Jaji Kiongozi, Mahakama Kuu
ya Tanzania, Mhe. Dkt. Eliezer Feleshi akitoa neno wakati wa hafla ya
kuwaaga rasmi Majaji Wastaafu wa Mahakama Kuu, Kanda ya Dar es Salaam,
walioketi ni sehemu ya Majaji Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam pamoja
na Divisheni walioshiriki katika hafla hiyo.
Jaji Kiongozi, Mahakama Kuu
ya Tanzania, Mhe. Dkt. Eliezer Feleshi akitoa neno wakati wa hafla ya
kuwaaga rasmi Majaji Wastaafu wa Mahakama Kuu, Kanda ya Dar es Salaam,
walioketi ni sehemu ya Majaji Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam pamoja
na Divisheni walioshiriki katika hafla hiyo.
Jaji Mstaafu wa Mahakama Kuu,
Mhe. Sekieth Kihio akipokea zawadi kutoka kwa Jaji Kiongozi wa Mahakama
Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Eliezer Feleshi, (katikati) ni Jaji wa
Mahakama Kuu, Kanda ya Dar es Salaam, Mhe. Jaji Munisi.
Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu
ya Tanzania, Mhe. Dkt. Eliezer Feleshi akimpatia zawadi, Jaji Mstaafu
Mhe. Laurence Kaduri ikiwa ni ishara ya pongezi kwa kumaliza utumishi wa
Mahakama salama.
Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Eliezer Feleshi akimpatia zawadi, Mhe. Jaji Mstaafu Gadi Mjemmas
Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Eliezer Feleshi akimpatia zawadi, Mhe. Jaji Mstaafu Fredrica Mgaya
Jaji Mstaafu wa Mahakama Kuu, Divisheni ya Kazi, Mhe. Ibrahim Mipawa akitoa neno la shukrani
Jaji Kiongozi, Mhe. Dkt.
Eliezer Feleshi (katikati) pamoja na baadhi ya Majaji wa Mahakama Kuu
waliohudhuria katika hafla ya kuwaaga Majaji Wastaafu wakiwa katika
picha ya pamoja na Majaji hao.
Jaji Kiongozi, Mhe. Dkt.
Eliezer Feleshi (katikati) pamoja na baadhi ya Majaji wengine wa
Mahakama Kuu waliohudhuria katika hafla wakiwa katika picha ya pamoja na
Majaji Wastaafu, wa kwanza kushoto ni Jaji Mstaafu, Mhe. Sekieth Kihio,
wa pili kushoto ni Jaji Mstaafu, Mhe. Laurence Kaduri, wa pili kulia ni
Jaji Mstaafu, Mhe. Fredrica Mgaya, wa kwanza kulia ni Jaji Mstaafu,
Mhe. Ibrahim Mipawa. Waliosimama wa pili kulia ni Jaji Mstaafu, Mhe.
Gadi Mjemmas, wa pili kushoto ni Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu, Kanda ya
Dar es Salaam, Mhe. Beatrice Mutungi, wa kwanza kushoto ni Jaji wa
Mahakama Kuu, Kanda ya Dar es Salaam, Mhe. Jaji Munisi na wa kwanza
kulia ni Jaji wa Mahakama Kuu, Kanda ya Dar es Salaam, Mhe. Ilvin
Mugeta.
……………………………………………………………………………….
Na Mary Gwera, Mahakama
JAJI Kiongozi, Mahakama Kuu ya
Tanzania, Mhe. Dkt. Eliezer Feleshi amewahakikishia Majaji Wastaafu kuwa
Mahakama itaendelea kushirikiana nao katika masuala mbalimbali licha ya
kuwa wamemaliza muda wao wa kazi.
Mhe. Jaji Feleshi aliyasema hayo,
Septemba 22 jijini Dar es Salaam, katika hafla fupi ya
kuwaaga jumla ya
Majaji Wastaafu tisa (9) kutoka Mahakama Kuu- Masjala Kuu, Kanda ya Dar
es Salaam, Mahakama Kuu Divisheni ya Ardhi na Kazi.
“Napenda kuwapongeza kwa Utumishi
wenu uliotukuka kwa Mahakama hadi kufikia siku ya leo, nipende
kuwahakikishia kuwa Mahakama itaendelea kuwa pamoja nanyi kwa kila hali,
iwe kwa shida au raha,” alisema Jaji Kiongozi.
Aidha; Mhe. Jaji Kiongozi
aliwataka Majaji hao kutosita kushiriki katika shughuli mbalimbali za
Mahakama ili kuendeleza maboresho ambayo Mahakama inakusudia kufikia
kupitia Mpango Mkakati wake.
Aliongeza kwa kuwasihi Majaji hao
Wastaafu kutosita kutoa ujuzi wao kwa Majaji ambao bado wapo kwenye
Utumishi wa Umma pindi wanapohitajika kutoa elimu katika Mafunzo
mbalimbali yanayofanyika ndani ya Mahakama.
Kwa upande wake, Jaji Mstaafu,
Mahakama Kuu Divisheni ya Ardhi, Mhe. Fredrica Mgaya ameushukuru Uongozi
wa Mahakama kwa kuwaandalia hafla hiyo kwani wamefurahi na kujisikia
kuwa wao bado ni sehemu ya Wanafamilia wa Mahakama.
Kwa ujumla Majaji hao Wastaafu
kila mmoja kwa nafasi yake waliishukuru Mahakama ya Tanzania kwa kuwalea
na kufanya kazi kwa ushirikiano katika kipindi chote cha utumishi wao.
Vilevile wametoa wito kwa Watumishi wa Mahakama ambao bado wapo kazini kufanya kazi kwa bidii na kupenda kazi zao.
Majaji Wastaafu walioagwa ni
pamoja na Mhe. Sekieth Kihio, Mhe. Projestus Rugazia, Mhe. Augustine
Shangwa, Mhe. Laurence Kaduri, Mhe. Gadi Mjemmas, Mhe. Fredrica Mgaya,
Mhe. Ibrahim Mipawa, Mhe. Aghaton Nchimbi, na Mhe. Pelagia Khaday.
No comments :
Post a Comment