Pages

Wednesday, November 25, 2015

TAMKO LA JUKWAA HURU LA WAZALENDO KUUNGA MKONO HOTUBA YA MAGUFULI


Mwenyekiti wa Jukwaa Huru la Wazalendo Ndugu Salum Ally Hapi akizungumza na waandishi wa habari kwenye hotel ya Travetine ,Magomeni jijini Dar es Salaam, kulia ni Katibu wa Jukwaa hilo Ndugu Mtela Mwampamba.
………………………………………………………………………………. 
Ndugu wanahabari,
Mbele yenu sisi tuliowaita hapa ni Jukwaa Huru la Wazalendo ambalo
limeitisha mkutano huu ili kufikisha yale tuliyoyakusudia kuwaeleza umma wa
watanzania.
Sote tunatambua kuwa nchi yetu imetoka katika uchaguzi mkuu ambao umetupatia
viongozi wapya wa awamu ya tano ya uongozi wa taifa letu chini ya Dr. John
Pombe Joseph Magufuli. Tunapenda kuwapongeza watanzania wote kwa uchaguzi wa
amani na utulivu. Aidha kwakua ndio mara yetu ya kwanza kuzungumza nanyi
tunapenda kuwapongeza wanahabari wote kwa kazi nzuri ambayo mmekua mkiifanya
kabla, wakati na baada ya uchaguzi mkuu nchini. Tunawashukuru sana.
Mkutano wetu huu umebeba madhumuni makubwa mawili.
Kwanza ni kumpongeza Mh. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa
 hotuba yake aliyoitoa Bungeni siku ya ufunguzi wa Bunge la 11 la Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania mnamo tarehe 19/11/2015. Tunaiunga mkono Hotuba yake
ambayo kwa kweli ilikuwa imebeba Uzalendo, Ujasiri, dira ya kweli ya maendeleo
ya taifa letu na muuelekeo mpya wa Serikali ya awamu ya tano. Mambo yote
aliyozungumzia Mh. Rais yamebeba maslahi mapana ya nchi yetu na yanalenga
kuijenga Tanzania mpya ambayo waasisi wa Taifa letu Mwalimu Julius Kambarage
Nyerere na Abeid Amani Karume walikusudia kuijenga.
Pili, pamoja na mambo mengi yaliyogusiwa na hotuba ya Mh. Rais, eneo la
kubana matumizi na kupunguza matumizi yasiyo ya lazima kwa Serikali ni
 moja katika mambo ambayo Jukwaa hili limeamua kuyaunga mkono kwa vitendo.
Mh. Rais alitoa mchanganuo wa eneo moja tu la safari za nje na jinsi lilivyo
ligharimu Taifa mabilioni ya shilingi na kuahidi kuwa serikali ya awamu ya tano
chini ya uongozi wake itajikita katika kupunguza matumizi yasiyo ya lazima.
Aidha Mh. Rais ameanza kutekeleza kwa vitendo ahadi yake hiyo ya kupunguza
matumizi yote yasiyo ya lazima Serikalini, ikiwemo hafla, warsha, makongamano
na safari za nje.
Jukwaa Huru la Wazalendo, linatambua kuwa kwa miaka kadhaa mbunge wa Kigoma
Mjini Mh. Zitto Kabwe amekuwa na msimamo wa kutokupokea posho za kitako tangu
akiwa mbunge wa Kigoma Kaskazini katika Bunge la 10. Pamoja na mh. Zitto,
Jukwaa pia limepokea taarifa za baadhi ya wabunge wa Bunge la 11 la Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania walioamua kuunga mkono juhudi za Mh. Rais za kupunguza
matumizi yasiyo ya lazima serikalini kwa kukataa hadharani kupokea posho ya
kitako ya mbunge (sitting allowance).
Mnamo tarehe 23/11/2015, mbunge wa Singida Magharibi (CCM) Mh. Elibariki
Imanuel Kingu alimwandikia barua Katibu wa Bunge akieleza msimamo wake wa
kukataa kulipwa posho ya kitako ya Bunge (sitting allowance) katika kipindi
chote cha miaka mitano (2015 –  2020). Huyu anakuwa ni mbunge wa pili
baada ya Mh. Zitto Kabwe kutoka hadharani na kukataa posho ambazo msingi wake
ni unyonyaji wa wanyonge na ubadhirifu wa kodi za wananchi.
Jukwaa linapenda kumpongeza Mh. Kingu Mbunge kwa ujasiri wake na Uzalendo
kwa Taifa lake, uliomfanya kuunga mkono juhudi za Mh. Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania kwa vitendo.
Jukwaa linatambua ya kwamba, mapambano ambayo Mh. Kingu Mbunge ameyaanzisha
ni makubwa, magumu na yanahitaji kuungwa mkono na watanzania wote wanaoipenda
nchi yao bila kujali itikadi za vyama. Tunafahamu, wapo baadhi ya wabunge
wabinafsi na wasio na huruma na wanyonge wa Taifa letu ambao hawajafurahishwa
na hatua hii ya wabunge kama Zitto na Kingu ya kukataa posho ya kitako. Baadhi
ya wabunge wameanza kumpigia simu na kumtumia jumbe (sms) za vitisho mh.
Elibariki Kingu (MB) na wengine wakibeza kuwa anatafuta cheo.
Jukwaa linalaani hatua za wabunge hao wanaopinga nia njema ya Mh. Elibariki
Kingu na Mh. Zitto Kabwe kwa uamuzi wao wa kukataa posho za kinyonyaji na hivyo
basi, Jukwaa linawaomba wananchi wote majimboni, kuwataka wabunge wao
waliowachagua kueleza misimamo yao hadharani juu ya kuunga mkono hatua ya
kukataa posho kama njia ya kupunguza matumizi ya Serikali yasiyo ya lazima.
Jukwaa linafahamu ya kwamba, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ndiye
mwenye mamlaka ya mwisho ya kuidhinisha masharti ya kazi za kibunge na stahiki
wanazopaswa kulipwa katika kazi hiyo.
Continue reading →

HAKUNA RATIBA YA SIKUKUU YA UHURU ILUYOTOLEWA NA KURUGENZI YA MAWASILIANO IKULU

01ba5967-5243-459e-9b80-1d1b71974b1b

SERIKALI YAAHIDI KUSHIRIKIANA NA MASHIRIKA NA WADAU WA HABARI KUTOKOMEZA VITENDO VYA UKATILI KWA WAANDISHI WA HABARI

IMG_2832
Mkuu wa ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linalohudumia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Zulmira Rodrigues (katikati) akisalimiana na Mjumbe wa bodi udhamini ya Mtandao wa Radio Jamii Tanzania (COMNETA), Balozi Mstaafu, Christopher Liundi alipowasili katika mkutano wa kitaifa wa mashauriano kuhusu hali ya usalama wa waandishi wa habari, uzinduzi wa kikosi kazi cha usalama wa waandishi wa habari na uandishi unaozingatia maadili ulioandaliwa na UNESCO. Kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Prof. Ole Sante Gabriel.
Na Rabi Hume, Modewjiblog
Serikali mpya ya awamu ya tano iliyochini ya rais Dr. John Magufuli, imeahidi kushirikiana na mashirika na wadau mbalimbali ambao wamekuwa wakipambana kuhakikisha waandishi wa habari wanakuwa salama na kufanya kazi zao kwa uhuru bili kuingiliwa ufanyaji wa kazi zao na mtu yoyote.
Ahadi hiyo imetolewa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Prof. Ole Sante Gabriel katika mkutano wa kitaifa wa mashauriano kuhusu hali ya usalama wa waandishi wa habari, uzinduzi wa kikosi kazi cha usalama wa waandishi wa habari na uandishi unaozingatia maadili ulioandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia na Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Prof. Gabriel amesema serikali ya awamu ya tano ipo tayari kushirikiana na mashirika na wadau mbalimbali ambao wapo kuwasaidia waandishi wa habari ili haki zao ziweze kutekelezwa kutokana na kuwepo kwa uvunjaji wa haki za wanahabari.
Amesema wanatambua kuwepo kwa changamoto hizo kwa waandishi wa habari na kwa serikali ya awamu ya tano itahakikisha kushirikiana na mashirika na wadau ili kutetea haki za wanahabari kwa kuwa na uhuru katika utendaji wa kazi zao bila kuingiliwa na mtu.
“Naahidi kuanzia sasa serikali itakuwa ikishirikiana nanyi kusaidia kuhakikisha kunakuwa na uhuru wa vyombo vya habari, nchi yetu kwa sasa haina sababu ya kuacha kuungana na ninyi kutokomeza vitendo hivyo kwa wanahabari, serikali ni mpya na tutalitekeleza jambo hilo kila tumaposhirikishwa kuhusu vitendo vibaya kwa wanahabari,” amesema Prof. Gabriel.
IMG_2843
Mkuu wa ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linalohudumia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Zulmira Rodrigues akitoa neno la ufunguzi katika mkutano huo kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi kufungua.
Aidha Katibu Mkuu huyo amewata waandishi wa habari kuwa pamoja na usaidizi ambao wizara imeamua kujitoa kuwasaidia pia wanapaswa kuandika habari zenye weledi na zilizo sahihi kwani kumekuwepo na kundi kubwa la waandishi wa habari ambao wamekuwa wakiandika habari ambazo hazina uhakika wala weledi na hivyo kuupotosha umma kwa habari wanazoandika ila kuanzia sasa wanabidi kubadilika kwa kuandika habari ambazo zitakuwa na fadia kwa jamii inayowazunguka.
Kwa upande wa UNESCO, kupitia kwa Mkuu wa ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Zulmira Rodrigues, amesema kumekuwepo na vitendo vingi ambavyo sio vya kibinadamu ambavyo wamekuwa wakifanyiwa waandishi wa habari na wao wameamua kujitoa kuhakikisha wanatokomeza vitendo hivyo.
Amesema kama jamii ikiungana kwa pamoja kutokomeza vitendo hivyo inawezekana kwani kutokuwepo uhuru wa waandishi wa habari katika utendaji wao wa kazi kunapelekea jamii kukosa baadhi ya taarifa muhimu ambazo kama kukipatikana uhuru wa habari kutawapa fursa wanahabari wa kuzitoa taarifa hizo.
IMG_2914
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Prof. Ole Sante Gabriel akisisitiza jambo wakati akifungua rasmi mkutano wa kitaifa wa mashauriano kuhusu hali ya usalama wa waandishi wa habari, uzinduzi wa kikosi kazi cha usalama wa waandishi wa habari na uandishi unaozingatia maadili ambao umeandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na Elimu, Sayansi (UNESCO).
“UNESCO tunapenda kuona vitendo hivyo havifanyiki kwa waandishi wa habari kama kuweka sheria ambazo zinawabana na kusababisha wanashindwa kufanya kazi zao kwa uhuru na tunaweza kuona kama serikali na kila mtu akiwa tayari tunaweza kumaliza tatizo hilo,” amesema Rodrigues.
Nae Makamu wa Rais wa Chama cha Kijamii cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS), Flaviana Charles amesema imekuwa ngumu kesi zinazokuwa zikiwahusu waandishi wa habari juu ya vitendo vya kikatili wanavyotendewa kutokana na ucheleweshwaji wa upelelezi unaofanywa na Jeshi la Polisi Tanzania akitolea mfano kesi ya mwandishi wa zamani wa Chaneli 10 mkoani Iringa, Daudi Mwangosi ambapo mpaka sasa ina miaka 4 na bado upelelezi haujakamilika.
IMG_3149
Makamu wa Rais wa Chama cha Kijamii cha Wanasheria wa Tanganyika, Bi. Flaviana Charles akifafanua jambo wakati wa mkutano huo.
IMG_2873
Pichani juu na chini ni wahariri wa vyombo vya habari, waandishi wa habari, wadau wa tasnia ya habari pamoja na maafisa wa UNESCO na taasisi mbalimbali walioshiriki mkutano huo.
IMG_2925
IMG_3178
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) katika tasnia ya Habari na Mawasiliano, Ayub Rioba akiwasilisha mada ya wajibu wa vyombo vya habari huku akitolea mfano wa moja ya habari iliyobeba kichwa cha habari “Uhuru wa habari watikiswa Zimbabwe” katika moja ya magazeti ya Serikali wakati wa mkutano wa kitaifa wa mashauriano kuhusu hali ya usalama wa waandishi wa habari, uzinduzi wa kikosi kazi cha usalama wa waandishi wa habari na uandishi unaozingatia maadili ulioandaliwa na UNESCO.
IMG_3115
Ofisa Miradi katika kitengo cha Mawasiliano na Tehama UNESCO, Nancy Kaizilege akiwasilisha mada ya Uhuru wa vyombo vya Habari katika mkutano huo.
IMG_3191
Mratibu wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), Mwanasheria Onesmo Olengurumwa akielezea jinsi mtandao wake unavyotoa msaada kwa wanahabari wanaokumbwa matukio mbalimbali katika utendaji wao hususan msaada wa kisheria.
IMG_3206
Mhariri Mtendaji wa Gazeti la Tanzania Daima, Neville Meena akiuliza swali kwa Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO), Assah Mwambene (hayupo pichani) katika mkutano wa kitaifa wa mashauriano kuhusu hali ya usalama wa waandishi wa habari, uzinduzi wa kikosi kazi cha usalama wa waandishi wa habari na uandishi unaozingatia maadili sambamba na kuadhimisha “International Day to #EndImpunity” ulioandaliwa na UNESCO.
IMG_3212
Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO), Assah Mwambene akitolea ufafanuzi wa swali la Mhariri Mtendaji wa Gazeti la Tanzania Daima, Neville Meena (hayupo pichani).
IMG_3227
Mkuu wa ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linalohudumia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Zulmira Rodrigues akitoa maoni katika katika mkutano wa kitaifa wa mashauriano kuhusu hali ya usalama wa waandishi wa habari, uzinduzi wa kikosi kazi cha usalama wa waandishi wa habari na uandishi unaozingatia maadili sambamba na kuadhimisha “International Day to #EndImpunity” ulioandaliwa na UNESCO.
IMG_3234
Mjumbe wa bodi udhamini ya Mtandao wa Radio Jamii Tanzania (COMNETA), Balozi Mstaafu, Christopher Liundi akitoa pongezi kwa Shirika la UNESCO katika kuhamasisha Amani kupitia, Redio za Jamii, makongamano mbalimbali pamoja na kuwashirikisha viongozi wa dini kuhubiri Amani nchini katika mkutano huo.
IMG_3237
Mwandishi wa habari mkongwe, Halima Sharrif akitoa maoni katika mkutano huo.
IMG_3047
IMG_3069
Kutoka kushoto ni Ofisa miradi katika kitengo cha Mawasiliano na Tehama UNESCO, Nancy Kaizilege, Mratibu wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), Mwanasheria Onesmo Olengurumwa, Mkuu wa ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linalohudumia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Zulmira Rodrigues pamoja na Makamu wa Rais wa Chama cha Kijamii cha Wanasheria wa Tanganyika, Bi. Flaviana Charles katika picha ya ukumbusho.
IMG_3107
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Prof. Ole Sante Gabriel (kushoto) akifurahi jambo na Mhariri Mtendaji wa Gazeti la Tanzania Daima, Neville Meena mara baada ya zoezi la picha ya pamoja.

Jumia.co.tz partners with Ecobank Tanzania for the launch of Black Friday in Tanzania

Jumia Tanzania (www.jumia.co.tz), Africa’s largest online shopping mall, launches its first edition of Black Friday on 27th November, in partnership with Ecobank Tanzania.
Dar es Salaam, November 24th, 2015 –Be ready for unbelievable discounts! On 27th November a unique online flash sale event, Black Friday, will take place on Jumia Tanzania (www.jumia.co.tz). Black Friday, one of the most popular shopping events in the world, is all about deals and bargain hunting during only one day. This year, Black Friday on Jumia Tanzania will start on Friday 27th November and will be extended until Monday 30th November.
Jumia is the first online mall in Africa (present in 11 countries in Africa) where customers can choose between a large range of products from fashion, to electronics such as phones and TVs. Jumia introduced Black Friday to the African market in 2013 and made it become the first and largest event of its kind in Africa. During this day, Africans search for the best deals and discounts that they would otherwise not get on a regular day.
“Originally established in the U.S. more than 50 years ago, Black Friday, which take place after Thanksgiving day, is now a well-known sales day both in the U.S. and Europe. People go mad for it. This year, we bring the concept to Tanzania. We’ve got mind blowing deals for our customers. And can’t wait to share them!” stated Jean-Philippe Boul, Managing Director of Jumia Tanzania.
For the 1st edition of Jumia Black Friday in Tanzania;Jumia has decided to partner with Ecobank Tanzania which isa Subsidiary of Ecobank Transnational Incorporated (ETI), a multinational bank presents in 36 African Countries.“With its wide network and a wide range of advanced electronic offering Ecobank is the right partner. The partnership will go beyond Black Friday, whereby Ecobank Customers will be able to purchase merchandise on Jumia.co.tz at a special discount of rate. The two companies will join their efforts to make payments on Jumia.co.tz an afterthought. Ecobank’s mission is to bring services closer to our all customers while connecting them to the rest of Africa through our wide network and diverse offering” said Eric Luyangi (Head of Altenative Channels)
In 2014, while more than 100 million Americans were shopping over the Black Friday holiday, millions more were shopping online on Jumia. Last year, Jumia reached an all-peak in sales within 24 hours and had over 1,500,000 online visitors. Over 50% of the visitors accessed the site through a mobile device viaAndroid oriOS. These sales represented an extraordinary tenfold order increase compared to 2013’s Black Friday.
“Africa’s disposable income & online consumption is growing at an extraordinary rate. In Tanzania, we expect to sell more in this year’s Black Friday than in the whole of 2014. But this is just the start. We are here for the long term and have plenty more surprises to come”, added Jean-Philippe Boul
Last year’s Black Friday sales primarily focused on consumer electronics, with particular interest in digital products such as flatscreen TVs, digital cameras and ventilation systems. This year, Jumia predicts that it will sell a lot more fashion & cosmetics too, with great deals such as all kinds of stylish dresses at 50% off. Jumia positions itself as the leading marketplace for high-end local and international brands. They work with everyone from local fashion brands such as Footstep (50% off!), to established mobile brands such as Samsung, Tecno or itel (up to 23% off –Tecno C8 below 274,000 TSH).  On Jumia’s Black Friday, you will be able to get your hands on the Samsung Tab4 7” tablet for less than 345,000 TSH (that’s 18% off!) and Sony 32” TV at 23% off.
Black Friday will also be a great occasion for Jumia Tanzania to launch InnJoo phones and tablet. InnJoo had already experienced a massive success in the other Jumia markets and is now ready to enter the promising Tanzanian market (InnJoo tablet F3, InnJoo Halo and Fire smartphones).
“By tapping into this global shopping phenomenon, with the support of our partner Ecobank Tanzania, we have created a powerful event that our customers will love.” concluded Jean-Philippe Boul.
About Black Friday
Black Friday is a popular label attached to the Friday following Thanksgiving Day in the US. This day marks the beginning of the busy shopping season during which most consumers typically start their Christmas/holiday shopping.

An explanation of the name « Black Friday » is that during that day so many people went out to shop that it caused traffic accidents and sometimes even violence. « Black Friday » officially opens the Christmas shopping season in center city, and it usually brings massive traffic jams and over-crowded sidewalks as the downtown stores are mobbed from opening to closing.”
Doorcrashers, special deals and heavy discounts on the most highly sought after holiday gifts are often offered by retailers in order to lure consumers into their stores in the hope that they will purchase other, more expensive, goods. Some bargain hunting consumers have even been known to camp out overnight in order to secure a place in line at a favorite store.Www.jumia.co.tz/black-friday
About Jumia
Jumia is Africa’s leading online shopping destination. Customers across the continent can shop amongst the widest assortment of high quality products at affordable prices – offering everything from fashion, consumer electronics, home appliances to beauty products. Jumia was the first African company to win an award at the World Retail Awards 2013 in Paris as the “Best New Retail Launch” of the year.
About Africa Internet Group
Africa Internet Group, the leading internet platform in Africa, promotes sustainable online growth that benefits both businesses and consumers. Firmly rooted in Africa’s startup ecosystem, the group provides easy-to-use services and smart solutions across the African internet sector. AIG is invested in furthering regional entrepreneurship and innovation through a passion for Africa, its culture and its people. AIG is the parent group of ten successful and fast-growing companies in more than 30 African countries. Its network of companies includes Carmudi, Easy Taxi, Everjobs, hellofood, Jovago, Jumia, Kaymu, Lamudi, Vendito and Zando.
About Ecobank Tanzania
Ecobank Tanzania is a Subsidiary of Ecobank Transnational Incorporated (ETI), a multinational bank Present in 36 African Countries. Ecobank began its operations in Tanzania on the 19th January 2010; the bank currently has 9 branches (Dar-es-salaam branches include:  Mwenge, Sokoine Drive, Uhuru, Msimbazi-Kariakoo, Quality Centre and Acacia- Kinondoni. Upcountry: Arusha, Mwanza and Mtwara); these branches are strategically located bringing financial advice closer to Tanzanians and ease of cross border trade due to the bank’s wide network. Ecobank Tanzania currently has 22 ATMs all accepting VISA, MasterCard’s, China Union Pay and Pan African Cards (PAC).

WANAHARAKATI WA TANZANIA WANATOA WITO KWA JAMII KUCHUKUA HATUA ILI KUMLINDA MTOTO APATE ELIMU BORA NA SALAMA

  Eda
Malick kutoka Tanzania Women and Children Welfare center akizungumza na
waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa siku 16 za kupinga ukatili wa
kijinsia
 Afande
Christina Onyango, Afisa wa Polisi, mkoa wa kipolisi Ilala akielezea
namna ambavyo dawati la jinsia wamejipanga kufikisha ujumbe wa siku 16
za kupinga ukatili wa kijinsia.
  Waandishi
wa habari kutoka vyombo mbalimbali nchini Tanzania wakihudhuria mkutano
na waandishi wa habari kuhusu uzinduzi wa siku 16 za kupinga ukatili wa
kijinsia.
 Bahati
Mandago kutoka shirika la Tanzania Human Rights fountain akielezea
mikakati ya shirika lake katika kufikisha ujumbe wa Funguka. Chukua
Hatua Mlinde Mtoto apate elimu.
 
Wadau
kutoka katika mashirika mbalimbali wanaoshiriki kikamilifu katika
utekelezaji wa maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia
wakiwa katika mkutano na waandishi wa habari
 Dr.
Judith Odunga Mkurugenzi wa Shirika la WiLDAF akisoma taarifa kwa
vyombo vya habari kuhusiana na kuanza kwa siku 16 za kupinga ukatili wa
kijinsia.
FUNGUKA! CHUKUA HATUA MLINDE MTOTO APATE ELIMU
Katika kuadhimisha Siku 16 za Kupinga Ukatili wa Kijinsia kuanzia
tarehe 25 Novemba mpaka 10 Desemba, WiLDAF, Mashirika ya Haki za Binadamu,
Wadau wa Maendeleo na Asasi za Kiraia watatoa elimu na kuhamasisha umma
kuchukua hatua kumlinda mtoto ili apate elimu bora na salama. Ulinzi wa mtoto ni
pamoja na kuzuia vitendo vyote  vya ukatili
wa kijinsia.
Maadhismisho ya SIku 16 za kupinga Ukatili wa kijinsia mwaka
huu yanalenga zaidi kuzungumzia suala zima la usalama  mashuleni, lengo kuu ikiwa kuhamasisha umma
kuhusu ukubwa wa tatizo la ukatili wa kijinsia kwa vijana na watoto wetu
mashuleni, kwani vitendo vingi vya ukatili wa kijinsa vimekuwa vikiripotiwa.
 
Utafiti uliyofanywa na Chuo cha Tiba Cha Muhimbili (MUHAS)
kwa kushirikiana na Shirika la Wanawake katika Sheria na Maendeleo Afrika,
(WiLDAF) umetambua hatari zinazochangia ukatili wa kijinsia ikiwa ni pamoja na
wazazi kutowajali watoto na kutoa adhabu kali kwao na hivyo kuwafanya watoto
kuwa na hofu. Wakati mwingine watoto kufanyiwa ukatili bila wao kufahamu. Aidha,
adhabu ya viboko inahusishwa kama moja ya aina za ukatili dhidi ya watoto. Hii
inaathiri maendeleo ya elimu ya watoto katika taifa letu.
 
Kukosekana kwa usawa kati ya watoto wa kiume na wa kike hunapelekea
kuwajengea hofu watoto wa kike,  na wakati
huo kuwajengea watoto wa kiume ujasiri wa kuona kuwa ni sahihi kwao kufanya  vitendo vya ukatili wa kijinsia.
Continue reading →
ST1

Muhimbili yapatiwa msaada wa vifaa vya kuokoa maisha ya watoto


Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) Tanzania, Dk Juma Gulaid akisoma taarifa kabla ya kukabidhi vifaa vya kuhudumia watoto katika hafla fupi iliyofanyika katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH). Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Donan Mmbando.Picha zote kwa hisani ya Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH).
ST2
Baadhi ya wauguzi wakisimsikiliza Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) Tanzania, Dk Juma Gulaid katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) .
ST3
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Donan Mmbando akizungumza katika hafla ya kupokea vifaa vya kisasa vya  kuhudumia watoto katika hospitali hiyo. Vifaa hivyo vimekabidhiwa  na Mwakilishi wa UNICEF Tanzania, Dk Juma Gulaid.
ST6
Mwakilishi wa UNICEF Tanzania, Dk Juma Gulaid akimkabidhi hati ya vifaa vya kuwahudumia watoto kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Donan Mmbando.
ST7
Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Profesa Lawrence Mseru akipokea hati ya vifaa kutoka kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Donan Mmbando. Vifaa hivyo vimetolewa  na UNICEF.
ST4
Baadhi ya wauguzi wakisimsikiliza Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) Tanzania, Dk Juma Gulaid katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH).
ST5
Baadhi ya vifaa vilivyokabidhiwa
………………………………………………………………………………….
Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) imepatiwa msaada wa vifaa kumi  vya tiba vya kuwahudumia watoto  mara wapougua na kufikishwa kwenye hospitali hiyo.
Vifaa hivyo vina thamani ya Dola za Kimarekani Laki moja sawa na zaidi Sh milioni 2 vimetolewa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF),kwa lengo la kupunguza vifo vya watoto walio chini ya umri wa miaka mitano.
Baadhi ya vifaa vilivyotolewa  ni Ventilator, medical, adult –child ,w/access pamoja na Warmer system , newborn, radiant, w/access.
Akizungumza wakati wa kukabidhi vifaa hivyo  Mwakilishi wa UNICEF Tanzania Dk Jama Gulaid amesema mchango wa UNICEF na michango ya wadau wengine itawezesha watumishi wa hospitali ya Muhimbili kuokoa maisha ya  watoto  ambao wanahitaji huduma za afya.
Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Donan Mmbando  amesema  hadi kufikia mwaka 2013  Tanzania imefanikiwa kupunguza vifo vya watoto hao kwa theluthi mbili.
Kwa mujibu wa Dk Mmbando, mwaka 2013 Tanzania imepunguza vifo hivyo na kufikia 54 kwa vizazi hai 1,000  na kufikia lengo la Milenia  na kwamba  mafanikio hayo yametokana na kiwango kikubwa cha chanjo , matumizi sahihi  ya dawa za Malaria pamoja na vyandarua.
Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa MNH, Profesa Lawrence Mseru amewashukuru UNICEF kwa msaada huo ambao utachangia kwa kiasi kikubwa kuokoa maisha ya watoto na kuboresha huduma za afya .



Serikali yajipanga kununua vivuko vipya 3 (VIDEO)

Kipindupindu chapungua DAR

Na Jaindexcquiline Mrisho- maelezo
 Idadi ya wagonjwa wa kipindupindu jijini Dar es salaam imepungua kufikia wagonjwa kumi na mbili (12) kwa mkoa mzima, huku wilaya ya Temeke ikiwa na wagonjwa saba,Kinondoni wagonjwa wanne na Ilala ikiwa na mgonjwa mmoja
.
Haya yamezungumzwa na Mratibu wa Magonjwa  ya kuambukiza wa Jiji la Dar es salaam  Bw. Alex Mkamba ofisini kwake leo akielezea jinsi gani mkoa umefanikisha kupambana na kipindupindu kwa kuzingatia usafi katika jiji.
Ameongeza kuwa katika kufanikisha mapambano dhidi ya kipundupindu wametoa mafunzo  juu ya mbinu shirikishi ya namna ya kujikinga na kipindupindu kwa watendaji wa mitaa na pia imewahimiza kukagua maeneo yao na kuwapa kibali cha kufunga maeneo ya biashara au maeneo yatoayo huduma za chakula  yasiyozingatia usafi.
Akielezea kuhusu huduma kwa wagonjwa wa kipindupindu jijini  Dar es salaam mratibu huyo amesema jiji lina dawa za kutosha za kuhudumia wagojwa ipasavyo  kwa kuwapatia huduma bora zaidi kuendana na kasi ya maambukizi yaliyopo.
“ hata leo Shirika la Afya Duniani (WHO) limetoa dawa za kusafishia maji (Water Guard) maboksi 45 kwa kila wilaya” Mkamba alifafanua.
Aidha alisema serikali imejipanga katika kudhibiti maambukizi mapya kwa kuwapima wagonjwa kabla na baada ya kuruhusiwa kutoka hospitalini  na aliwashauri wananchi kubadili tabia kwa kuhakikisha usafi unafanyika pia  kuchemsha maji na kuufanya usafi kuwa ni tabia yao ya kila siku.
Mpaka sasa jumla ya watu 55 wamefariki dunia kwa ugonjwa wa kipindupindu jijini Dar es salaam.

WANANCHI WAHIMIZWA KUJITOKEZA KWA WINGI KUPIMA AFYA ZAO KUELEKEA DESEMBA MOSI, 2015.

index 
Mwenyekiti Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Kudhibiti UKIMWI nchini Tanzania Dkt. Fatma Mrisho  akizungumza na waandishi wa Habari kuhusu Maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani mwaka huu ambayo inaadhimishwa kwa  kuwahimiza wananchi kujitokeza kwa wingi  kupima afya zao na kupata elimu ya kujikinga  na maambukizi ya ugonjwa huo.
……………………………………………………………………………………………
Na. Nyakongo Manyama- MAELEZO.
Dar es salaam.
Wito umetolewa kwa wananchi kote nchini kuyatumia maadhimisho ya Siku ya UKIMWI duniani ambayo huadhimishwa kila ifikapo Desemba 1 ya kila mwaka kupima afya zao ili kudhibiti maambukizi mapya ya VVU.
Akizungumza na waandishi wa Habari leo jijini Dar es salaam Mwenyekiti Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Kudhibiti UKIMWI nchini Tanzania Dkt. Fatma Mrisho amesema  Siku ya Ukimwi Duniani nchini itaadhimishwa kwa  kuwahimiza wananchi kujitokeza kwa wingi  kupima afya zao na kupata elimu ya kujikinga  na maambukizi ya ugonjwa huo.
Ameeleza kuwa  maadhimisho ya mwaka huu yataambatana na shughuli mbalimbali zikiwemo za Utoaji wa Elimu ya Afya na Upimaji wa hiari wa VVU katika maeneo mbalimbali kote nchini kupitia vituo vitakavyowekwa, Kufungua kituo cha maarifa cha udhibiti UKIMWI eneo la Manyoni mkoani Singida ambayo ni njia kuu kuelekea mikoa ya Kanda ya Ziwa na nchi za Jirani za Burundi na Rwanda.
Ameongeza kuwa Tume kwa kushirikiana na wadau mbalimbali itaendesha mikutano ya kitaalam kuhusu UKIMWI, Zoezi la upimaji wa hiari wa VVU kwa wananchi, Kupokea tamko litakalotolewa na Baraza la Watu wanaoishi na VVU pamoja na Uzinduzi wa taarifa ya tathmini ya Sheria zinazotumika  zinazohitaji kurekebishwa zinazozuia malengo ya sifuri 3.
 Aidha Tume itapokea taarifa ya hali ya maambukizi ya VVU duniani itakayotolewa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki Moon kuhusu dunia na mapambano dhidi ya VVU.
Dkt. Fatma amefafanua kuwa mgeni rasmi katika maadhimisho hayo anatarajiwa kuwa  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli ambapo pamoja na mambo mengine atazindua Mfuko wa UKIMWI ambao utakuwa chachu ya kupunguza maambukizi ya VVU nchini.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa ufuatiliaji na tathmini kuhusu UKIMWI wa TACAIDS Dkt.Jerome Kamwela amesema kuwa kiwango cha maambukizi ya UKIMWI kwa mujibu wa takwimu za mwaka 2011/2012 kimepungua na kufikia asilimia 5.3 huku mikoa ya nyanda za juu kusini ya Njombe, Iringa  na Mbeya ikiongoza kwa kuwa na maambukizi zaidi  na mikoa ya Manyara, Tanga na Lindi  ikiwa na maambukizi ya chini ya asilimia mbili.
Dkt. Kamwela amesema kuwa maambukizi ya VVU ni mengi hasa kwa kundi la watu wenye umri wa miaka 19-24 huku makundi ya wanaojidunga, wanaume wanaofanya mapenzi ya jinsia moja, wanawake wanaofanya biashara ya ngono yakiendelea kuwa katika hatari ya kuathiriwa zaidi na maambukizi ya VVU.

WAZIRI MKUU ATAKA KILA MKURUGENZI ASOME HOTUBA YA RAIS, AIFANYIE KAZI

index 
WAZIRI MKUU Majaliwa Kassim Majaliwa amewataka wakurugenzi wa vitengo na wakuu wa taasisi katika Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI) wapate nakala ya hansard ya hotuba ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli ya kuzindua Bunge la 11, waisome na kufanyia kazi maeneo yote aliyoyaainisha.
“Katibu Mkuu hakikisha umepata hansard ya hotuba ya Mheshimiwa Rais wakati akizindua Bunge na uhakikishe kila mkurugenzi ana nakala na kila mmoja wenu lazima ahakikishe anafanyia maeneo ambayo Mheshimiwa Rais ameyaainisha. Ni lazima tuelewane ni nini tunapaswa tufanye,” alisema.
Ametoa kauli hiyo leo mchana (Jumanne, Novemba 24, 2015) wakati akizungumza na wakuu wa taasisi, wakurugenzi na watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI) kwenye mkutano uliofanyika ofisi ndogo ya TAMISEMI, barabara ya Kivukoni, jijini Dar es Salaam.
“Ninatamani kuona mabadiliko ya utendaji kazi Serikalini katika kipindi kifupi. Natamani kila mmoja asiridhike na uzembe unaofanywa huku chini. Ni nyote ni wataalamu, kwa hiyo mnapaswa kudhirisha elimu yenu na ujuzi mlionao,” aliwasisitizia Wakurugenzi hao.
Alisema kila mkurugenzi na mkuu wa taasisi anapaswa kuongeza usimamizi na ufuatiliaji wa kazi kwenye sekta yake kwani hilo litasaidia kukidhi matarajio ya Watanzania ya kuona mabadiliko ya utendaji kazi kwenye Serikali ya Awamu ya Tano. “Ninyi wakurugenzi siyo desk officers bali ni field officers. Nataka muweke utaratibu wa kwenda vijijini mkasimamie watu wenu, pia mhimize uadilifu, uaminifu na weledi wa kazi,” alisisitiza.
“Mambo ninayotaka mhimize watendaji waliopo chini yenu ni pamoja na haya yafuatayo: muda wa kuripoti kazini uzingatiwe, muda wa kukaa kazini uzingatiwe, utokaji kazini kwenda kwenye chai na chakula cha mchana udhibitiwe, na mipango na malengo ya kazi kwa siku ni lazima yafikiwe,” alisema.
“Tunataka kujua mtumishi amefanya nini tangu alipoingia ofisini. Suala siyo kukaa tu ofisini, kwani kuna mtu anakaa ofisini, hajaenda hata kunywa chai lakini ukiuliza amefanya nini hupati jibu la kueleweka. Sisi kama vongozi wao ni lazima tujue wanafanya kazi gani wanapokuwa maofisini,” alisisitiza.
Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu Majaliwa ameitisha kikao ofisini kwake kesho saa 4 asubuhi akitaka kupatiwa taarifa ni kwa nini mradi wa mabasi yaendayo kasi (DART) haujaanza kazi hadi sasa. “Kesho saa 4 asubuhi Katibu Mkuu, Mkurugenzi Mkuu DART na watendaji wako mje ofisini. Nataka kupata maelezo ni kwa nini mabasi hayajaanza kazi hadi leo, je ni lini yataanza kazi, je ni nani anakwamisha. Na hata kama ni sheria, ni kwa nini tusiziharmonise ili kuondoa hivyo vikwazo,?” alihoji Waziri Mkuu.
“Ninataka kupata haya maelezo kwa sababu Watanzania na hasa wana-Dar es salaam, wamesubiri kwa muda kuona mradi ukianza kazi ili uondoe kero ya usafiri. Wao wanajua anayehusika ni TAMISEMI,” aliongeza.
Mapema, akimkaribisha Waziri Mkuu kuzungumza na watumishi na viongozi wa TAMISEMI, Katibu Mkuu wa OWM-TAMISEMI, Bw. Jumanne Sagini alimweleza baadhi ya mafanikio na changamoto ambazo wizara hiyo imekabiliana nazo katika utendaji wake wa kazi.
Kuhusu ujenzi wa vyumba vya maabara kwa ajili ya kuimarisha ufundishaji wa masomo ya sayansi, Bw. Sagini alisema vyumba hivyo vimeongezeka kutoka 247 mwaka 2005/2006 na kufikia 6,161 mwaka 2014/2015. Pia alisema vyumba 4,228 viko kwenye hatua za kukamilika ujenzi wake.
Kuhusu utengaji wa madirisha ya kuhudumia makundi yenye msamaha kama wazee na watu wenye ulemavu hospitalini na kwenye vituo vya afya, Katibu Mkuu alisema nayo yameongezeka kutoka madirisha 5,074 mwaka 2010 na kufikia 7,903 mwaka 2014/2015 sawa na ongezeko la asilimia 55

No comments:

Post a Comment