Mmoja wa wafanyakazi waandamizi wa mradi huo, ambaye hakutaka jina lake
kuandikwa kwenye gazeti, alisema kuwa kasi ya ujenzi imepungua kutokana
na fedha kidogo zinazotolewa kwa ajili ya uendelezaji.PICHA|MAKTABA
Na Fina Lyimo Mwananchi.
Kwa ufupi
Masaki alisema mbali na kupatiwa mikopo kwa wanachama, pia watatibiwa bure na tegemezi wao bila kulipa chochote.
Siha. Shirika la Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), limeanza kuingia kwenye vyama vya kuweka na kukopa (Saccos).
Kwa mujibu wa mfuko huo, sasa imeziasa Saccos
kushawishi wanachama wao wajiunge na NSSF ili wapate fursa zinazotolewa
na mfuko huo.
Meneja wa NSSF, Mkoa wa Kilimanjaro, Delfina
Masaki, alisema hayo jana kwenye mkutano maalumu wa wanachama wa Saccos
ya Ivueny iliyopo Siha mkoani Kilimanjaro. Alisema wanachama wa Saccos
wakijiunga na mfuko huo watapewa mkopo kwa riba nafuu.
Masaki alisema kupitia Saccos wanachama wa NSSF
wanapatiwa mikopo yenye riba ndogo, hali itakakayowafanya watumie mikopo
hiyo kwa kufanya biasara na kuinua kipato cha kwa ujumla.
Masaki alisema mbali na kupatiwa mikopo kwa wanachama, pia watatibiwa bure na tegemezi wao bila kulipa chochote.
Meneja huyo alisema mfuko huo huwa unachukua riba
ya asilimia 9.2 kwa wanachama wanaokopeshwa kuanzia Sh50 milioni na
kuendelea. Kwa upande wake Mweneykiti wa Saccos ya Ivaeny Rodrick Maimu,
alipongeza uongozi wa NSSF kwa kuwahamasisha na kuweza kupata fursa
ambazo zinatolewa na mfuko huo. Alisema wanafanya linalowezekana
kuimarisha uhusiano baina yao kwa lengo la kuleta tija kila upande.
No comments:
Post a Comment