Meza kuu katika warsha ya wadau wa ajira
kwa vijana iliyofadhiliwa na Mpango wa Shirika la Utafiti wa Maendeleo
ya Kimataifa kutoka Canada (IDRC) na kuratibiwa na ESRF. Kutoka kushoto
ni Afisa kutoka Wizara ya Kazi na Ajira kitengo cha Ajira, Joseph
Nganga, Mkurugenzi wa Kazi katika Wizara ya Kazi na Ajira, Ally M.
Ahmed, Mkuu wa utafiti na machapisho Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na
Kijamii (ESRF), Profesa Fortunata Makene, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya
Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel na
Mratibu Kazi wa Shirika la Kimataifa la Kazi (ILO) Dk. Annmarie
Kiaga.(Picha zote na Zainul Mzige wa Modewjiblog)
Na Mwandishi wetu
PAMOJA na kuwepo na
maendeleo ya kuridhisha katika suala la ajira kwa vijana, serikali
imekiri kwamba ukosefu wa ajira bado ni tatizo kubwa duniani na kwa
taifa kwa ujumla.
Kutokana na hali hiyo suala la ajira kwa vijana limebaki kuwa ajenda kuu nchini.
Kauli hiyo imetolewa na
Mkurugenzi wa Kazi katika Wizara ya kazi Ally M. Ahmed wakati akifungua
warsha ya siku moja ya wadau wa ajira kwa vijana iliyofanyika hoteli ya
Double Tree by Hilton.
Alifanya ufunguzi huo kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Eric Shitindi.
Alisema Tanzania
inaendelea kukabiliana na tatizo la ajira kutokana na wigo mdogo wa
fursa za ajira, tatizo la utaalamu na ukosefu wa uzoefu .
Alisema hata hivyo vijana
wanaoamua kujiajiri wenyewe wamekuwa wakikabiliana na tatizo kubwa la
mtaji, maeneo ya kufanyia kazi na utaalamu katika ujasiriamali
utakaowawezesha kuendesha miradi wanayoibuni.
Alisema kutokana na uwapo
wa sera, mipango na miradi ya maendeleo kuhusu ajira kwa vijana
inayoendeshwa kitaifa na kimataifa kumekuwepo na dalili njema za
kupungua kwa ukosefu wa ajira.
Alisema utafiti wa mwaka
2014 (ILFS) umeonesha kwamba ukosefu wa ajira umepungua kutoka asilimia
11.7 kwa mwaka 2006 hadi kufikia asilimia 10.3 ka mwaka 2014 huku kwa
vijana (wenye umri wa miaka 15 hadi 35) ukipungua kutoka asilimia 13.2
kwa mwaka 2006 hadi asilimia 11.7 kwa mwaka 2014.
Mkuu wa Utafiti na mchapishi wa Taasisi
ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii (ESRF), Profesa Fortunata Makene
akitoa hotuba ya utangulizi katika warsha ya vijana na ajira
iliyofanyika hoteli ya Double Tree by Hilton. Katika hotuba yake ya
ufunguzi alitoa wito wa washiriki kuangalia kwa undani tatizo la ajira
kwa vijana na kutoa mwelekeo utakaosaidia watunga sera kuwa na sera
madhubuti kuhusu ajira kwa vijana.
Alisema mafanikio
yaliyopatikana hayaondoi ukweli kuwa kuna tatizo kubwa la ajira miongoni
mwa vijana na kutokana na mazingira ya sasa ni vyema wadau wa ajira
kuangalia kwa undani tatizo la ajira la sasa ili kutoa ushauri wa
kukabiliana nalo kwa kipindi kifupi na kirefu.
Shitindi alisema kwamba
serikali inafurahishwa na juhudi zinazofanywa na wadau mbalimbali
kutafuta majibu ya tatizo la ajira, majibu ambayo alisema yakifanywa
vyema yatasaidia sana wataalamu wa serikali kutengeneza sera na kanuni
zitakazo kidhi haja.
Alisema ipo haja kwa
wachambuzi (watafiti) kuelekeza nguvu zao katika kutafiti soko la ajira
ili kusaidia watengeneza sera kuona mahitaji ya soko katika miaka kadhaa
ijayo.
Alisema wakati uchumi wa
Tanzania unakua kwa asilimia 7 kwa mwaka kwa miaka kumi iliyopita ajira
zimekuwa haziendi sambamba na ukuaji wa uchumi na hivyo kuleta maswali
mengi ya sintofahamu.
Alisema serikali kwa sasa
inataka kuhakikisha kwamba inaboresha upatikanaji wa ajira lakini hilo
linawezekana kama taasisi zake zinazotengeneza sera na kuweka mipango
zinatambua tatizo na kuona namna ya kuliangalia.
Alisema watafiti wana
wajibu mkubwa wa kusaidia serikali kuwezesha vijana kuwa na kazi zenye
staha kama sera ya ajira ya taifa inavyotaka.
Mkurugenzi wa kazi wizara ya kazi na
ajira, Ally Msaki Ahmed, akisoma hotuba kwa niaba ya Katibu Mkuu Wizara
ya Kazi na Ajira, Eric Shitindi katika warsha ya kitaifa ya ajira kwa
vijana iliyofanyika hoteli ya Duble Tree by Hilton. Katika hotuba yake
aliwataka washiriki kujadili kwa makini matatizo ya vijana na kutoa
suluhu itakayosaidia watendaji kutunga sera na kutoa mwelekeo mpya wa
kukabiliana na tatizo hilo.
Alisema kwa kuangalia
ukuaji wa kisekta, sekta ambayo sasa hivi inahitaji watu ndio ambayo
haina wataalamu wa kutosha na hivyo ukuaji wa sekta hizo kama za
mawasiliano hauendi sanjari na utaalamu uliopo katika soko.
Katibu Mkuu huyo alitoa
wito kwa watu binafsi na serikali kuhakikisha kwamba wanakabiliana na
vikwazo vya ajira kwa kutoa elimu na taaluma ili fursa zionekane na
kutumika ipasavyo.
Alisema tija inaweza
kuonekana katika ukubwa wa utaalamu, ubunifu na namna mafunzo
yanavyowawezesha wanafunzi kuwa na uhakika na kazi wanazotaka.
Alisema ipo haja kwa wadau
mbalimbali kushirikiana na serikali katika kuhakikisha kwamba vijana
wanaingizwa katika soko la ajira na tatizo la ajira linapunguzwa.
Kiongozi Mpango wa ukuaji na ajira wa
taasisi hiyo, Shirika la Utafiti ya Maendeleo ya Kimataifa kutoka Canada
(IDRC), Dk. Arjan de Haan akielezea sababu za taasisi hiyo kuunga
mkono tafiti kwa ajili ya kusaidia kupatikana ufumbuzi wa tatizo la
ajira katika warsha ya ajira na vijana iliyofanyika Double Tree by
Hilton hotel.
Katika moja ya maazimio
yaliyotolewa na washiriki vijana, walitaka kuwepo na mabadiliko makubwa
katika utoaji elimu, ambapo walisema elimu itolewe kwa Kiswahili lakini
pia wanafunzi waandaliwe kuwa wabunifu na kujiajiri.
Aidha wametaka kurejeshwa kwa shule za ufundi na shule maalumu kama ilivyokuwa zamani.
Walisema vijana Wanatakiwa
kushiriki katika utengenezaji wa sera na kanuni na si kushirikishwa na
kutaka matakwa yao yanastahili kuangaliwa na kuzingatiwa ili mtu
ajifunze kila anachoona anaweza kukifanya vyema.
Warsha hiyo ya ajira kwa
vijana imewezeshwa na IDRC na kuratibiwa na ESRF na mada mbalimbali
ziliwasilishwa ambazo zilichambua masuala ya elimu, elimu ya ufundi,
changamoto na fursa za vijana katika ajira.
Aidha kulikuwa na mada za majukumu ya serikali na sera katika kuboresha mchakato wa ajira kwa vijana.
Mchumi na Mshauri huru Bi. Mahjabeen
Haji akiwasilisha mada kuhusu hali ya ajira kwa vijana nchini katika
warsha ya vijana na ajira ilyofanyika hoteli ya Double Tree by Hilton,
katika mada yake alielezea mazingira ya ajira ambapo elimu katika sekta
zinazokua kwa kasi kama Tehama ni kikwazo kikubwa katika kuwezesha ajira
kwa vijana.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara
ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel
(kulia) akijadiliana jambo na Mkuu wa Utafiti na mchapishi wa Taasisi ya
Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii (ESRF), Profesa Fortunata Makene wakati
warsha hiyo ikiendelea.
Mkurugenzi wa Salama Foundation,
Shadrack John Msuya akiwasilisha mapendekezo ya vijana juu ya namna
ambavyo vipaji, elimu na ubunifu vinavyoweza kutengeneza ajira kwenye
maeneo ya Sayansi, Teknolojia, Kilimo na Ufugaji.Moja ya azimio ni kuwa
na sera mpya ya vijana yenye mpango mkakati na tafiti zinazotekelezeka
katika warsha ya vijana na ajira.
Mshauri mwelekezi katika uanzishwaji na
uendelevu wa biashara na maendeleo ya jamii, Gidufana Gafufen
akiwasilisha mapendekezo yaliyowasilishwa katika vikundi nini kifanyike
ili vijana wapende kilimo katika warsha ya vijana na ajira iliyofanyika
katika hoteli ya Double Tree by Hilton.
Pichani juu na chini ni sehemu ya wadau
pamoja na makundi ya vijana waliohudhuria warsha ya wadau wa ajira kwa
vijana iliyofadhiliwa na Mpango wa Shirika la Utafiti wa Maendeleo ya
Kimataifa kutoka Canada (IDRC) na kuratibiwa na ESRF.
Mmoja wa washiriki akitoa maoni kwenye
warsha ya wadau wa ajira kwa vijana iliyofadhiliwa na Mpango wa Shirika
la Utafiti wa Maendeleo ya Kimataifa kutoka Canada (IDRC) na kuratibiwa
na ESRF.
Pichani juu na chini ni wadau kutoka Taasisi mbalimbali walioshiriki warsha hiyo wakibadilishana mawazo.
Mratibu Kazi wa Shirika la Kimataifa la Kazi (ILO) Dk. Annmarie Kiaga (kulia) akiteta jambo na baadhi ya washiriki.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,
Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel (kushoto)
akifurahi jambo na Mtafiti Mwandamizi ESRF, Dk. Georgina Ole Saibul mara
baada ya kumalizika kwa warsha hiyo.
Mratibu wa Mradi wa Madhara ya Tumbaku
(TPHA) Dk. Bertha T.A. Maegga akizungumza wakati akifungua kongamano
hilo lililo washirikisha wadau mbalimbali kwa kutoa muhutasari wa
Madhara ya Tumbaku. (Picha na Geofrey Adroph).
Na Andrew Chale, modewjiblog
[Dar es Salaam] Chama cha Afya ya Jamii nchini (TPHA), kimeendesha
kongamano maalum kwa wanafunzi wa shule msingi zaidi ya Saba ndani ya
Manispaa ya Kinondoni kwa lengo la kutoa elimu ya madhara yatokanayo na
utumiaji wa bidhaa za Tumbaku pamoja na kujikinga na athari zake mbaya
baadae.
Akielezea katika kongamano hilo, Afisa wa TPHA ambaye pia ni msimamizi
na mtaafiti wa masuala ya kupambana na madhara ya Tumbaku, Dk. Bertha
Maegga amebainisha kuwa, kwa sasa Chama hicho kinaendesha mradi
uliopewa jina la “80 CHILDREN STRONG” ukitoa elimu kwa vijana wadogo
wenye umri wa miaka 10-14, hasa wa shule za msingi.
Dk. Maegga akihutubia umati wa wanafunzi wa shule hizo saba katika
kongamano hilo lililofanyika shule ya Msingi Kijitonyama Visiwani,
aliwataka wazazi, walimu, walezi na jamii kuwalinda na kukemea watoto
wao kuachana na vitendo vya matumizi ya bidhaa za Tumbaku ikiwemo
sigara, ugoro, shisha na Tumbaku yenyewe.
Aidha, amebainisha kuwa, wameweza kulenga kundi hilo kutokana na kuwa
na changamoto za kiukuaji wa kiakili na kisaikolojia.
“Umri huu kuna utundu na utukutu mwingi na akili nazo bado hazijakomaa
kuepuka ushawishi wa namna mbalimbali ukiwemo na wa matendo yasiyofaa
katika maisha yao ya baadaye.
Tukiweza kuwalinda katika umri huo. watabaki salama hadi
watakapojitambjua nafsi zao na kuamua mambo ya busara na salama katika
maisha yao ya baadae” alibainisha Dk. Maegga.
Mwalimu Margareth William mshereheshaji
katika siku hiyo ya kongamano la uelimishaji vijana kuhusu Tumbaku na
madhara yatokanayo na bidhaa zake.
Naye Mratibu wa Elimu Kata ya Makumbusho
ambaye pia alikuwa mgeni katika kongamano hilo, alitoa wito kwa walimu
na wazazi kuwa waangalifu kwa watoto wao ikiwemo kufuatilia nyendo zao
mara kwa mara ili kuwakinga na vishawishi hivyo vya matumizi ya bidhaa
zitokanazo na tumbaku kwani zina madhara makubwa hasa kwa afya za watoto
wadogo.
Mradi huo wa ’80 Children Strong’,
unaosimamiwa na Chama cha Afya ya Jamii (TPHA) unafadhiliwa na
Shirika dogo la Conquer Cancer Foundation ambalo linahusiana na
American Society for Clinical Oncology (ASCO) ya nchini Marekani
(Chama cha kitabibu cha masuala ya uchunguzi wa tiba ya saratani.
Hata hivyo, TPHA imedhamiria kuwa kila
mtoto anapata haki ya kuelimishwa kujikinga na matumizi hayo mabaya ya
tumbaku, ambapo kwa darasa la watoto 80, asiwepo hata mmoja
atakayeingia kwenye viashiria vibaya vya matumizi ya tumbaku hivyo
wataendelea kutoa elimu hiyo sehemu mbalimbali nchini.
Kwa upande wa shule hizo zilizohudhuria
kongamano hilo ni pamoja Shule ya Msingi Mapambano, Kijitonyama
Visiwani, Victoria, Mwananyamala B, Mwananyamala Kisiwani, Mashujaa,
Shekilango na Mapambano.
Kwa upande wa watoto hao walipata pia
wasaha wa kuuliza maswali na kupatiwa majibu huku pia kukifanyika na
masuala ya maigizo, ngoma, shahiri na ngonjera zilizokuwa na jumbe
mbalimbali za kupambana na matumizi ya tumbaku.
Wanafunzi wakisoma na kuelekezana jarida lililochapishwa mahususi kwa ajili ya kuelimisha matumizi mabaya ya Tumbaku.
Baadhi ya wageni waalikwa kutoka mashirika na vyuo mbalimbali.
Kikundi cha majigambo ya jukwaani
(ngonjera) kikitoa ujumbe kwa wageni waalikwa pamoja na wanafunzi wenzao
kuhusiana na kupambana na kudhibiti matumizi hatari ya Tumbaku.
Wanafunzi wakionesha vipaji vyao vya
kuigiza kwa kuelimisha kuhusiana na na madhara ya Tumbaku na ni namna
gani ya kuweza kujikinga.
Bernard Temba kutoka Chuo cha Afya cha
Muhimbili akitoa somo kwa wanafunzi wa shule za msingi zilizohudhuria
kongamano hilo lililofanyiaka katika shule ya Msingi ya Kijitonyama
Kisiwani
Shairi mahususi likiimbwa na wanafunzi
hao likiwa limebeba ujumbe wa kijana jiepushe na matumizi ya Tumbaku na
bidhaa zitokanazo na Tumbaku.
Mwanafunzi wa darasa la tano, Tadei
Ladislausi kutoka shule ya msingi Shekilango (kulia)akisoma madhara
yanayo wakumba watumiaji wa Tumbaku.
Wawili kulia ni wanafunzi kutoka Chuo
cha Afya Muhimbili, kushoto ni wanafunzi wa shule ya msingi Kijitonyama
Kisiwani wakiwa wanasikiliza kwa makini maada zilizo kuwa zikiendelea
katika kongamano hilo.
Wanafunzi wakiuliza maswali kwa watoa mada inayo husiana na afya kwa kijana na kuepuka matumizi mabaya ya Tumbaku
Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Kijitonyama Kisiwani, Bw. Charles Nombo akijibu baadhi ya maswali yaliyoulizwa na wanafunzi.
Baadhi ya wanafunzi kutoka shule mbalimbali walioweza kuhudhuria katika kongamano hilo.
Mjumbe wa Chama cha Afya ya Jamii Bi.
Elizabeth Nchimbi akitoa nasaa kwa vijana walioweza kuhudhuria na wale
walioko nje wasiweze kutumia Tumbaku kwani ni hatari kwa afya za
binadamu
Waandhishi wa habari wakiwa kazini.
Afisa Elimu kata ya Kijitonyama, Mwalimu
Shangwe Temba akifunga kwa kutoa neno kwa vijana kuacha kujiingiza
katika makundi mbalimbali kwani ndio yanayo pelekea vijana wengi
kuhamasika na kuanza kutumia Tumbaku ambayo huwaletea vijana wengi
matatizo hususani kwa wanafunzi kuacha shule kwa kuugua vifua vikuu na
magonjwa mengine mengi
Picha ya umoja wa kikundi cha wanafunzi kinacho elimisha matumizi mabaya ya bidhaa zinazotokana na Tumbaku.
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha
Mapinduzi (CCM),Dkt John Pombe Magufuli akifafanua jambo kwa msisitizo
mkubwa wakati akiwahutubia wakazi wa Chato na vitongoji vyake jioni ya
leo kwenye mkutano wa hadhara wa Kampeni uliofanyika uwanja wa shule ya
sekondari Chato mkoani Geita.PICHA NA MUCHUZI JR-CHATO,GEITA.
Wakazi wa Chato na Vitongoji vyake wakifuatilia na kusikiliza sera za
Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli alipokuwa akijinadi na
kuomba ridhaa mbele yao jioni ya leo kwenye mkutano wa kampeni
uliofanyika kwenye uwanja wa shule ya sekondari chato mkoani Geita.
Wakazi
wa Chato wakishangilia kuonesha kuwa watampa kura za ushindi Mgombea
Urais wa CCM Dkt Magufuli kwenye uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika
Oktoba 25 mwaka huu,kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni uliofanyika
katika shule ya sekondari Chato,jioni ya leo mkoani Geita.
Mgombea
Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi
(CCM),Dkt John Pombe Magufuli akiwahutubia wakazi wa Chato na vitongoji
vyake jioni ya leo kwenye mkutano wa hadhara wa Kampeni uliofanyika
katika uwanja wa shule ya sekondari Chato mkoani Geita.
Mgombea
Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi
(CCM),Dkt John Pombe Magufuli akimnadi Mgombea Ubunge wa jimbo la
Chato,Dkt Meedad Kalemani mbele ya wakazi wa Chato waliojitokeza kwa
wingi kwenye mkutano wa hadhara wa Kampeni uliofanyika kwenye uwanja wa
shule ya sekondari Chato,jioni ya leo mkoani Geita.
Wakazi
wa Chato na Vitongoji vyake wakifuatilia na kusikiliza sera za Mgombea
Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli alipokuwa akijinadi na kuomba
ridhaa mbele yao jioni ya leo kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika
kwenye uwanja wa shule ya sekondari chato mkoani Geita.
Wakazi wa Chato ilkuwa ni shangwe tu kila kona ya uwanja.
Mwenyekiti
wa CCM Mkoa wa Geita ,Joseph Kasheku almaarufu King Msukuma akiwaomba
ridhaa wananchi wa Chato ya kumchagua Mgombea Urais wa chama cha
Mapinduzi (CCM),Dkt John Pombe Magufuli ili aweze kuwa Rais wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania katika awamu ya tano.
Mke wa Mgombea Urais wa CCM,Mama Janeth John Magufuli akiwasalimia
wananchi wa Chato na kuwaomba ridhaa ya kumchagua Dkt John Pombe
Magufuli kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika awamu ya
tano,kweney uchaguzi mkuu unaotarajiwa kuwafanyika Oktoba 25 mwaka huu.
Mke wa Mgombea Urais wa CCM,Mama Janeth John Magufuli akiwasalimia
wananchi wa Chato na kuwaomba ridhaa ya kumchagua Dkt John Pombe
Magufuli kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika awamu ya
tano,kweney uchaguzi mkuu unaotarajiwa kuwafanyika Oktoba 25 mwaka huu.
Wakazi
wa Chato wakishangilia kwa shangwe kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni
uliofanyika katika shule ya sekondari Chato,jioni ya leo mkoani Geita.
Mgombea
Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi
(CCM),Dkt John Pombe Magufuli akiwahutubia wakazi wa Chato na vitongoji
vyake jioni ya leo kwenye mkutano wa hadhara wa Kampeni uliofanyika
katika shule ya sekondari Chato mkoani Geita.
Wakazi
wa Chato wakishangilia kwa shangwe kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni
uliofanyika katika uwanja wa shule ya sekondari Chato,jioni ya leo
mkoani Geita.
Mke
wa Mgombea Urais wa CCM,Mama Janeth John Magufuli akipeana mkono na
Mgombea Ubunge wa jimbo la Chato,Dkt Meedad Kalemani mara baada ya
kuwasalimia wananchi wa Chato na kuwaomba ridhaa ya kumchagua Dkt
Magufuli kuwa Rais wa awamu ya tano,pichani kati anaeshuhudia ni Mgombea
Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli.
Mgombea
Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi
(CCM),Dkt John Pombe Magufuli akiwaaga wakazi wa Chato mara baada ya
kumaliza mkutano wa hadhara wa Kampeni uliofanyika kwenye uwanja wa
shule ya sekondari Chato,jioni ya leo mkoani Geita.
Dkt.
John Pombe Joseph Magufuli akisalimia katika uwanja wa Shule ya
Sekondari ya Chato mkoani Geita tayari kuhutubia mkutano wa kampeni
uliohudhuriwa na mamia ya wananchi muda huu.
Dkt.
John Pombe Joseph Magufuli akisalimia katika uwanja wa Shule ya
Sekondari ya Chato mkoani Geita tayari kuhutubia mkutano wa kampeni
uliohudhuriwa na mamia ya wananchi muda huu.
Mgombea
Urais kwa tiketi ya CCM Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akiwasili
katika uwanja wa Shule ya Sekondari ya Chato mkoani Geita tayari
kuhutubia mkutano wa kampeni uliohudhuriwa na mamia ya wananchi muda
huu.
Sehemu ya maelfu ya wananchi katika uwanja wa Shule ya Sekondari ya Chato mkoani Geita tayari mkutano wa kampeni
Sehemu ya maelfu ya wananchi katika uwanja wa Shule ya Sekondari ya Chato mkoani Geita tayari mkutano wa kampeni.
Picha na Ahmad Michuzi Jnr.






















No comments:
Post a Comment