Rais
Dkt. John Pombe Magufuli, akimkabidhi nyaraka za Serikali baada ya kumwapisha Mhe.
Majaliwa Kassim Majaliwa, kuwa Waziri Mkuu wa awamu ya tano, wakati wa sherehe
hizo zilizofanyika leo kwenye Viwanja vya Ikulu ndogo Chamwino
mjini Dodoma.
THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE
OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
|
Telephone: 255-22-2114512,
2116898
E-mail: press@ikulu.go.tz
Fax: 255-22-2113425 |
![]() |
PRESIDENT’S
OFFICE,
STATE HOUSE,
1 BARACK OBAMA ROAD,
11400 DAR ES SALAAM.
Tanzania.
|
TAARIFA
KWA VYOMBO VYA HABARI
Baada ya kulihutubia
na kulizindua bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Rais wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania Dkt JOHN POMBE MAGUFULI amehudhuria hafla fupi
iliyoandaliwa kwa ajili ya wabunge katika viwanja vya Bunge Mjini Dodoma na
kuagiza fedha zilizochangwa kwa ajili ya kugharamia hafla hiyo zipelekwe Katika
Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa ajili ya kununulia vitanda vya wagonjwa
Mheshimiwa
Magufuli ametoa agizo hilo
baada ya kupokea taarifa kuwa wadau mbalimbali wamechanga kiasi cha shilingi
milioni 225 kwa ajili ya kugharamia hafla ya wabunge katika siku ya uzinduzi wa
Bunge
Dkt Magufuli
amesema alipata taarifa za kuwepo kwa michango hiyo ya fedha na kutoa maelekezo
kuwa zitumike kwa kiasi kidogo kwa ajili ya hafla hiyo na sehemu kubwa
zipelekwe katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ili zikatumike kununulia
vitanda na hivyo kupunguza tatizo la wagongwa wanaolala chini kutokana na uhaba
wa vitanda unaikabili hospitali hiyo
“Nilipoambiwa
kwamba zimechangwa shilingi milioni 225 zimekusanywa kwa ajili ya sherehe,
nikasema fedha hizo zipelekwe katika hospitali ya Taifa Muhimbili zikasaidie
kununua vitanda” alisema Dkt Magufuli na kusisitiza kuwa “kwa kufanya hivyo
tutakua tumejinyima sisi wenyewe lakini tutakua tumewanufaisha wenzetu ambao
wanamatatizo makubwa yanayoweza kutatuliwa kwa fedha hizo”
Awali akitoa
taarifa ya michango hiyo Ofisa wa Spika wa Bunge Bwana SAID YAKUBU amesema
jumla michango iliyopatikana ni shilingi milioni 225 na kwamba fedha
zilizotumika katika hafla hiyo ni shilingi milioni 24 tu baada ya kuzingatia
maagiza ya Rais Magufuli
Katika Hafla hiyo
Rais Magufuli amekabidhi vyeti vya kutambua mchango wa wadau waliochangia fedha
wakiwemo Benki za NMB, CRDB na Benki ya Afrika pamoja na Mifuko ya Hifadhi ya
Jamii ya PSPF na PPF.
Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa
Mawasiliano IKULU
November 20, 2015


No comments:
Post a Comment