Na Mwandishi wetu, Globu ya Jamii
MAHAKAMA
ya Rufaa imebatilisha uamuzi wa Mahakama Kuu wa kuruhusu
makosa yasiyo na dhamana yadhaminiwe na kubainisha kwamba kifungu kinachozuia dhamana hakikinzani na Katiba na kukubali rufaa iliyokatwa na Mkurugenzi wa Mashitaka Nchini (DPP) na Mwanasheria Mkuu wa serikali (AG)
makosa yasiyo na dhamana yadhaminiwe na kubainisha kwamba kifungu kinachozuia dhamana hakikinzani na Katiba na kukubali rufaa iliyokatwa na Mkurugenzi wa Mashitaka Nchini (DPP) na Mwanasheria Mkuu wa serikali (AG)
Uamuzi
wa kukubaliwa kwa rufaa hiyo ulisikilizwa na jopo la majaji watano,
Stella Mugasha, Gerald Ndika, Jacobs Mwambegele, Mwanaisha Kwariko na
Ignas Kitusi, na umesomwa leo Agosti 5, 2020 na msajili Mwandamizi wa
mahakama ya rufaa Eva Nkya
Katika
uamuzi wao wamesema kifungu namba 148(5) A mpaka E havikinzani na
Katiba na vinakidhi masharti na kwamba kifungu hicho kinachobainisha
makosa ambayo hayadhaminiki kinakidhi matakwa ya Kikatiba.
"Baada ya kupitia hoja za pande zote mbili, mahakama inatamka kwamba uamuzi wa Mahakama Kuu umebatilishwa.
Baadhi
ya makosa yaliyo katika kifungu hicho ni makosa ya mauaji, unyang'anyi
wa kutumia siraha, uhaini, ugaidi, utakatishaji fedha na kesi za dawa za
kulevya.
Makosa
mengine ni mtu aliyewahi kufungwa miaka 30 jela hataweza kupata
dhamana, mtu aliyepewa dhamana akashindwa kutekeleza masharti ya dhamana
au akaruka dhamana, pale ambapo mtu anatakiwa kukaa ndani kwa ajili ya
usalama wake, pale ambapo kosa linazidi milioni 10.
Mapema,
DPP na AG walikata rufaa hiyo wakipinga uamuzi wa Mahakama Kuu katika
shauri lililofunguliwa na Dickson Sanga akitaka makosa hayo yawe na
dhamana kwa sababu kifungu kilichokuwa kinazuia kinakiuka Katiba ya
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Mei
18, mwaka huu mahakama Kuu ilitoa uamuzi dhidi ya Maombi hayo na kusema
kwamba Kifungu cha 148 (5) cha sheria ya makosa ya jinai kinakiuka
Katiba.
Katika
rufaa yake DPP na AG walidai kifungu hicho hakikiuki Katiba ya Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania na kuwa Mahakama Kuu ilikosea kisheria kutamka
kuwa kifungu namba 148(5) kinakiuka Ibara ya 13(3) ya Katiba ya Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania.
Pia
mahakama hiyo ilifanya makosa ya kisheria kutamka kuwa Kifungu hicho
namba 148 cha sheria ya makosa ya jinai hakithibitishwi na Ibara ya
15(1) na (2)(a ) ya Katiba wa Jamhuri ya Muungano, kwamba kifungu hicho
kilikiuka Katiba pamoja na kwamba mjibu rufaa alishindwa kuthibitisha
madai yake pasi kuacha shaka.
Katika
hoja nyingine ya warufani hao walidai kwamba Mahakama kuu ilikosea
kupinga kifungu hicho bila kuzingatia shida zinazoweza kusababishwa
katika mfumo mzima wa utawala wa haki za Jinai nchini.
No comments :
Post a Comment