Friday, January 11, 2019

WAFANYABIASHARA VIGOGO WAFIKISHWA MAHAKAMA YA KISUTU KWA MAKOSA 601


suu
Mfanyabiashara maarufu Mohamed yusufali na mfanyakazi wake Arital Maliwala wamefikishwa katika mahakama ya Hakimu mkazi Kisutu wakikabiliwa na mashtaka 601 likiwemo la kuisababishia serikali hasara ya zaidi ya bilioni 14.
Washtakiwa hao wamesomewa mashtaka yao na jopo la mawakili wa kutoka Takukuru wakiongozwa na Hashimu Ngole, Pendo Makondo, Leornad Swai ambao walikuwa wakisaidiana na wakili wa serikali Patrick Mwita mbele ya hakimu Mkazi Mkuu Wilbard Mashauri.
Katika mashtaka hayo, washtakiwa wanakabiliwa na mashtaka ya kula njama, kughushi, kuwasilisha taarifa za mwezi za mahesabu ya uongo kwa TRA, kukwepa kodi na kuisababishia serikali hasara ya sh. 14,987,707,044.58
Katika shtaka la kuisababishia serikali hasara, washtakiwa hao wanadaiwa kutenda kosa la kusabisha hasara ambayo imetokana na kukwepa kodi ya serikali kwa kipindi cha mwaka 2008 hadi 2015 kupitia kampuni ya Pamplant ltd iliyokuwa inamilikiwa na mshtakiwa Yusufali ambapo mshtakiwa Paliwala alikuwa mfanyakazi wake.
Imeendelea kudaiwa kuwa washtakiwa walitenda kosa hilo wakiwa wanatumia stakabadhi za kughushi pamoja na kutumia makampuni ya kughushi wakidai kuwa wamenunua vitu kutoka katika makampuni mbali mbali wakati wakijua baadhi ya kampuni hizo ni za kughushi huku zikiwa hazijasajiliwa brella.
Pia imedaiwa kampuni hizo zina majina ya makampuni ambayo hayapo brella na yana namba  za usajili ambazo brella haijazifikia huku pia wakiwa wanaghushi stakabadhi za malipo.
Hata hivyo washtakiwa hawakuruhusiwa kujibu kitu chochote mahakamani hapo kwa kuwa mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu haina mamlaka ya kusikiliza kesi za uhujumu uchumi isipokuwa kwa kibali kutoka kwa DPP.
Kwa mujibu wa upande wa mashtaka upelelezi katika kesi hiyo umeishakamilika na kesi hiyo itakuja tena mahakamani hapo January 24  mwaka huu kwa ajili ya washtakiwa kusomewa maelezo yao (commital).

No comments :

Post a Comment