Monday, June 11, 2018

MKUTANO WA KIMATAIFA WA MASUALA YA JINSIA NA MAHAKAMA WAFUNGULIWA LEO MJINI ARUSHA


15
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Majaji Wakuu kutoka nchi za Afrika waliohudhuria Mkutano wa Kimataifa unaohusu Jinsia na Mahakama Afrika ulioandaliwa na Mahakama ya Tanzania kwa kushirikiana na Benki ya Dunia na kufanyika kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC), Wengine pichani kulia ni Jaji Mkuu wa Ghana Sophia  Akuffo,Jaji Mkuu wa Zimbabwe Luke Malaba na Jaji Mkuu wa Zanzibar Omar Othman Makungu wengine kushoto ni Jaji Mkuu wa Kenya David Maraga, Jaji Mkuu wa Tanzania Profesa Ibrahim Hamis Juma, Jaji Mkuu na Jaji Mkuu wa Benin Batoko Ousmane.
23
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Jaji Mkuu Mstaafu Augustino Ramadhan mara baada ya kufungua Mkutano wa Kimataifa unaohusu Jinsia na Mahakama Afrika ulioandaliwa na Mahakama ya Tanzania kwa kushirikiana na Benki ya Dunia na kufanyika kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC)
5 9 12
Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais
……………..
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amesema Licha ya changamoto kadhaa, Tanzania Imepiga hatua kubwa katika jitihada zake za kupunguza unyanyasaji na ubaguzi wa kijinsia.
Makamu wa Rais ameyasema hayo leo wakati wa Mkutano wa Kimataifa unaohusu masuala ya
Jinsia na Mahakama Afrika ulioandaliwa na Mahakama ya Tanzania kwa kushirikiana na Benki ya Dunia na kuhudhuriwa na Majaji Wakuu kutoka nchi za Afrika.
Makamu wa Rais amesema Tanzania imepiga hatua kwa Marekebisho ya sheria kupitia makosa ya kijinsia ya mwaka 1998 ,pili Utekelezaji wa Sheria ya Ardhi na Sheria ya Ardhi ya Kijiji mwaka 1999 ilifanya mabadiliko makubwa katika kuzingatia haki za wanawake juu ya upatikanaji wa ardhi, Tatu Utekelezaji wa sheria ya sheria ya mtoto mwaka 2009, ambayo kati ya mambo mengine, imewekwa kwa namna sahihi ya haki za mtoto na kuanzishwa kwa madawati maalum kwenye vituo vya polisi ili kuboresha msaada kwa waathirika wa unyanyasaji wa kijinsia.
Makamu wa Rais aliwaambia Majaji Wakuu kutoka nchi za Afrika kuwa pamoja na uzoefu walionao, wana nafasi ya kufahamu umuhimu wa kuimarisha jinsia katika mfumo wa haki.
“Ni matumaini yangu kwamba mkutano huu utakuja na mapendekezo yenye manufaa ambayo yatafungua  njia ya kuwa na mifumo ya mahakama yenye uaminifu wa kijinsia na wajibu”
Akizungumzia Mkutano uliofanyika kwenye Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC), Jaji Mkuu wa Tanzania profesa Ibrahim Hamis Juma mkutano huo umejikita kuona namna gani kunakuwa na usawa katika kutoa haki, kusogeza huduma za kimahakama kuangalia sheria za mirathi ambapo bado mwanamke ameonekana kukandamizwa na sheria ya kujamiiana.
Mkutano huo ambao ulihudhuriwa na Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia Bi. Sandie Okoro, Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia Bi. Bella Bird, Majaji Wakuu kutoka nchi za Afrika na wadau mbali mbali wa sekta za kimahakama na sheria.

No comments :

Post a Comment