Makamu wa Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa meza kuu
na viongozi wenzake wakati wa ufunguzi wa mkutano wa Kilele wa kawaida
wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) katika ukumbi wa hoteli
ya Safari mjini Windhoek nchini Namibia leo Ijumaa Agosti 17, 2018
Makamu wa Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa meza kuu
na viongozi wenzake wakati wa ufunguzi wa mkutano wa Kilele wa kawaida
wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) katika ukumbi wa hoteli
ya Safari mjini Windhoek nchini Namibia leo Ijumaa Agosti 17, 2018
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt.
Augustine Mahiga akiwa na ujumbe wa Tanzania wakati wa ufunguzi wa
mkutano wa Kilele wa kawaida wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika
(SADC) katika ukumbi wa hoteli ya Safari mjini Windhoek nchini Namibia
leo Ijumaa Agosti 17, 2018
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia
Suluhu Hassan akiwa katika picha ya pamoja ya kumbukumbu na viongozi
wenzake wakati wa ufunguzi wa mkutano wa Kilele wa kawaida wa Jumuiya ya
Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) katika ukumbi wa hoteli ya Safari
mjini Windhoek nchini Namibia leo Ijumaa Agosti 17, 2018
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia
Suluhu Hassan akiwa katika picha ya pamoja ya kumbukumbu na viongozi
wenzake wakati wa ufunguzi wa mkutano wa Kilele wa kawaida wa Jumuiya ya
Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) katika ukumbi wa hoteli ya Safari
mjini Windhoek nchini Namibia leo Ijumaa Agosti 17, 2018
Kaimu
Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS)
mkoa wa Mbeya mhandisi Selemani Lawena wa kwanza (kulia), akitoa taarifa ya
ujenzi wa barabara ya Chunya –Makongolosi KM 39, kwa Naibu Waziri wa Ujenzi Mhe.
Elias John Kwandikwa (wa tatu kulia), alipokagua ujenzi huo, (katikati) ni Mkuu
wa Wilaya ya Chunya Mary-Prisca Mahundi.
NA
WUUM, CHUNYA
SERIKALI
imesema haitamwongezea mkataba mkandarasi China Railway 15 Bureau Group
Corporation anayejenga barabara ya Chunya –Makongolosi kwa kiwango cha lami
muda wake utakapomalizika.
Naibu
Waziri wa Ujenzi, Mhe. Elias John Kwandikwa amesema muda wa miezi 27 aliyopewa
kujenga barabara hiyo yenye urefu wa KM
39 unatosha na hivyo ni jukumu lake kuhakikisha kuwa anakuwa na vifaa na
wafanyakazi wa kutosha wakati wote.
“Mkishindwa
kukamilisha barabara hii kwa wakati hamtapata tena kazi hapa nchini kwani
mtakuwa mmeshindwa kazi kwa kukiuka mkataba na kuiongezea Serikali gharama”,
amesema Mhe. Kwandikwa.
Naye
Kaimu meneja wa wakala wa barabara (TANROADS) mkoa wa Mbeya Mhandisi Selemani
Lawena amesema barabara ya Chunya –Makongolosi ni sehemu ya barabara ya Mbeya-Rungwa
yenye urefu wa KM 293 ambayo inaunganisha kwa njia fupi mkoa wa Mbeya na mikoa
ya Singida na Tabora.
“Barabara
hii ikikamilika itafungua uchumi wa mikoa ya Mbeya na Songwe na kuhuisha
shughuli za kilimo,mifugo, uchimbaji madini na ufugaji nyuki na hivyo kuongeza
fursa za maendeleo kwa jamii na serikali kwa ujumla”, amesema mhandisi Lawena.
Mhandisi
lawena amesema sehemu ya Mbeya- Chunya KM 72 imekamilika na ujenzi wa Chunya –Makongolosi
KM 39 unatarajiwa kukamilika Januari 2020.
Katika
hatua nyingine Naibu Waziri Kwandikwa amekagua ujenzi wa barabara ya mchepuo ya
Iwambi-Mbalizi KM 6.5 jijini Mbeya ambayo
itatumiwa na magari madogo ili kupunguza msongamano na ajali katika mlima Mbalizi
na kusisitiza umuhimu wa wadau wote wa usafiri kushirikiana ili kupunguza ajali
na hivyo kulinda maisha na mali.
Ujenzi
wa daraja la Kikamba wilayani Songwe linalounganisha Mkoa wa Songwe na Katavi
ukiendelea daraja hilo linatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwaka huu.
Muonekano
wa barabara ya Chunya –Makongolosi KM 39 ambayo ujenzi wake unaendelea,
barabara hiyo ni sehemu ya barabara ya Mbeya-Rungwa yenye urefu wa KM 293
inayounganisha kwa njia fupi mkoa wa Mbeya na mikoa ya Singida na Tabora.
Naibu
Waziri wa Ujenzi Mhe. Elias John Kwandikwa akisisitiza jambo kwa Mbunge wa
Songwe Mhe. Philipo Mulugo alipokagua ujenzi wa daraja la Kikamba wilayani
Songwe, daraja hilo linaunganisha Mkoa wa Songwe na Katavi.
No comments :
Post a Comment