Lisa akiwa (kushoto) akiwa na mwenzake katika mpango wa GMT, Raj
Chandarana wakipanda mti wilayani Hai katika mradi wa mazingira wa TBL.
Lisa (wa pili kutoka kushoto)
akiwa na baadhi ya wafanyakazi wenzake wa TBL baada ya kushiriki katika
mradi wa mazingira mkoani Kilimanjaro hivi karibuni
“Wakati serikali ya Tanzania
inakwenda kasi katika kutekeleza mpango wa kuifanya Tanzania kuwa nchi
ya viwanda,kunahitajiwa uwekezaji wenye mipango mikubwa ya kuvifanya
viwanda vilivyopo na vinavyoanzishwa kuwa endelevu.Sio tu kuwekeza
kwenye fedha na teknolojia bali
kunahitajika kuwekeza katika kupata
wataalamu wa kuviendesha kwa kipindi cha sasa na miaka ya mbele ili
viweze kuwa endelevu”,anasema Lisa Cheche, mhitimu wa Chuo Kikuu ambaye
kwa sasa yupo katika programu ya kipekee, ya mafunzo ya kuwandaa
wahitimu wa vyuo vikuu kushika nafasi za uongozi ijulikanayo kama,
Global Management Trainee Program (GMT), ya kampuni ya kimataifa ya
ABinBev ambayo ni kampuni mama ya Tanzania Breweries Limited Group (TBL
Group) akiwa anafanyika kazi katika kiwanda cha (TBL).
Lisa, anaeleza kuwa bila kufanya
uwekezaji wenye mtazamo wa kujenga biashara endelevu kwa miaka mingi,
kuna hatari ya biashara nyingi hususani viwanda vinavyoanzishwa kutofika
mbali; badala yake historia ya nyuma kujirudia ambapo Tanzania ilikuwa
na viwanda vingi kuanzia katika awamu ya kwanza ya utawala ambapo vingi
vilikufa kutokana na sababu mbalimbali mojawapo ikiwa ni kukosekana kwa
mipango endelevu katika uwekezaji.
Akiwa msomi aliyehitimu Shahada ya
Kwanza ya Sayansi katika mchepuo wa Viwanda, Utawala,Uhusiano katika
masuala ya kazi na Kifaransa, kutoka Chuo Kikuu cha Cornell nchini,
Marekani, anashauri kuwa kuna haja ya kuanzishwa Progamu mbalimbali za
kuwanoa vijana wa kitanzania wahitimu wa vyuo vikuu na vyuo vya ufundi
kwa kuwapatia mafunzo ya vitendo kwa ajili ya kuwaanda kushika nafasi za
uongozi katika miaka ya mbele.
Akiongea kuhusu kupata nafasi ya
kujiunga na Programu ya kuwaandaa vijana wahitimu wa vyuo vikuu kushika
nafasi za uongozi ya ABInBev na TBL, Lisa, anaeleza kuwa anajivunia kuwa
miongoni mwa wahitimu waliochaguliwa kwenye programu hii kwa kuwa
ushindani wa kuipata nafasi ulikuwa mkubwa sambamba na mchujo mkali
uliofanywa na wataalamu mbalimbali ili kuhakikisha na kujiridhisha kuwa
wanachukua watu wenye uwezo,, makini na waliopo tayari kujifunza.
“Kwa muda mfupi ambao nimeanza
mafunzo ya vitendo katika kampuni ya TBL nimegundua kuwa programu hii ni
muhimu sana kwa kuwa katika kipindi cha muda mfupi nimejifunza mambo
mengi ambayo huko nyuma sikupata kukumbana nayo na kila kukicha nakutana
na mambo mengi mageni ya kujifunza”, anasema LisaAnasema moja ya ndoto
kubwa aliyokuwa nayo katika maisha yake ni kufanya kazi katika kampuni
kubwa na yenye mifumo mizuri ya kazi, jambo ambalo limetimia kutokana na
mazingira ya kazi aliyoyakuta kwenye kampuni ya TBL,amekuta na timu ya
wafanyakazi waliobobea katika fani mbalimbali na ambao wako tayari kutoa
utaalamu wao kwa wengine wanaojifunza.
Kitu kingine ambacho
kinamfurahisha Lisa ,katika safari yake ya mafunzo kupitia programu ya
GMT ni kukuta kampuni aliyojiunga nayo, ina mifumo thabiti iliyotokana
na uwekezaji makini,kuanzia mifumo ya uzalishaji,usambazaji wa
bidhaa,masoko na mauzo na kuwa na sera zenye mtazamo wa kujenga jamii
endelevu zinazoenda sambamba na utekelezaji wa malengo endelevu ya
milenia ya umoja wa mataifa.
“Inafurahisha kuona kampuni
inayapa kipaumbele masuala ya msingi katika kujenga biashara endelevu
kama vile utunzaji wa mazingira na vyanzo vya maji,usalama wa
wafanyakazi wake ,kushirikiana na jamii zilizopo katika maeneo
inakofanyia biashara zake kama ambavyo inafanya kazi na wakulima wa zao
la Shahiri na mazao mengine,kuhakikisha inapata malighafi zake nchini
,kuendesha mafunzo ya ujasiriamali wadogo wanaosambaza biashara zake ili
nao biashara zao ziwe endelevu bila kusahau kufanikisha miradi
mbalimbali ya kusaidia jamii mojawapo ikiwa ni miradi ya maji ,kelimisha
jamii matumizi ya vinywaji kistaarabu na kushirikiana na serikali na
wadau wengine kutoa elimu ya usalama barabarani”
Anaeleza kuwa katika safari yake
ya mafunzo atafanya kazi katika vitengo mbalimbali vya kampuni ndani na
nje ya nchi ili kupata ujuzi,na katika kipindi cha muda mfupi tayari
ameshiriki katika miradi ya mazingira,ukuzaji wa vipaji vya wanafunzi na
mradi wa promosheni ya bia ya Kilimanjaro inayowezesha washindi kwenda
nchini Urusi,kushuhudia mashindano ya kombe la Dunia mubashara.
Lisa, anaeleza kuwa anaamini kuwa
hadi kufikia mwishoni mwa programu hii ya mafunzo atakuwa amejifunza
mambo mengi yatakayomsaidia katika safari yake ndefu ya kukabiliana na
changamoto za uongozi sambamba na ubunifu na kutoa mawazo ya kitaalamu
yanayowezesha kukabili changamoto na kusonga mbele kibiashara kwa
mafanikio.
Lisa,alimalizia kwa kutoa ushauri
kwa wawekezaji wengine nchini kuwa na mtazamo wa kujenga biashara
endelevu sambamba na kuwa na programu za kuandaa wataalamu wa kuendesha
biashara wanaopata mafunzo ya vitendo kutoka kwa wataalamu waliopo kama
ilivyo programu ya GMT ya ABInBev na TBL.”Programu kama hii ni muhimu
kwa kuwanoa vijana wasomi kupata ujuzi na uzoefu zaidi,natamani kuona
pia idadi ya vijana wanaochukuliwa katika Programu hii kuongezwa zaidi
ya sasa ili inufaishe vijana wengi zaidi”alisisitiza.
Akiongea juu ya Programu ya Global
Management Trainee (GMT),Mkurugenzi wa Raslimali Watu wa TBL,David
Magese,alisema hii ni progamu inayolenga vijana wasomi ambapo
wanaobahatika kujiunga nayo hupatiwa mafunzo ya vitendo kwa kipindi cha
miezi 10 kwa ajili ya kuwaandaa kushika nafasi za juu za uongozi ndani
ya biashara za kampuni mama ya TBL ya ABIn Bev.
Alisema programu ni moja ya
mkakati wa kampuni wa kuendeleza vipaji vya vijana na kuongeza kuwa
waliochaguliwa kwenye GMT mwaka huu ambao ni 2 kwa hapa nchini mbali na
kupata mafunzo ndani ya nchi pia watapata mafunzo kwenye viwanda
mbalimbali vya kampuni vilivyopo nje ya nchi kwa kuwa wanaandaliwa kuwa
viongozi sio kwa hapa Tanzania bali wanaweza kufanya kazi katika nchi
yoyote.
Magese,alimalizia kwa kusema kuwa
kampuni itaendelea na mpango wa kuendeleza wahitimu wa vyuo vikuu nchini
kwa kuwapatia fursa za kukuza vipaji vyao kupitia programu hii ya GMT
ambayo imepata mafanikio makubwa katika nchi mbalimbali zilipo biashara
za kampuni ya ABInBev.
No comments :
Post a Comment