbalimbali na Bw. Ojuku
Mgedzi, Mkuu wa Kituo cha Makazi ya Wazee na Watu Walemavu cha Nunge, Kigamboni,
jijini Dar es salaam alikotembelea na kusikiliza mahitaji yao pamoja na
kutoa msaada wa mchele kilo 3000, Unga kilo 3000 na Maharage Kilo 1200
ikiwa msaada wake kwa wazee na walemavu hao.
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli
akisalimiana na wagonjwa waliofika kupata huduma katika zahanati ya
Kituo cha Makazi ya Wazee na Watu Walemavu cha Nunge, Kigamboni,
jijini Dar es salaam alikotembelea na kusikiliza mahitaji yao pamoja na
kutoa msaada wa mchele kilo 3000, Unga kilo 3000 na Maharage Kilo 1200
ikiwa msaada wake kwa wazee na walemavu hao.
Mke
wa Rais Mama Janeth Magufuli akitembelea chumba cha kujifungulia cha
zahanati ya Kituo cha Makazi ya Wazee na Watu Walemavu cha Nunge,
Kigamboni, jijini Dar es salaam alikotembelea na kusikiliza mahitaji yao
pamoja na kutoa msaada wa mchele kilo 3000, Unga kilo 3000 na Maharage
Kilo 1200 ikiwa msaada wake kwa wazee na walemavu hao.
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akisalimiana kwa furaha na wakaazi wa Kituo cha Makazi ya Wazee na Watu Walemavu cha Nunge, Kigambo
ni, jijini Dar es salaam alikotembelea na kusikiliza mahitaji yao
pamoja na kutoa msaada wa mchele kilo 3000, Unga kilo 3000 na Maharage
Kilo 1200 ikiwa msaada wake kwa wazee na walemavu hao.
Mkuu
wa wilaya ya Temeke Mhe Sophia Mjema akimkaribisha Mke wa Rais Mama
Janeth Magufuli kuhutubia wakaazi wa Kituo cha Makazi ya Wazee na Watu
Walemavu cha Nunge, Kigambo
ni, jijini Dar es salaam alikotembelea na kusikiliza mahitaji yao
pamoja na kutoa msaada wa mchele kilo 3000, Unga kilo 3000 na Maharage
Kilo 1200 ikiwa msaada wake kwa wazee na walemavu hao.
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akihutubia wakaazi wa Kituo cha Makazi ya Wazee na Watu Walemavu cha Nunge, Kigambo
ni, jijini Dar es salaam alikotembelea na kusikiliza mahitaji yao
pamoja na kutoa msaada wa mchele kilo 3000, Unga kilo 3000 na Maharage
Kilo 1200 ikiwa msaada wake kwa wazee na walemavu hao.
Mke wa Rais
Mama Janeth Magufuli akimkabidhi mchele, unga na maharage Mzee Anthony
Kingongoti Mwenyekiti wa wakaazi wa Kituo cha Makazi ya Wazee na Watu
Walemavu cha Nunge, Kigambo ni, jijini Dar es salaam alikotembelea na
kusikiliza mahitaji yao pamoja na kutoa msaada wa mchele kilo 3000, Unga
kilo 3000 na Maharage Kilo 1200 ikiwa msaada wake kwa wazee na walemavu
hao.
Mke wa Rais
Mama Janeth Magufuli akipokea shukurani kutoka kwa Mzee Anthony
Kingongoti Mwenyekiti wakaazi wa Kituo cha Makazi ya Wazee na Watu
Walemavu cha Nunge, Kigambo ni, jijini Dar es salaam
alikotembelea na kusikiliza mahitaji yao pamoja na kutoa msaada wa
mchele kilo 3000, Unga kilo 3000 na Maharage Kilo 1200 ikiwa msaada wake
kwa wazee na walemavu hao.
Mke
wa Rais Mama Janeth Magufuli akimshukuru Mzee Anthony Kingongoti
Mwenyekiti wakaazi wa Kituo cha Makazi ya Wazee na Watu Walemavu cha
Nunge, Kigambo ni,
jijini Dar es salaam alikotembelea na kusikiliza mahitaji yao pamoja na
kutoa msaada wa mchele kilo 3000, Unga kilo 3000 na Maharage Kilo 1200
ikiwa msaada wake kwa wazee na walemavu hao.
PICHA NA IKULU
TAARIFA KUHUSU WATUMISHI WA UMMA KUUZIWA FOMU ZA OPRAS
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
OFISI YA RAIS
OFISI YA RAIS
FOMU YA TATHMINI YA UTENDAJI KAZI (OPRAS) HAIUZWI
Ofisi
ya Rais-Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora inawaelekeza
waajiri wote nchini kuhakikisha watumishi katika sehemu zao za kazi
wanapata Fomu ya Wazi ya Mapitio na Upimaji Utendaji Kazi (OPRAS) kwa
utekelezaji bila usumbufu.
Fomu
za OPRAS zinapatikana katika Tovuti ya Ofisi ya Rais-Menejimenti ya
Utumishi wa Umma yenye anuani, www.utumishi.go.tz. Waajiri wote
wanaelekezwa kutembelea tovuti hii na kutoa nakala za kutosha kwa idadi
ya watumishi katika maeneo yao ya kazi. Kwa watumishi wanaoweza kutoa
fomu hizi wenyewe wanaruhusiwa kufanya hivyo.
Imebainika
kuwa katika baadhi ya Taasisi za Umma watumishi wanaelekezwa kununua
fomu za OPRAS kutoka kwa watu binafsi. Kitendo hiki ni kwenda kinyume
cha Sheria, Kanuni na Taratibu zilizopo na pia ni usumbufu kwa
watumishi. Fomu za OPRAS haziuzwi na watumishi hawatatakiwa kuzinunua.
Endapo Mtumishi atashawishiwa au kulazimishwa kununua fomu za OPRAS atoe
taarifa Ofisi ya Rais-Utumishi na Utawala Bora ili hatua stahiki
zichukuliwe. Waajiri wote wanakumbushwa kuwa ni wajibu wao kuwapatia
watumishi walio chini yao fomu hizi na kuzihifadhi baada ya
utekekelezaji na si vinginevyo.
Serikali
ilianzisha matumizi ya Mfumo wa Wazi wa Mapitio na Tathmini ya Utendaji
Kazi (OPRAS) Mwezi Julai 2004, kupitia Waraka wa Utumishi Na. 2 wa
mwaka 2004. Hivyo kutoka wakati huo, OPRAS ilifuta mfumo wa zamani wa
kupima utendaji kazi wa mtumishi kwa njia ya siri.
Mabadiliko
ya kutathmini utendaji kazi wa Watumishi wa Umma kwa uwazi yanakwenda
sambamba na Sera ya Menejimenti na Ajira katika Utumishi wa Umma ya
mwaka 1998 kama ilivyorekebishwa mwaka 2008 ambazo zote zinasisitiza
uwekaji wa mifumo ya menejimenti ya utendaji bora wa kazi inayojali
matokeo.
Utekelezaji
wa OPRAS katika taasisi za Umma ni hatua muhimu kwa Serikali katika
kuboresha utendaji kazi na utoaji huduma kwa Umma. Hivyo ni wajibu wa
kila mwajiri kusimamia na kuhakikisha kuwa watumishi wote walio chini
yao wanajaza fomu hizo na kuwasilisha taarifa za utekelezaji katika
Ofisi ya Rais-Utumishi na Utawala Bora bila kukosa.
IMETOLEWA NA KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI Kny: KATIBU MKUU OFISI YA RAIS-UTUMISHI
MKOA MPYA SONGWE NA WILAYA MPYA ZAANZISHWA
…………………………………………………………………………………….
(Na Raymond Mushumbusi-maelezo)
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.John Pombe Joseph Magufuli
ameidhinisha kuanzishwa kwa mkoa mpya wa Songwe na wilaya nyingine mpya
nchini.
Akitoa tamko hilo kwa niaba ya Rais Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI) Mhe George Simachawene amesema kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 imempa Mamlaka Rais ya kugawa Nchi kwa kadri ambavyo atakapoona inafaa.
Mhe George Simachawene amesema kutokana na mamlaka hayo aliyopewa Rais jumla ya Wilaya sita na Mkoa mmoja wa Songwe umeanzishwa kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 na Mkoa mpya wa Songwe umeanzishwa kutoka Mkoa wa Mbeya.
Amezitaja Wilaya mpya zilizoanzishwa kuwa ni Wilaya ya Songwe Mkoa wa Songwe,Wilaya ya Ubungo Mkoa wa Dar es salaam, Wilaya ya Kibiti Mkoa wa Pwani, Wilaya ya Kigamboni Dar es salaam, Wilaya ya Mlanyi Mkoa wa Morogoro na Wilaya ya Tanganyika Mkoa wa Katavi.
“ Nichukue fursa hii kuwaagiza Wakuu wa Mikoa wote ambao Wilaya mpya zimeanzishwa kufanya maandalizi rasmi ili Mkoa na Wilaya hizo ziweze kuanza kufanya kazi,aidha mkazo uwekwe kwenye upatikanaji wa Ofisi na huduma zote muhimu kupatikana kwa urahisi katika Mkoa naWilaya hizo mpya” Alisema Mhe Simbachawene.
Akitoa tamko hilo kwa niaba ya Rais Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI) Mhe George Simachawene amesema kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 imempa Mamlaka Rais ya kugawa Nchi kwa kadri ambavyo atakapoona inafaa.
Mhe George Simachawene amesema kutokana na mamlaka hayo aliyopewa Rais jumla ya Wilaya sita na Mkoa mmoja wa Songwe umeanzishwa kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 na Mkoa mpya wa Songwe umeanzishwa kutoka Mkoa wa Mbeya.
Amezitaja Wilaya mpya zilizoanzishwa kuwa ni Wilaya ya Songwe Mkoa wa Songwe,Wilaya ya Ubungo Mkoa wa Dar es salaam, Wilaya ya Kibiti Mkoa wa Pwani, Wilaya ya Kigamboni Dar es salaam, Wilaya ya Mlanyi Mkoa wa Morogoro na Wilaya ya Tanganyika Mkoa wa Katavi.
“ Nichukue fursa hii kuwaagiza Wakuu wa Mikoa wote ambao Wilaya mpya zimeanzishwa kufanya maandalizi rasmi ili Mkoa na Wilaya hizo ziweze kuanza kufanya kazi,aidha mkazo uwekwe kwenye upatikanaji wa Ofisi na huduma zote muhimu kupatikana kwa urahisi katika Mkoa naWilaya hizo mpya” Alisema Mhe Simbachawene.
MATUKIO YA PICHA KATIKA KIKAO CHA BUNGE MJINI DODOMA
Mwenyekiti wa Bunge Mhe.Andrew
Chenge pamoja na Waziri wa Nchi Ofisi Utumishi na utawala Bora
Mhe.Angellina Kairuki wakiwasili katika viwanja vua Bunge kwa ajili ya
kushiriki kikao cha 7 cha Bunge la 11 linaloendelea Mjini Dodoma.
Mwenyekiti wa Bunge Mhe.Andrew
Chenge akiwasili katika ukumbi wa Bunge tayari kwa kuongoza kikao cha 7
cha Bunge la 11 linaloendelea Mjini Dodoma.
Mwenyekiti wa Bunge Mhe.Andrew
Chenge akiongoza sala kwa ajili ya Bunge na Wabunge wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania katika kikao cha 7 cha Bunge la 11 linaloendelea
Mjini Dodoma.
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya
Waziri Mkuu Sera,Bunge Kazi, Vijana na Ajira Mhe Anthony Mavunde akijibu
hoja toka kwa Wabunge mbalimbali katika kikao cha 7 cha Bunge la 11
linaloendelea Mjini Dodoma
Waziri wa Nchi Ofisi Utumishi na
utawala Bora Mhe.Angellina Kairuki akijibu hoja toka kwa Wabunge
mbalimbali katika kikao cha 7 cha Bunge la 11 linaloendelea Mjini Dodoma
Wairi wa Ulinzi na Jeshi la
Kujenga taifa Mhe dkt Hussein Mwinyi akiteta jambo na Waziri wa
Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe William Lukuvi katika kikao cha 7
cha Bunge la 11 linaloendelea Mjini Dodoma
Waziri wa Ujenzi,uchukuzi na
Mawasiliano Mhe.prof Makame Mbalawa akijibu hoja toka kwa Wabunge
mbalimbali katika kikao cha 7 cha Bunge la 11 linaloendelea Mjini Dodoma
Mwanasheria Mkuu wa Serikali
Mhe.George Masaju akijibu hoja toka kwa Wabunge mbalimbali katika kikao
cha 7 cha Bunge la 11 linaloendelea Mjini Dodoma
Picha na Raymond Mushumbusi MAELEZO
TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA KWA VYOMBO VYA HABARI
JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA LINAWASHIKILIA RAIA WAWILI WA NCHINI ETHIOPIA KWA KOSA LA KUINGIA NCHINI BILA KIBALI.
JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA LINAWASHIKILIA WATU 08 KWA MAKOSA MBALIMBALI.
KATIKA TUKIO LA KWANZA:
MTU MMOJA [DEREVA] WA GARI LENYE NAMBA ZA USAJILI T. 321 CSV AINA YA TOYOTA COASTER AITWAYE LWIMIKO MWANSASU [36] MKAZI WA UYOLE ALIFARIKI DUNIA BAADA YA GARI LENYE NAMBA ZA USAJILI T. 877 CWE AINA YA SCANIA BASI MALI YA KAMPUNI YA SUPERSHEM LILILOKUWA LIKIENDESHWA NA DEREVA EMANUEL JOHN [42] MKAZI WA MWANZA KUGONGANA NA GARI HILO NA KISHA KULIGONGA GARI JINGINE LENYE NAMBA ZA T. 321 CSV AINA YA TOYOTA HIACE LILILOKUWA LIKIENDESHWA NA DEREVA AMBAKISYE MBOMA [45] MKAZI WA AIRPORT.
TUKIO HILO LIMETOKEA MNAMO TAREHE 02.02.2016 MAJIRA YA SAA 06:30 ASUBUHI HUKO ENEO LA SOWETO, KATA YA ILOMBA, TARAFA YA IYUNGA, JIJI NA MKOA WA MBEYA.
CHANZO CHA AJALI HIYO NI MWENDO KASI WA BASI HILO LILILOKUWA LINATOKA MBEYA KUELEKEA MWANZA. DEREVA AMEKAMATWA. MWILI WA MAREHEMU UMEHIFADHIWA KATIKA HOSPITALI YA RUFAA MBEYA. UPELELEZI UNAENDELEA.
MTU MMOJA [DEREVA] WA GARI LENYE NAMBA ZA USAJILI T. 321 CSV AINA YA TOYOTA COASTER AITWAYE LWIMIKO MWANSASU [36] MKAZI WA UYOLE ALIFARIKI DUNIA BAADA YA GARI LENYE NAMBA ZA USAJILI T. 877 CWE AINA YA SCANIA BASI MALI YA KAMPUNI YA SUPERSHEM LILILOKUWA LIKIENDESHWA NA DEREVA EMANUEL JOHN [42] MKAZI WA MWANZA KUGONGANA NA GARI HILO NA KISHA KULIGONGA GARI JINGINE LENYE NAMBA ZA T. 321 CSV AINA YA TOYOTA HIACE LILILOKUWA LIKIENDESHWA NA DEREVA AMBAKISYE MBOMA [45] MKAZI WA AIRPORT.
TUKIO HILO LIMETOKEA MNAMO TAREHE 02.02.2016 MAJIRA YA SAA 06:30 ASUBUHI HUKO ENEO LA SOWETO, KATA YA ILOMBA, TARAFA YA IYUNGA, JIJI NA MKOA WA MBEYA.
CHANZO CHA AJALI HIYO NI MWENDO KASI WA BASI HILO LILILOKUWA LINATOKA MBEYA KUELEKEA MWANZA. DEREVA AMEKAMATWA. MWILI WA MAREHEMU UMEHIFADHIWA KATIKA HOSPITALI YA RUFAA MBEYA. UPELELEZI UNAENDELEA.
TAARIFA ZA MISAKO:
JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA LINAWASHIKILIA WATU WAWILI RAIA NA WAKAZI WA NCHINI ETHIOPIA 1. AYNO ASATA [21] NA 2. CHARU SUMESO [18] KWA KOSA LA KUINGIA NCHINI BILA KIBALI.
WAHAMIAJI HAO WALIKAMATWA MNAMO TAREHE 02.02.2016 MAJIRA YA SAA 09:00 ASUBUHI HUKO ENEO LA MAJENGO, KATA YA NSALAGA, TARAFA YA IYUNGA, JIJI NA MKOA WA MBEYA. TARATIBU ZA KUWAKABIDHI IDARA YA UHAMIAJI ZINAENDELEA.
JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA LINAWASHIKILIA WATU WAWILI RAIA NA WAKAZI WA NCHINI ETHIOPIA 1. AYNO ASATA [21] NA 2. CHARU SUMESO [18] KWA KOSA LA KUINGIA NCHINI BILA KIBALI.
WAHAMIAJI HAO WALIKAMATWA MNAMO TAREHE 02.02.2016 MAJIRA YA SAA 09:00 ASUBUHI HUKO ENEO LA MAJENGO, KATA YA NSALAGA, TARAFA YA IYUNGA, JIJI NA MKOA WA MBEYA. TARATIBU ZA KUWAKABIDHI IDARA YA UHAMIAJI ZINAENDELEA.
JESHI
LA POLISI MKOA WA MBEYA LINAWASHIKILIA WATU WATANO 1. HAIDAN RODRICK
[35] 2. JULIUS BUTEMELE [53] 3. VISENT MAPILE [29] 4. DOTO MWASHITETE
[25] NA 5. JOSEPH BUTEMELE [40] WOTE WAKAZI WA ISANGAWANA WILAYA YA
CHUNYA MKOA WA MBEYA WAKIWA WANAKUNYWA POMBE MOSHI [GONGO] UJAZO WA LITA
TANO [5].
WATUHUMIWA KWA PAMOJA WALIKAMATWA MNAMO TAREHE 02.02.2016 MAJIRA YA SAA 14:45 MCHANA HUKO KIJIJI NA KATA YA ISANGAWANA, TARAFA YA KIPEMBAWE, WILAYA YA CHUNYA, MKOA WA MBEYA.
WATUHUMIWA KWA PAMOJA WALIKAMATWA MNAMO TAREHE 02.02.2016 MAJIRA YA SAA 14:45 MCHANA HUKO KIJIJI NA KATA YA ISANGAWANA, TARAFA YA KIPEMBAWE, WILAYA YA CHUNYA, MKOA WA MBEYA.
MTU MMOJA MKAZI WA IYULA WILAYA YA
MBOZI MKOA WA MBEYA ALIYEFAHAMIKA KWA JINA LA JUMANNE HAONGA [32]
ANASHIKILIWA NA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA AKIWA NA POMBE MOSHI
[GONGO] UJAZO WA LITA KUMI [10].
MTUHUMIWA ALIKAMATWA MNAMO TAREHE 02.02.2016 MAJIRA YA SAA 11:20 ASUBUHI HUKO KIJIJI, KATA NA TARAFA YA IYULA, WILAYA YA MBOZI, MKOA WA MBEYA.
MTUHUMIWA ALIKAMATWA MNAMO TAREHE 02.02.2016 MAJIRA YA SAA 11:20 ASUBUHI HUKO KIJIJI, KATA NA TARAFA YA IYULA, WILAYA YA MBOZI, MKOA WA MBEYA.
MTU
MMOJA MKAZI WA ILOLO WILAYA YA MBOZI MKOANI MBEYA ALIYEFAHAMIKA KWA JINA
LA DANIEL NZUNDA [30] ANASHIKILIWA NA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA
AKIWA POMBE MOSHI [GONGO] UJAZO WA LITA TANO [5].
MTUHUMIWA ALIKAMATWA KATIKA MSAKO ULIOFANYIKA MNAMO TAREHE 02.02.2016 MAJIRA YA SAA 13:40 MCHANA HUKO KIJIJI NA KATA YA ILOLO, TARAFA YA VWAWA, WILAYA YA MBOZI, MKOA WA MBEYA.
WATUHUMIWA WATAFIKISHWA MAHAKAMANI MARA BAADA YA UPELELEZI KUKAMILIKA.
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI MWANDAMIZI WA POLISI AHMED Z. MSANGI ANATOA WITO KWA JAMII KUACHA KUTUMIA POMBE HARAMU YA MOSHI [GONGO] KWANI NI KINYUME CHA SHERIA NA NI HATARI KWA AFYA YA MTUMIAJI. AIDHA ANATOA WITO KWA WAGENI KUFUATA TARATIBU ZILIZOWEKWA ZA KUINGIA NCHINI ILI KUJIEPUSHA NA MATATIZO.
Imesainiwa na:
[AHMED Z. MSANGI – SACP]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.
MTUHUMIWA ALIKAMATWA KATIKA MSAKO ULIOFANYIKA MNAMO TAREHE 02.02.2016 MAJIRA YA SAA 13:40 MCHANA HUKO KIJIJI NA KATA YA ILOLO, TARAFA YA VWAWA, WILAYA YA MBOZI, MKOA WA MBEYA.
WATUHUMIWA WATAFIKISHWA MAHAKAMANI MARA BAADA YA UPELELEZI KUKAMILIKA.
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI MWANDAMIZI WA POLISI AHMED Z. MSANGI ANATOA WITO KWA JAMII KUACHA KUTUMIA POMBE HARAMU YA MOSHI [GONGO] KWANI NI KINYUME CHA SHERIA NA NI HATARI KWA AFYA YA MTUMIAJI. AIDHA ANATOA WITO KWA WAGENI KUFUATA TARATIBU ZILIZOWEKWA ZA KUINGIA NCHINI ILI KUJIEPUSHA NA MATATIZO.
Imesainiwa na:
[AHMED Z. MSANGI – SACP]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.
WANANCHI WAASWA KUTOKUVAMIA MAENEO YA VIWANJA KIHOLELA KWANI WANACHANGIA MIGOGORO YA ARDHI
NA VICTOR MASANGU, KISARAWE
…………………………………………………
JAMII
hapa nchini imetakiwa kuachana na vitendo vya kuvamia mashamba na
viwanja vya waatu kiholela bila ya kuzingatia na taratibu na
zilizizowekwa kwani kufanya hivyo kunachangia kwa kiasi kikubwa
kuchochea vurugu na na uvunjifu wa amani kutokana na kuwepo kwa migogoro
ya ardhi.
Hayo
yamesemwa na Afisa mtendaji wa Tarafa ya Sungwi iliyopo Wilayani
Kisarawe, Mkoa wa Pwani Thomas Mollel wakati alipokuwa akijibu
malalamiko kwa waandishi wa habari yaliyoyotolewa na baadhi ya wananchi
wa kiluvya ‘B’ kuhusina na suala la uvamizi wa maeneo yao ya viwanja
kinyume na taratibu.
Mollel
alisema kwamba anashangazwa kuona baadhi ya wananchi wamekuwa
wakijichukulia sheria wenyewe kwa kuvamia maeneo ya watu na kuanza
kufanya ujenzi kitu ambacho kimesababisha kuwepo kwa hali ya uvunjifu wa
amani, ambapo ameongeza hawezi kuifumbia macho na atalivaia njuga suala
hio hili haki iweze kutendeka kwa kila mtu mwenye eneo lake kihalali.
“Kwa
kweli mimi sipendi kuoana wanannchi wanavunja sheria ambazo zimewekwa
kwa kuamua kuvamia maeneo ya watu na kuanz akufanya ujenzi hii sio
sahihi kwani kufanya hivyo mwisho wa siku kunaweza kusababisha uvunjifu
wa amani kutokaja na kuibuka kwa migogoro hiyo ya ardhi kwa ahiyo naomba
waachane na tabia hiyo,” aisema Mollel.
Aidha
Afisa Mtendaji huyo alibainisha kwamba wananchi wanapswa kubadiika na
kuzingatia sheria za nchi ziizowewekwa ii kuepekuna na hali ya
kugombania maeneo ya viwanja na mashamba kitu amabcho amedai ni kitendo
cha kujichukulia sheria mikononi.
Kwa
upande wake mmoja wa wananchi ambao wameingia katika mgogoro mkubwa
kutokana na eneo lake kuvamia anayejulikana kwa jina la Januaris Maganga
alimwomba Waziri mwenye dhamana kuliingilia kati sakata hilo kwani kwa
sasa limedumu kwa muda mrefu bila ya kutafutia ufumbuzi jambo ambalo
linamweka katika hali ya kuishi kwa mashaka kutokana na vitisho
anavyovipata kwa sasa.
“Mimi
nina eneo langu kama hekai mbili na nusu lakini nashangaa kuna mzee
mmoja ameamua kulivamia kinyume cha sheria kabisa wakati mimi eneo hii
ni langu kihaai na nina hati ambayo ninayo lakini bado analeta ukorofi
kwa hiyo mimi hai kama hii inabadi waziri mwenye dhamana atusaidie ili
tuweze kutatua mgogoro huu na mimi niweze kupata haki yangu,”alisema
Maganga.
Naye
mmoja wa wazee wa siku nyingi katika kijiji hicho cha kiluvya ‘B;
Rashid Kilusungu akizungumza kwa niaba ya wananchi wenzake kuhusina na
tabia ya wananchi kuvamia maeneo kiholela alisema sio jambo zuri kwani
linaweza kuchochea kutokea kwa vurugu hivyo ni vema busara zikatumika
ili hali ya amani na upendo iwepo.
MIGOGORO
ya viwanja na mashamba katika maeneo ya Wilaya ya Kisarawe bado
inaonekana kuwa ni sugu kutokana na mamlaka ambazo zinahusika
zinachangia kwa kiasi kikubwa kutokana na kuchelewesha kutoa hati za
wamiliki halali wa maeneo hayo, hali ambayo inasababisha wananchi kuamua
kuvamia na kujenga bila ya kuwa na kibali halali.
POLISI KUDHIBITI UPORAJI WA FEDHA KWENYE MABENKI
……………………………………………………………………………..
(Na Raymond Mushumbusi-MAELEZO)
Wizara
ya Mambo ya Ndani ya Nchi kupitia Jeshi la Polisi imejipanga kudhibiti
uhalifu unaofanywa na na baadhi watu kwa kupora fedha za wafanyabiashara
au watu binafsi kwa kutumia usafiri wa Pikipiki maarufu kama bodaboda.
Akijibu swali la Mhe. Oscar Rwegasira Mukasa Mbunge wa Biharamulo Magharibi (CCM) lililouliza ni zipi takwimu sahihi za matukio ya ujambazi yanayohusiana na uporajiwa fedha,Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Hamad Yussuf Massauni amesema matukio ya ujambazi yanayohusisha uporaji wa fedha kwa kipindi cha kuanzia mwaka 2013 hadi 2015 kama takwimu zinavyosema , kwa mwaka 2013 matukio 1.266, mwaka 2104 matukio 1,127 na mwaka 2015 yalikuwa 931.
” Jeshi la polisi limechukua hatua kwa kufanya kazi karibu na mabenki nchini ili kubaini kama kuna wafanyakazi wa mabenki wanashirikia na majambazi kufanya uporaji huo na watakaobainika tutawachukulia hatua kali za kisheria ikiwa ni pamoja na kuwafikisha mahakamani watakaokamatwa”
“ Napenda kuwaomba wananchi kutupa ushirikiano na hasa kwa wafanyabiashara wanaochukua fedha nyingi ili tuweze kuwapatia ulinzi ili kupunguza, ama kuondoa kabisa vitendo hivi vya uporaji wa fedha vilivyokothiri nchini kwa sasa” Alisema Mhe Massauni.
Aidha amewaomba waheshimiwa Wabunge kutoa elimu kwa wananchi wao kuhusu maswala ya ulinzi na usalama ili kupunguza vitendo vya uhalifu hasa uporaji wa fedha kwa wafanyabiashara kwa kutoa taarifa kwa Jeshi la Polisi wakiona tukio lolote linalopangwa kwa ajili ya kupora fedha.
Serikali kupitia Jeshi la Polisi linafanya ukaguzi wa pikipiki zote nchini ili kubaini uhalali wake na uhalali wa wamiliki wake ili kuweza kubaini pikipiki na wamiliki wanaohusika na vitendo vya uporaji wa fedha vinavyoshamiri siku hadi siku
Akijibu swali la Mhe. Oscar Rwegasira Mukasa Mbunge wa Biharamulo Magharibi (CCM) lililouliza ni zipi takwimu sahihi za matukio ya ujambazi yanayohusiana na uporajiwa fedha,Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Hamad Yussuf Massauni amesema matukio ya ujambazi yanayohusisha uporaji wa fedha kwa kipindi cha kuanzia mwaka 2013 hadi 2015 kama takwimu zinavyosema , kwa mwaka 2013 matukio 1.266, mwaka 2104 matukio 1,127 na mwaka 2015 yalikuwa 931.
” Jeshi la polisi limechukua hatua kwa kufanya kazi karibu na mabenki nchini ili kubaini kama kuna wafanyakazi wa mabenki wanashirikia na majambazi kufanya uporaji huo na watakaobainika tutawachukulia hatua kali za kisheria ikiwa ni pamoja na kuwafikisha mahakamani watakaokamatwa”
“ Napenda kuwaomba wananchi kutupa ushirikiano na hasa kwa wafanyabiashara wanaochukua fedha nyingi ili tuweze kuwapatia ulinzi ili kupunguza, ama kuondoa kabisa vitendo hivi vya uporaji wa fedha vilivyokothiri nchini kwa sasa” Alisema Mhe Massauni.
Aidha amewaomba waheshimiwa Wabunge kutoa elimu kwa wananchi wao kuhusu maswala ya ulinzi na usalama ili kupunguza vitendo vya uhalifu hasa uporaji wa fedha kwa wafanyabiashara kwa kutoa taarifa kwa Jeshi la Polisi wakiona tukio lolote linalopangwa kwa ajili ya kupora fedha.
Serikali kupitia Jeshi la Polisi linafanya ukaguzi wa pikipiki zote nchini ili kubaini uhalali wake na uhalali wa wamiliki wake ili kuweza kubaini pikipiki na wamiliki wanaohusika na vitendo vya uporaji wa fedha vinavyoshamiri siku hadi siku
Millioni 300 kujenga Barabara Rukwa
……………………………………………………………………………………
(Na Raymond Mushumbusi-MAELEZO )
Serikali
katika mwaka wa fedha 2015/2016 ilitenga Shillingi million 300 kwa
ajili matengenezo na ujenzi wa Barabara ya Kitosi- Wampembe katika
Wilaya ya Nkasi Mkoa wa Rukwa kupitia Wakala wa Barabara (TANROADS) ili
kufanya Barabara hiyo iweze kupitika katika kipindi chote cha mwaka.
Akijibu
swali la Mhe.Desdelius John Mipata Mbunge wa Nkasi Kusini (CCM)
liliouliza ni lini Serikali itaitikia kilio hiki cha wananchi wanaopata
shida kwa Barabara hizo kutopitika katika kipindi chote cha mwaka,Naibu
Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Mhandisi Edwin Ngonyani
amesema Serikali kupitia Wizara yake imesikia kilio cha wananchi wa
Wilaya ya Nkasi na inaendelea kutoa fedha za matengenezo ya Barabara ya
Kitosi-wampembe.
“ Kwa
mwaka wa fedha 2014/2015 Serikali ilitoa jumla ya Shillimgi Millioni
500 ili kufanya matengenezo ya Barabara ya Kitosi-Wampembe ili ziweze
kupitika katika kipindi chote cha mwaka” Alisema Mhe Ngonyani.
Aidha
,katika kipindi cha mwaka wa fedha 2014/2015 Serikali ilitenga jumla ya
Shillingi Millioni 45 na Shillingi Millioni 60 zimetengwa katika mwaka
wa fedha 2015/2016 kwa ajili ya matengenezo ya aina mbalimbali ya
barabara ya Nkana-Kala kupitia Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi ili
kuhakikisha inapitika kwa kipindi chote cha mwaka.
Ukarabati
wa barabara ya Kitosi-Wampembe yenye urefu wa kilomita 67 na Barabara
ya Nkana –kala yenye urefu wa kilometa 68 uko chini ya Mfuko wa Barabara
ikisimamiwa na Wakala wa Barabara (TANROADS) na Barabara zote hizi ziko
chini ya Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi ambayo inawajibika kuwezesha
Barabara zinapitika kwa kipindi chote cha mwaka.
SIDA WARIDHISHWA NA MIRADI YA REA
Mtambuzi
wa miradi kutoka Wakala wa Nishati Vijini, Mhandisi Elneema Mkumbo
akitoa maelezo juu ya utekelezaji wa miradi ya REA, kwa Mkuu wa Shirika
la Kimataifa la Maendeleo la Sweden( SIDA) Maria Van Berlokom (
aliyeweka mikono kifuania) ambao ni miongoni mwa wafadhili wa miradi
hiyo akiwa na ujumbe wake pamoja na wadau wengine wa maendeleo ikiwemo
Shirika la Maendeleo la Ujerumani( GIZ) wakati wakikagua utekelezaji wa
miradi ya REA katika mikoa ya kanda ya kaskazini.
Muonekano
wa nyumba zilizounganishwa na huduma ya umeme unaotekelezwa na Wakala
wa Nishati vijijini REA katika kijiji cha Kwedizinga mkoani Tanga.
……………………………………………………………………………………
Na Mwandishi Wetu
Shirika
la Kimataifa la maendeleo la Sweden( SIDA), limeridhishwa na
utekelezaji wa miradi ya Umeme inayofahiliwa na Shirika hilo hususan
usambazaji wa umeme vijijini unaotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini
REA kwa kushirikiana na Shirika la Umeme nchini( Tanesco), katika
maeneo mbalimbali nchini.
Mkuu wa Shirika la Kimataifa la maendeleo la Sweden( SIDA) Maria Van Berlekom amesema hayo mara baada ya kuona maendeleo ya wananchi wa vijijini wakati wa ziara yake ya kutembelea utekelezaji wa miradi hiyo katika mikoa ya kanda ya kaskazini .
Mkuu wa Shirika la Kimataifa la maendeleo la Sweden( SIDA) Maria Van Berlekom amesema hayo mara baada ya kuona maendeleo ya wananchi wa vijijini wakati wa ziara yake ya kutembelea utekelezaji wa miradi hiyo katika mikoa ya kanda ya kaskazini .
Diaego akitoa hotuba















No comments:
Post a Comment