Pages

Sunday, October 4, 2015

HON.PRESIDENT OF INDIA PRESENTING AN AWARD FOR BEST MEDICAL TOURISM FACILITY TO APOLLO HEALTH,CITY HYDERABAD


Mr. Radhey Mohan (Vice president – International Marketing, Apollo Health City, Hyderabad), Dr. Mahesh Verma (Ministry of Tourism & Civil Aviation), Hon. Sh. Pranab Mukherjee (Hon. president of India), Ms. Sangita Reddy (Joint Managing Director, Apollo Hospitals Group) and Mr. Vinod Zutshi (Secretary – Ministry of Tourism, Govt. of India).
Hon. President of India presenting an Award for Best Medical Tourism facility to Apollo Health City, Hyderabad. This is the third consecutive year that Apollo Health City, Hyderabad is receiving this prestigious award.
WANAWAKE TOFAUTI ZENU ZA ITIKADI ZA VYAMA ZISIWAZUIE KUSHIRIKIANA KATIKA SHUGHULI ZA KIMAENDELEO
Wanawake wa mkoa wa Mara wameaswa kushirikiana kwa pamoja katika shughuli za maendeleo bila kuangalia tofauti ya itikadi zao za vyama kwa kufanya hivyo watajiletea  maendeleo yao kama wanawake.

Rai hiyo imetolewa jana na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete wakati akiongea na wanawake wa mkoa huo katika ukumbi wa mikutano wa Musoma Community Center (MCC) uliopo mjini Musoma. 

Mama Kikwete ambaye ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM kupitia wilaya ya Lindi mjini alisema masuala yanayowahusu  wanawake hayana itikadi za vyama kwani maendeleo ni ya wote, katika mambo ya msingi waungane na kuwa kitu kimoja wasitenganishwe na watu.

Alisema ili wanawake waweze  kujiletea maendeleo ni lazima washikamane, wafanye kazi  kwa umoja na kutumia fursa zilizopo kwani  Serikali inasehemu yake ya kuwaleta maendeleo lakini maendeleo mengine yanahitaji jitihada zao binafsi. 

“Sisi kama wanawake tunafanana kwa kila kitu tofauti iliyopo ni wajibu wa kila mmoja wetu katika jamii yake, shirikini kuchangia shughuli za maendeleo kama ujenzi wa barabara na shule kwa ajili ya watoto wetu na kuchangia huduma ya afya ili tuweze kupata huduma bora”.

Msiache kuzitumia fursa zilizopo wasimamieni  watoto wa kike wasome kwani wakiwa na elimu wataweza kujiajiri au kuajiriwa, wengine watakuwa viongozi wazuri miaka michache ijayo watawasaidia siku za baadaye”, alisisitiza Mama Kikwete.

Aidha Mama Kikwete alitumia nafasi hiyo kuwaaga wanawake hao na kuwashukuru kwa jinsi walivyokuwa wanamtia moyo katika kipindi chote cha miaka 10 ya utawala wa mme wake Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete jambo ambalo lilimpa ujasiri katika kufanya kazi zake za kuwasaidia wanawake na watoto wa Tanzania.

Mama Kikwete alisema, “Kazi yangu ninayoifanya kama mke wa Rais nimeitekeleza nilisema nitawasomesha watoto wa kike wanaoishi katika mazingira magumu nimewasomesha, nimejenga shule ya watoto wa kike, nimewainua wanawake kiuchumi na nimesaidia kuimarisha afya ya mama na mtoto”, alisema Mama Kikwete. 

Katika mkutano huo wanawake walipata fursa ya kuuliza  maswali mbalimbali na kuzitaja kero na changamoto zinazowakabili katika  maisha yao kama vile upatikanaji wa maji, uongozi, uchumi  na elimu.

Kwa upande wake Theresia Chacha ambaye ni mkazi wa Nyamagugu  wilaya ya Rorya alimshukuru Mama Kikwete kwa kumsomesha mtoto wake wa kike aitwaye Paschazia ambaye yupo kidato cha nne katika Shule ya Sekondari ya WAMA-Nakayama iliyopo Rufiji Mkoani Pwani.

“Mama Kikwete anasomesha watoto 15 kutoka mkoa wa Mara katika shule yake,  mwanangu ni mmoja wa watoto hao, anamgharamia  kila kitu hata nauli mama huyu  analipa mimi silipo chochote”. 

Miaka yote hiyo sijawahi kumuona ndiyo namuona leo nakushukuru sana Mama, Mwenyezi Mungu akubariki naomba kiongozi ajaye aige mfano wako wa kuwasidia wanawake na watoto wa Tanzania”, Mama Chacha alishukuru.
Naye Anastazia Sangarya mkazi wa kata ya Mwisege ambae ni mjasiriamali alizitaja changamoto wanazokutana nazo kuwa ni pamoja na kupanda kwa ada ya ushiriki wa Maonyesho ya kimataifa ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere maarufu kama sabasaba yanayofanyika kila mwaka jijini Dar es Salaam kutoka shilingi 50,000 hadi 100,000.

Mama Anastazia alisema, “Sisi wanawake wajasiriamali tunaumizwa na ada kubwa ya ushiriki wa maonyesho ya sabasaba kwani tukishiriki licha ya kulipa kiingilio bado kuna gharama ya nauli na malazi”.

Kwa upande wa  mikopo tunayokopa benki riba yake ni kubwa na kama ikatokea umechelewa kurejesha kutokana na matatizo ya kifamilia benki haikuelewi tunakuomba mama yetu utusaidie kutatua changamoto hizi ambazo zinarudisha nyuma maendeleo ya wanawake wajasiriamali wa mkoa huu,”. 

Mama Kikwete aliahidi kuzifanyia kazi changamoto zinazowakabili wanawake hao na kuwataka viongozi wao kuitisha mikutano ya mara kwa mara itakayosaidia kutatua kero zinazowakabili.
MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA CHUMBUNI USSI SALUM PONDEZA AMJADI, AWAHUTUBIA WANANCHI WA JIMBO HILO KATIKA MKUTANO WAKE WA KAMPENI VIWANJA VYA MABANDA YA NGOMBE CHUMBUNI UNGUJA.

Msoma Utenzi akisoma Utenzi maalum wakati wa Uzinduzi wa Mkutano wa Kampeni wa Jimbo la Chumbuni Unguja uliofanyika katika Viwanja vya Mabanda ya Ngombe Chumbuni Zanzibar.
Mwanachama wa Chama cha Mapinduzi akiwa katika viwanja vya mkutano akishangilia na Picha ya Mgombea wake wa Ubunge kupitia CCM Ndg. Ussi Salum Pondeza AMJADI wakati wa mkutano huo
Wananchi wa Jimbo la Chumbuni wakiwa katika viwanja vya mkutano wa Kampeni ya Mbunge na Mwakilishi wa Jimbo hilo uliofanyika viwanja vya Mabanda ya Ngombe Chumbuni Unguja.
Wagombea Ubunge Uwakilishi na Udiwani wakiwapungia mikono Wananchi waliohudhuria mkutano huo wa kampeni wakati msoma utenzi akitaja majina ya Wagombea.
Wanachama wa CCM wa Tawi la Masumbani Jimbo la Chumbuni wakifuatilia mkutano huo wa kampeni uliofanyika viwanja vya mabanda ya ngombe chumbuni Unguja
Mgombea Ubunge Jimbo la Mfenesini Kanali Mstaaf Masoud akimtunza msoma Utenzi wakati wa mkutano wa Uzinduzi wa Jimbo la Chumbuni Unguja. 
Katibu wa CCM Jimbo la Chumbuni akisoma utaratibu wa mkutano huo wa kampeni wa jimbo hilo. 
Aliyekuwa Mwakilishi wa Jimbo la Chumbuni Unguja Mhe Machano Othman, akiwasalimia Wananchi wa Jimbo hilo na kuwaombea Kura Wagombea wote wa CCM wanaogombea katika Jimbo la Chumbuni kuazi Mbunge Mwakilishi na Madiwani kuwa kura ya Ndio kuendelea maendeleo katika jimbo hilo walioyawacha wao.kwa sasa anagombea Jimbo la Mfenesini nafasi ya Uwakilishi 
Mgombea Ubunge Jimbo la Mfenesini Kanal Mstaaf Masaud, akiwasalimia Wananchi wa Jimbo la Chumbuni wakati wa Mkutano wa Kampeni ya Uzinduzi ya Jimbo zilizofanyika katika viwanja vya mpira mabanda ya ngombe chumbuni Unguja. 

Mwenyekiti wa Wazazi Mkoa wa Kusini Unguja Mhe Haji Ameir akizungua mkutano wa Kampeni wa Jimbo la Chumbuni Unguja uliofanyika katika viwanja vya mpira mabanda ya ngombe chumbuni na Kuwatambulisha Wagombea wa CCM wa Jimbo hilo.na kuwaombea Kura siku ya Uchaguzi Mkuu kwa kura ya Ndio, pamoja na Rais wa Zanzibar Dk Shein, na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dk John Pombe Magufuli.
Wanachama wa CCM wakiwa katika viwanja vya Kampeni wakishangilia na Vipeperushi vya wagombea wa Jimbo la Chumbuni Unguja.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Kusini Unguja Mhe Haji Ameir akimtambulisha Mgombea Ubunge wa Jimbo la Chumbuni Ussi Salum Pondeza AMJADI, wakati wa mkutano wa Kampeni wa Jimbo la Chumbuni uliofanyika katika viwanja vya Mabanda ya Ngombe Chumbuni.

Mgombea Ubunge Jimbo la Chumbuni Ussi Salum Pondeza AMJADI akiwataka Wananchi wa Jimbo la Chumbuni kujiandaa na Maendeleo katika Jimbo hilo katika kipindi chake cha miaka mitano kuweza kulibandilisha Jimbo hilo katika maendeleo kwa Vijana na Wazee katika sekta mbalimbali zikiwemo za Elimu, Maji, Kujiajiri Wenyewe na Afya. amewataka kumpigia Kura ya Ndio kuweza kuwaletea maendeleo hayo. 

Mgombea Ubunge wa Jimbo la Chumbuni akimwaga Serazake kwa Wananchi wa Jimbo la Chumbuni wakati wa mkutano wake wa kampeni katika viwanja vya mpira mabanda ya ngombe chumbuni Unguja.
Wanachama wa CCM wakishangilia wakati wa mkutano wa kampeni wa Jimbo la Chumbuni Unguja
Wanachama wa CCM wakishangilia wakati wa mkutano wa kampeni wa Jimbo la Chumbuni Unguja wakati akihutubia Mgombea Ubunge wa Jimbo hilo Ussi Salum Pondeza AMJADI, uliofanyika viwanja vya mabanda ya ngombe chumbuni Unguja.
Wananchi wa Jimbo la Chumbuni wakifuatilia Mkutano wa Kampeni wa Jimbo hilo uliofanyika viwanja vya mabanda ya ngombe chumbuni.

Mgombea Uwakilishi wa Jimbo la Chumbuni Miraj Kwaza akiwahutubia Wananchi wa Jimbo la Chumbuni Unguja wakati wa mkutano wa kampeni wa Jimbo hilo na kusoma baadhi ya vipengele vya Ilani ya Uchaguzi ya CCM jinsi itakavyotekelezwa katika kipindi cha miaka mitano ijayo ya Dk Shein. 

Wanachama wa CCM wakishangilia wakati wa mkutano huo wa Kampeni ya Jimbo la Chumbuni Unguja



 Msanii wa Bendi ya Yamoto, akitowa burudani kwa Wanachama wa CCM wa Jimbo la Chumbuni wakati wa Mkutano wa Kampeni wa Jimbo hilo.
Wanachama wa CCM wakishangilia wakati wa mkutano huo wa Kampeni ya Jimbo la Chumbuni Unguja
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Kusini Unguja Mhe Haji Ameir, akimtambulisha Mgombea Udiwani wa Wadi ya Chumbuni, Ndg. Mussa Haji Idrisa kwa Wananchi  wa Jimbo hilo 
Mgombea Udiwani Wadi ya Chumbuni Ndg Mussa Haji Idrisa. akiwasalimia Wananchi wakati akitambulishwa na kuomba Kura.
Mgombea Udiwani Wadi ya MuembemakundiNdg Haji Juma, akiwasalimia Wananchi wakati akitambulishwa na kuomba Kura.
Mgombea Udiwani Wadi ya MuembemakundiNdg.Haji Juma.  akiwasalimia Wananchi wakati akitambulishwa na kuomba Kura

No comments:

Post a Comment