Thursday, October 11, 2018

NAIBU WAZIRI, MHE. JAPHET HASUNGA AAGIZA USAJILI WA WATOA HUDUMA ZA UTALII NCHINI


1a
Naibu Waziri wa  Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga(kulia) akizungumza na Mtendaji Mkuu wa Chuo cha Taifa cha Utalii, Dkt. Shogo Sedoyeka(kushoto)  mara baada ya Naibu Waziri huyo kufanya ziara katika chuo ambapo alizungumza na watumishi wa chuo hicho katika Kampasi ya Temeke, jijini Dar es Salaam.
2a
  1. aibu Waziri wa  Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga(wa pili kushoto)  akizungumza na watumishi wa chuo hicho katika Kampasi ya Bustanini , jijini Dar es Salaam. Wa pili kulia ni Mtendaji Mkuu wa Chuo cha Taifa cha Utalii, Dkt. Shogo Sedoyeka
3a
Naibu Waziri wa  Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga (katikati) akiwa  na Mtendaji Mkuu wa Chuo cha Taifa cha Utalii, Dkt. Shogo Sedoyeka  wakiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya watumishi wa Chuo mara katika Kampasi ya Bustanini   jijini Dar es Salaam.
4a
Naibu Waziri wa  Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga(kulia) akizungumza na Mtendaji Mkuu wa Chuo cha Taifa cha Utalii, Dkt. Shogo Sedoyeka(kushoto)  mara baada ya Naibu Waziri huyo kufanya ziara katika chuo ambapo alizungumza na watumishi wa chuo hicho katika Kampasi ya Temeke, jijini Dar es Salaam.
5a
Naibu Waziri wa  Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga(kulia) akiwa ameongoza na  Mtendaji Mkuu wa Chuo cha Taifa cha Utalii, Dkt. Shogo Sedoyeka(kushoto)  mara baada ya Naibu Waziri huyo kufanya ziara katika chuo hicho katika Kampasi ya Temeke, jijini Dar es Salaam.
6a
Naibu Waziri wa  Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga(katikati) akipewa maelezo na  Mtendaji Mkuu wa Chuo cha Taifa cha Utalii, Dkt. Shogo Sedoyeka(kushoto) kuhusiana na vyumba vipya vya kulala wageni  vilianzishwa katika chuo hicho mara baada ya Naibu Waziri huyo kufanya ziara katika chuo hicho katika Kampasi ya Bustanini  jijini Dar es Salaam.
7
  1. Naibu Waziri wa  Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga akinagalia baadhi ya majiko ambayo yamekuwa yakitumiwa na wanafunzi  wa Chuo cha Taifa cha Utalii wakati wa mafunzo kwa vitendo.
……………………….
Serikali imekiagiza Chuo cha Taifa cha Utalii ifikapo Januari mwakani kianze kutoa usajili na utambulisho kwa watu wanaotoa huduma kwa watalii.
Usajili huo unapaswa kwenda sambamba na mitihani watakayofanya walengwa kuhakikisha kama wamebobea kutoa huduma hizo kwa watalii.
Agizo hilo limetolewa leo na Mhe.Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga  alipokutana  na watumishi wa chuo hicho jijini Dar es Salaam.
Mhe.Hasunga ameelekeza watu wote wanaohusika kuhudumia watalii kufanya mitihani hiyo ya kuhakikiwa ili kutambulika na kupata usajili kwa hiari baada ya hapo wasiosajiliwa hawataruhusiwa kufanya kazi hizo.
Amesema lengo la usajili huo ni kulinda fani ya huduma za utalii na ukarimu inayoonekana kuvamiwa na watu wasiokuwa na sifa.
“Mtalii hawezi kurudi nchini kama amehudumiwa na watu wasiokuwa na ukarimu na sifa zisizofaa, 
“Ukipita kwenye hoteli huko unakutana na vitu ambavyo havivutii kabisa kwa sababu kuna wavamizi wamevamia, sasa hilo lifike mwisho nataka kuanzia Januari wote watambulike,”
Mhe.Hasunga pia ameagiza wakufunzi wa chuo hicho kufanya tafiti na kuandika machapisho ya kitaaluma kwenye eneo la utalii na maliasili.
Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa Chuo hicho Dk Shogo Sedoyeka changamoto kubwa waliyonayo ni kupata eneo kwa ajili ya kampasi ya Temeke.
Amesema,” Lile eneo tunatakiwa kuhama kwahiyo tunahangaikia kupata ardhi ili tuhamishe kampasi na itakuwa huru kwetu kwa sababu litakuwa eneo letu,”.

No comments :

Post a Comment