Sunday, September 23, 2018

MAAFA YA MV NYERERE: IDADI YA WALIOFARIKI YAONGEZEKA NA KUFIKIA 224 HADI KUFIKIA MCHANA WA LEO



NA K-VIS BLOG/Khalfan Said

WAZIRI Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa, leo Septemba 23, 2018 ameongoza mamia ya waombolezaji kwenye mazishi ya miili 9 kati ya 224 waliofariki kwenye ajali ya kivuko cha Mv. Nyerere pembezoni mwa ziwa Victoria eneo la Bwisya, Ukara, Wilayani Ukerewe Mkoani Mwanza

Miili hiyo 9 ni kati ya minne (4) ambayo haikuweza kutambuliwa na jamaa zao, na mingine mitano iliyotambuliwa lakini ndugu zao wameonelea wazikwe pamoja chini ya usimamizi wa serikali, amesema Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Issack Kamwelwe, wakati akitoa taarifa ya maafa hayo.

Akitoa taarifa ya maafa hayo, Mhandisi Kamwelwe alisema hadi leo Septemba 23, 2018 wakati wa mazishi ya wenzetu hao, imethibitishwa kuwa jumla ya watu 224 wamepoteza ,maisha kwenye ajali hiyo.” Alsiema na kufafanua kuwa

Wanawake (watu wazima) walikuwa  126, wanaume  (watu wazima) walikuwa 71, watoto wa kike 17, watoto wa kiume 10na hivyo kufanya jumla ya watu 224 waliopoteza maisha.” Alisema.

Alizungumza saa chache kabla ya mazishi hayo, Waziri Mkuu alisema,uchunhguzi wa awali unaonyesha kivuko hicho kilipata ajali kutokana na kubeba uzito kupita kiasi, ambapo alisema wakati kivuko kina uwezo wa kubeba watu 101, siku hiyo kilibeba watu zaidi ya 224.

Akitoa historia ya kivuko hicho cha Mv Nyerere, Waziri Kamwelwe alisema, kivuko cha Mv Nyerere kilitengenzwa rasmi 2004 na kikaanza kufanya kazi, 2013 kikafanyiwa ukarabati mkubwa na kurudishwa katika upya, mwaka 2015 kivuko kilifanyiwa ukarabati tena.

“Tuliona injini zimechakaa kidogo mwak 2017 tulinunua injini mpya 2 na gea box zake zilifungwa kwa hiyo kivuko kilikuwa katika hali nzuri.

“Kivuko kilikuwa na uwezo wa kubeba  tani 25, magari matatu na mizig” Alisema.

Alisema kivuko hicho kilipinduka siku ya Alhamisi Septemba 20, 2018 majira ya saa 7:48 na ilipofika saa 8:40 mchana taarifa za kutokea kwa ajali hiyo zilipelekwa ofisini kwa mkuu wa mkoa na haraka Mkuu wa Mkoa akiwa na kamati yake ya ulizni na usalama walielekea eneo la tukio.

“Tunawashukuru wananchi wa hapa kwani baada tu ya kutokea ajali  walianza kufanya kazi ya uokoaji na kupatikana miili 43 na kuokoa watu wengine kadhaa.” Alsiema.

Waziri Mkuu Mhe. Majaliwa amesema zoezi la uokoaji litaendelea nay eye mwenyewe binafsi atabaki huko huko Ukara kusimamia zoezi hilo na kwamba serikali itaunda Tume ya uchunguzi itakayohusisha wataalamu na vyombo vya dola ili kuchunguza chanzo cha ajali ili watakaobainika waweze kuchukuliwa hatua’ Waziri Mkuu.

Alisema serikali inafanya mpango wa kuleta kivuko kingine cha dharura Mv Nyahunge ili kiweze kutoa huduma kwa wananchi.

Wakati huo huo, serikali imetangaza namba ya Tigopesa kwa jina la RAS Mwanza-0677030000. Na hadi sasa tayari zimekusanywa shilingi milioni 190 za rambirambi hadi kufikia siku ya Septemba 23, 2018.

Aidha serikali pia imefungua akaunti maalum ya benki yenye jina MAAFA MV NYERERE, namba 31110057246

No comments :

Post a Comment