Baadhi ya wakazi wa
Manispaa ya Tabora wakishiriki mazoezi ya kukimbia jana ikiwa ni sehemu
ya kuadhimisha uzinduzi wa wiki ya Kampeni ya kupambana na kudhibiti
magonjwa yasiyoyakuambukizwa.
Mkuu wa Wilaya ya
Tabora Komanya Kitwala (aliyekaa) akipima Shinikizo la Damu jana ikiwa
ni sehemu ya kushiriki uzinduzi wa wiki ya maadhimisho ya Kampeni ya
kupambana na kudhibiti magonjwa yasiyoyakuambukizwa kwa Mkoa wa Tabora.
Baadhi ya wakazi wa
Manispaa ya Tabora wakishiriki mazoezi ya viuongo jana ikiwa ni sehemu
ya kuadhimisha uzinduzi wa wiki ya Kampeni ya kupambana na kudhibiti
magonjwa yasiyoyakuambukizwa.
Baadhi ya wakazi wa
Manispaa ya Tabora wakisikiliza mada mbalimbali ikiwa ni sehemu ya
kuadhimisha uzinduzi wa wiki ya Kampeni ya kupambana na kudhibiti
magonjwa yasiyoyakuambukizwa kwa Mkoa wa Tabora jana.
Katibu Tawala
Msaidizi (Afya) Mkoa wa Tabora Dkt. Honoratha Rutatinisibwa akitoa
taarifa kuhusu ongezeko la magonjwa yasiyoambukizwa Mkoa wa Tabora jana
ikiwa ni sehemu ya wiki ya maadhimisho ya Kampeni ya kupambana na
kudhibiti magonjwa hayo.
Kaimu Katibu Tawala
Mkoa wa Tabora Hamis Mkunga akitoa salamu za Mkoa jana wakati wa wiki
ya maadhimisho ya Kampeni ya kupambana na kudhibiti magonjwa
yasiyoyakuambukiza.
Mkuu wa Wilaya ya
Tabora Komanya Kitwala akizundua jana wiki ya maadhimisho ya Kampeni ya
kupambana na kudhibiti magonjwa yasiyoyakuambukiza kwa Mkoa wa Tabora.
Mkuu wa Wilaya ya
Tabora Komanya Kitwala(katikati) akipima uzito jana wakati wa uzinduzi
wa wiki ya maadhimisho ya Kampeni ya kupambana na kudhibiti magonjwa
yasiyoyakuambukiza kwa Mkoa wa Tabora.
Picha na Tiganya Vincent
………………….
NA TIGANYA VINCENT
IDARA ya Afya Mkoani Tabora
imesema kuwa jitihada za makusudi zinahitajika kuzuia na kudhibiti
ongezeko kubwa la magonjwa yasiyoambukiza mkaoni humo.
Baadhi ya magonjwa yasiyoambukizwa ni kisukari, shinikizo la damu, seli mundu, saratani , magonjwa ya akili na pumu.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa
Kampeni wa kuzuia na kudhibiti magonjwa hayo Katibu Tawala Msaidizi
(Afya) Dkt. Honoratha Rutatinisibwa alisema toka mwaka 2017 hadi 2019
kumekuwepo na ongezeko la magonjwa hayo Mkoani humo.
Alitaja baadhi ya wagonjwa wa
magonjwa yasioambukizwa waliongeza kuwa ni kisukari ambapo mwaka 2017
walikuwa 4,345 na kuongezaka hadi kufikia 6,732 mwaka 2019 ikiwa ni
ongezeko la wagonjwa 2,387 sawa na asilimia 35.
Dkt. Rutatinisibwa alisema kwa
upande ugonjwa wa Shikizo la Damu, wagonjwa wameongezeka katika kipindi
hicho hicho kutoka 13,940 hadi kufikia 19,460 ikiwa ni ongezeko wagonjwa
5,520 sawa na asilimia 28.
Aliongeza kuwa upande wa ugonjwa
wa pumu umeongezeka kutoka wagonjwa 5,338 hadi kufikia wagonjwa 8,434
ikiwa kuna ongezeko la wagonjwa 3,096 sawa na asilimia 37 ndani ya
kipindi hicho hicho.
Akizungumza wakati wa kilele cha
wiki ya maadhimisho ya Kapambana na magonjwa hayo ,Mkuu wa Wilaya ya
Tabora Komanya Kitwala aliwataka wakazi wa Mkoa wa Tabora kujenga tabia
ya kuchunguza afya zao mapema walau mara mbili kwa mwaka.
Alisema hatua hiyo itasaidia
kugundua matatizo mapema na kuwahi kukabiliana nalo likiwa bado katika
hatua za awali kwa kutumia gharama kidogo.
Kitwala aliongeza kuwa suluhisho
jingine ambalo halihitaji gharama kubwa kukabiliana na tatizo hilo ni
pamoja na wakazi wa Tabora kubadili mfumo wa maisha juu ya ulaji wa
vyakula na kushiriki mazoezi.
No comments :
Post a Comment