Utangulizi
Kwa mujibu wa Sheria ya Benki Kuu ya
Tanzania, Sura ya 197, Benki Kuu inatoa Tamko la Sera ya Fedha linaloweka
bayana mwelekeo wa...
sera ya fedha kwa mwaka 2019/20. Tamko hili linajumuisha
mapitio ya mwenendo wa uchumi na utekelezaji wa sera ya fedha ya mwaka 2018/19,
na kuainisha malengo ya sera ya fedha kwa mwaka 2019/20 yanayoendana na
mahitaji ya malengo mapana ya kiuchumi ya Serikali ya kusimamia utulivu wa bei
na ukuaji wa uchumi. Tamko hili pia linaelezea hatua zinazokusudiwa kuchukuliwa na Benki Kuu ili
kukia malengo hayo.
Mwenendo wa Uchumi wa Dunia
Kulingana na taarifa ya Mwelekeo wa
Hali ya Uchumi wa Dunia iliyotolewa na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF)
mwezi Aprili 2019, uchumi wa dunia ulikua kwa wastani wa asilimia 3.6 mwaka
2018, ikilinganishwa na wastani wa asilimia 3.8 mwaka 2017. Ukuaji mdogo wa
uchumi wa dunia ulichangiwa zaidi na athari za kiuchumi kutokana na majanga ya
asili yaliyoikumba Japan, kuongezeka kwa vikwazo vya kibiashara baina ya
Marekani na China, kudorora kwa upatikanaji wa rasilimali fedha, na
kutokutabirika kwa athari za Uingereza kujitoa kwenye Umoja wa Kiuchumi wa Nchi
za Ulaya.
Ukuaji wa uchumi wa nchi
zilizoendelea ulikia asilimia 2.2 mwaka 2018, ukilinganishwa na ukuaji wa
asilimia 2.4 kwa mwaka 2017. Hali hiyo ilichangiwa zaidi na kupungua uzalishaji
wa magari nchini Ujerumani kutokana na kuanza matumizi ya sheria mpya za
uchafuzi wa mazingira; kudorora kwa uwekezaji nchini Italia; na kupungua kwa
matumizi ya walaji nchini Ufaransa.
Ukuaji wa uchumi nchini Uingereza ulipungua na kukia asilimia 1.4 kutoka
asilimia 1.8, hasa kwa sababu ya hofu ya kujitoa kutoka katika Jumuiya ya Ulaya
(Brexit). Nchini Japan, ukuaji wa uchumi ulipungua hadi asilimia 0.8 kutoka
asilimia 1.7, kutokana na kudorora kwa shughuli za kiuchumi katika robo ya tatu
ya mwaka 2018, kulikosababishwa na hali mbaya ya hewa na maafa. Hata hivyo,
ukuaji wa uchumi nchini Marekani umebakia kuwa imara, ukikua kwa asilimia 2.9
mwaka 2018, ikilinganishwa na asilimia 2.3 mwaka 2017, ingawa kumekuwa na
kusuasua kwenye uwekezaji katika nusu ya pili ya mwaka 2018. Ukuaji wa uchumi
wa nchi zinazoibukia kiuchumi na zile zinazoendelea kukua ulikia asilimia 4.5 mwaka 2018
ukilinganishwa na asilimia 4.8 mwaka
2017. Ukuaji huu ulisababishwa na kudorora kwa masoko ya fedha katika nusu ya
pili ya mwaka 2018. Ukuaji wa uchumi nchini China ulipungua hadi asilimia 6.6
mwaka 2018 kutoka asilimia 6.8 mwaka 2017, ukichangiwa zaidi na kupungua
uwekezaji wa ndani, kupungua kwa mauzo ya magari pamoja na mvutano wa
kibiashara na Marekani. Ukuaji wa uchumi nchini India ulikuwa asilimia 7.1
mwaka 2018, ukilinganishwa na asilimia 7.2 mwaka 2017. Ukuaji wa uchumi wa nchi
za kusini mwa jangwa la Sahara umeendelea kuimarika katika mwaka 2018,
japo kwa kasi ya chini, huku wastani wa Pato Halisi la Taifa ukikadiriwa kukua
kwa asilimia 3.0 mwaka 2018, kutoka
asilimia 2.8 iliyokiwa mwaka 2017.
Taarifa ya Mwelekeo wa Hali ya
Uchumi wa Dunia iliyotolewa na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) mwezi Aprili
2019, inakadiria uchumi wa dunia utakua kwa asilimia 3.3 mwaka 2019, kutokana
na matarajio ya ukuaji mdogo wa uchumi katika nchi zilizoendelea. Ukuaji wa
uchumi wa mataifa yaliyoendelea unakadiriwa kupungua na kukia asilimia 1.8 mwaka 2019, kutokana na kuendelea kwa
mvutano wa kibiashara baina ya China na Marekani, hofu ya nchi ya Uingereza
kujitoa kutoka katika Jumuiya ya Ulaya (Brexit), na makadirio ya ukuaji mdogo
wa uchumi wa nchi katika bara la Ulaya kutokana na kudorora kwa mahitaji ya
sekta binafsi na uzalishaji viwandani. Ukuaji wa uchumi katika nchi
zinazoibukia kiuchumi na zile zinazoendelea kukua, unatarajiwa kukua chini ya
asilimia 5.0 mwaka 2019, kutokana na kupungua kwa ukuaji wa uchumi wa China, na
kudorora kwa uchumi wa Uturuki na Iran. Wakati huo huo, inakadiriwa kuwa ukuaji
wa uchumi wa nchi za kusini mwa Jangwa la Sahara, utaongezeka na kukia
asilimia 3.5 mwaka 2019 kutoka asilimia
3.0 mwaka 2018, kutokana na kuongezeka kwa kasi ya ukuaji uchumi kunakochangiwa
zaidi na uwekezaji katika miundombinu. Viwango vya mfumuko wa bei katika nchi
zilizoendelea na zile zinazoibukia kiuchumi vimeendelea kubaki katika viwango
vya chini kutokana na kushuka kwa bei za chakula na nishati. Katika nchi za
Jumuiya ya Afrika ya Mashariki (EAC), kasi ya mfumuko wa bei umeendelea kubakia
katika kiwango kilichokubaliwa cha chini ya asilimia 8.0 kutokana na
upatikanaji mzuri wa chakula. Katika nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), wastani wa mfumuko wa bei
uliongezeka na kukia asilimia 11.9
mwezi Aprili 2019 kutoka asilimia 8.5 mwezi Aprili 2018, ukichangiwa zaidi na
kupanda kwa bei za chakula, mavazi na gharama za usarishaji.
Kulingana na taarifa ya mwelekeo wa
hali ya uchumi wa dunia iliyotolewa na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) ya
mwezi Aprili 2019, viwango vya mfumuko wa bei katika nchi zilizoendelea
unatarajiwa kupungua na kukia wastani wa asilimia 1.6 mwaka 2019, kutoka
asilimia 2.0 mwaka 2018 kutokana na
matarajio ya kupungua kwa bei za bidhaa. Wakati huohuo, mfumuko wa bei katika
nchi zinazoibukia kiuchumi na zile zinazoendelea
kukua unatarajiwa kuongezeka kidogo hadi kukia wastani wa asilimia 4.9 mwaka 2019, kutoka asilimia
4.8 mwaka 2018; kutokana na matarajio ya kuimarika kwa mahitaji nchini India na
kupanda kwa bei za vyakula kwenye baadhi ya nchi.
Mwenendo wa Uchumi wa TanzaniaTanzania
Bara
Uchumi wa Tanzania umeendelea kukua
kwa kasi ya juu, ambapo kwa mwaka 2018 uchumi ulikua kwa wastani wa
asilimia 7.0 ikilinganishwa na ukuaji wa asilimia 6.8 na asilimia 6.9 kwa mwaka
2017 na 2016, kwa mpangilio huo. Ukuaji huu umechochewa zaidi na uwekezaji
katika huduma za kijamii na miundombinu, kutengemaa kwa ugavi wa umeme, hali
nzuri ya hewa na utekelezaji wa sera ya fedha ya kuongeza ukwasi kwenye uchumi.
Shughuli za kiuchumi zilizokua kwa kasi ya juu zaidi ni pamoja na sanaa, burudani na starehe;
ujenzi; usarishaji na uhifadhi;
sayansi na teknolojia; na
mawasiliano. Shughuli za ujenzi zimeendelea kuwa na mchango mkubwa kwenye
ukuaji wa uchumi zikifuatiwa na usarishaji na uhifadhi, mazao na viwanda.
Uchumi unatarajiwa kukua kwa asilimia
7.1 mwaka 2019, kufuatia uwekezaji unaoendelea katika kuboresha miundombinu na
huduma za jamii, upatikanaji wa uhakika wa umeme, kuimarika kwa ukuaji wa
mikopo kwa sekta binafsi, na uzalishaji
1 Kizio cha mwaka 2015
5
viwandani. Matarajio ya ukuaji wa
juu wa uchumi yatatokana pia na maboresho yanayofanywa na serikali katika
sheria na kanuni mbalimbali, mageuzi ya sera katika kujenga mazingira ya
kuongeza uwazi katika kufanya biashara, pamoja na mkakati wa utekelezaji wa
sera ya viwanda.Katika kipindi cha Julai 2018 mpaka Aprili 2019, mfumuko wa bei
umeendelea kubakia ndani ya lengo la muda wa kati la asilimia 5.0, na ndani ya
vigezo vya muunganiko wa kiuchumi katika Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC)
usiozidi asilimia 8.0, na wigo uliokubalika katika Jumuiya ya Maendeleo Kusini
mwa Afrika (SADC) wa kati ya asilimia 3.0 na 7.0. Hali hii ilichangiwa na
kuongezeka kwa uzalishaji na upatikanaji wa chakula nchini, utekelezaji thabiti
wa sera ya fedha na kibajeti, na kutengemaa kwa uzalishaji na ugavi wa umeme.
Katika kipindi hicho, mfumuko wa bei ulikuwa wastani wa asilimia 3.2
ikilinganishwa na asilimia 4.5 katika kipindi kama hicho mwaka 2017/18. Aidha,
mfumuko wa bei usiojumuisha bei za vyakula na nishati ulikuwa wastani wa
asilimia 2.7 ukilinganishwa na asilimia 1.6. Mfumuko wa bei unatarajiwa kubakia
ndani ya lengo la asilimia 5.0 katika mwaka 2019/20, kutokana na matarajio
mazuri ya upatikanaji wa chakula cha kutosha, kuendelea kutengemaa kwa
usambazaji wa umeme na utekelezaji thabiti wa sera ya fedha na kibajeti.Katika
kipindi cha Julai 2018 mpaka Aprili 2019, mapato yaliyokusanywa na kuwekwa
kwenye akaunti za Serikali zilizoko Benki Kuu ya Tanzania yalikuwa shilingi
bilioni 14,690.4, ikiwa ni asilimia 3.4 zaidi ya mapato yaliyokusanywa na
kuwekwa kwenye akaunti hizo katika kipindi kama hicho mwaka 2017/18. Kiasi
hicho ni sawa na asilimia 93.1 ya makadirio ya makusanyo katika kipindi hicho.
Mwenendo huu wa makusanyo ya mapato kwa sehemu kubwa umetokana na jitihada
zinazotekelezwa na Serikali katika kuongeza matumizi ya teknolojia katika
ukusanyaji wa kodi kupitia Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), na kuongezeka kwa
jitihada za usimamizi wa ukusanyaji wa mapato. Katika kipindi hicho,
jumla ya matumizi ya Serikali yaliyofanywa kupitia katika akaunti zake zilizoko
Benki Kuu yalikia shilingi bilioni 16,363.6 kati ya hizo shughuli za maendeleo
ziligharimu shilingi bilioni 4,864.6.Urari wa malipo nje ya nchi (balance of
payments) ulikuwa na nakisi ya dola za Marekani milioni 1,089.2 katika kipindi
cha Julai 2018 mpaka Aprili 2019, ikilinganishwa na ziada ya dola za Marekani
milioni 299.2 katika kipindi kama hicho mwaka 2017/18. Hali hii ilichangiwa na
kuongezeka kwa nakisi ya urari wa biashara ya bidhaa, huduma na uhamisho mali
nchi za nje (current account decit). Nakisi ya urari wa biashara ya bidhaa, huduma na uhamisho mali nchi za nje
iliongezeka na kukia dola za Marekani milioni 2,132.6 ikilinganishwa na nakisi
ya dola za Marekani milioni 1,709.5 katika kipindi kama hicho mwaka 2017/18
kufuatia kuongezeka kwa thamani ya bidhaa za mitaji zilizoagizwa kutoka nje ya
nchi kwa ajili ya miradi mikubwa ya maendeleo, hasa ya miundombinu. Nakisi ya
urari wa biashara ya bidhaa, huduma na uhamisho mali nchi za nje inatarajiwa
kukia asilimia 4.4 ya Pato la Taifa mwaka 2018/19, kutoka asilimia 3.5 mwaka
2017/18.Akiba ya fedha za kigeni imeendelea kuwa ya kuridhisha na kuendelea
kukidhi mahitaji ya fedha za kigeni kwa ajili ya kuagiza bidhaa na huduma kutoka
nje ya nchi. Hadi kukia mwishoni mwa mwezi Aprili 2019, akiba ya fedha za
kigeni ilikuwa dola za Marekani milioni 4,395.2, kutoka wa viashiria halisi vya
ukwasi kwenye mabenki na hatimaye kusaidia usimamizi wa utekelezaji wa sera ya
fedha na uhalisia wa riba katika masoko ya fedha. Wakati huo huo, Benki Kuu ipo
katika hatua za mwisho za ukamilishaji wa mwongozo wa makubaliano ya uendeshaji
wa soko la mikopo ya muda mfupi baina ya mabenki kwa kuweka dhamana (Global Master
Repurchase Agreement ) ambao ni muhimu katika utekelezaji wa sera ya
fedha.Ujazi wa fedha kwa tafsiri pana zaidi (M3) umeendelea kukua kwa wastani,
wakati ukuaji wa mikopo kwa sekta binafsi ukiendelea kuimarika kwa kasi. Ukuaji
wa mwaka wa ujazi wa fedha kwa tafsiri pana zaidi ulikia
asilimia 4.9 mwezi Aprili 2019 ambao
ni chini ya lengo la asilimia 12.2 kwa mwaka unaoishia mwezi Juni 2019. Ukuaji
huu wa fedha unaakisi ongezeko la matumizi ya kielektroniki katika kufanya
malipo, hali ambayo imeongeza kasi ya mzunguko wa fedha katika shughuli za
uchumi. Mikopo kwa sekta binafsi imeendelea kukua na kukia asilimia 10.6 mwezi
Aprili 2019, kiwango ambacho ni cha juu kuwahi kutokea tangu mwezi Oktoba
2016 na juu ya lengo la ukuaji wa
asilimia 10.2 ikapo Juni 2019. Ukuaji wa mikopo kwa sekta binafsi unaenda
sambamba na muendelezo wa utekelezaji wa sera ya fedha inayolenga kuongeza
ukwasi kwenye uchumi, pamoja na hatua zinazochukuliwa katika kupunguza mikopo
chechefu kwenye benki za biashara kulikotokana na matumizi ya kanzi data ya
taarifa za wakopaji katika kuidhinisha mikopo.Thamani ya shilingi ya Tanzania
dhidi ya sarafu mbalimbali duniani imeendelea kuwa tulivu kwa kipindi chote cha
kuanzia mwezi Julai 2018 mpaka Aprili 2019, japo kulikuwa na mabadiliko ya juu
kiasi mwezi Januari na Februari 2019. Mabadiliko hayo yalitokana zaidi kwa kuwa
kipindi hicho ni msimu wa mapato madogo yatokanayo na mauzo ya mazao nje ya
nchi na shughuli za utalii, sambamba na ongezeko la uagizaji wa bidhaa za
mitaji kutoka nje ya nchi kwa ajili ya miradi mikubwa ya maendeleo.
Matarajio ya Uchumi na Malengo ya Sera ya Fedha ya Mwaka
2019/20
Katika mwaka 2019/20, Serikali ya
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar zitaendelea
kutekeleza Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Miaka Mitano (Second Five Year Development Plan 2016/17 – 2020/21) na Mpango
wa Kukuza Uchumi Zanzibar (MKUZA III 2015-2020) zinazolenga kuendeleza
jitihada za kuweka misingi imara ya uendelezaji wa viwanda na kukuza uchumi
shirikishi kama hatua ya kuukisha uchumi wa nchi kuwa wa kipato cha kati.
Katika mwaka 2019/20, Serikali zinalenga yafuatayo: i. Ukuaji wa Pato la Halisi
Taifa la asilimia 7.1 kwa Tanzania Bara kwa mwaka 2019;ii. Mfumuko wa bei ulio
ndani ya kiwango cha tarakimu moja; naiii. Nakisi ya bajeti ikijumuisha misaada
kutoka nje (grants) ya asilimia 2.3 ya Pato la Taifa kwa Serikali ya Jamhuri ya
Muungano kwa mwaka 2019/20.
Kwa upande wa Zanzibar, Pato la
Taifa linatarajiwa kukua kwa asilimia 7.8 mwaka 2019, wakati nakisi ya bajeti
ya serikali ya Zanzibar inatarajiwa kuwa asilimia 3.9 ya Pato la Taifa mwaka
2019/20.
Ili kukia malengo ya Serikali ya
uchumi mpana kwa mwaka 2019/20, Benki Kuu ya Tanzania itaendelea kutekeleza
sera ya fedha inayolenga kuimarisha
utulivu wa bei pamoja na utulivu wa riba katika masoko ya fedha. Kwa mwaka 2019/20, Benki Kuu
imepanga kukia malengo yafuatayo:i. Ukuaji wa wastani wa fedha taslim wa
asilimia 9.0;ii. Ukuaji wa ujazi wa fedha kwa tafsiri pana zaidi (M3) wa asilimia
10.0;iii. Ukuaji wa mikopo kwa sekta binafsi wa asilimia 13.5; naiv. Kuwa na
akiba ya fedha za kigeni inayotosha kuagiza bidhaa na huduma kutoka nje ya nchi
kwa kipindi kisichopungua miezi minne.Katika utekelezaji wa majukumu yake,
Benki Kuu itaendelea kuboresha ufanisi wa masoko ya fedha kuendana na
mabadiliko ya utekelezaji wa sera ya fedha itakayotumia riba ya Benki Kuu. Vile
vile, Benki Kuu itaendelea kutekeleza sera ya fedha kwa uwazi na kwa kutumia
zana mbalimbali za sera ya fedha ili kuhakikisha kuwa kiasi cha ukwasi kwenye
benki za biashara kinabakia katika kiwango kinachoendana na mahitaji ya wakati
huo, na hivyo kuleta utulivu wa riba katika soko la fedha baina ya mabenki.
Hitimisho
Uchumi wa Tanzania unatarajia
kuendelea kuwa imara kutokana na jitihada za Serikali katika kuendelea na
uwekezaji katika huduma za jamii na miundombinu chini ya awamu ya Pili ya
Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano na Mpango wa Kukuza Uchumi Zanzibar. Miradi
inayotekelezwa katika mipango hii ni chachu katika kukuza sekta binafsi na
kuwezesha uchumi wa viwanda. Kuendelea kuimarika kwa kasi ya ukuaji wa mikopo kwa
sekta binafsi kutokana na utekelezaji wa sera ya fedha inayolenga kuongeza
ukwasi katika uchumi, kuongezeka kwa uzalishaji viwandani pamoja na maboresho
ya kanuni, sheria na sera zinazolenga mageuzi ya uchumi wa viwanda yatachangia
katika ongezeko la Pato la Taifa katika mwaka 2019/20. Hata hivyo, athari
zinazotokana na kuongezeka kwa vikwazo vya kibiashara baina ya mataifa makubwa
duniani zinaweza kuathiri ukuaji wa uchumi wa Tanzania siku zijazo.Mfumuko wa
bei unatarajiwa kubakia ndani ya lengo la muda wa kati la asilimia 5.0 kutokana
na kuimarika kwa uzalishaji wa chakula; kuimarika upatikanaji wa nishati; na
utekelezaji wa sera thabiti za fedha na kibajeti. Hata hivyo, kupanda kwa bei
ya mafuta katika soko la dunia pamoja na hali ngumu ya upatikanaji rasilimali
fedha katika soko la dunia kunaweza kuathiri thamani ya shilingi ya Tanzania na
hivyo kusababisha mfumuko wa bei.Benki Kuu itaendelea kufuatilia kwa karibu
mwenendo wa uchumi wa dunia na wa nchi katika kusimamia utekelezaji wa sera ya
fedha inayolenga kudumisha utulivu wa mfumuko wa bei, na kuchukua hatua
kulingana na uwiano wa sera na mikakati ya nchi katika kukuza uchumi. Hivyo,
kutokana na tathmini ya mwelekeo wa uchumi wa dunia na uchumi wa ndani, pamoja
na sera zinazotarajiwa kutekelezwa, ni matarajio ya Benki Kuu kuwa malengo ya
sera ya fedha kwa mwaka 2019/20 yatakiwa.
No comments :
Post a Comment