Mwakilishi wa Mkurugenzi
Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti Mifuko ya Hifadhi ya Jamii, SSRA, Omar Kahlfan, (katikati),
Mkurugenzi wa Uendeshaji wa PSPF, Neema Muro, (wa pili kushoto), Meneja wa
Mpango wa Uchagiaji wa Hiari wa PSPF,Mwanjaa Sembe, (wa kwanza kushoto) na
maafisa wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, NHIF, (kulia waliosimama),
wakishuhudia Mkurugenzi Mkuu wa PSPF, Bw. Adam Mayingu, (kushoto) na Kaimu
Mkurugenzi Mkuu wa NHIF, Michael Mhando, wakitia saini makubaliano ambayo
yatawezesha taasisi hizo mbili kushirikiana ambapo Wanachama wa PSPF wa mpango
wa Uchangiaji wa Hiari, watadhaminiwa na Mfuko huo ili waweze kuingizwa kwenye
utaratibu wa kupatia bima ya afya kutoka NHIF.
Na Christian Gaya Majira Ijumaa
Novemba 20, 2015
MFUKO wa Pensheni wa PSPF, na Mfuko
wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) wameingia makubaliano yatakayowezesha wanachama
wa PSPF, kupitia mpango wa Uchangiaji wa Hiari yaani PSS, kuanza kupata
matibabu bure kwenye hospitali zote zenye mkataba na NHIF.
Makubaliano hayo yalitiwa saini
Novemba 18, 2015, kati ya Mkurugenzi Mkuu wa PSPF, Bw. Adam Mayingu, na Kaimu
Mkurugenzi Mkuu wa NHIF, Bw. Michael Mhando na kufuatiwa na uzinduzi rasmi
ambapo wanachama wa kwanza zaidi ya 10 wamepatiwa kadi za Bima ya Afya.
Hafla hiyo ilifanyika makao makuu ya
PSPF, jingo la Jubilee Towers jijini Dar es Salaam.
Akizungumza katika hafla hiyo,
Mkurugenzi Mkuu wa PSPF, Bw. Mayingu alisema, uamuzi huo wa PSPF kushirikiana
na NHIF, ni utekelezaji wa malengo na ahadi za serikali ya awamu ya tano chini
ya Rais, Dtk. John Pombe Magufuli, ambaye aliwaahidi Watanzania wote wanapata
huduma za afya zilizo bora. “ Katika kuhakikisha ahadi hiyo ya Mheshimiwa
Rais inaaanza kutimizwa: PSPF kwa kushirikiana na wenzetu wa Mfuko wa Taifa wa
Bima ya Afya tutatoa huduma za afya kwa wanachama wa Mpango wa Uchangaji wa
Hiari wa PSPF.” Alisema Bw. Mayingu katika hotuba yake.
Naye Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa NHIF,
Bw. Michael Mhando alisema, wakati PSPF wamebobea katika suala la pensheni,
NHIF wao wamebobea katika kutoa huduma za afya, hivyo ushirikiano wa Taasisi
hizi mbili zenye uzoefu wa kuhudumia maisha ya Watanzania, utakuwa umewapa
unafuu mkubwa wa maisha. wajasiriamali wadogo ambao
kwa kuwekeza katika afya kutawawezesha ushiriki kikamilifu katika shughuli za
ujenzi wa uchumi wa mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla
Kwa kutoa kinga ya huduma ya bima ya
afya kwa wanachama wake na familia zao PSPF inatambua kwamba wananchi walio na
afya bora ni nguvukazi na raslimali kubwa katika kukuza uchumi na kupunguza
umaskini. Kwa kutoa mafao ya huduma ya bima ya afya PSPF itaisaidia serikali
katika kuinua hali ya afya ya wananchi wote na hasa wale walioko na wanaofanya
kazi kwenye sehemu hatari zaidi, kwa kutoa mafao ya huduma za afya PSPF
itachangia serikali katika kukidhi mahitaji ya wananchi na kuongeza umri wa
kuishi wa watanzania.
Tangu
kuzinduliwa kwake mapema Machi mwaka 2013 tayari wanachama zaidi ya 5,000
wamejiunga na mpango huo wa hiari ambapo makundi zaidi ya 25 yamejiunga na
mfuko huu kutokana na ubora wa mafao yake na mikopo inayotolewa kwa wanachama
waliojiunga na mfuko huo kwa miaka mitano
No comments:
Post a Comment