Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii,
Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu akizungumza katika Hospitali
ya Taifa Muhimbili (MNH) ambako maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma
yanafaniyika kwa siku tatu mfulilizo. Wananchi mbalimbali wamefika kwa
wingi katika hospitali hiyo kwa ajili ya kuona huduma mbalimbali
zinazotolewa na hospitali hiyo pamoja na kupima afya bure. Kushoto ni
Mjumbe wa Bodi ya Muhimbili, Bw. Juma Muhimbi na Mkurugenzi wa Tiba
katika wizara hiyo, Dkt. Doroth Gwajima.
Wananchi mbalimbali wakiwamo
wataalamu wa MNH wakifuatilia hotuba ya Waziri wa Afya, Mhe. Ummy
Mwalimu wakati akizungumza kwenye viwanja vya Muhimbili.
Daktari Bingwa wa Magonjwa ya
Figo, Dkt. Onesmo Kisanga akifafanua jambo kwa Waziri Ummy Mwalimu
kuhusu magonjwa ya figo. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Muhimbili,
Prof. Lawrence Museru wakati kulia ni mjumbe wa bodi ya Muhimbili, Bw.
Juma Muhimbi.
Bw. Paul Mayengo akipima dawa ya
methadone kwa watu wenye tatizo la uraibu wa heroin katika Hospitali ya
Taifa Muhimbili (MNH). Dawa hiyo inatumiwa na wataalamu wa afya kwa
ajili ya kutibu uraibu.
Prisca akimweleza waziri kuhusu
maendeleo yake baada ya kupandikizwa figo katika hospitali hiyo. Kushoto
ni Mkuu wa Idara ya Mahonjwa ya Figo, Dkt. Jacqueline Shoo.
Waziri Ummy Mwalimu akiwa kwenye
banda la lishe ambako ampatiwa maelezo kuhusu lishe bora. Kushoto ni
mmoja wa watu akipimwa afya baada ya kutembelea banda hilo leo.
Ofisa Ustawi wa Jamii wa Hospitali
ya Taifa Muhimbili (MNH), John Mwakyusa akitoa huduma ya ushauri kwa
mmoja wa watu waliotembelea banda hilo.
Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu
akimsikiliza Msimamizi wa wodi ya Kangaroo, Cleopatra Mtei jinsi ya
kuwabeba watoto wanaozaliwa kabla ya muda (premature).
Mtoto, Mnyaman Omary Mohammed
akizungumza na Waziri Ummy Mwalimu leo katika viwanja vya Muhimbili
ambako maonesho ya wiki ya Utumishi wa Umma yanaendelea.
Mkuu wa Idara ya Afya ya Akili, Dkt. Frank Masao akieleza shughuli mbalimbali za tiba zinazofanywa na idara hiyo.
No comments :
Post a Comment