Saturday, November 18, 2017

Mkandarasi Maginga Business Holding Co. L.t.d asitishiwa mkataba

image1
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Seleman Jafo akitoa maelekezo kwa Mkurugenzi Mtendaji wa TARURA Bw. Victor Seif wakati alipokuwa akikagua  ujenzi wa barabara ya kutoka Namelock hadi Sanya iliyopo  Wilayani Kiteto Mkoani Manyara.
image2
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Seleman Jafo akiwahutubia wananchi wa kijiji cha Sunya katika Wilaya ya Kiteto Mkoani Manyara.
image3
Ujenzi unaoendelea wa Barabara ya Namelock hadi Sunya kwa kiwango cha Changarawe yenye urefu wa kilometa 88.1 zilizoko katika wilaya ya Kiteto, Mkoani Manyara.
………………………………………………………………………………
Angela Msimbira OR –Tamisemi Kiteto
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mheshimiwa Seleman Jafo  amesitisha  mkataba wa  Mkandarasi Maginga Business Holding Co. L.t.d  aliyekuwa akijenga  barabara  kutoka  Namelock hadi Lopeltes  kwa kushindwa kumaliza ujenzi huo kwa wakati wilayani Kiteto , Mkoani Manyarai.
Akikagua  barabara hiyo Mhe Suleman Jafo amesema ...
hajarizishwa na kazi inayofanywa na Mkandarasi Maginga Business Holding Co. Ltd ambaye anajenga barabara ya kutoka  Namelock hadi Lukelo  kwa kuwa mkataba wake ulianza tangu tarehe 17/6/2017  na kupewa miezi Tisa kukamilisha kazi hiyo lakini mpaka leo barabara yenye kilometa 44.1  imesafishwa kilometa kumi na saba, hivyo dhamani ya kazi iliyotekelezwa  hadi sasa ni asilimia saba
Amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa TARURA Bw. Victor Seif  kuhakikisha wanaongea ndani ya siku saba ili kupata muafaka wa ujenzi wa barabara hiyo na asipojitokeza atolewe kwenye lisiti ya wakandarasi ambao hawataruhusiwa kufanyakazi za TARURA nchi nzima.
Amesema kuwa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa imepewa dhamana ya kusimamia na kutekeleza ujenzi wa miundombinu kwa  kuona hivyo imeanzisha wakala maalum wa kusimamia ujenzi wa barabra vijijini (Tarura) lengo likiwa ni kusimamia ujenzi wa barabara katika Mamlaka ya Serikali za Mitaa, barabara za vjijini na mijini
“Hakutakuwa na masiahara yeyote fedha zinazotengwa hizi zitasimamiwa kwa kiwango kisichorizisha, Serikali haitasita kuwachukulia hatua wafanyakazi wazembe ambao hawataki kuwafikia wananchi ili wapate huduma nzuri
Amesema barabara hiyo ya Namelock  hadi Sunya itajengwa  kwa kiwango kinachotakikana  na Serikali na lengo la serikali ni kujenga barabara ili uchumi wa kiteto uweze kupanda kutokana na miundombinu ya barabara iliyowekwa na Serikali
Amesema kuwa Maginga construction alipewa siku ishirini na nane kwa ajili parfomance appraisal lakini hakufanya hivyo  hii inaonyesha kuwa si mwaminifu  na uwezo wake wa kufanya kazi hauendani na kiwango cha kazi kilichotekelezwa, hivyo fedha ya serikali ingepotea na barabara ingekuwa haipo katika ubora unaotakiwa
Amesema barabara hiyo inatumia zaidi ya shilingi bilioni sita kwa ajili ya ujenzi wa barabara kutoka Namelock hadi Sunya,ukilinganisha na barabara zote zilizotengenezwa  yenyyewe inatumia fedha nyingi hivyo mkandarasi  ameonyesha dhahiri kwamba hakuweza kutekeleza kazi alizopewa katika mkataba wake na Serikali
Ameiagiza TARURA kuwaangaliwa wakandarasi ambao si waaminifu kutokupewa tenda za ujenzi wa barabara nchini  kwa kuona kuwa serikali ndio kichaka cha wadanganyifu kwa kuwa hivi sasa Serikali haitaji makanjanja katika suala zima la ujenzi wa barabara nchini.
Amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Taruara kuhakikisha mkandarasi huyo hapati kazi yeyote ndani ya  jamhuri ya muungano wa Tanzania,na kuwaonya wakandarasi wengine kutokufanyakazi kwa ubabaishaji bali wafanye kazi kwa weledi ili kutimiza malengo ya serikali ya ujenzi wa miundombinu bora kwa jamii.
Aidha Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Seleman Jafo amewaagiza Wakuu wa Mikoa na wakuu wa Wilaya kote nchini kusimamia miradi ya maendeleo nchini ili dhamani ya fedha inayotolewa na Serikali iendane na dhamani ya miradi inayotekelezwa nchini.
Mhe. Jafo amesema kazi kuu ya Wakuu wa  Mikoa nchini ni kusimamia maagizo yanayotolewa na serikali hasa katika suala zima la kusimamia maendeleo katika maeneo yao ili fedha zinazotolewa ziendane na kazi zinazotekelezwa katika jamii
Naye Mkurugenzi Mtendaji Mkuu Bw. Victor Seif amesema Serikali haitasita kuwachukulia hatua wakandarasi ambao wanaenda kinyumbe na mikataba wanayopatiwa na Serikali hasa katika suala zima la ujenzi wa miundombinu ya barabara.
Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Fedha iliingia makubaliano na shirika la kimataifa la Maendeleo la Marekani USAID kufadhili  miradi ya barabara katika wilaya  za Mvomero, Kilombero, Kongwa na Kiteto kwa mwaka wa  fedha 2014/2018.

No comments :

Post a Comment