MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AFUNGA RASMI MATANGAZO YA TELEVISHENI YA MFUMO WA ANALOJIA.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
akihutubia wakati wa sherehe za Ukomo wa matangazo ya Televisheni ya
Analojia, zilizofanyika leo Juni 17, 2015 kwenye Ukumbi wa Mlimani City
jijini Dar es Salaam.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
akibofya kitufye cha Lap Top kuashiria kufunga rasmi Matangazo ya
Televisheni ya Analojia, baada ya kufikia ukomo rasmi hii leo Juni 17,
2015 baada ya kufanikiwa kuzima mitambo ya Analojia kwa nchi nzima.
Sherehe hizo za ukomo zimefanyika leo kwenye Ukumbi wa Mlimani City
jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na
Michezo, Dkt. Fenella Mukangara.
Wadau wa masiliano.
RATIBA YA BARCLAYS PREMIER LEAGUE HADHARANI, KUANZA KUTIMUA VUMBI AUGUST 08' 2015
Mabingwa wa ligi kuu England 2014/2015, Cheslea
Shirikisho
la soka nchini England ( FA ) limetoa ratiba ya msimu mpya wa ligi kuu
nchini humo ambayo imepangwa kuanza kutimua vumbi August 08' 2015 katika
viwanja kumi tofauti.
BALOZI SEIF AWATAKA WAZAZI KUWAPOKEA WATOTO WAO WALIOACHANA NA MATUMIZI YA DAWA ZA KULEVYA
Wazazi wameaswa kuwa tayari kuwapokea Vijana au watoto wao walioamua kuacha matumizi ya dawa za kulevya ili kuwalinda na vishawishi vinavyoweza kutoa nafasi ya kuwarejesha tena kwenye matumizi ya Dawa hizo pamoja pombe haramu.
Mbunge wa Jimbo la Kitope Balozi Seif Ali Iddi ametoa wosia huo wakati wa kuwapokea Vijana Sita wa Kijiji cha Fujoni walioamua kuacha kutumia Dawa za kulevya na kupata mafunzo watakayoyatumia kuwasomesha wenzao kuachana na Dawa hizo hapo katika Skuli ya Fujoni Wilaya ya Kaskazini “ B “.
Balozi Seif ambae pia ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar alisema wapo Wazazi na Familia Nchini ambao bado wanaendelea na tabia ya kuwatenga Vijana wao walioathirika na Dawa za kulevya kwa kuchelea kufanyiwa matendo ya maudhi kama wizi.
MAHAKAMA YA NCHINI MISRI IMEUNGA MKONO ADHABU YA KIFO KWA MOHAMMED MORSI
Mahakama ya nchini Misri imeunga
mkono adhabu ya kifo iliyotolewa kwa rais aliyeng'olewa madarakani wa
nchi hiyo Mohammed Morsi, kwa kosa la kusababisha kutoroka kwa
wafungwa wengi.
Hukumu hiyo ilitolewa awali mwezi
Mei, sasa imethibitishwa baada ya majadiliano na viongozi wa kidini
wa juu wa Misri pamoja na Mufti Mkuu.
Hukumu ya kifo kwa viongozi wakuu wa
chama cha Muslim Brotherhood, akiwemo kiongozi wao mkuu Mohammed
Badie, pia nayo imeridhiwa kutekelezwa.
ECUADOR ZAANZISHA UHUSIANO WA KIDIPLOMASIA
DKT. MAGUFULI AWASILI ZANZIBAR KUTAFUTA WADHAMINI
Waziri
wa Ujenzi ambaye pia ni Mbunge wa Chato Mheshimiwa Dkt. John Pombe
Magufuli akiangalia mchakato wa uhakiki wa kadi za wanachama wa CCM
Wilaya ya Mfenesini Kisiwani Zanzibar waliojitokeza kumdhamini.
Waziri
wa Ujenzi ambaye pia ni Mbunge wa Chato Mheshimiwa Dkt. John Pombe
Magufuli akikabidhiwa fomu yenye orodha ya Wadhamini waliojitokeza
kumdhamini katika mbio za kuwania Urais wa Jamhuri ya Muungano kupitia
chama hicho kutoka kwa Mussa Haji Katibu wa CCM Wilaya ya Mfenesini
Kisiwani Zanzibar
Dkt. Magufuli akifurahia mara baada ya kukabidhiwa fomu za Wadhamini kutoka kwa Katibu wa CCM wilaya ya Kaskazini B-Unguja.
Dkt.
John Magufuli akisomewa dua katika Wilaya ya Wete Pemba mara baada ya
kumaliza zoezi la kupata wadhamini katika katika kisiwa cha Pemba. Dkt.
Magufuli amepata Wadhamini katika mikoa mitano kisiwani Zanzibar, Mitatu
Unguja na Miwili Pemba
WAZIRI MKUU APATA WADHAMINI 9,141 KATAVI
Waziri
Mkuu, Mizengo Pinda akiwapungia wanaCCM waliofika kwenye Ofisi ya CCM
ya kata ya Kibaoni kumdhamini katika nia yake ya kuwania uteuzi wa CCM
katika kugombea nafasi ya urais Juni 15, 2015.
Waziri
Mkuu, Mizengo Pinda akisalimian na baadhi ya wananchi wa Mpanda
waliofika kwenye ofisi ya CCM ya Wilaya ya Mpanda kushuhudia na
kumdhamini ilia pate sifa za kuteuliwa kuwa mgombea urais kwa tiketi ya
CCM, Juni 15, 2015.


















No comments:
Post a Comment