Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya
pamoja na Majaji Wakuu kutoka nchi za Afrika waliohudhuria Mkutano wa
Kimataifa unaohusu Jinsia na Mahakama Afrika ulioandaliwa na Mahakama ya
Tanzania kwa kushirikiana na Benki ya Dunia na kufanyika kwenye Kituo
cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC), Wengine pichani kulia ni Jaji
Mkuu wa Ghana Sophia Akuffo,Jaji Mkuu wa Zimbabwe Luke Malaba na Jaji
Mkuu wa Zanzibar Omar Othman Makungu wengine kushoto ni Jaji Mkuu wa
Kenya David Maraga, Jaji Mkuu wa Tanzania Profesa Ibrahim Hamis Juma,
Jaji Mkuu na Jaji Mkuu wa Benin Batoko Ousmane.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Jaji Mkuu
Mstaafu Augustino Ramadhan mara baada ya kufungua Mkutano wa Kimataifa
unaohusu Jinsia na Mahakama Afrika ulioandaliwa na Mahakama ya Tanzania
kwa kushirikiana na Benki ya Dunia na kufanyika kwenye Kituo cha
Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC)
Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais
……………..
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amesema Licha ya
changamoto kadhaa, Tanzania Imepiga hatua kubwa katika jitihada zake za
kupunguza unyanyasaji na ubaguzi wa kijinsia.
Makamu wa Rais ameyasema hayo leo
wakati wa Mkutano wa Kimataifa unaohusu masuala ya
Jinsia na Mahakama
Afrika ulioandaliwa na Mahakama ya Tanzania kwa kushirikiana na Benki ya
Dunia na kuhudhuriwa na Majaji Wakuu kutoka nchi za Afrika.
Makamu wa Rais amesema Tanzania
imepiga hatua kwa Marekebisho ya sheria kupitia makosa ya kijinsia ya
mwaka 1998 ,pili Utekelezaji wa Sheria ya Ardhi na Sheria ya Ardhi ya
Kijiji mwaka 1999 ilifanya mabadiliko makubwa katika kuzingatia haki za
wanawake juu ya upatikanaji wa ardhi, Tatu Utekelezaji wa sheria ya
sheria ya mtoto mwaka 2009, ambayo kati ya mambo mengine, imewekwa kwa
namna sahihi ya haki za mtoto na kuanzishwa kwa madawati maalum kwenye
vituo vya polisi ili kuboresha msaada kwa waathirika wa unyanyasaji wa
kijinsia.
Makamu wa Rais aliwaambia Majaji
Wakuu kutoka nchi za Afrika kuwa pamoja na uzoefu walionao, wana nafasi
ya kufahamu umuhimu wa kuimarisha jinsia katika mfumo wa haki.
“Ni matumaini yangu kwamba mkutano
huu utakuja na mapendekezo yenye manufaa ambayo yatafungua njia ya
kuwa na mifumo ya mahakama yenye uaminifu wa kijinsia na wajibu”
Akizungumzia Mkutano uliofanyika
kwenye Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC), Jaji Mkuu wa
Tanzania profesa Ibrahim Hamis Juma mkutano huo umejikita kuona namna
gani kunakuwa na usawa katika kutoa haki, kusogeza huduma za kimahakama
kuangalia sheria za mirathi ambapo bado mwanamke ameonekana kukandamizwa
na sheria ya kujamiiana.
Mkutano huo ambao ulihudhuriwa na
Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia Bi. Sandie Okoro, Mkurugenzi Mkazi wa
Benki ya Dunia Bi. Bella Bird, Majaji Wakuu kutoka nchi za Afrika na
wadau mbali mbali wa sekta za kimahakama na sheria.
No comments :
Post a Comment