Pages

Friday, November 20, 2015

Mfumo wa malipo kwa njia ya kielektroniki wapunguza ufujaji wa kodi


index
Mkurugenzi Msaidizi Mifumo ya TEHAMA kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu- TAMISEMI Bw. Mtani Yangwe akifafanua kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) leo jijini Dar es Salaam namna mfumo wa wa ukusanyaji mapato kwa njia ya kielektroniki unavyorahisisha ulipaji wa kodi mbalimbali kwa kuhusisha mifumo ya kielektroniki ya malipo na mifumo ya kibenki. Kulia ni Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano Serikalini wa ofisi hiyo Bi. Rebecca Kwandu.
…………………………………………………………………………………
NA Jovina Bujulu-maelezo- Dae es salaam
Mfumo wa malipo kwa njia ya miamala ya kielektroniki umeweza kudhibiti, kupunguza na kuondoa mianya ya ufujaji wa mapato na kuongeza uwazi katika ukusanyaji kodi kwa baadhi ya miji hapa nchini.
Hayo yamesemwa leo jijini Dar es salaam na Mkurugenzi Msaidizi wa Mifumo ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano Ofisi ya Waziri Mkuu- TAMISEMI Bwa. Mtani Yangwe.
“Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI iliamua kuanzisha mfumo wa kielektroniki wa kukusanya mapato ya mamlaka za serikali za mtaa ili kusaidia mamlaka katika kuongeza mapato ya ndani na kuondokana na utegemezi wa ruzuku kutoka serikali kuu” alisema Bwa. Yangwe
Kabla ya kuanzishwa kwa mfumo huo halmashauri nyingi zimekuwa zikikabiliwa na changamoto za kutofikia malengo ya makusanyo ya kodi ukilinganisha na makisio waliyopanga.
Bwa. Yangwe aliendelea kusema kwamba changamoto walizokuwa wanakutana nazo ni pamoja na kutokuwa na orodha ya kumbukumbu za walipa kodi, uwazi katika makusanyo, uwajibikaji wa watumishi na upotevu wa mapato yaliypkuwa yanakusanywa.
Aidha, alisema kwamba malengo mengine ya kuanzisha mfumo huo ni pamoja na kupata taarifa za walipa kodi wa Mamlaka za Serikali za mitaa na kuhifadhiwa kwa usahihi katika kanzi data ya mfumo.
Mfumo huu pia hutoa hati za madai umetengenezwa kuwa na dirisha linaloruhusu matumizi ya mifumo mingine ya miamala ya kielektroniki kuwezesha ukusanyaji wa mapato katika eneo la ndani ya halmashauri husika ama eneo lolote nchini pale mlipa kodi anapopaswa kulipa kodi zinazomuhusu.
“Tamisemi imedhamiria  kuboresha huduma ya makusanyo ya kodi na tozo mbalimbali za mamlaka ya serikali ya mitaa ili iwafikie wananchi mahali walipo na kuondoa kero za kufuata huduma na kupanga foleni muda mtefu” aliongeza Bwa. Yangwe
Mifumo ya kielektroniki inayotumika katika ukusanyaji huo ni point of sale, huduma za kampuni ya simu za m-pesa, Tigo-pesa, Airtel Money, Zpesa, mabenki na Maxmalipo.
Bwa, Yangwe alitaja faida za mfumo huo kuwa ni pamoja na kutambua walipa kodi na eneo walipo, kupunguza mianya ya ukwepaji kodi na kuongeza mapato na makisio sahihi ya makusanyo.
Mradi huu wa malipo kwa njia ya elektroniki uko chini ya Benki ya dunia na umeanzia katika miji ya Dodoma, Mwanza-manispaa ya ilemela, Kigoma ujiji Manispaa, Arusha, Mbeya, Tanga na Mtwara- manispaa ya Mikindani.

No comments:

Post a Comment